Arusha: Daladala zagoma tena Arusha, leo Agosti 14, 2023

Arusha: Daladala zagoma tena Arusha, leo Agosti 14, 2023

Watu wa bajaji ilitakiwa wawe wanatoa abiria uko ndani na kuwasogeza stendi za daladala au ziwe zinapaki kwa ajili ya kukodishwa sasa kwa sasa hawa bajaji wamekuwa kama daladala, nakumbuka huko nyuma mgomo kama huu ulishawai tokea mbeya ufumbuzi wa tatizo ulipatikana nashauri watu wa arusha wajifunze huko mbeya

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app

Mbeya walisitisha usajili wa bajaji baada ya kuona zimekuwa kelo...., Kinachofanyika Sasa bajaji ikichoka unauza usajili.

Ilo swala Ni gumu na limekaa kimaslahi kwa Mbeya ili sumbua kwakuwa miongo mwa viongozi wa juu wa mkoa walikuwa wanamiliki/wanamiliki Hadi sasa bajaji zaidi ya 30 Kila mmoja Sasa hapo unategemia watakubali kuondoa bajaji barabarani mkuu?
 
Ndugu wana Arusha na watanzania wote kwa ujumla mkuu wa mkoa wa Arusha, mkurugenzi na mamlaka husika za usafiri walipaswa wawe waneshatumbuliwa mpaka sasa kutokana kushindwa kutatua mgomo uliopo wa magari ya usafirishaji ulioleta adha kwa wananchi mara ya pili sasa ndani ya muda mfupi.

Hali ni mbaya na hatari kwa aina ya usafiri unaotumika sasa,tena kwa watoto wadogo wa shule na wananchi kwa ujumla

Wawe wamejiuzulu mpaka sasa au mama yetu Samia wafukuzwe wahusika wote kabla siku hizi ya leo haijaisha
 
Kwa mara nyingine tena daladala zote zinazoenda katikati ya jiji. zimegoma kufanya biashara ikiwa ni mgomo wa pili ndani ya kipindi kisichozidi mwezi na nusu.

Mussa njuga ambae ni katibu wa daladala amesema mgomo huo hauna kikomo hadi wapate kauli kutoka kwa waziri Mkuu au Makamu wa Rais.

Sababu za mgomo huo inatajwa ni Serikali kushindwa kufikia muafaka kati yao na Bajaji kwa kuruhusu Bajaji kufanya kazi kama daladala ndani ya Jiji la Arusha

Uongozi huo umeeleza kuwa mbali na kuandika barua kwa mkuu wa mkoa kuikumbusha Serikali kutekeleza maadhimio ya vikao vya kamati ya suluhu lakini barua hiyo haikupatiwa majibu jambo ambalo limewakatisha tamaa madereva na viongozi wao.

Aidha viongozi hao wanataka kauli kutoka kwa waziri Mkuu Au makamu wa Rais kwa madai kuwa viongozi wa Arusha wameshindwa kutekeleza madai yao.

Zaidi ya Bajaji 2500 zinafanya kazi ndani ya jiji la Arusha kama daladala.



=============

LATRA YASEMA MGOMO UKIENDELEA WATAFUTA LESENI ZA DALADALA
Joseph Michael, Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Mkoa wa Manyara anazungumzia kinachoendelea:

Tunasikitika kitendo cha Daladala kufanya mgomo kwa kuwa tayari Serikali inafanyia kazi suala hilo chini ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye alishaunda Kamati inayohusisha watu wa Bodaboda, Daladala, Bajaj, Barabara na taasisi za Serikali zinazohusisha masuala ya Usafirishaji.

Kamati iliundwa maalum kufuatilia suala hilo na ilishamaliza kazi yake, kilichokuwa kinafuata ni kwenda kwenye hatua ya pili ya utekelezaji, kinachoshangaza wamefanya mgomo wakati wao watu wa Daladala wana wawakilishi wao kwenye Kamati.

Tunashauri warejee kutoa huduma na Kamati iendelee kutoa mchakatoa, mgomo una madhara, waliendelea hivyo Sheria inaeleza kuwa tutafuta leseni.

Nimeenda kuzungumza nao watu wa Daladala pale Kilombero Kituoni, inavyoonekana Wanachama wa Daladala hawawaheshimu viongozi wao wanaowawakilisha, kwenye umoja wao huo kuna shida.

Pia tumeruhusu Coaster za Arusha – Moshi zianze kufanya kazi wakati huu wa mgomo huku tukiwasisitiza watu wa Daladala wasitishe mgomo, wafuate Sheria na Taratibu kwa kuwa wakiendelea hivyo tutafuta leseni zao, tupo ‘serious katika hilo.
Wajifunze tu ya moahi ,kwa sasa amna dalala zinazoenda kcmc mambo ya bajaji
 
Ila nawasifia watu wa daladala wa Arusha wana msimamo siku nzima wamekaza.
Ila waache uduanzi bodaboda nao wanatafuta riziki waende kula na kuhonga wapunguze genye.
 
Hapa ndipo akili za madereva hasa wa daladala huwa nashindwa kuzielewa.Utawakataaje watu wanaotafuta riziki kama wewe tu?Hizi siyo zama za ujima kwamba usafiri uwe wa aina moja tu.Watu wana haraka zao na wanataka privacy.Daladala hujaza abiria wengi na kuwabananisha.Watu wengi hawapendi.Ni uchumi mfinyu tu.
 
Tatizo la daladala za Arusha hawaoni mbele zaidi kwamba route fupi lazima zitakufa kama ambavyo kwenye miji mingine imekuwa especially dar es salaam.

Zamani tulikuwa na route ya mwenge - africana lakini kulingana na ufupi wa hiyo route naona imekufa yenyewe automatically sababu mtu anaona heri apande bajaj ya kuchangia anafika haraka sababu route ni fupi na nauli ni kidogo anaongeza analipa 1000 tu.

Arusha mji umeanza kupanuka daladala lazima waangalie route za mbali ila hawawezi kulazimisha route fupi ambazo bajaj anaenda fasta tu kuliko kukaa stendi kusubiri gari ijae na muanze kusimama kila kituo.
 
Bajaj na bodaboda,watakua wanaombea mgomo uendelee.Watakua wamepiga hela sana leo.
 
Bahati za wenzao wasilalie mlango wazi, riziki kugawana.
 
Huo ni unyimi na roho mbaya waache watu watafute pesa mbona Morogoro bajaji na daladala wanapiga ruti moja na husikii kulalamika

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Vita Ya Viongozi Wa Serikali wamiliki wa Bajaj na Viongozi Wa Serikali wamiliki wa Daladala.
 
Wakumbuke kuwa kabla ya daladala kulikuwepo na coaster.... coaster hazikuzuia daladala kufanya kazi , zilijiongeza na kuanza safari ndefu badala ya kuung'ang'ania kufanya safari fupi fupi hapo mjini. Kama daladala hawawezi kuwa na adabu kuruhusu biashara huria wakauze gari zao wanunue bajaji... Pumbavu kabisa.

Sent from my Infinix X6517 using JamiiForums mobile app
Wanaoteseka Wanafunzi ambao ndo wengi kuliko wazazi.
 
Kwa mara nyingine tena daladala zote zinazoenda katikati ya jiji. zimegoma kufanya biashara ikiwa ni mgomo wa pili ndani ya kipindi kisichozidi mwezi na nusu.

Mussa njuga ambae ni katibu wa daladala amesema mgomo huo hauna kikomo hadi wapate kauli kutoka kwa waziri Mkuu au Makamu wa Rais.

Sababu za mgomo huo inatajwa ni Serikali kushindwa kufikia muafaka kati yao na Bajaji kwa kuruhusu Bajaji kufanya kazi kama daladala ndani ya Jiji la Arusha

Uongozi huo umeeleza kuwa mbali na kuandika barua kwa mkuu wa mkoa kuikumbusha Serikali kutekeleza maadhimio ya vikao vya kamati ya suluhu lakini barua hiyo haikupatiwa majibu jambo ambalo limewakatisha tamaa madereva na viongozi wao.

Aidha viongozi hao wanataka kauli kutoka kwa waziri Mkuu Au makamu wa Rais kwa madai kuwa viongozi wa Arusha wameshindwa kutekeleza madai yao.

Zaidi ya Bajaji 2500 zinafanya kazi ndani ya jiji la Arusha kama daladala.



=============

LATRA YASEMA MGOMO UKIENDELEA WATAFUTA LESENI ZA DALADALA
Joseph Michael, Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Mkoa wa Manyara anazungumzia kinachoendelea:

Tunasikitika kitendo cha Daladala kufanya mgomo kwa kuwa tayari Serikali inafanyia kazi suala hilo chini ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye alishaunda Kamati inayohusisha watu wa Bodaboda, Daladala, Bajaj, Barabara na taasisi za Serikali zinazohusisha masuala ya Usafirishaji.

Kamati iliundwa maalum kufuatilia suala hilo na ilishamaliza kazi yake, kilichokuwa kinafuata ni kwenda kwenye hatua ya pili ya utekelezaji, kinachoshangaza wamefanya mgomo wakati wao watu wa Daladala wana wawakilishi wao kwenye Kamati.

Tunashauri warejee kutoa huduma na Kamati iendelee kutoa mchakatoa, mgomo una madhara, waliendelea hivyo Sheria inaeleza kuwa tutafuta leseni.

Nimeenda kuzungumza nao watu wa Daladala pale Kilombero Kituoni, inavyoonekana Wanachama wa Daladala hawawaheshimu viongozi wao wanaowawakilisha, kwenye umoja wao huo kuna shida.

Pia tumeruhusu Coaster za Arusha – Moshi zianze kufanya kazi wakati huu wa mgomo huku tukiwasisitiza watu wa Daladala wasitishe mgomo, wafuate Sheria na Taratibu kwa kuwa wakiendelea hivyo tutafuta leseni zao, tupo ‘serious katika hilo.
Msitafutane uchawi bure huo mji ni mdogo hauwezi kuhimili dalala vibajaji na pikipiki lazima mmoja atolewe knockout.

hapo..remind you daladala ni vile vipanya..
Bado bolt, farasi , uber hawajagonga hodi.

Muiheshimu dar nyie watu wa chuga

Arusha bado sana ila makelel ndio mengi.
 
Back
Top Bottom