Pre GE2025 Arusha: RC Makonda aiagiza TAKUKURU kumhoji Mrisho Gambo upotevu wa Tsh. Milioni 400 zilizochangwa na wadau kwa ajili ya kusaidia bodaboda

Pre GE2025 Arusha: RC Makonda aiagiza TAKUKURU kumhoji Mrisho Gambo upotevu wa Tsh. Milioni 400 zilizochangwa na wadau kwa ajili ya kusaidia bodaboda

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
CCM ndio magwiji wa siasa hizi za majitaka.
Na yule mzee wa 80 naye ni mpenzi kweli wa hii mambo.
Nani ndani ya CCM anaweza kusimama na kutoa hoja ya maana!!?
Chama ambacho kinalea matatizo ya wananchi kweli kinaweza kueleza hoja za kutatua hayo matatizo!!???
Siasa za maji taka
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Arusha kufanya uchunguzi wa upotevu wa kiasi cha fedha shilingi milioni 400 zilizochangwa na wadau kwa ajili ya kusaidia waendesha pikipiki maarufu bodaboda.

Fedha hizo zimepotea na hazijapata majibu kuanzia mwaka 2016, baada ya harambee iliyoongozwa na Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo, wakati akiwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Makonda ameelekeza TAKUKURU kumuhoji Mbunge Gambo kwa kuwa alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa ukusanyaji wa fedha hizo.

Maelekezo haya ameyatoa leo kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichowakutanisha wadau mbalimbali na taasisi za serikali.

"Fedha ni ngumu, tulishachangiwa hapa na matajiri shilingi milioni 400, iliwekwa kwenye akaunti, lakini ilipowekwa tukaambiwa kuwa hizi fedha ni za bodaboda na wametuchangia matajiri zetu hapa mjini. Tulipochaguliwa kuwa viongozi wa bodaboda na kwenda kuangalia kwenye akaunti hatukukuta hata shilingi mia moja, sasa tunauliza zimeliwa na nani? Mimi nilipambana hadi TAKUKURU," alisema mmoja wa viongozi wa waendesha bodaboda na kuongeza,

"Mbunge (Gambo) alielekeza shilingi milioni 120 iende kwa akina mama kwenye kikundi kinachoitwa UWAWAJA."

Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda, amesema kwamba, alikumbana na madai ya upotevu wa fedha hizo hata alivyokuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi pindi alipofanya ziara katika mkoa huo.

"Hata nilipokuja hapa niliambiwa kuna hela za boda, sasa hivi mkiniambia kuwa mna milioni 20 ambazo Mheshimiwa Rais amechanga na mnatakiwa milioni 100 ili mpewe pikipiki, najiuliza hizi fedha zinazochangwa sasa zitakuwa salama vipi wakati zile milioni 400 hazijulikani ziko wapi?" aliongeza Makonda.

Kwa sasa, wananchi wanajiuliza ni nani alihusika na upotevu wa fedha hizo, huku matumaini yakielekezwa kwa TAKUKURU kufanya uchunguzi wa haki na kutoa majibu kwa umma.

Pia soma
Gambo ndio alisema wameshirikiana na TAKuKURU kuzuia Ufisadi wa Watendaji wanaosimamiwa na Bashite Sasa hapo anahojiwa Ili kitokee nini? 🤣🤣

Mbona Bashite anatapatapa?

Mwisho uliwahi ona wapi TAKuKURU akakamata mwanasiasa tofauti na Watendaji wa Serikali?
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Arusha kufanya uchunguzi wa upotevu wa kiasi cha fedha shilingi milioni 400 zilizochangwa na wadau kwa ajili ya kusaidia waendesha pikipiki maarufu bodaboda.

Fedha hizo zimepotea na hazijapata majibu kuanzia mwaka 2016, baada ya harambee iliyoongozwa na Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo, wakati akiwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Makonda ameelekeza TAKUKURU kumuhoji Mbunge Gambo kwa kuwa alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa ukusanyaji wa fedha hizo.

Maelekezo haya ameyatoa leo kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichowakutanisha wadau mbalimbali na taasisi za serikali.

"Fedha ni ngumu, tulishachangiwa hapa na matajiri shilingi milioni 400, iliwekwa kwenye akaunti, lakini ilipowekwa tukaambiwa kuwa hizi fedha ni za bodaboda na wametuchangia matajiri zetu hapa mjini. Tulipochaguliwa kuwa viongozi wa bodaboda na kwenda kuangalia kwenye akaunti hatukukuta hata shilingi mia moja, sasa tunauliza zimeliwa na nani? Mimi nilipambana hadi TAKUKURU," alisema mmoja wa viongozi wa waendesha bodaboda na kuongeza,

"Mbunge (Gambo) alielekeza shilingi milioni 120 iende kwa akina mama kwenye kikundi kinachoitwa UWAWAJA."

Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda, amesema kwamba, alikumbana na madai ya upotevu wa fedha hizo hata alivyokuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi pindi alipofanya ziara katika mkoa huo.

"Hata nilipokuja hapa niliambiwa kuna hela za boda, sasa hivi mkiniambia kuwa mna milioni 20 ambazo Mheshimiwa Rais amechanga na mnatakiwa milioni 100 ili mpewe pikipiki, najiuliza hizi fedha zinazochangwa sasa zitakuwa salama vipi wakati zile milioni 400 hazijulikani ziko wapi?" aliongeza Makonda.

Kwa sasa, wananchi wanajiuliza ni nani alihusika na upotevu wa fedha hizo, huku matumaini yakielekezwa kwa TAKUKURU kufanya uchunguzi wa haki na kutoa majibu kwa umma.

Pia soma
Tangu 2016 miaka 9 nyuma. Siasa ama kweli zina vituko.
 
Ikumbukwe ushahidi wa upande wa RAS utakuwa mgumu sababu alifariki kwa ajali ya gari (Richard Kwitega) - sasa hapa Gambo ataogelea mwenyewe

Akibainika kutumia fedha hizo nje ya malengo jasho litamtoka
 
Shamba la Bwana Heri na Mbuzi ni wa Bwana Heri😀😀 .Mimi Ngoja niendelee tu hapa kutafuta kura za ndio za Rais Samia huku mitaani.
Hapana mimi na imani kuwa wewe lucas ni timu Lissu na utakuwa front kupigania matokeo ya Lissu 2025 election .
 
Hahaha Makonda huwa hakai kimya mpaka apigwe Ban kutoka Ikulu.

Alipambana na Marehemu Dr.Ndugulile Kigamboni, akidai maagizo kutoka ikulu kwamba yeye Makonda ndiye alitakiwa agombee Kigamboni.

Na alimuaminisha kila mtu wakakaa pembeni. Ndicho anakifanya sasa kwa Gambo Arusha.

Magufuli alipopata taarifa alimkaanga hadharani, akasema mimi sijatuma mtu kugombea Kigamboni, wewe kama unataka kugombea kigamboni, ngoja nikupumzishe ukuu wa mkoa sasa ukapambane huko kutafuta jimbo.

Baada ya kauli ya Magufuli hapo hapo zile nguvu zikayeyuka, Makonda akawa kama toilet paper iliyolowa maji.

Hata yule Sheik wa Mkoa Alhaji ASAD akatoka na kumkataa Makonda, na yote yapo mitandaoni, alikuwa akidai waislamu wanamtaka yeye Kigamboni.

Huyo Makonda akiachwa anaweza hata kudhuru kwa madai kwamba katumwa kutoka ikulu.

Inabidi Ikulu impige Ban mapema, kama anataka ubunge wamtoe ukuu wa Mkoa, ili asitumie madaraka vibaya.
 
Gambo ndio alisema wameshirikiana na TAKuKURU kuzuia Ufisadi wa Watendaji wanaosimamiwa na Bashite Sasa hapo anahojiwa Ili kitokee nini? 🤣🤣

Mbona Bashite anatapatapa?

Mwisho uliwahi ona wapi TAKuKURU akakamata mwanasiasa tofauti na Watendaji wa Serikali?
Gambo alichosema kazuia ni hela za kununulia eneo la kujenga shule. Hizi 400m ni za zamani akiwa RC.
 
Ikumbukwe ushahidi wa upande wa RAS utakuwa mgumu sababu alifariki kwa ajali ya gari (Richard Kwitega) - sasa hapa Gambo ataogelea mwenyewe

Akibainika kutumia fedha hizo nje ya malengo jasho litamtoka
Hizo hela kashawahi kuulizwa sana anatoa majibu ya kisiasa. Halafu kwanini hela za bodaboda azimege na kuwapa mama ntilie?
 
  • Nzuri
Reactions: Tui
Hahaha Makonda huwa hakai kimya mpaka apigwe Ban kutoka Ikulu.

Alipambana na Marehemu Dr.Ndugulile Kigamboni, akidai maagizo kutoka ikulu kwamba yeye Makonda ndiye alitakiwa agombee Kigamboni.

Na alimuaminisha kila mtu wakakaa pembeni. Ndicho anakifanya sasa kwa Gambo Arusha.

Magufuli alipopata taarifa alimkaanga hadharani, akasema mimi sijatuma mtu kugombea Kigamboni, wewe kama unataka kugombea kigamboni, ngoja nikupumzishe ukuu wa mkoa sasa ukapambane huko kutafuta jimbo.

Baada ya kauli ya Magufuli hapo hapo zile nguvu zikayeyuka, Makonda akawa kama toilet paper iliyolowa maji.

Hata yule Sheik wa Mkoa Alhaji ASAD akatoka na kumkataa Makonda, na yote yapo mitandaoni, alikuwa akidai waislamu wanamtaka yeye Kigamboni.

Huyo Makonda akiachwa anaweza hata kudhuru kwa madai kwamba katumwa kutoka ikulu.

Inabidi Ikulu impige Ban mapema, kama anataka ubunge wamtoe ukuu wa Mkoa, ili asitumie madaraka vibaya.
Uko sahihi ila anayempiga spana ndo mfitini aliyekubuhu. Acha wapelekeane moto kwanza.
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Arusha kufanya uchunguzi wa upotevu wa kiasi cha fedha shilingi milioni 400 zilizochangwa na wadau kwa ajili ya kusaidia waendesha pikipiki maarufu bodaboda.

Fedha hizo zimepotea na hazijapata majibu kuanzia mwaka 2016, baada ya harambee iliyoongozwa na Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo, wakati akiwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Makonda ameelekeza TAKUKURU kumuhoji Mbunge Gambo kwa kuwa alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa ukusanyaji wa fedha hizo.

Maelekezo haya ameyatoa leo kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichowakutanisha wadau mbalimbali na taasisi za serikali.

"Fedha ni ngumu, tulishachangiwa hapa na matajiri shilingi milioni 400, iliwekwa kwenye akaunti, lakini ilipowekwa tukaambiwa kuwa hizi fedha ni za bodaboda na wametuchangia matajiri zetu hapa mjini. Tulipochaguliwa kuwa viongozi wa bodaboda na kwenda kuangalia kwenye akaunti hatukukuta hata shilingi mia moja, sasa tunauliza zimeliwa na nani? Mimi nilipambana hadi TAKUKURU," alisema mmoja wa viongozi wa waendesha bodaboda na kuongeza,

"Mbunge (Gambo) alielekeza shilingi milioni 120 iende kwa akina mama kwenye kikundi kinachoitwa UWAWAJA."

Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda, amesema kwamba, alikumbana na madai ya upotevu wa fedha hizo hata alivyokuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi pindi alipofanya ziara katika mkoa huo.

"Hata nilipokuja hapa niliambiwa kuna hela za boda, sasa hivi mkiniambia kuwa mna milioni 20 ambazo Mheshimiwa Rais amechanga na mnatakiwa milioni 100 ili mpewe pikipiki, najiuliza hizi fedha zinazochangwa sasa zitakuwa salama vipi wakati zile milioni 400 hazijulikani ziko wapi?" aliongeza Makonda.

Kwa sasa, wananchi wanajiuliza ni nani alihusika na upotevu wa fedha hizo, huku matumaini yakielekezwa kwa TAKUKURU kufanya uchunguzi wa haki na kutoa majibu kwa umma.

Pia soma
🤣😂🤣😂🤣🙌
 
  • Thanks
Reactions: Okk
Back
Top Bottom