Annunaki created Man: Binadamu tunaoishi sasa tulitengenezwa (tuliumbwa) na Annunaki

Maswali yako ni ya kiubishi zaidi, nimeelezea jinsi alivyoumbwa mtu scientifically zaidi kuliko nadharia ya kiimani, kama hukuona sayansi iliyotumika siyo kosa, sijuhi neno Sayansi kwako wewe lina maana ipi.
Hapana Mkuu, hakuna sehemu ambayo nimeku-accuse kwamba maswali yako au majibu yako ni ya kibishi, nimekua calm katika mjadala naomba sana tuendelee kwenye hoja kwa kurelax. Ukiniambia maswali yangu ya kibishi huko ni kuninyima haki ya kuhoji. Katika mjadala huu nimejikita kujadili kiimani(Spiritual) na kisayansi (Physical). Unasema umeelezea "MTU ALIVYOUMBWA KISAYANSI" na kiumbe annunaki.

Kwa mujibu wa (Science Methodology), ni kwamba Science haiamini katika imani inaamini katika facts and proving. nilikuuliza kuna kiumbe chenye mwili na uhai kinachoweza kujiumba chenyewe na kuumba kiumbe mwingine? Ukanijibu "HAKUNA".

Sasa, kama unasema umeeleza kiumbe annunaki alivyomuumba binadamu kisayansi, HUONI UNAJICHANGANYA? KAMA KISAYANSI HAKUNA KIUMBE CHENYE MWILI NA UHAI KINACHOWEZA KUUMBA KIUMBE MWINGINE MWENYE MWILI NA KUMPA UHAI, SASA KIUMBE ANNUNAKI MWENYE MWILI NA UHAI AMEWEZAJE KUUMBA KIUMBE MWENYE MWILI NA KUMPA UHAI?

Unajitetea kwa kusema kiumbe annunaki alikua ni EXTRAORDINARY, HUONI KAMA UKISEMA HIVYO UNAKUA UMEINGIA KWENYE IMANI/MIUJIZA? PIA UNAKUA UNAJICHANGANYA KWA KUMVISHA HUYO KIUMBE ANNUNAKI KWAMBA ANA UWEZO WA EXTRAORDINARY (IMANI/MIUJIZA) IKIWA HUYO KIUMBE ANNUNAKI KAUMBWA NA MUUMBAJI, ANA MWILI NA UHAI, ANAZALIANA NA ANAKUFA NA MABAKI YAKE YA MIFUPA YAPO, NA KISAYANSI HAKUNA KIUMBE MWENYE MWILI ANAYEWEZA KUUMBA KIUMBE MWINGINE MWENYE MWILI NA KUMPA UHAI.


Unaweza kuona labda maswali yako ni magunu sana kwamba umenikamata, lakini sivyo maswali yako ni mazuri sana na yenye logic ila majibu uliyokusidia kuyapata ni ya kiimani zaidi katika misingi ya kiimani hatuwezi kupata hitimisho la pamoja kihoja
Hiyo unasema wewe, mimi sipo katika misingi ya kukukamata. Nipo katika misingi ya HOJA (kiimani/Spiritual/Miujiza na Science/Physical) kwa sababu MUNGU ndiye muasisi na muumbaji wa (Spiritual&Physical Universe).


Mwisho niseme hao viumbe uwezo wao ni extraordinary level siyo kama sisi, kwa uwezo huo waliweza kumuumba mtu.
Hapa sasa ndipo unapojichanganya, unaingia katika imani/miujiza. Hii ina maana huna tofauti na mimi ambae hoja yangu ipo katika imani na sayansi (Spiritual&Physical).

Pia ukisema kiumbe annunaki yupo extraordinary, kisayansi yeye ni kiumbe tu chenye mwili na uhai amewezaje kuumba kiumbe mwingine (binadamu) mwenye mwili na kumpa uhai? ikiwa tumeshakubaliana kisayansi yeye hawezi kujiumba mwenyewe na kuumba kiumbe mwingine.


Kama Mungu amemuumba mtu kwa mfano wake, ila yeye unakubali kwamba ni extraordinary na hafananishwi na chochote, kwa nini nisiamini kwamba mtu ameumbwa na Anu & Anu is extraordinary level than his creature?
Mungu ni Extraordinary kwa sababu yeye MUNGU NDIYE MUUMBAJI WA ULIMWENGU USIOONEKANA KWA MACHO (SPIRITUAL) NA ULIMWENGU UNAOONEKANA KWA MACHO (Physical)

Nakuambia usiamini annunaki ameumba kiumbe binadamu. Kwa sababu:-

(i) kwa mujibu wa maelezo yako, kiumbe annunaki ni kiumbe tu kama viumbe wengine wenye mwili na uhai. Hivyo annunaki ameumbwa na hawezi kuumba kiumbe mwingine mwenye mwili na kumpa uhai. Hii ni (Scientifically Proved)

(ii) Mabaki ya mifupa yao yanathibitisha kwamba wao annunaki ni viumbe wenye mwili, wameumbwa, wamezaliana na wamekufa. Kisayansi hakuna kiumbe chenye mwili kinachoweza kuumba kiumbe mwingine mwenye mwili wa nyama na kumpa uhai.

(iii) ukisema annunaki ni extraordinary, unakua unakua umeingia kwenye (imani/miujiza) na kwamba annunaki wameumba binadamu kimiujiza, ikiwa wao annunaki wana mwili kama viumbe wengine. Hivyo kisayansi haikubaliki kwamba kiumbe chenye mwili na uhai kinachozaliana na kufa kiumbe kiumbe kingine chenye mwili na kumpa uhai.


Mkuu, haukuniuliza swali hili lakini kwa kuwa umeliuliza sasa nakujibu kama ifuatavyo:-

(Scientific Methodologically on how GOD created man)

Baada ya Mungu kufanya uumbaji wa vitu vyote katika ulimwengu unaoonekana kwa macho (Physical Universe) vitu kama jua, nyota, mwezi na sayari zote. Akaichagua sayari DUNIA na kuumba ardhi yenye rutuba, mimea na mazao ya kila aina, miti ya matunda ya kila aina, mito, maziwa na bahari, madini, mafuta, gas ardhini, upepo, vipindi vya majira mbalimbali ya mvua, joto n.k viumbe hai wa kila aina kama samaki, ndege, wanyama na mwisho kabisa MUNGU AKAMUUMBA MTU(BINADAMU)

How God created Man(human being)

Mungu alianza kwa kuumba mwili na organs zake zote na mifumo mbali mbali ya mwili wa kiumbe MTU(Binadamu) mwanaume kwa udongo na kumpulizia pumzi ya uhai, mtu huyo mwanaume akawa "NAFSI HAI" kisha akaumba kiumbe binadamu mwanamke pia.

Kwa pamoja akawa ameumba kiumbe binadamu wa "KIUME" na wa "KIKE". Kisha viumbe hao binadamu wa kiume na kike wakazaliana(REPRODUCTION)na kuijaza sayari dunia.

HIVYO NDIVYO MUNGU ALIVYOUMBA SAYANSI NA VIUMBE HAI WOTE KATIKA ULIMWENGU HUU UNAOONEKANA KWA MACHO (Physical Universese)
 
Wewe umetengenezwa na Annunaki vipi kuhisu dunia unayoishi , Jua na Mwezi vimetengenezwa na nani?

Mungu anasema kuna binaadamu wengine akiwaingiza peponi atakuwa amewadhurumu yani wao haki yao ni kuingia motoni
 
Unajitahidi sana kuandika na kujibu, ila mimi sijaona unachokitaka ni nini, unarudia vitu vile vile ambavyo nshajibu na kujadili, sehemu zote za huu uzi, haya yote unayokazana nshaelezea, ndiyo maana nimekwambia kama unaongozwa na imani ya dini hatutapata muhafaka.

Mimi ntakuwa wa mwisho kuamini binadamu wa sasa ameumbwa na huyo Mungu wa imani za dini, hata hii universe siyo yeye, utauliza ni nani?, Nshakwambia naendelea kuutafuta ukweli.

Kwahiyo kwa kuzingatia yaliyoandikwa kwenye vitabu vitakatifu na references zangu nilizotumia na ninazoendelea kuzisoma na kuzitafakari naamini Annunaki amemuumba mtu.
 
Wewe umetengenezwa na Annunaki vipi kuhisu dunia unayoishi , Jua na Mwezi vimetengenezwa na nani?

Mungu anasema kuna binaadamu wengine akiwaingiza peponi atakuwa amewadhurumu yani wao haki yao ni kuingia motoni
Umesahau ya kwamba Mungu anasamehe dhambi ukiungama, kwahiyo ukichinja watu kama kuku, ukazini n.k, ukitubu unasamehewa na peponi unaenda.
 
Ninachofurahi ni huyo Mungu kuwashughulikia wanaoabudu hiyo miungu anavyotaka na pia ndio Mungu mshindi wa kila vita against hiyo miungu. Pamoja na hizo historia nzuri ulizosema lakini kikubwa ni kumuabudu Mungu mwenye nguvu kuliko miungu yote.
 
Ninachofurahi ni huyo Mungu kuwashughulikia wanaoabudu hiyo miungu anavyotaka na pia ndio Mungu mshindi wa kila vita against hiyo miungu. Pamoja na hizo historia nzuri ulizosema lakini kikubwa ni kumuabudu Mungu mwenye nguvu kuliko miungu yote.
Wapi Huyo Mungu aliwashughulikia wanaoabudu miungu mingine nami nijiridhishe na source ya kuaminika?
 
Mkuu, annunaki ni kiumbe mwenye mwili na uhai amewezaje kuumba kiumbe mwingine mwenye mwili(Binadamu) na kumpa uhai? Ikiwa kisayansi hakuna kiumbe chenye mwili wa nyama na uhai kinachoweza kuumba kiumbe mwingine mwenye mwili na uhai.
 
Inna lillahi wa inna ilayhi rajiun
 
Mtoa mada kanichanganya kidogooo ila wewe UMENIVURUGA MKUU,HAPA UMENIVURUGA KABISAA
 
Sasa gharika TU inamuondoa ANNUNAKI????aisee Sasa kwanini nisimuabudu huyo aloleta GHARIKA?KUANZIA LEO NAKUABUDU NA KUKULILIA WEWE TU..
 
Hivi Annunaki walikuwa miungu au viumbe tu?

Anunaki ni viumbe tuu ambao wapo wa namna 2 mkuu aina ya kwanza ni wale supreme beings of pure green light ndio asili yao na kuna anunaki wengine wa impure amber light asili yao ni moto. Hawa pure supreme annunaki wa green light wameumbwa na mwanga wa kijani na hao impure sub-supreme beings wameumbwa kwa moto mfano wao ndio majini, vampires, na negqtive energies zote za uharibifu na hao annunaki wa kijani ndio wanadamu tunawaita Malaika.

Annunaki mfano wao ni kama binadamu kuna wazuri na wakarimu na kuna wabaya wenye roho mbaya. Kama wewe ni mtu mwema msaada wako upo kwa hao annunaki wema ambao ni wakijani na kama una roho mbaya msaada wako utaupata kwa hao annunaki wa moto ambao ndio majini.

Ili kuwafikia annunaki supreme beings unatakiwa uwe na pure of heart. Lakini ili uwafikie majini annunaki ambao ni amber light fire uwe mchawi na mwenye roho mbaya. Ndio mana kuna watu wakienda kwa mganga hawqfanikiwi na wengine wakienda wanafanikiwa. Jua asili ya chimbuko lako ndio utapata msaada sahihi.
 
Umenikosha sana, mungu akubariki kweli
Kuna machizi masomi humu duhhh Ni magumu kuelewa dahhh[emoji16][emoji16]
 
Ina maana kumbe hawa majini na malaika ndio Annunaki na ndio miongoni mwao wametuumba sisi binaadamu kama mleta mada alivyoeleza?
 
...Tukifa tunarejea Wapi? Kwa Annunaki ama kwa Mungu??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…