Application za kutoa mikopo wanapata wapi haki ya kuingilia faragha kwenye simu ya mteja na kuhack majina?

Application za kutoa mikopo wanapata wapi haki ya kuingilia faragha kwenye simu ya mteja na kuhack majina?

Uliipa ruhusa ndio maana

Nikupe mbinu sasa, install kwenye simu isiyo na contacts hata kidogo... thank me later
 
Wakati unajisajili uriruhusu mwenyewe waingilie phone contact zako sasa tulia dawa ikuingie
 
Sasa ukikopa pesa si unajaza application +majina na taarifa zako!kwanini sasa wasiwe na taarifa zako

Ila elewa tu kukopa harusi
Kulipa msiba

Ova
 
Hivi hawa pesa X ni wakweli maana wanasema unatoa akiba kwanza kabla ya kupewa mkopo isije kuwa ni wapigaji.
 
Kilichofanya usilipe deni lao ni kipi?
Haipo hivyo, hawa jamaa wanaenda kwenye contacts za mdaiwa wao halafu wanachagua namba na kuzitumia sms ya kuwa Wanamdai mhusika na uwasaidia kumwambia alipe deni Lao..
Hii case imenitokea nikabaki nashangaa, kuna fundi wangu alikuwa anadaiwa na hao watu wakanitumia SMS ikinitaka nimwambie jamaa alipe deni, Lao.
 
App gani?
Wanaokopesha wako mamia
Nenda Facebook wanajitangaza, chukua mkopo then pesa ikiingia block kama nilivyokuambia ili kuepuka udhalilishaji. Ila ukipata pesa walipe

.

Mkuu kwa hiyo iwapo mara ya kwanza uliwaruhusu, then pesa imeingia halafu ukuwablock access wanakuwa hawana zile contacts walizo-access mara ya kwanza?
 
Hizi ni pesa za bure kabisa kopa walipe mpaka uweze kukopa laki 9 ,fanya kama mimi block Access,kisha futa app na kuwa mkali kwa kila simu ,wanakuacha maana ni matapeli hawana kibali popote cha kukopesha
 
Hizi ni pesa za bure kabisa kopa walipe mpaka uweze kukopa laki 9 ,fanya kama mimi block Access,kisha futa app na kuwa mkali kwa kila simu ,wanakuacha maana ni matapeli hawana kibali popote cha kukopesha
Namba wanabaki nazo labda simu yako isiwe na contacts kabisa.
 
Hakuna eneo wananchi wanapigwa kama hili, mobile loan ni tatizo kubwa Tanzania na halina weledi kabisa .. Imagine mtu anakopewa pesa kiduchu riba lundo ! Wakopaji wanafedheheshwa, wanazalilishwa, wananyanyasika .. Serikali ikomeshe huu wizi, sauti zaidi zipazwe. USTAWI LOANS Mr. Finance wanaongoza kuzalilisha watanzania kupitia hii mikopo haramu.
 
Back
Top Bottom