Arusha: Wananchi watishia kugoma kudai lami, wachoshwa na ubovu wa barabara

Arusha: Wananchi watishia kugoma kudai lami, wachoshwa na ubovu wa barabara

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Wakazi wa kata ya Sinoni, na Ungalimited wanaotumia barabara kuu ya Engosengiu inayotokea mjini kuelekea katika Kata hizo mbili wamedai kuchoshwa na ubovu wa barabara hiyo kiasi cha kuwaletea usumbufu mkubwa hata katika vyombo vyao vya moto.

Baadhi ya madereva wa Bajaji na Hiace wanaotumia njia hiyo wamesema ubovu wa barabara hiyo pamoja na mashimo unawaharibia magari yao mara kwa mara.

Baadhi ya wananchi wanaotumia barabara hiyo wamedai wakati wa jioni madereva kubadilisha ruti na pia kupandishiwa nauli hivyo kuwaletea usumbufu hasa nyakati za jioni.

Wananchi wamekuwa wakilalamika kuwa kila mwaka hudanganywa na viongozi kuwa barabara hiyo itawekwa Lami lakini hadi sasa hakuna kinachoendelea.

Miaka mitatu iliyopita madereva wa Hiace waligoma wakishinikiza kuwekewa lami lakini badala yake wakawekewa kifusi cha udongo na kuahidiwa kuwekewa lami lakini hadi sasa hali ni Ile ile.

Bara bara hiyo ipo katika halmashauri ya jiji la Arusha.

IMG-20211118-WA0006.jpg
 
Bila kusahau barabara ya Kijenge--- Mwanama---Engutoto ,hakika inawakwaza wananchi licha ya kuhudumia wakazi wengi na wafanyakazi wengi wa viwanda vilivyopo Kata za Themi na Engutoto(Njiro)

Pia ni barabara itakayowafikisha Wananchi kirahisi Kituo cha Afya cha Moshono,iwapo itawekwa lami

Vilevile ni barabara inayopita kwenye taasisi muhimu kama chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru,tawi la Kijenge Mwanama,Kituo cha Afya cha Kijenge(Kijenge Community Health Centre),MaKanisa,Misikiti, shule za sekondari na msingi Olerian,bila kusahau shule binafsi za St Patrick na zingine nyingi

Nikuombe Mh Mbunge Gambo uiangalie barabara hii Ya Kijenge --- Mwanama- Engutoto kwa jicho la tatu,

Kama mliweza kuwapelekea lami Matajiri wa Kijenge PPF Complex, kwa nini sisi msiweze?..hamuoni kama mnajenga chuki kwenye jamii?
 
Kama mliweza kuwapelekea lami Matajiri wa Kijenge PPF Complex, kwa nini sisi msiweze?..hamuoni kama mnajenga chuki
Matajiri wa PPF wanaishi maisha safi hakuna vumbi wamewekewa Lami hadi milangoni.
 
Back
Top Bottom