Arusha: Aliyekuwa Mgombea wa Ujumbe katika Serikali ya Mtaa akutwa kwake akiwa amefariki huku akiwa na alama kukatwa shingoni

Arusha: Aliyekuwa Mgombea wa Ujumbe katika Serikali ya Mtaa akutwa kwake akiwa amefariki huku akiwa na alama kukatwa shingoni

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Aliyekuwa Mgombea katika nafasi ya Ujumbe wa Serikali ya Mtaa ya eneo la Mnara wa Voda, kupitia CHADEMA kabla ya Chama hicho hakijajitoa kushiriki, Sirili Homary amekutwa amefariki dunia nyumbani kwake huku akidaiwa kukatwa na kitu chenye ncha kali shingoni

9A4EC4CA-E0F8-42EF-AC48-9B49278E3740.jpeg

Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jonathan Shana, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kifo hicho kina muda wa siku tatu tangu kimetokea.

Amesema Marehemu Homary amekutwa ndani ya nyumbani kwake katika eneo la Mnara wa Voda, huku funguo ikiwa ndani akiwa amefariki Dunia.

“Bado tunachunguza na tutatoa taarifa maana mtu amekutwa ndani na funguo ikiwa ndani inawezekana pia amejidhuru mwenyewe kutokana na labda msongo wa mawazo” amesema Shana.

Aidha amesema wako wanasiasa wanaleta uchochezi juu la kifo hicho na ameahidi wakiendelea atawachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

“Naomba watupe muda vyombo rasmi vya uchunguzi vifanye kazi yake, jambo kama hilo lina taratibu linapotokea tunachunguza kwa kuhusisha vyombo vinavyoaminiwa na wananchi na tutatoa taarifa kupitia Vyombo vya Habari”amesema Shana.

Naye Mbunge wa Arusha, Godibless Lema akihojiwa na Nipashe, amesema jambo hilo ni la kikatili na la kuhuzunisha na kwamba amezungumza na Kamanda wa Polisi mkoani humo ambaye amemuambia watu kadhaa wanashikiliwa kuhojiwa juu ya tukio hilo.

Amesema CHADEMA mkoani Arusha wameunda Kamati Maalum kufuatilia Mauaji hayo maana yana utata kwani Homary ni Kada Maarufu na mwaminifu wa Chama hicho.

“Sio kawaida kwa polisi kukaa kimya hapa kuna utata, RPC alipaswa aite kikao na wanahabari na waulize majibu na ajibu sasa ukimya huu unatushangaza maana jamii itapata picha gani?”amehoji Lema.
 
Poleni sana kwa wafiwa

Jeshi la polisi lichunguze hili tukio

Watanzania tunapendana
 
Siasa hizi, akili inaweza kuwa twisted kufikiria kitu flani hadi ukaona ni halisi tofauti na ukweli wenyewe

anyway apumzike anapostahili
 
vijana wadogo mnatafuta umaarufu kupitia siasa kama vile hamjui kua siasa ni.mchezo mchafu! hivi hakuna issue nyingine za kufanya??
 
Aliyekuwa Mgombea katika nafasi ya Ujumbe wa Serikali ya Mtaa ya eneo la Mnara wa Voda, kupitia CHADEMA kabla ya Chama hicho hakijajitoa kushiriki, Sirili Homary amekutwa amefariki dunia nyumbani kwake huku akidaiwa kukatwa na kitu chenye ncha kali shingoni


Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jonathan Shana, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kifo hicho kina muda wa siku tatu tangu kimetokea.

Amesema Marehemu Homary amekutwa ndani ya nyumbani kwake katika eneo la Mnara wa Voda, huku funguo ikiwa ndani akiwa amefariki Dunia.

“Bado tunachunguza na tutatoa taarifa maana mtu amekutwa ndani na funguo ikiwa ndani inawezekana pia amejidhuru mwenyewe kutokana na labda msongo wa mawazo” amesema Shana.

Aidha amesema wako wanasiasa wanaleta uchochezi juu la kifo hicho na ameahidi wakiendelea atawachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

“Naomba watupe muda vyombo rasmi vya uchunguzi vifanye kazi yake, jambo kama hilo lina taratibu linapotokea tunachunguza kwa kuhusisha vyombo vinavyoaminiwa na wananchi na tutatoa taarifa kupitia Vyombo vya Habari”amesema Shana.

Naye Mbunge wa Arusha, Godibless Lema akihojiwa na Nipashe, amesema jambo hilo ni la kikatili na la kuhuzunisha na kwamba amezungumza na Kamanda wa Polisi mkoani humo ambaye amemuambia watu kadhaa wanashikiliwa kuhojiwa juu ya tukio hilo.

Amesema CHADEMA mkoani Arusha wameunda Kamati Maalum kufuatilia Mauaji hayo maana yana utata kwani Homary ni Kada Maarufu na mwaminifu wa Chama hicho.

“Sio kawaida kwa polisi kukaa kimya hapa kuna utata, RPC alipaswa aite kikao na wanahabari na waulize majibu na ajibu sasa ukimya huu unatushangaza maana jamii itapata picha gani?”amehoji Lema.
Naona CDM mmeanza yenu. Tunawafahamu sana.
 
Back
Top Bottom