Ardhi University wasitisha utaratibu wa kuweka sahihi ya mahudhurio kazini kwa watumishi wake

The Assassin

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2018
Posts
4,942
Reaction score
20,077
Chuo kikuu cha ardhi kimesitisha utaratibu wa kuweka sahihi ya mahudhurio kazini kwa watumishi wote kwa sababu zisizojulikana hadi itakapotangazwa hapo baadae.

Watumishi wameombwa kuendelea kujali muda wa kufika kazini kama walivyozoea na wakuu wa vitengo wameombwa kuendelea kufuatilia mahudhurio ya watumishi walio chini ya idara zao.

 
Kila mtu aguse palepale kwa dole gumba. Transfer inatokea.
 
Kwanini kumtafutia mwenzako balaa? Nasepa
 
''Unajua zile mashine za kuweka sahihi zimesumbua kidogo ndio maana wamesitisha huo utaratibu'' alisikika buku 7 mmoja.
 
Huyo Boss wa hapo hafai hata kidogo.
 
Ni utaratibu wa kijinga sana eti mahudhurio kuwa kidole. Muhimu no kuweka namna ya kuhakiki performance.
 
Ni utaratibu wa kijinga sana eti mahudhurio kuwa kidole. Muhimu no kuweka namna ya kuhakiki performance.
Sahihi cha kungalia na perfomance na sio maudhurio. Isitoshe katika kipindi hiki cha korona kuna kufanyakazi ukiwa nyumbani
 
Hiyo ni hatua ya kuchukua tahadhari. Utiaji sahihi kwa alama za vidole unaweza kuchangia maambukizi ya maradhi kama corona.
Hivi inashindikanaje Hapo pembeni ya hiyo Biometric mashine hamna soap dispenser au maji kwa ajili ya kusanitize?
 
Hivi inashindikanaje Hapo pembeni ya hiyo Biometric mashine hamna soap dispenser au maji kwa ajili ya kusanitize?
Sisi kazini kwetu Kuna matank ya maji ya dawa lakini bado haurusiwi kupanch kwa kidole.

Wamegawa kadi tu kwa wafanyakazi wote
 
Waweke daftari kwa muda na Kila mtu aje na kalamu yake hapo hawana afisa utumishi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…