Armageddon: Nuclear Winter - Matokeo ya vita vya nuclear na Mwisho wa mwanadamu kuishi duniani

Armageddon: Nuclear Winter - Matokeo ya vita vya nuclear na Mwisho wa mwanadamu kuishi duniani

Venus Star

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2018
Posts
26,519
Reaction score
78,311

Utangulizi​

Za leo wana JF.

Kama kawaida yangu katika kuelisha watanzania ili waweze kuijua kweli.
Matishio haya na uvumbuzi wa hizi silaha za maangamizi hayana nia njema katika dunia yetu hii.
Leo nitaongelea kuhusu Mabomu ya nuclear na matokeo ya Neclear Winter na mwisho wa binadamu kuishi duniani.

Armageddon ni concept iliyo andikwa kwenye biblia katika kitabu cha ufunuo 16:16. Ukitaka kuelewa zaidi kuhusu concept hii unatakiwa uisome sura yote ya 16. Kwa ufupi ni kwamba sehemu hiyo watakutana wafalme wa dunia na vita kuu ya dunia itapigwa. Siku hiyo inaitwa Siku ya Mungu (Day of God). Na itakuwa ndio mwisho wa dunia, maana watu wengi sana watakufa.

Concept hiyo ninaiweka sasa katika hali hii ya sasa dunia ikishuhudia nchi kumiliki silaha za maangamizi zaidi ya mabomu 13,000. Huku vita vya kuchokozana hapa na pale zikiendelea bila sababu kubwa za msingi. Wakubwa kutishiana na kuonesha ubabe wao wa silaha za maangamizi. Je, tunaelekewa wapi? hatuwezi kuifanya dunia yetu ikawa ya amani?

Mathara ya Mlipuko wa Mabomu ya Nuclear​

Dunia tunayoishi kwa sasa imeshuhudia mambo mawili ya Nuclear yaliyoangushwa huko Japan
Hiroshima liliangushwa bomu lenye uwezo wa 15 kilotons of TNT
Nagasaki liliangushwa lenye uwezo wa 20 kilotons of TNT

Haya kwa pamoja yapo na 35 kilotons of TNT yanauwezo wa kuzalisha nishati 1.5 x 10^14 joules

Kutokana na kuendelea kwa teknolojia nchi zinamilki mabom ya nuclear yenye uwezo kuanzia 100 kilotons of TNT na zaidi.
Uchambuzi wa kisomi unaeleza kuwa inahitajika mabomu ya nuclear yenye uwezo wa 10,000 kilotons kwa pamoja kuleta maangamizi ya dunia na kusababisha nuclear winter

Kwa mujibu wa hali ya sasa ni mambomu 100 tu yenye uwezo wa 100 kilotons yanaweza kuzalisha 10,000 kilotons

Nuclear winter ni nini?​

Nuclear winter ni hali ya hewa ya kupungua kwa joto duniani inayotokana na vita vya nyuklia. Iwapo mabomu ya nyuklia mengi yatalipuliwa, hasa kwenye maeneo yenye majiji au misitu mikubwa, milipuko hiyo inatoa moshi, majivu, na vumbi nyingi sana angani. Uchafu huu ukizuia mwanga wa jua kufikia uso wa dunia kwa muda mrefu, labda kwa miezi au hata miaka kadhaa unasababisha baridi kwenye uso wa dunia.

Baridi linakuwa kali, mimea inashindwa kupata mwanga wa jua, maji kukosekana, barafu kuwepo kila sehemu, hewa kuwa ya ukaa na mambo mengi kutokea. Hili jambo likitokea ndani ya mwezi mmoja biandamu wote wanaweza wasiwepo kwenye uso wa dunia.

Je, Silaha za Nuclear ni maandalizi ya maangamizi ya dunia​

Mabomu ya nuclear kwa sasa ni zaidi ya 13,000 na kuweza kusababisha Nuclear Winter ni mabomu 100 tu. Mlipuko wa mabomu hauna madhara makubwa ya papo kwa hapo. Lakini baada ya hapo vumbi kubwa na moshi utakuwa angani.

Switzerland ndiyo iliyojiandaa na kukabiliana na Nuclear Winter japo kwa Mwezi mmoja​

Serikali ya Switzerland ilipisha utaratibu wa nchi kuchimba mahandaki ambayo yatasaidia watu kujificha humo baada ya jambo hili la vita vya nuclear kutotea.
Kuna mambo ya msingi makuu manne ambayo bado kila nchi inahangaika kuyatatua ambayo yatatokea baada ya nuclear winter:
  1. Kujikinga na baridi kuu
  2. Upatikanaji wa Hewa safi
  3. Upatikanaji wa maji safi na salama
  4. Upatikanaji wa Chakula
Nitaendelea kueleza... Karibuni tujadili...
 

Kipi kitatokea kama Marekani na Russia wakitumia Mabom ya nuclear kila mmoja akimtupia mwenzake Mabomu 200​


Mlipuko wa nyuklia utasababisha moto mkubwa wa misitu, majengo, na mafuta, na moshi mzito utapanda hadi angani, kufika kwenye sehemu za juu za anga (stratosphere). Hii itasababisha kutanda kwa wingu zito la moshi na majivu duniani kote.

Wingu hili litaweza kuzuia mwanga wa jua kufika kwenye uso wa dunia, na hivyo kushusha joto la dunia kwa kiwango kikubwa. Hii itasababisha hali ya “majira ya baridi ya nyuklia,” ambapo dunia inaweza kuwa na majira ya baridi yenye baridi kali hata katika maeneo ambayo kawaida huwa na hali ya joto.

Inakadiriwa kuwa majira ya baridi ya nyuklia yanaweza kudumu kwa miaka kadhaa, ambapo mamilioni ya tani za moshi zitaendelea kutanda angani na kuzuia mwanga wa jua kuifikia dunia.

Kutokuwa na mwanga wa jua wa kutosha na kupungua kwa joto duniani kutaleta athari kubwa kwa mimea, upatikanaji wa chakula, na ekolojia kwa ujumla. Maeneo yanayolima chakula yatashindwa kutoa mazao ya kutosha, na hii inaweza kusababisha njaa kubwa duniani.

Vita vya nyuklia vya kiwango hiki si tu vinaweza kuua watu mamilioni moja kwa moja, bali vinaweza kubadili kabisa mfumo wa ikolojia duniani na kusababisha kutoweka kwa maisha kama tunavyoyajua.
 
Russia na US ni tishio zaidi ktk kuwa na hizi silaha za Nuclear.
 
Vita kuu ya Tatu ndio hii mnayoiona kwenye Media na hakuna nyingine.

Ni Vita ya Media.
 
Walipue tu sababu ukichunguza kwa umakini utagundua maisha hayana maana yoyote...ni kama vile kuna wajanja walituumba alafu wakatutekeleza
Hakuna kitu kama hiko! Mawazo yako tu.
 
Walipue tu sababu ukichunguza kwa umakini utagundua maisha hayana maana yoyote...ni kama vile kuna wajanja walituumba alafu wakatutekeleza
Walitukabidhi kwa chama tawala babu, mpaka siku ya qiama tunao tu.
 
Miaka 10 ya nuclear Winter kama mabomu yote ya Nuclear yaliyopo tuniani yakilipuliwa.
 
Back
Top Bottom