Arusha hata miaka 50 ijayo haiwezi fikia Nairobi, wala huwezi shindanisha Dar na Nairobi.Arusha ipo over rated sana.
Lakini pia serikali imefeli kabisa kuujenga huu mji.
Ilipaswa kabisa uweze kutoa ushindani na jiji la Nairobi.
Lakini umebakia kuwa jiji la hovyo,hata ukipita pale East Africa Hq, AICC ile barabara inatia aibu.
Ndio maana leo google,microsoft na int offices nyingi zinawekwa nairobi.
Kahama stand kubwa imebanana Sana, japo wanasema zipo stand ndogo tatu za mikoa jirani.Arusha ndio mnataka kuifananisha na Mwanza kweli?
Arusha inapambana na miji kama Musoma, Geita, Katoro, nk. Kahama sasa sio level za Arusha tena.
Soon senta kama Kagongwa ama Runzewe zinaipita Arusha.
Sijui kama wale Wameru na Waarusha kindaki ndaki watakuelewa. Nilijaribu kuwaeleza nikaambulia matusi...Kuna miji inastahili kuwa na stand zaidi ya moja ila Halmashauri hawajaliona hilo, ile ya Arusha ((kama ndio ile ile nayoijua mie ukitokea Sheikh Amri Abeid kwenda Jogoo House maana nilitoka Arusha kitambo) inatakiwa ibaki pale pale na ikajengwa nyingine na ile ikawa ni ya kupita tu hasa magari yanapoingia usiku yaani yanashusha stand hizo za mbali alafu yanamalizia hapo yanaenda ku-park na kujaza mafuta vivyo hivyo asubuhi wakati yanaenda stand kuu yanapita pale yanakula vichwa alafu linaenda stand kuu ila hasara yake abiria wa pale ni kama hisani maana kama gari linaondoka saa 12 alfajiri basi pale linapita mapema zaidi maana safari inahesabiwa kuanzia stand kuu.
Mwanza waliliona hili kitambo sana zaidi ya miaka 15 kwa kuwa na stand ya Nyegezi na Buzuruga yaani hapo gari zinazotokea Nairobi au Musoma zinaishia Buzuruga ila kama zipo zinazounganisha Dar zinashusha hapo na kula vichwa kisha zinakwenda Nyegezi na zinaendelea na safari na gari zikiingia usiku hata jioni zinashusha Nyegezi alafu zinawasogeza abiria Natta (mjini kati) na zingine mpaka Buzuruga. Na katika utaratibu huu wa kujenga stand mpya na zote zinajengwa ila hii ya Buzuruga wametafuta eneo lingine na imeshakamilika bado kuizindua ambapo hii ya zamani inaweza ikatafutiwa matumizi mengine hata kuwa ya daladala au magari ya kwenda vijijini / wilayani.
Mikoa ya Dar, Mwanza, Arusha na Dodoma zinahitaji stand kuu zaidi ya moja, wenzao Mwanza walishaonyesha mfano tangu kitambo na sasa wanakamilisha stand kubwa 2
Stendi zipelekwe nje ya mji zikasaidie kukuza maeneo ya pembezoni.Hapoa Arusha wanaweza wakafanya mpango wakahamisha hayo makaburi nyuma ya stendi Ndogo kisha eneo lote mpaka huku stendi ndogo likiwa stendi kubwa ya mabasi.Yaani kuanzia hapo stadium kote kunakuwa ni STAND.Inawezekana kabisa
...na wasilalamike maana mjini patapoa kama makaburini
uwanja wa Abeid Karume ndio upi huo?wakazi gani hao wa Arusha wameyasema hayoWananchi jijini Arusha pamoja na abiria wanaotumia stand kubwa ya mabasi wamailalamikia uongozi wa jiji la Arusha kuwa wameshindwa kuwaletea mabadiliko kwa kuwajengea stand nyingine mpya ya kisasa tofauti na iliyopo sasa ambayo ipo tangu kabla ya uhuru hadi sasa.
Kutokana na udogo wa kituo hicho cha Mabasi umefanya baadhi ya makampuni kushusha na Kupakia abiria katika sehemu mbalimbali na wengine katika ofisi zao zilizopo sehemu tofauti tofauti jijini hapo na hivyo kuleta usumbufu kwa abiria na wageni kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Mfano gari za kwenda Namanga kuna ambazo zinapaki stand kubwa na. Nyingine nje ya uwanja wa mpira wa. Abeid karume.
Magari ya Kwenda Dar es Salaam kuna machache yanapaki ndani ya kituo hicho, mengine stand ndogo na. Mengine yamekuwa yakipakiza na kushusha abiria katika ofisi zao
Za kwenda karatu nazo kuna ambazo zinapaki ndani ya kituo na nyingine mbali na kituo hicho maeneo ya Sabena
Kituo hicho kikubwa cha mabasi hakina sehemu ya kusubiri abiria wala Wasindikizaji.
Hakuna sehemu ya kuwakinga na Mvua wala jua.
Na. Pia Usalama ni mdogo usiku na. Mchana kutokana na miundombinu ya kituo hicho cha mabasi na hivyo Kuwa na. Idadi kubwa ya vibaka, wezi, wavutaji wa madawa yote na vijana wa mitaani ambao ni tishio kwa wageni na abiria.
Wananchi wa jiji la Arusha wamekuwa wakilalamika miaka Nenda miaka rudi lakini hawaoni mabadiliko yoyote hadi sasa,kituo cha mabasi kilichopo hakiendani na hadhi ya jiji kwani jiji hili limekuwa likipokea wageni wengi ndani Na Nje ya nchi hivyo kituo hicho ambacho hakina uwezo hata wa kupaki mabasi (10)kumi kwa wakati mmoja, kinaharibu taswira ya jiji.
Kusema kuwa serikali inashindwa kupata maeneo ni kukiri kuwa udhaifu wa serikali. Mbona serikali ikitaka kufanya miradi kama ya barabara, umeme au maji chap chap wanafidia watu na kutekeleza miradi husika??Hata hivyo Arusha ni mji mkubwa wenye eneo finyu angalau sasa hivi watakuwa wameongeza mipaka ya jiji na mbaya zaidi kule maeneo mengi yanamilikiwa na watu tangu enzi hizo na wanajua thamani ya ardhi hivyo hata serikali inapata wakati mgumu wa kupata maeneo ya shughuli za maendeleo zaidi ya kwenda pembezoni nako lazima walipe fidia ndefu
shida kubwa ya tanzania ni planning. serikali imewaachia watu waendeleze miji kiholela, miji ikikua (kiholela) ndipo inajifnaya kuanza kujaliMjini kupoa pia ni maendeleo. Kwa sasa ule mji wa Arusha unatia kichefu chefu
🤣🤣 Hizo Zitakuwa stand au vituo vya daladalaIli mji wa Arusha upanuke na ukue kwa haraka wahusika wazingatie yafuatayo:
1. Ondoa stendi na masoko yale pale mjini kati.
2. Stendi mabasi ya kutoka Dodoma road inatakiwa iwe Kisongo. Weka soko huko.
3. Stendi mabasi kutoka Moshi road iwe USA au Chekereni. Weka soko huko.
4. Stendi magari kutoka Nairobi iwe Ngaramtoni ya Juu. Weka soko huko.
5. Stendi magari kutoka Simanjiro/Kiteto iwe Oljoro. Weka soko huko.
NB: Lakini msije mkalalamika kuwa stendi na masoko yako mbali!
Ooh kumbe Stand na vituo vina utofauti??🤣🤣 Hizo Zitakuwa stand au vituo vya daladala