Vitu vitatu vinavyowamaliza vijana wa Kitanzania kwasasa: bodaboda, kamari, pombe kali za bei poa. Vyote hivi vitatu vina baraka ya chama cha wala.
Kijana wa bodaboda anaungaunga, akipata anaenda kucheza kamari ili apate nyingi aachane na bodaboda. Akifika huko analiwa zote, anapatwa na usongo mkubwa wa mawazo anapitia kwenye kibanda kinachouza pombe kali, anachukua kichupa cha buku 2 na kukiputa chote.
Anapata stimu na kuondoka na bodaboda yake! Hafiki salama nyumbani, aliinywa ile pombe kwa spidi kubwa na ikapanda kwa haraka akiwa barabarani tayari, akapata ajali na kukimbizwa hospitalini. Kufika huko, aliumia vibaya miguu au mikono. Upasuaji laki 5, lakini hana kato ka ya maskini, daktari ili kuokoa maisha ya kijana, anakatwa kiungo chake na kuingia rasmi kwenye ulimwengu wa walemavu.
Kwa baraka na usaidizi wa chama cha wala, walioleta bodaboda ndio haohao walioleta kamari. Huu ni uhujumu uchumi, lakini chama haki yaoni haya!