Anzeni kuwekeza kwenye Crypto

Anzeni kuwekeza kwenye Crypto

Unapatikana wapi?

Kipindi kile hizi mambo za Crypto zinaingia duniani huku kwenu hatukuwa na uelewa nazo kabisa kwahiyo ilikuwa ni ngumu sana kuchukua maamuzi. Angalau kwa sasa watu wana ufahamu nazo, ni masuala ambayo yapo na ni kweli kabisa. Binafsi bado sina uelewa wa hayo mambo ila nafahamu tu kuna kitu inaitwa crypto watu wanafanya miamala huko.

Nimekuuliza hapo juu unapo patikana nia yangu nataka nikufuate ulipo kisha tufungue akaunti baada ya hapo ninunue hizo coin ni hold kwa muda kadhaa, sijui chochote kile kuhusu hayo mambo kwahiyo sijui naanzia wapi mpaka kununua hizo coin.

Naamini hizi mambo za Crypto zitapanda thamani sana hasa kipindi hichi Trump anaingia madarakani maana yeye mwenyewe ni mfuasi wa hayo masuala, jana kuna video nimeona akilipia burger kwa kutumia Crypto ndio maana kwa sasa zina panda kw kasi sana.
Ndiyo mkuu. Uzuri ni kwamba Unaweza Kufungua Akaunti Mwenyewe Hapo Hapo Ulipo. Unachotakiwa ni kujifunza Vitu Vidogo Kuhusu Mtandao. Unaweza Kuangalia Video Online Mkuu Nakupata Uelewa.
 
Ndiyo mkuu. Uzuri ni kwamba Unaweza Kufungua Akaunti Mwenyewe Hapo Hapo Ulipo. Unachotakiwa ni kujifunza Vitu Vidogo Kuhusu Mtandao. Unaweza Kuangalia Video Online Mkuu Nakupata Uelewa.
Umemkataa mwamba kiutamu sana🤣🤣
 
Hizi bitcoin sijui dodge coin ukitaka fedha kamili za madafu unazipataje? Tatizo tunaogopa hii mifumo ya mitandao ni rahisi kupigwa na ofisi ya kwenda kulalamikia hamna😀
Naona sasa umelielewa vizuri somo la Nape na jinsi alivyokuwa anapambana na Stralink ili kumlinda mtanzania😁
1000015807.jpg
 
Tatizo la crypto currency ni volatility, yaani ni rahisi sana kupata faida ndan ya muda mfup na ni rahisi sana pia kupata hasara ndan ya muda mfupi.

Kiufupi kuwekeza kwenye crypto ni hatar kama ilivo betting.
 
Tatizo la crypto currency ni volatility, yaani ni rahisi sana kupata faida ndan ya muda mfup na ni rahisi sana pia kupata hasara ndan ya muda mfupi.

Kiufupi kuwekeza kwenye crypto ni hatar kama ilivo betting
🤣🤣🤣🤣🤣 Dah aisee!
 
Hapana mkuu sijamkataa, ila ni vizuri akafungua mwenyewe.
Mkuu umejitahidi sana kuelezea, kiukweli mimi nishaacha kuelezea watu kuhusu crypto kwasababu hata ndugu zangu tu hakuna alieniamini pia watu wengi sana walipigwa kwenye maswala ya platform sababu transaction zilikuwa zinafanyika inform ya bitcoin yaani walitumua USDT.

Sasa wengi wanazani na coin zina mifumo hiyo hiyo. Kitu cha kujiuliza kama serikali ya marekani imeamua kuikubali crypto na yenyewe inataka kuwa dominator wa bitcoin dunian na pia wanamiliki bitcoin na other coins sisi ni nani mpaka tuwapinge?

Kikubwa wewe piga pesa zako tulia wakiuliza umepata wapi hela waambie ulienda kwa mganga, maana kuwaambia habari za crypto hawatakuelewa.

Au hata wakielewa wanaweza kuzan ni swala la kupata hela haraka haraka kitu ambacho sio kweli hivyo wanaweza wakawekeza na matarajio makubwa mwisho wakapoteza lawama zikawa kwako.

Mimi nilianza kununua crypto 2021 mwishoni baada ya kuona watu wamepiga hela, kumbe wakati nanunua ndio ilikuwa mwisho wa msimu kunakipindi nilihisi huu ni utapeli lakini nikaamua kujifunza ndio nikagundua crypto inapanda kila baada ya miaka minne na mwaka wa tano ndio hupanda zaidi.

Huu mwaka baada ya trump kushinda nimeshangaa ile hasara yote imerudi na faida juu tena kubwa tu sasa jiulize kile kipindi ningemshawishi ndugu yangu je angeweza kuvumilia au saiz ningekuwa naitwa tapeli wa ukoo??.
Hizi mambo zinahitaji kujifunza kwanza kabla ya kuwekeza maana ni very risk pia zina returns nzuri kama ukielewa jinsi zinavyooperate kikubwa mtu ajifunze kwanza kabla ya kuinvest.

Mwaka jana kuna coin kama tatu nilinunua kwa $250 jumla kwenye exchange ya mexc baada ya miezi minne nakuja kuangalia sizioni kufatilia kumbe zilikuwa scamm token hela ikawa imeenda hivyo.

Je ningekuwa nimemshauri na mtu mwingine anunue kama mimi ingekuwaje??. Mwisho wa siku tunasema kabla ya kuinvest do your own research pia invest money your can afford to lose.
 
Kabisa mkuu. Tuendelee ku take risk
 
Tatizo la crypto currency ni volatility, yaani ni rahisi sana kupata faida ndan ya muda mfup na ni rahisi sana pia kupata hasara ndan ya muda mfupi.

Kiufupi kuwekeza kwenye crypto ni hatar kama ilivo betting.
Ngoja nikueleze kitu moja...

Crypto trading ni biashara tu kama biashara nyingine, na kawaida ya biashara huwa ina vipengele tofauti. Mfano; wewe unaweza fungua duka ukauza kwa jumla tu, mimi naweza fungua duka nikauza reja reja, lakini zote ni biashara za duka! Ndivyo ilivyo crypto, kuna aina nyingi za trading ambazo baadhi ni very risk na nyingine ni low risk, sasa maamuzi ni yako!

Wengi huoata hasara kwenye crypto sababu wana mitaji midogo, unakuta mtu ana 100K lakini anataka apate faida 10x ya uwekezaji wake tena kwa muda mfupi tu! Hapo sasa itakuwa ni betting na siyo crypto trading. Ila kuna wenye mitaji ya 10M+ ambao wana-target faida ya angalau 5% kwa wiki ambayo unaweza kuipata vizuri tu.

Mfano kuna aina ya trading inayoitwa futures, hii inafaida sana ila ni hatari mno na hasa zaidi kwa wenye mtaji mdogo! Hii aina ya trading inaweza kupa 100x return ndani ya dakika 10 tu! Lakini pia inaweza kukuacha na $0 ndani ya dakika 5 tu! Ila pia unaweza punguza hatari ya futures ukiwa na mtaji mzuri, kwasababu tunatumia kitu kinaitwa leverage, unavyoweka leverage kubwa ndio faida inakuwa kubwa zaidi na hiki ndicho kina wa-cost wenye mitaji midogo sababu wanatumia leverage kubwa wapate faida kubwa! Ila mwenye mtaji mdogo anatumia leverage ndogo maana hata akipata 2% ya mtaji wake bado anakuwa na faida nzuri tu!

Kuna aina nyingine ya trading inaitwa Day trading au Spot trading. Hii pia sio hatari sana, hapa huwa tuna-target sarafu zinazopanda na kushuka kila siku, unasoma charts za sarafu husika kisha unafanya technical analysis (unaweza tumia Trading View) na hapo utapata jibu either ununue sarafu hiyo au usinunue. Kwenye spot trading unaweza nunua sarafu saa 1 asubuhi na ukauza saa 7 mchana na ukapata faida yako nzuri tu, na hii haina risk sana uki-target sarafu nzuri.

Pia kuna arbitrage trading! Hii naipenda sana, nadhani kuliko zote (ingawa napenda futures pia). Kwenye arbitrage ni unanunua sarafu kutoka kwenye exchange moja na kuiuza kwenye exchange nyingine kwa faida kidoooogo tu! Yaani unaangalia labda $TRX Binance ni $0.1442 na $TRX hiyo hiyo KuCoin ni $0.1447 kwahiyo hapo pana difference ya $0.0005 ambayo faida yako inaweza range Kati ya $0.0002 - $0.0005 kulingana na kubadilika kwa soko pamoja na cost za ununuzi, uuzaji, na TX fee. Sasa hapo utapata faida bila risk yoyote, ingawa utahitaji mtaji mkubwa, na pia utatakiwa utulize kichwa haswa kupitia utofauti wa bei kwenye walau exchanges 3/5.

Na nyingine isiyo na risk kubwa ni P2P trading (peer to peer) hii trading inafanywa na waTZ wengi sana pale Binance, kuna watu wana pesa aise! Hapa ni unafanya biashara ya kubadilisha sarafu locally, yaani mimi nna $1000 USDT na wewe una 3M TZS, kwahivyo nakuomba wewe nikuuzie USDT zangu kwa bei ya juu kidogo ya soko ili upate faida, na kisha wewe unanitumia pesa ya TZ kwenye account zangu za pesa kulingana na kiasi cha USDT nilichokuuzia, hii ni sawa pia kwa upande kununua USDT.

Yoooote kwa yote, kuna aina zaidi ya tajwa hapo za ku-trade crypto, la kuzingatia zaidi ni kufanya uchambuzi wa masoko na sarafu unayotaka kununua ili usijikute kwenye hasara!

Unaweza ukaogopa kununua crypto ukihofia itashuka upate hasara, ila ukanunua mahindi gunia 100 kwa Tsh 35,000 kwa gunia na ukaweka stoo ili uuze kwa 50K kwa gunia, na mwisho wa siku soko likashuka ukaja kuuza kwa hasara ya 20K kwa gunia! Mafuta, mchele, sukari, na hata mazao mengine kama vitunguu, nyanya, tikiti... zooote hizo hupanda/hushuka/na huweza kuharibika ukapata hasara kubwa! Kiufupi ni kwamba hakuna biashara isiyo na hasara! Muhimu ni kufanya biashara yako kwa umakini mkubwa ili kupunguza hasara na kuongeza faida.
 
Mazee kama mpaka 2030 huja hold coin. Utajiulaumu🥱
Ushauri wa bure sahiv XRP ina thamani ya dolla 2.4 ,wengine wataona kwamba imepanda thamani sana ila kiuhalisia ipo chini sana jaribu kuhold hata za dolla 100. ujumbe huu baada ya miaka mitano ijayo utaukumbuka leo tarhe 07/12/2024
 

Attachments

  • Screenshot_20241207-172802.jpg
    Screenshot_20241207-172802.jpg
    163.4 KB · Views: 8
Ushauri wa bure sahiv XRP ina thamani ya dolla 2.4 ,wengine wataona kwamba imepanda thamani sana ila kiuhalisia ipo chini sana jaribu kuhold hata za dolla 100. ujumbe huu baada ya miaka mitano ijayo utaukumbuka leo tarhe 07/12/2024
Anvalia nyingine ni meme coin
 
Wakuu Kuna Haja Ya Kuanza Kuwekeza Kwenye Crypto Kama Bado Huja Anza.

Dogecoin Mwezi Uliopita Yaani Tarehe 31/10 Ilikuwa Inauzwa Dollars 0.168146 Sawa na kama TZS 200 Kwa Exchange Rate Ya Tarehe 31/10/2024.

View attachment 3150202

Wakati leo hii Dogecoin Imepanda Thamani na Kufikia 1100 mpaka sasa hivi na inaendelea kupanda. Jana mchana saa 9 jioni ilikuwa ina thamani ya 679 Ila leo imeamka Na TZS 1100.

View attachment 3150199

Mpaka Kufika Jioni Itaweza Kupanda Zaidi.

Fikiria kama ungenunua dogecoin za thamani Ya 100000 Tarehe 31/10 leo ungepata dogecoin 500 kwa bei ya 200. Sasa chukua dogecoin thamani ya dogecoin ya leo ya 1100 zidisha mara dogecoin zako 500 utapata 550000. Ungekuwa umetengeneza faida ya TZS 400000 kufikia leo hii.

Bitcoin ilikuwa Ina Thamani Ya milioni 170TZS mwezi uliopita leo Hii Ina Thamani Ya million 236,012,506.25 TZS. Piga Hesabu Ya Faida Aliyopata Mtu Aliyenunua Mwezi Uliopita.

View attachment 3150198

Tuachane Na Bitcoin Kwa Sababu Wachache Wanaweza Kununua. Sisi tuanze kununua Dogecoin Au Anza kununua Currency Za Bei Ya Chini Zaidi.

Naona Utajiri Mkubwa Kwenye Sarafu Ya Mtandaoni Kwa Wale Watakaochukua Hatua Sasa Hivi.

Elon Musk And Trump Effects.
Ok
 
Kiukweli huko mtandaoni kuna hela nyingi sana za bure. Mwaka 2021 kuna company nilijiunga kwa USD 100 ndani ya miezi 6 nikatoa 200(500000) nikaacha 200$ iendelee kuzaa bahati mbaya nikakaa nje ya mtandao kidogo nikashtuka mifumo imebadilika nikawa nishapoteza zaid ya 300$ , baada ya hapo mwaka huu nimerudi kwenye business na company mpya saivi nataka kua serious kidogo maana kipindi kile nilikua na mawenge yakutapeliwa mda wote!
 
  • Thanks
Reactions: Ser
Hizi bitcoin sijui dodge coin ukitaka fedha kamili za madafu unazipataje? Tatizo tunaogopa hii mifumo ya mitandao ni rahisi kupigwa na ofisi ya kwenda kulalamikia hamna😀

Nikikumbuka scam za FTX na benance ndo naona Crypto ni betting kama betting zingine

Hi biashara ya kunambia ninunue crypto kisha utajiri wake eti ninhold sababu ni long investment ila cha ajabu hao wanaokwambia ununue then hold and dont sell because after few years you will make a fortune ndo hao wanaotaka kukuuzia.. mbona wao hawa hold

Crypto nyigi wanatengeneza hype kuwauzia watu baadae unaona zinashuka thaman baada ya demand kupungua.. yotube ziko video nyingi watu waliopiga pesa na watu walioliwa
Pesa yaan ukiuliza hiii crypto currency thaman yake inalindwa na nini utasikia inalindwa kwa kuwa na demands kubwa... nje ya demand hakuna backup ya kitu chochote demand ikishika then na thamani inapotea

bitcoin ina thaman kubwa sasa hivi ila
Thaman yake iko kwenye demand sababu kila mtu hataki kuuza ila bado haijawa universal kuitumia kama pesa maana haikubaliki na nchi zote.. na bitcoin ziko 21milion tu ikijiti hiyo 21m basi huwez ku mine new bitcoi. Labda wabadili chainblocks ..

so sasa hivi Bitcoin ni kama Antiques au zile paintings za kina Picasso au ile ya monalisa .. lakini haiwez kuja kuwa as a currency kama dollar

crypto currency wakat zinaanza watu walipiga chapuo kuwa ndio altrnative ya FIAT money ila baada ya kugundulika mapungufu mengi na scammers kuwa wengi watu wameanza kuziogopa sababu hakuna regulation ya ku control hata wewe kesho unaweza kuanzisha crypto currency yako ni swala kuweza kuipigia debe watu wakulipe dollar uwauzie digital currency wakiwa na imani itapanda thaman wauze wapige pesa
 
Back
Top Bottom