Tetesi: Ansbert Ngurumo: Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba, wamejivua uanachama wa CCM

Tetesi: Ansbert Ngurumo: Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba, wamejivua uanachama wa CCM

Status
Not open for further replies.
Kinana, Makamba wajivua uanachama CCM

Ansbert Ngurumo8th February 20200 Comments

MAKATIBU wakuu wastaafu wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba, wamejivua uanachama wa chama hicho.

Habari zilizoifikia SAUTI KUBWA zinasema Kinana na Makamba walijiondoa rasmi CCM kwa maandishi. Barua zao, kila mmoja na ya kwake, zilifikishwa ofisini kwa Katibu Mkuu wa CCM tarehe 7 Februari 2020.

Chanzo kinachoaminika kutoka CCM Makao Makuu kimeiambia SAUTI KUBWA: “Barua zao zimefika kwa nyakati tofauti, zimepokelewa. Lakini inaonekana kama walikuwa wameziandika muda mrefu baada ya kushauriana, maana zinafanana na zimewasilishwa siku moja. Taarifa hizi zilipofikishwa kwa Mzee (Rais John Magufuli) zilimvuruga kwa kweli.”

Kwa mujibu wa chanzo hicho, ambacho hakitatajwa hapa, Rais Magufuli, baada ya kupokea ujumbe wa Kinana na Makamba kujivua uanachama, aliwaomba wazee wawili waandamizi – Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Spika Mstaafu Pius Msekwa – wamsaidie kuzungumza na akina Kinana ili kuwashawishi wabadili msimamo wao.

Hata hivyo, Kinana na Makamba wamegoma kusikiliza ushawishi wa mtu yeyote. Katika barua zao za kujiondoa CCM, kwa mujibu wa chanzo chetu, Kinana na Makamba waliambatanisha pia kadi zao za uanachama.

“Tayari wameturudishia kadi zetu, maana yake wao si wanachama wetu tena,” kimesema chanzo hicho.

Kinana na Makamba ni miongoni mwa makatibu wakuu wanaoheshimika katika CCM, wenye ushawishi, na ambao wametumikia nchi katika nyadhifa mbalimbali kuanzia jeshini hadi serikalini na kwenye chama.

Siku ambayo walikabidhi barua na kadi zao na kutangaza rasmi kujiondoa CCM, ndiyo siku walipotarajiwa kuhojiwa na Kamati ya Maadili ya CCM iliyoagizwa na Rais Magufuli katika kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), ili wajieleze kuhusu waraka walioanidika kwa Baraza la Wazee la chama hicho wakilalamikia kubezwa na kudhalilishwa na mhuni mmoja anayetumia jina la rais kudhihaki na kushambulia wakosoaji wa rais na serikali.

Mbali na Kinana na Makamba, mwingine aliyeitwa kuhojiwa na kamati hiyo ni Bernard Membe, waziri wa zamani wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ambaye aliunga mkono waraka wa wazee hao, na pia alidukuliwa akizungumza katika simu mambo ambayo hayakumfurahisha Rais Magufuli.

Yeye alikutana na kamati hiyo Mjini Dodoma Ijumaa tarehe 7, Februari 2020; na baada ya mahojiano alionekana mwenye kujiamini na mwenye furaha. Mmoja wa wajumbe walioshiriki mahojiano hayo amezungumza na SAUTI KUBWA kwa sharti la kutotajwa, akisema: “Tulijuta kumuita Membe. Kuna maswali amehoji na masuala amezungumza nasi hadi tukahisi yeye ndiye anayetuhoji. Ukweli ni kwamba chama chetu kinahitaji mabadiliko makubwa ya kimsingi, maana kuna shida mahali. Bwana mkubwa anatupelekesha, na watu jasiri wa kumwambia ukweli hawapo, tunaishia kuagizwa tu, hata kutenda mambo yaliyo kinyume cha misingi ya CCM. Membe ametukumbusha yote haya. Kwa kweli, sijui kinachoofuata.”

Hata hivyo, SAUTI KUBWA iliambiwa wiki iliyopita kuwa agizo la kamati kuwahoji wakongwe hao lilikuwa kama igizo tu, kwani Rais Magufuli na watu wake walishaamua kuwa Membe na Kinana wavuliwe uanachama, na Mzee Makamba apewe onyo kali.

Kwa Kinana na Makamba kujivua uanachama na kugoma kuhojiwa, wamewaza hatua mbili mbele ya Magufuli. Chama hakiwezi kuwahoji kwa kuwa wao hawafungwi tena na nidhamu wala maadili ya CCM kwa kuwa si wanachama CCM.

Ingawa barua zao zilipelekewa kimya kimya, na uongozi wa juu wa CCM umekuwa unahangaika kuzuia taarifa hizi kuvuja, zilivuja mapema mno; na kitendo chao cha kutofika mbele ya kamati kuhojiwa kimezua maswali na mjadala mpana ndani nanje ya CCM.

Baadhi ya wadau wa siasa za Tanzania wanasema inawezekana kitendo hiki kikawaingiza wote wawili, au mmoja wao, kwenye matata makubwa, kwani uongozi wa CCM ni wa visasi, unaweza kutaka kuwakomoa na kuwadhalilisha.

Profesa mmoja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam amesema: “Tusishangae sasa kusikia siku moja Kinana au Makamba wametiwa mbaroni na wanashitakiwa kwa utakatishaji fedha, maana hii ndiyo fimbo mpya ambayo inatumika kuumiza wanaotofautiana na watawala. Lakini iwapo watashitakiwa umma utajua kuwa sababu hasa si uhalifu wao bali ni hii barua yao na uamuzi wao.”

Kiongozo mmoja mwandamizi wa CCM ameiambia SAUTI KUBWA: “Kiukweli, Mzee Kinana na Mzee Makamba hawana cha kupoteza. Nadhani sisi ndio tuna cha kupoteza, maana ukisoma waraka unaowasababishia haya yote utagundua kuwa wao ni watetezi wa misingi ya chama chetu. Wanachotetea ndicho wanaCCM wote tunapaswa kutetea, lakini sasa tofauti iliyopo kati yetu na wao ni kwamba wao wameonyesha ujasiri ambao sisi hatuna. Wengi wetu tumebaki kutii maagizo ya bwana mkubwa, huku chama kinaporomoka!”

SAUTI KUBWA inatambua kuwa kuna mtifuano mkubwa ndani ya CCM ambao haujawahi kutokea tangu uwepo wa chama hicho, ingawa wanafanikiwa kuufunika kwa kutishana – kwa kutumia vuombo vya dola.
Duh!, kama ni kweli, hii ni kali ya mwaka, ila mimi ni mmoja katika kundi la kina Tomaso, siamini mpaka CCM wenyewe waseme!.
P
Tena ni kweli aloo!!
Hata Mkapa na JK wakirudisha kadi bado chama letu halitetereki.

JPM ni mwisho wa maarifa.
Anazo mbinu zaidi ya elfu moja za kuimarisha chama cha mapinduuzi
Kwa mwenye kufuatilua siasa hawa. Mabwana hata wakitoka ,sidhani hata kama ccm itayumba,ccm waliikuta na wataicha,wengi tulijua kuwa mwaka 2015 baada ya Mh lowasa kuikimbia ccm,hapo ndo ilikuwa mwisho wake,cha ajabu hadi sasa ccm inachanja mbuga,

Eti jpm awabembeleze,kwa lipi? Ccm kila siku unavuna wanachama wapya sasa itateteleshwaje na tu watu tuwili?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Reading between the lines ni wazi mleta mada umekuwa planted na kikundi cha Membe, Makamba, Kinana na like minds wenzao ambao wamepania kuhakikisha JPM anakuwa one term President - hilo ndilo lengo lao kuu!! Taarifa zinazo sambazwa kwenye Social media na wanao jihita "SAUTI KUBWA" habari hizo ni za kutunga tu, watu wachache wanajifungia kwenye chumba wanatunga hadithi za kufikirika tu ndio maana wanazuga wasomaji kwa kudai taarifa zao wanazipata kutoka kwa mjumbe wa kikao cha kuhoji akina Membe,Kinana na Makamba eti mjumbe huyo hataki jina lake lijulikane, mara sijui taarifa zimepatikana kutoka kwa Professa ambaye hana jina, taarifa nzima na ufafanuzi unaonekana ni wa kitoto kabisa.

Kundi hili linalo pania kumu - undermine JPM linakuwa driven na jeuri ya pesa hicho ndicho kinawafanya wajiamini sana na kujaribu ku-black mail Chama tawala, kama wanataka kujiondoka CCM waondoke zao - Uongozi wa CCM unapashwa kuwa imara na msimamo thabati, after all as I said CCM can afford to do without the trios. Serikali hisiruhusu wasaliti kutumia uwezo wao kifedha kueneza propaganda za kutunga tu kwa kutumia mbinu za misinformation and disinformation lengo likiwa ni kutaka kutoa impression ili CCM ionekana hiko mbioni kugawanyika vipande vipande kama ilivyo kuwa KANU ya Kenya, hicho ndicho wanacho lenga.

Narudia kisisitiza kwamba Genge hili halina nia njema na mstakabali wa Taifa letu hata kidogo, in other words si watu wa kuchukulia lightly na wanaonekana wako highly organised kutaka kuvuruga Chama,JPM na Taifa kwa ujumla.
Hapa ishu ni serikali au chama?
 
SAUTI KUBWA wamechafua na kudhalilisha jina lao na kada nzima ya uandishi huru.

Vyanzo vyao vimewaambia Bwana Mkubwa amefedheheka mpaka kutafuta watu wa kwenda kuwabembeleza kina Makamba.

Na vyanzo hivyo hivyo vimewataarifu Mzee alishapanga kuwapiga paranja uanachama na hivi vikao ni ghereaha tu, na wakileta mbwai watafanyiwa mbwai za utakatishaji, usanifu, uratibu na ufadhili wa genge la uhalifu na uhujumu wa uchumi.

Mwandishi si tu anafika aya ya tano keshasahau aya ya pili alidanganya nini bali hata kupitia andiko kabla ya kurusha hewani anasahau.
Mkuu hujawahi sikia msemo unsema , "A week is a very long time in politics". Aya zote mbili zinaweza kuwa sahihi. Inaweza wiki moja alipanga na wiki iliyofuate akapangua
 
Reading between the lines ni wazi mleta mada umekuwa planted na kikundi cha Membe, Makamba, Kinana na like minds wenzao ambao wamepania kuhakikisha JPM anakuwa one term President - hilo ndilo lengo lao kuu!! Taarifa zinazo sambazwa kwenye Social media na wanao jihita "SAUTI KUBWA" habari hizo ni za kutunga tu, watu wachache wanajifungia kwenye chumba wanatunga hadithi za kufikirika tu ndio maana wanazuga wasomaji kwa kudai taarifa zao wanazipata kutoka kwa mjumbe wa kikao cha kuhoji akina Membe,Kinana na Makamba eti mjumbe huyo hataki jina lake lijulikane, mara sijui taarifa zimepatikana kutoka kwa Professa ambaye hana jina, taarifa nzima na ufafanuzi unaonekana ni wa kitoto kabisa.

Kundi hili linalo pania kumu - undermine JPM linakuwa driven na jeuri ya pesa hicho ndicho kinawafanya wajiamini sana na kujaribu ku-black mail Chama tawala, kama wanataka kujiondoka CCM waondoke zao - Uongozi wa CCM unapashwa kuwa imara na msimamo thabati, after all as I said CCM can afford to do without the trios. Serikali hisiruhusu wasaliti kutumia uwezo wao kifedha kueneza propaganda za kutunga tu kwa kutumia mbinu za misinformation and disinformation lengo likiwa ni kutaka kutoa impression ili CCM ionekana hiko mbioni kugawanyika vipande vipande kama ilivyo kuwa KANU ya Kenya, hicho ndicho wanacho lenga.

Narudia kisisitiza kwamba Genge hili halina nia njema na mstakabali wa Taifa letu hata kidogo, in other words si watu wa kuchukulia lightly na wanaonekana wako highly organised kutaka kuvuruga Chama,JPM na Taifa kwa ujumla.
Mapimbi utawajua tu, kwani ccm ndiyo taifa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Propaganda at work
Kinana, Makamba wajivua uanachama CCM

Ansbert Ngurumo8th February 20200 Comments

MAKATIBU wakuu wastaafu wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba, wamejivua uanachama wa chama hicho.

Habari zilizoifikia SAUTI KUBWA zinasema Kinana na Makamba walijiondoa rasmi CCM kwa maandishi. Barua zao, kila mmoja na ya kwake, zilifikishwa ofisini kwa Katibu Mkuu wa CCM tarehe 7 Februari 2020.

Chanzo kinachoaminika kutoka CCM Makao Makuu kimeiambia SAUTI KUBWA: “Barua zao zimefika kwa nyakati tofauti, zimepokelewa. Lakini inaonekana kama walikuwa wameziandika muda mrefu baada ya kushauriana, maana zinafanana na zimewasilishwa siku moja. Taarifa hizi zilipofikishwa kwa Mzee (Rais John Magufuli) zilimvuruga kwa kweli.”

Kwa mujibu wa chanzo hicho, ambacho hakitatajwa hapa, Rais Magufuli, baada ya kupokea ujumbe wa Kinana na Makamba kujivua uanachama, aliwaomba wazee wawili waandamizi – Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Spika Mstaafu Pius Msekwa – wamsaidie kuzungumza na akina Kinana ili kuwashawishi wabadili msimamo wao.

Hata hivyo, Kinana na Makamba wamegoma kusikiliza ushawishi wa mtu yeyote. Katika barua zao za kujiondoa CCM, kwa mujibu wa chanzo chetu, Kinana na Makamba waliambatanisha pia kadi zao za uanachama.

“Tayari wameturudishia kadi zetu, maana yake wao si wanachama wetu tena,” kimesema chanzo hicho.

Kinana na Makamba ni miongoni mwa makatibu wakuu wanaoheshimika katika CCM, wenye ushawishi, na ambao wametumikia nchi katika nyadhifa mbalimbali kuanzia jeshini hadi serikalini na kwenye chama.

Siku ambayo walikabidhi barua na kadi zao na kutangaza rasmi kujiondoa CCM, ndiyo siku walipotarajiwa kuhojiwa na Kamati ya Maadili ya CCM iliyoagizwa na Rais Magufuli katika kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), ili wajieleze kuhusu waraka walioanidika kwa Baraza la Wazee la chama hicho wakilalamikia kubezwa na kudhalilishwa na mhuni mmoja anayetumia jina la rais kudhihaki na kushambulia wakosoaji wa rais na serikali.

Mbali na Kinana na Makamba, mwingine aliyeitwa kuhojiwa na kamati hiyo ni Bernard Membe, waziri wa zamani wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ambaye aliunga mkono waraka wa wazee hao, na pia alidukuliwa akizungumza katika simu mambo ambayo hayakumfurahisha Rais Magufuli.

Yeye alikutana na kamati hiyo Mjini Dodoma Ijumaa tarehe 7, Februari 2020; na baada ya mahojiano alionekana mwenye kujiamini na mwenye furaha. Mmoja wa wajumbe walioshiriki mahojiano hayo amezungumza na SAUTI KUBWA kwa sharti la kutotajwa, akisema: “Tulijuta kumuita Membe. Kuna maswali amehoji na masuala amezungumza nasi hadi tukahisi yeye ndiye anayetuhoji. Ukweli ni kwamba chama chetu kinahitaji mabadiliko makubwa ya kimsingi, maana kuna shida mahali. Bwana mkubwa anatupelekesha, na watu jasiri wa kumwambia ukweli hawapo, tunaishia kuagizwa tu, hata kutenda mambo yaliyo kinyume cha misingi ya CCM. Membe ametukumbusha yote haya. Kwa kweli, sijui kinachoofuata.”

Hata hivyo, SAUTI KUBWA iliambiwa wiki iliyopita kuwa agizo la kamati kuwahoji wakongwe hao lilikuwa kama igizo tu, kwani Rais Magufuli na watu wake walishaamua kuwa Membe na Kinana wavuliwe uanachama, na Mzee Makamba apewe onyo kali.

Kwa Kinana na Makamba kujivua uanachama na kugoma kuhojiwa, wamewaza hatua mbili mbele ya Magufuli. Chama hakiwezi kuwahoji kwa kuwa wao hawafungwi tena na nidhamu wala maadili ya CCM kwa kuwa si wanachama CCM.

Ingawa barua zao zilipelekewa kimya kimya, na uongozi wa juu wa CCM umekuwa unahangaika kuzuia taarifa hizi kuvuja, zilivuja mapema mno; na kitendo chao cha kutofika mbele ya kamati kuhojiwa kimezua maswali na mjadala mpana ndani nanje ya CCM.

Baadhi ya wadau wa siasa za Tanzania wanasema inawezekana kitendo hiki kikawaingiza wote wawili, au mmoja wao, kwenye matata makubwa, kwani uongozi wa CCM ni wa visasi, unaweza kutaka kuwakomoa na kuwadhalilisha.

Profesa mmoja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam amesema: “Tusishangae sasa kusikia siku moja Kinana au Makamba wametiwa mbaroni na wanashitakiwa kwa utakatishaji fedha, maana hii ndiyo fimbo mpya ambayo inatumika kuumiza wanaotofautiana na watawala. Lakini iwapo watashitakiwa umma utajua kuwa sababu hasa si uhalifu wao bali ni hii barua yao na uamuzi wao.”

Kiongozo mmoja mwandamizi wa CCM ameiambia SAUTI KUBWA: “Kiukweli, Mzee Kinana na Mzee Makamba hawana cha kupoteza. Nadhani sisi ndio tuna cha kupoteza, maana ukisoma waraka unaowasababishia haya yote utagundua kuwa wao ni watetezi wa misingi ya chama chetu. Wanachotetea ndicho wanaCCM wote tunapaswa kutetea, lakini sasa tofauti iliyopo kati yetu na wao ni kwamba wao wameonyesha ujasiri ambao sisi hatuna. Wengi wetu tumebaki kutii maagizo ya bwana mkubwa, huku chama kinaporomoka!”

SAUTI KUBWA inatambua kuwa kuna mtifuano mkubwa ndani ya CCM ambao haujawahi kutokea tangu uwepo wa chama hicho, ingawa wanafanikiwa kuufunika kwa kutishana – kwa kutumia vuombo vya dola.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh! Bora angalau angalau Makamba! Lakini Kinana? Kinana ni fisadi mkubwa aliyepora na kujilimbikizia mali kwa kofia ya Katibu mkuu wa CCM! Safishasafisha ya Magufuli ndani ya CCM ilimuacha hoi bin taabani na kuanza fitna! Maji yamewafika shingoni! Kuondoka CCM sio dawa! Dawa ni kurudisha Mali za Chama na hela za umma na kuwaomba wananchi msamaha madharara waliyowasababishia kwa wizi huo! Chini JPM kila jiwa litapinduliwa. Lowassa, Kingunge na Sumaye sasa hivi wako wapi! Usicheze na CCM!
Una ushahidi wa wizi walioufanya?
 
Huyu Ansbert Ngurumo ni kanjanja tu ... hanna ukweli
 
Mtu mmoja aliwahi sema "Sometimes revolutions eat their own children"

Kama ni kweli, wapewe pole, hasa hasa aliyesema "tutabatizwa kwa moto"
 
Hakuwa weak..niseme alikuwa na tamaa. Tamaa yake iliizidi akili akashindwa kufanya maamuzi sahihi wakati alipotakiwa kufanya hivyo.

Ndo weaknesses zenyewe...
Hata 'aliposhinda' bado aliendelea kuwa very weak!
 
Tena ni kweli aloo!!
Hata Mkapa na JK wakirudisha kadi bado chama letu halitetereki.

JPM ni mwisho wa maarifa.
Anazo mbinu zaidi ya elfu moja za kuimarisha chama cha mapinduuzi

Sent using Jamii Forums mobile app

Tatizo la JPM ni kuwa anaiuza nchi kwa Kagame...
Ajenda zote za Kagame dhidi ya TZ zinatekelezeka kirahisi rahisi tu...!!
 
Kwa mwenye kufuatilua siasa hawa. Mabwana hata wakitoka ,sidhani hata kama ccm itayumba,ccm waliikuta na wataicha,wengi tulijua kuwa mwaka 2015 baada ya Mh lowasa kuikimbia ccm,hapo ndo ilikuwa mwisho wake,cha ajabu hadi sasa ccm inachanja mbuga,

Eti jpm awabembeleze,kwa lipi? Ccm kila siku unavuna wanachama wapya sasa itateteleshwaje na tu watu tuwili?

Sent using Jamii Forums mobile app
Haohao unaowabeza ndio walio mbeba huyo mtuwako, kwenye 10 wanaandika 10000 ili mradi huyo apite kwa halali au kwa haramu!
 
Drama hizi za ccm sio za kuamini sana.. Kuna wakati hao wazee wakiwa madarakani walikuwa untouchables lakini pia wana tuhuma lukuki kama viongozi wengine wote wa ccm... Tusubiri yatokanayo

Jr[emoji769]
Alafu mzee mmoja mwizi wa twiga wetu hatujasahau file lake tunalo
 
Hata kama wanatuhuma (kama ambavyo viongozi wote walivyo nazo) utaratibu ulipaswa kufuatwa.
Hatuwezi chama chetu kukubali kiendeshwe kihuni na kukoseana heshima kwa kuwatumia kina Musiba na Makonda kutukana na kudhalilisha watu.
Julai tunambwaga mwenyekiti (anayepeleka mambo kihuni) kwa kumnyima kubeba bendera uchaguzi 2020 kisha baada ya hapo tunamfyeka. Inatosha sasa

Sent using Jamii Forums mobile app


Unachekesha wewe, Mwenyekiti wa CCM ni Raisi na Amiri Jeshi mkuu was JMTZ, na Raisi wa JMTZ ni Raisi mpaka pale Raisi mwingine atakapoapishwa, sasa huyo ni mtu kubagwa? Unaota.
 
Viongozi wote hata Uncle anatuhuma suala ni kubadli katiba ili baada awamu kuisha wasiwe na kinga ya kushitakiwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom