Arusha: Mwanamke aliyeenda kutafuta pochi yake mtoni, mwili wake wakutwa kando ya mto

Arusha: Mwanamke aliyeenda kutafuta pochi yake mtoni, mwili wake wakutwa kando ya mto

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Mwanamke mmoja ambae bado hajajulikana ameuliwa na watu wasiojulikana na kutupwa mto Themi akiwa bila nguo.

Tukio hilo ambalo limezua taharuki miongoni mwa watu limetokea kata ya Sinoni katika mtaa wa onjavutian.

Mwenyekiti wa mtaa wa onjavutian ambapo tukio hilo limetokea Lesioni Joseph amethibitisha kutokea kwa tukio hilo leo jumanne na kueleza kuwa alifika mtoni baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi na kwenda kuona maiti ya mwanamke huyo, na kupiga simu polisi ambapo polisi wamekuja na kuchukua mwili huo.

=============
Updates...

Mwenyekiti wa Onjavutian katika Kata ya Sinoni, Lesioni Joseph anaelezea kilichotokea:

Hakuna taarifa kama ni kweli ameuawa au amekufa kwa sababu zingine, baada ya kupata taarifa za mwili kuonekana kando ya mto niliita Askari na baada ya uchunguzi wa awali wakabaini kuwa mwili haukuguswa kwa maana ya kushambuliwa.

Marehemu anaitwa Suzan au mama Dorcas, taarifa za uchunguzi wa awali zinaonesha kuwa aliporejea nyumbani jana usiku (Mei 15, 2023) akamwambia dada wa jirani kuwa amepoteza pochi yake ambayo ilikuwa na Tsh. 25,000.

Hakurejea nyumbani tangu alipoondoka, Askari walipokuja na kufanya uchunguzi wamesema inawezekana alidondoka au aliumia akashindwa kutoka kwenye maji.

Mwili wake umekutwa ukiwa hauna nguo ya chini, alikuwa amesaliwa na nguo ya juu tu.. Umri wake ni kati ya miaka 40 hadi 45.
 
....baada ya kupata taarifa Mwenyekiti wa mtaa alienda kuona maiti na kuwapigia police ambao walifika na kuuchukua mwili!!!,nikisema nataka kuvunja hili jeshi la police wengi hawanielewi, kitendo cha Mwenyekiti kuingia kwenye crime scene ni makosa makubwa mno,stay stay away from crime scene utaharibu vielelezo vya ushahidi, pale walitakiwa waende foresinc cops sio hao police wa defenda!!,ushahidi umepotea, maana hakukufanyika ukusanyaji wa vielelezo kama foot prints etc etc,hii nayo ni cold case kama ya yule msichana mwingine hapo hapo Arusha, yule mwanachuo kimyaaa, royal family it walk away with murder
 
....baada ya kupata taarifa Mwenyekiti wa mtaa alienda kuona maiti na kuwapigia police ambao walifika na kuuchukua mwili!!!,nikisema nataka kuvunja hili jeshi la police wengi hawanielewi, kitendo cha Mwenyekiti kuingia kwenye crime scene ni makosa makubwa mno,stay stay away from crime scene utaharibu vielelezo vya ushahidi, pale walitakiwa waende foresinc cops sio hao police wa defenda!!,ushahidi umepotea, maana hakukufanyika ukusanyaji wa vielelezo kama foot prints etc etc,hii nayo ni cold case kama ya yule msichana mwingine hapo hapo Arusha, yule mwanachuo kimyaaa, royal family it walk away with murder
HIVI TUNA HIKI KITENGO TANZANIA? AU HADI TUOMBE MSAADA WA MABEBERU? CRIME ZOZOTE ZIKITOKEA UASIKIA POLISI WAMEONDOKA NA MWILI
 
....baada ya kupata taarifa Mwenyekiti wa mtaa alienda kuona maiti na kuwapigia police ambao walifika na kuuchukua mwili!!!,nikisema nataka kuvunja hili jeshi la police wengi hawanielewi, kitendo cha Mwenyekiti kuingia kwenye crime scene ni makosa makubwa mno,stay stay away from crime scene utaharibu vielelezo vya ushahidi, pale walitakiwa waende foresinc cops sio hao police wa defenda!!,ushahidi umepotea, maana hakukufanyika ukusanyaji wa vielelezo kama foot prints etc etc,hii nayo ni cold case kama ya yule msichana mwingine hapo hapo Arusha, yule mwanachuo kimyaaa, royal family it walk away with murder
Hizi series unazoangaliaga Netflix usidhani pia ziko bongo. Siyo kila kitu tuwaige mabeberu.
 
Hizi series unazoangaliaga Netflix usidhani pia ziko bongo. Siyo kila kitu tuwaige mabeberu.
Pumbavu ila kila kukicha unawaza kwenda kwa mabeberu, kuna refugee criss pale Sudan, upo kimya na unasubiriq mabeberu waje kusaidia, royal families wanafia huko huko kwa mabeberu
 
Arusha ni hatari sana na utumiaji wa Bangi uko juu mnooo ukiongeza na Malezi ya Kimasai hasira kama Ngiri muda woooote basi tambua kwamba wale watu wa Arusha ni Hatari muda wooote kaa nao kwa tahadhari.
Tuliaminishwa kwamba Tarime/Mara kuna watu wakatili lkn mind you Arusha watu wamepinda na hamjibizani mara mbili na kama wewe ni mgeni hata ukiuliza kuelekezwa hawakupi msaaada so jamaaa wako very rude
 
Arusha ni hatari sana na utumiaji wa Bangi uko juu mnooo ukiongeza na Malezi ya Kimasai hasira kama Ngiri muda woooote basi tambua kwamba wale watu wa Arusha ni Hatari muda wooote kaa nao kwa tahadhari.
Tuliaminishwa kwamba Tarime/Mara kuna watu wakatili lkn mind you Arusha watu wamepinda na hamjibizani mara mbili na kama wewe ni mgeni hata ukiuliza kuelekezwa hawakupi msaaada so jamaaa wako very rude
mmteule Umewajumuisha wote ? sio sawa hii.
 
Back
Top Bottom