Arudisheje hisia kwa mumewe? ...Msaada tafadhali


bacha nafikiri inategemea na situation maana kuna wakati mume anakuwa si mfariji tena bali anageuka kuwa mvunja amani, mvunja faraja yaani anakuwa jitu badala ya mtu. Najaribu kufikiria mume anayetelekeza familia anakimbilia kwa kimada, miezi na miaka akikumbushiwa ya familia yake ni matuc , kejeli na vipigo miaka na miaka hadi unakata tamaa ya kuwa atarejea tena,,,,,,,,,,,,,,,,,wanawake wengi ni wazito kudai talaka katika situations kama hizi wengi wetu tumekolezwa na mafundisho ya vumilia, ndoa ndivyo zilivyo na ukishindwa sana basi OKOKA na umkbidhi situation nzima MUNGU wako.

Sasa ukiangalia kizazi chetu cha sasa ambako MUNGU anawekwa mbali na maadili ya dini yanazidi kumomonyoka matokeo yake ndo haya, option ya OKOKA na umkabidhi MUNGU matatizo yako imekuwa replaced na .........TOKA NJE NAWE UFURAHIE MAISHA KATIKA MWANGA BORA! Nadhani ndicho alichokifanya dada huyu.

So pole mpenzi wangu kwa mshtuko huu.
 
<br />
<br />

Maisha ya maigizo haya yanatesa wengi (jamii itanionaje....kiruka njia)

Sasa mamii, kama hisia zimehama kasheshe mpauko ndo hiyo....

Aaaahh ....
 
Khaaa Maisha Katika Mwanga Bora Zaidi....yeomii!
 
Hahaaaaaaa bht acha utani hili litopic linahuzunisha sana, lakini huyo jamaa/mshefa naona kama vile ni wale watu wabinafsi fulani hapendi kuona ndoa ya huyo dada imesimama labda kwa sababu kwake kuna matatizo au kuna kitu anafaidi kwake so anaona ngumu kumpoteza aendelee kujifaidia sema siku tu mwenzie akipigwa chali anachapa mwendo.

 


unajua bht, kosa lilishafanyika toka mwanzo.......................
huyu bibie alifanya kosa sana kwenda nje kutafuta hiyo tunayosema ''faraja''
hainiingii akilini anaposema kuwa hivi sasa amemzimia mazima huyo ''mshefa''...........
sasa huyu bibie hata akirudi kwa mumewe kweli atadiriki kusema kuwa anampenda kweli?

Au sasa itakuwa ni kuishi bora liende, kwakuwa tayari meshajifunga hilo nyororo la ndoa?

makosa yaaina yote kwenye ndoa yaweza fanyika na yakapata misamaha,
lakini hili la kutembea nje ya ndoa......lol....limepitiliza mpaka basi.......!
 

kuna baadhi ya wanawake cwaelewi kabisa, kwani wakitaka ku cheat c wa cheat 2 bila kuelezea matatizo ya waume zao kwa hao washefa wao?...mxsiii...huyu ndugu yako anampenda sana mshefa hajaamua kuachana nae, mbona ni cmple sana, unakata mawacliano ASAP....
 

Duh hii post kali..yaani hata Judge anaweza kuchanganyikiwa kutoa hukumu..

Binafsi..mara nyingi nashauri watu kuangalia mbele na wala sio nyuma. Tunaangalia nyuma tu kujua tulijikwaaje ili tusirudie kujikwaa tena.

Sasa hapa mume ameshapona kujikwaa kwake. Mke ameshagundua kujikwaa na pia anaona machungu ya kujikwaa (kujijua) lakini mke ataki kula dawa ili apone machungu ya kujikwaa.. Mke anaona dawa ya krolowkini ni chungu...Sasa kama unajijua unakidonda.. unajua madhara ya kidonda na unaogopa kula dawa, hutaweza pona kamwe...

Ushauri mkubwa kwa dada ni kuwa akae chini angalie miaka ya mbele kwa kuchukua scenario hizo mbili..yaani tabia ya sasa ya mume na usemi wa zimwi likujualo ... na pia angalie mapenzi ya huyo hawara akijua yanaweza chuja siku yeyote..halafu aamue kuendelea na ndoa au kupiga chini..

Dada ajue ndoa hailazimishwi na mapenzi ya kinafiki ni sumu. Dada ajue alishachukua uamuzi wa kukaa na mume kwa furaha na machungu... Lakini anatakiwa kujiangalia na kuamua kama yuko tayali kuchukua maamuzi mengine ya kumwacha mume kwa furaha ya baadaye au machungu ya baadaye.. Maamuzi yako mikononi mwake na wa sio mikononi mwa mume wake au hawara yake...
 

Ah chauro huyu mume ni one in a million na akimchezea atampoteza kimoja! Ingawa naye alimtesa vilivyo lakini nadhani ameligundua kosa lake na ameamua kutengeneza sasa baki iko kwa bidada................walah ngekuwa mie na hivi mume ashajua ningeongozana naye kwenda kumpiga kibuti huyo Mshefa LOL..................................
 
<br />
<br />

Chauro, basi bora huyo mshefa angekuwa singo useme hata labda kuna matumaini....lakini mshefa was looong taken

Sasa dada hapa anaintertain nini? Ngono tu basi.

Mshefa nae sasa ndo nini kutaka kote kote lakini?

Mi ndo maana nasema ni vema tu wajue huo msiba uliisha, wasubiri mwingine...
 


kiukweli MJ1, mimi siyaoni hayo mnayoyaita maisha katika mwanga bora huko nje......?
zaidi ni temporal relief tu ndo inayokudanganya, amabayo kimsingi naweza kusema kuwa unazidi kujifukia shimo tu,
labda kidogo ningekuelewa kama tu huyo mshefa angekuwa single, yumkini unaweza predict kuwa lolote laweza tokea mbele ya safari!

Tatizo siku hizi wanandoa wengi tumejawa sana na maisha ya kukomoana na kulipana visasi!kila upande unaona unaweza kuchukua maamuzi magumu.......

haya hata kama ukisema unaenda kupata faraja huko nje, je ni faraja gani hiyo isiyokuwa na uhuru?
kwani nategemea appointments nyingi hapo zitakuwa za vichochoroni tu, je hiyo ndo faraja?
 

kama na mpaka uzeeni tunadanganywa bac kazi ipo....hakuna cha kudanganywa wala nn huyu dada anampenda sana mshefa na hayupo tayari kumwacha, kuja kumwelezea MJ1 ni kama anampa taarifa tu ya kinachoendelea coz na mr wake kashajua so cku ya cku yakibumburuka bac wakina MJ1 wawe ameshawataarifu....
 
MJI acha utani ...mwe mume kasamehe na bado unambeba kwenda kupiga kibuti sipati picha.........nafikiri dada bado anampenda mumewe asingeweza kujisikia vibaya kama hana hisia zozote kwa mumewe ushauri ajaribu kuwa karibu sana na mume muda utabadili hisia zake.


 


sasa hapa bht naona tupo pamoja...........
nadhani hiyo faraja ambayo anaipata hapo huyo dada ni uhakika wa ngono tu,
tena yumkini waweza kuta ni ngono ile ''hardcore sex'' ambayo yawezekana mumewe alikuwa hampi hiyo.........

ngoja niwaambie nyie akina dada, MJ1, CHAURO , bht na wengineo....................

''wanaume wengi huwa tunapenda sana pale penye mteremko hasa katika kukata kiu ya kingono,
huyo mshefa keshatambua kuwa huyo dada ana kiu ya ngono, na once akipata hiyo kitu anakuwa ametulia kwatu....
sidhani kabisa katika hiyo faraja kuna mambo mengine mazito ya kimaisha ambayo wanatimiziana ukijali kwanza muda ni mchache wa kuonana.......
sasa kwa style hii huyo mshefa anaona amepata penye unafuu wa kuponea hiyo kiu yake, kwa wakati wowote na isitoshe bila gharama........''
 
ulifanya kosa, ulilikubali na ukaomba msamaha pia ukaahidi kuwa hautorudia tena, sasa inakuwaje unasema eti unashindwa kurudisha hisia kwa mumeo?, uliposema samahan kwa mumeo si inamaana uliamua kumpokea mumeo na kuendelea na ndoa yako?, hapo kigumu kipo wapi?. Acha kuchezea ndoa yako, usiendekeze matatizo, tuliza akili yako achana na huyo mshefa kwani yupo kukuharibia ndoa yako. Kuwa na msimamo acha unafiki,unaomba msamaha ili hali haumaanishi?. Tulia,tunza,linda,heshimu,ipende,ithamini ndoa yako ili uweze kuifurahia na ipate kubarikiwa na MUNGU. Ndoa ni sehemu ya maisha so matatizo hayakwepeki lililo muhimu ni kutumia busara na hekima ktk kuyatatua, pia usitumie mwili kuyatatua bali utumie akili.
 
<br />
<br />
umesema jambo la maana sana. Tabia yetu kwenda kujieleza eleza kwa wanaume wengine mataizo ya mahusiano yetu, mara nyingi lazima mtu aangukie humo.

Mae, huyu dada anageresha tu, ni msanii na hajataka kumuacha mshefa.

Sijaona uzito wa hiyo blackmailling technique yq mshefa.
 
Nyamayao sidhani kama iko sawa ukisema binti hataki kumuacha mshefa kumbuka binti alitengeneza mapenzi anajaribu kila awezalo lakini mshefa anakuja na blackmail zake labda sababu anajua dada anampenda au ndio ule ubinafsi wa baadhi ya watu kama navosema .........halafu waeza kuta mshefa ni mtu ambaye labda mazingira yanawafanya kuwa karibu.


 

wotw wanao cheat wana cheat vichochoroni, iwe ni mwanamke/mwanaume....na kama mnaona hakuna uhuru bac wanaume mngetuonyesha mifano ya kutulia na wake zenu yote haya yacngetokea, mie cmlaumu huyu dada hata kidogo kwa waliopitia hizo kashkash za waume 2najua inavyoumiza, sasa inategemea na vipi mtu anavyoweza kupambana na hiyo hali,kwa mdada yeye akaona atafute wa kumpooza, ishu yangu na huyu dada ni kwamba haitaji kuomba ushauri wa kuachana na mshefa coz ni kitu cha yeye mwenyewe kuamua, acpoamua yeye hakuna anaeweza kumuamulia.
 
<br />
<br />

Bacha kwenye kosa nakubaliana na wewe mia ya mia.

Sasa hapa uzuri wote walichiti kila mtu kwa sababu zake (justifications )

Na wakasameheana (naona kiusanii), sasa ni mke tu ndo hapaswi kuchiti? Maana mume ndo alianza tena kwa miaka mke kavumilia mwisho akaamua na yy akayaone maisha ktk mwanga bora zaidi.... (lol nacheka lakini kwa masikitiko)
 

yap....hataki na hana nia ya kumwacha....hivi mshefa atakufanyia lipi wewe uharibu ndoa yako yake ikichanua? mdada bado anampenda mshefa ndio mana hajaamua bado kumwacha.
 
Pole zake, ila anatakiwa aangalie sana mana unaweza kuta mume anasema katulia kumbe huko alikokuwa kahamishia makazi kapewa kibuti hivyo anavuta pumzi kwanza then aendelee na mambo yake , unaweza poteza mshefa wako bure na huku kwa mume akarudia tabia zake zile zile, hivyo bidada kuwa makini sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…