April '09 Bomb Blasts in Dar (Mbagala) and responses

Kuna mdau nimemtuma aelekee eneo la tukio na anatoa ripoti hii:

Kuna maandamano ya wananchi ambao wanatembea kwa miguu na wamefunga barabara ya Kilwa wakielekea eneo la tukio, hali inavyoonyesha likitokea jambo baya basi wanaoweza kufa ni wengi... Serikali ilitakiwa kuzuia raia yeyote asiye na sababu maalum kwenda eneo hili.

Polisi wanawazuia raia kukaribia eneo hilo kwani wandai mabomu yaliyolipuka ni 'cha mtoto' (akimaanisha madogo) na kuna bomu moja kubwa sana likilipuka basi litaweza kuzua mengine.

Ataendelea kunifahamisha kinachoendelea nami nitajitahidi kuwafahamisha nini kimejiri. Wasiwasi wangu ni endapo litalipuka hilo wanalodai ni kubwa, najiuliza pia, hakuna zimamoto ya haraka hapo kambini?
 


Invisible

Mbona hapa unasema 'Kutakuwa na milipuko flani mnaisikia' nilikuwa nafikiria hii ni accident? au ni mambo yaliyopangwa? tuambie nini kinaendelea au kilikuwa kinaendelea mpaka yaho mabomu yamelipuka
 
kibondemaji ndio wanapakana na eneo hilo la jeshi kwa hiyo inawezekana madhara yakawa makubwa duh.
 
HApa sasa tujiwekee picha kuwa tuko katika nchi ya vita. ni nafasi yetu ya kujua yale ambayo wenzetu wa mogadishu, Palestina, Irak r.t.c wanaishije kwa kihoro kama hiki, tena kwao kiukwelii na si kama hapa.

wabongo hawako hivyo, wametangaza watu wasiende huko kama hawako na shughuli lakini huwezi amini kuna watu wanatafuta njia ya kufika huko kuona hayo mabomu yanafananaje!!!!
 
Vibaka wameanza kuiba kwenye daladala zilizosimama kwenye barabara. Wanajeshi wanwashughulikia vibaka hawa. Wanajeshi wanafanya kukabiliana na raia.

Gari na T926AES dereva wake anakula kibano kwa kukaidi amri ya wanajeshi.

Inasemekana kuna bomu ambalo linaweza kulipuka anytime limehifadhiwa kwenye ghala hilo. Zimamoto wanajitahidi kwa kushirikiana na Knight Support na Ultimate Security.

Watu watatu wameshakufa.

Kuna nyumba zimeungua na barabara imefungwa. Kuna bomu ambalo limelipuka katikati ya barabara maeneo ya Mbagala Zakhem

Samahani naandika haraka kadiri ninavyoelezwa kwenye simu
 
kwani hii ya leo inatofauti na ile ya jana?

maana jana i was so uncomfortable..unajua tena you never know hawa CHADEMA hawaaminiki

GT,

Quite the contrary, I have not so serious reasons to muse that it is CCM trying to scare the masses to vote it back in 2010!

And all who can't see the farcical nature of the above need to get their eyes checked, and are probably not too good for the gene pool.
 
Bomu liliolipuka katikati ya barabara limefikaje hapo?
 
Tatizo kubwa ni kuwa Polisi hawana vipaza sauti, wanawapiga raia kwa kuwaonea maana hawajui kinachoendelea na hawajatangaziwa. Polisi ni wengi lakini hawana vipaza sauti na kuwapiga raia ni uonevu maana hakuna mawasiliano na makelele ya wananchi yanazidi sauti ya askari bila kipaza sauti!
 
GT isije ikwa makundi ya CCM dar yameanza kukabiliana a la KYELA!!
 
Habari toka ITV, naibu waziri wa ulizi Emannuel Nchimbi anawatangazia wakazi wa mbagala wote kuhama na pia wafanyakazi walioko kwenye majengo marefu kushuka
 
Nimeongea na jamaa yangu yuko jeshini ni accident tu sio makusudi.Nafikiri watu amourly walijisahau kudispose-off yaliyoisha mda wake.Inasikitisha wananchi wanaenda sehemu ambayo tayari kuna hatari.
 
T969AAS daladala ya Mbagala - Ubungo imepata ajali na inachukuliwa na polisi. Inaelekea kuna majeruhi waliokuwa ndani ya kipanya hicho.
 
...Inasemekana kuna bomu ambalo linaweza kulipuka anytime limehifadhiwa kwenye ghala hilo. Zimamoto wanajitahidi kwa kushirikiana na Knight Support na Ultimate Security...

...jamani, 25kms sio mchezo.... ndio kusema hata wakazi wa Tandika wakae 'mkao wa kula.'

siwalaumu hao zimamoto, kama bomu 'baba lao' litalipuka wakati wowote, yanini kujitoa mhanga?

(mjeshi) JK upo nchini? hebu tangaza hali ya hatari mkoani Dar es salaam, labda wananchi watakusikiliza! (marais) wenzio muda kama huu ndipo wanapochukua majukumu!
 

Polisi hawana vipaza sauti, I cannot effin believe this!
 
Gari la polisi lenye vipaza sauti limewasili na linawatangazia wananchi kutawanyika kwani kuna mlipuko mkubwa sana unakaribia.
 

Mlioko kwenye majengo marefu mmetahadharishwa kutoka nje. Naambiwa tahadhari hii imetoka na naibu waziri - mambo ya ndani?
Mwenye hakika ya tahadhari hii atujulishe.
 
Sasa kuwa 25 km mbali hao watu watapaaa wakati barabara kuu imefungwa?? Serikali haijufunzi kukabiliana na maafa... heri ingetokea ikulu labda jamaa angeelewa..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…