Asante 2022, nilipata mil. 4.5 kimasihara

Asante 2022, nilipata mil. 4.5 kimasihara

Every action there is equal and opposite to the reaction ...
Niliuziwa mabati ya wizi kwa bei ya mteremko

Baadae wizi ukagundulika wakakamatwa watu kibao waliokuwa wanahusika kwenye huo mradi wa serikali,wengi wao wakiwa wamewaonea tu maana walikamata mpaka wasomba maji na mlinzi ambae walikuwa hawajamlipa hata mshahara toka aanze kuwa hapo

Nikaogopwa kutajwa au kufanya upekuzi nyumbani kwangu,nikaamua niyakimbize mabati mbali ninapoishi kwenye nyumba nyingine umbali kama km 30 niliyasafirisha usiku sana

Ile narudi baada ya kuyafikisha salama,nikapata ajari nilimgonga boda boda,hela iliyonitoka ni nyingi mno kuna wakati hadi nawaza ni zile laana za wale lala hoi waliobambikiziwa kesi maana walitoa hela kutoka polisi hawakuachiwa hv hv
 
Nikiwa nimepitia misukosuko mingi tangu Januari ya mwaka 2022 Nitaikumbuka zaidi siku ya Alhamis tar 29 majira ya saa saba za mchana, nikiwa nimekaa kijiweni na jamaa zangu huku nikiwa sina ramani ya kazi na sikuwa hata na uhakika wa mlo wa mchana kwa siku hiyo iliingia sms ya muamala kwenye simu yangu kuwa nimepokea kiasi cha ml 4.5 kutoka kwa wakala.

Hakika sikuamini nilichokiona, kwa haraka hiyo pesa nikaihamishia kwenye lain yangu ya tigo pesa ml 2 na laini ya voda nikahamishia ml 2, mbio hadi kwa wakala nikaitoa pesa kwenye lain zote na ile iliyokuwa imebaki kwenye namba niliyotumiwa ya airtel nayo nikaitoa.

Na laini iliyopokea muamala sijaiweka hewani hadi sasa na kabla sijaitoa hewani sikupigiwa na mtu kwamba ametuma hela kwangu kimakosa na wala mimi sikuwa na ahadi na mtu eti anitumie hela.

Kwahiyo ninashukuru sana aliyenitumia hiyo hela, kiukweli hata kama angenipigia na kuniambia eti kakosea muamala asingeambulia kitu. Mungu amlinde sana nilikuwa nina Magumu sana asante Mungu, na nitakukumbuka 2022.
Je umeiingiza kwenye biashara ili ikusaidie zaidi? Nina shaka na jibu utakalotoa.
 
Kuna boss wangu mmoja anaweza akakutumia pesa na asikupigie hata wiki ndio akakuambia hiyo pesa ni ya matumizi fulani alafu ana tabia ya kutuma pesa nyingi sana,

sasa nafikiria tu mimi ningekuwa kama wewe sijui ingekuaje!! By the way , karma haiongopi! Hiyo ni jasho ya mtu na utaitapika kwa njia yeyote ilee yaani utalipa gharama tu Na usisahau kutupa mrejesho yakisha kurudia.
 
Kipindi nipo chuoo niliwahi kutumiwa pesa kimakosa laki 8 nikajifanya mjanja nikaitoa nikakusanya marafiki nikaenda nao kunywa pombe ile laini niliswitch off kwa wiki 3.ikapita miezi 8 kimya..baadae bibi alipata shida ya figo ilitakiwa afanyiwe dialysis kila mwezi so michango ya kifamilia ikatembea, bila kujua ili wala lile shangazi akanitumia mchango pesa ya matibabu laki 9.5 niitoe ili nimpatie mzee kumbe alituma katika ile line niliyotumiwa pesa kwa bahati mbaya..tigo hawajuchelewesha sms ikaingia hapo hapo
Ndugu mteja umekatwa sh laki 8 salio lako jipya ni laki na nusu niliishiwa pozi aisee.
Ili kuuawa soo nikaingia hasara nikatoa pesa yangu ya mkopo nikampatia mzee uku moyoni nina maumivu.
Juzi kati kuna mtu alikosea tena akanitumia pesa kimakosa mwenyewe nikamtafuta nikampigia cm nikamwambia umenitumia pesa kimakosa nakurudishia pesa yako..yaanini mie
Hahahaaa Kuna jamaa yangu alikuwa mwalimu shule za serikali, baadaye akasomea Mambo ya maabara akapata kazi za halmashauri moja hivi lkn ni serikalini. Akawa anapata mishahara miwili kwa mwaka mzima. Unajua nn kilimtokea? Ilijulikana wakamsimamishia mshahara kwa miaka 3 alafu ana mke na watoto, nusu awe chizi *****
 
Niliuziwa mabati ya wizi kwa bei ya mteremko

Baadae wizi ukagundulika wakakamatwa watu kibao waliokuwa wanahusika kwenye huo mradi wa serikali,wengi wao wakiwa wamewaonea tu maana walikamata mpaka wasomba maji na mlinzi ambae walikuwa hawajamlipa hata mshahara toka aanze kuwa hapo

Nikaogopwa kutajwa au kufanya upekuzi nyumbani kwangu,nikaamua niyakimbize mabati mbali ninapoishi kwenye nyumba nyingine umbali kama km 30 niliyasafirisha usiku sana

Ile narudi baada ya kuyafikisha salama,nikapata ajari nilimgonga boda boda,hela iliyonitoka ni nyingi mno kuna wakati hadi nawaza ni zile laana za wale lala hoi waliobambikiziwa kesi maana walitoa hela kutoka polisi hawakuachiwa hv hv
Kama nakuona vile ulivokua unakimbiza mabati[emoji23]
 
Kama hiyo laini imesajiliwa NIDA watakukama tu, utake usitake. Ili usikamatwe labda uhame nchi!!
 
Dah nisemeje Mimi niliwahi kupata hela kwa staili hiyo haikua kubwa lakini ilikuja kuniletea matatizo Sana ilikua hivi.

Siku hiyo nilikua nimekaa na njaa kwa masaa 42 bila kula chochote njaa imetamalaki na msaada nilikosa kabisa mpaka leo najiuliza ilikuaje nilikosa hata 500 na hakuna hata mtu aliyenisave hadi home..hii ilitokana na Mimi kulazimisha kuhama nyumbani na kwenda kupanga pasipo ridhaa za wazee.

Basi bwana nikiwa nimejilaza napiga hesabu nimgongee mpangaji mwenzangu na hapo ndo kwanza Nina wiki mbili kwenye hiyo nyumba ,akaja rafiki yangu na yeye choka mbaya tukawa tunapiga stori na yeye alikuja kunililia njaa tangu Jana yake hakula...Mara pa mlio wa sms kwenye laini ya tigo kucheki ni elfu 30 moyo ukafanya paah bila kuchelewa nikaenda kuitoa ile hela nikapata elfu 28.

Hao Cha kwanza mgahawani ita menyu gonga pale sahani mbili kila mtu Mara simu ikaita napokea ni mdada akaomba arudishiwe hela japo elfu 20 tu maana alikua anamtumia kaka yake atoe ili apate elfu 20 ya matibabu ya kijana wake na iliyobaki apate rizki ya chakula...dah kwa ukaidi nikagoma sijaona hela ,aliniomba Sana nikamwambia sijaona hela Basi akaniambia neno moja "Kama hiyo rizki ni yako halali Basi Mungu atakuacha Ila Kama sio ya halali utapoteza vingi na utajutia kwa dhulma yako" nikakata simu nikamblock(blacklist).Ila hakukoma alitumia namba nyingine alinisumbua siku nzima nikaamua kutoa laini.

Sijui Kama ilihusiana na lile tukio lakini miezi 11 baadae nikapata pesa za kutosha kwangu(kiuanafunzi) Ila zilipotea vibaya nilipata uchungu balaa.ikabdi nikatoe sadaka ile 30 kwa nia kua namlipa Yule dada niliichenji na kugawa kwa wale omba omba kila niliyemkuta mpaka ikaisha ile siku yote,maana sikua na namna ya kumpata.

Now Sina shida ila fikra zangu naamini nililipia ile hela kwa njia nyingine ndo nikawa salama.

NB😀hulma haifai wazee
 
Mimi kuna mtu alikosea akatuma hela kwangu kwa roho nzuri tu nikampigia nimuulize katuma ya nini au kakosea akawa anakata simu mwishoe naona txt ikisema "uliniona maskini chukua kihela chako usinisumbue unaonekana una njaa sana hela ndogo inakutoa povu" aloo ilikua 240k nilifurahi sana nikamjibu nashukuru nikaitoa nikaendelea na harakati siku kama mbili akanipigia sikusave namba ndipo ananiambia samahani nilituma hela kimakosa na mm nikamwambia nishaitumia samahani sana. Nahisi alijiskia kufa huko alipo.

Fundisho ni kwamba alikua na dharau huenda alisaidiwa na mtu alafu kwenye kudaiwa akawa mgumu katoa na maneno ya dharau wakati aliponitafuta ili nirudishe muamala alikua anaomba kwa upole[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hahahahahaha
 
Munadanganyana sana mara sijui karma mara hivi,hebu niwaambie kitu kimoja acheni imani za kijinga mimi ukikosea muamala kuanzia laki 2 sikurudishii hata iweje nakumbuka kuna demu mmoja wa kichaga alikosea hela akatuma kwangu laki 5 aisee nilikodi bodaboda mpakka town kwenda kuipakua hela yangu ya bure yule dada alipiga simu sana ananiomba nimrudishie nikawa namuambia niko barabarani dada nikifika hom tu nakurudishia kumbe nipo barabarani kwenda kwa wakala na mpaka leo hakuna cha karma wala nini
 
Munadanganyana sana mara sijui karma mara hivi,hebu niwaambie kitu kimoja acheni imani za kijinga mimi ukikosea muamala kuanzia laki 2 sikurudishii hata iweje nakumbuka kuna demu mmoja wa kichaga alikosea hela akatuma kwangu laki 5 aisee nilikodi bodaboda mpakka town kwenda kuipakua hela yangu ya bure yule dada alipiga simu sana ananiomba nimrudishie nikawa namuambia niko barabarani dada nikifika hom tu nakurudishia kumbe nipo barabarani kwenda kwa wakala na mpaka leo hakuna cha karma wala nini
usijisifie dhulma mkuu, yajayo yanafurahisha
 
Hizo namba zilizotumika kwenye miamala si zimesajiliwa kwa majina yako na ulitumia kitambulisho, basi kaa kwa kutulia hakuna ujanja wowote uliofanya hapo utanaswa kiulaini kama kuku bandani.....
 
Dah nisemeje Mimi niliwahi kupata hela kwa staili hiyo haikua kubwa lakini ilikuja kuniletea matatizo Sana ilikua hivi.

Siku hiyo nilikua nimekaa na njaa kwa masaa 42 bila kula chochote njaa imetamalaki na msaada nilikosa kabisa mpaka leo najiuliza ilikuaje nilikosa hata 500 na hakuna hata mtu aliyenisave hadi home..hii ilitokana na Mimi kulazimisha kuhama nyumbani na kwenda kupanga pasipo ridhaa za wazee.

Basi bwana nikiwa nimejilaza napiga hesabu nimgongee mpangaji mwenzangu na hapo ndo kwanza Nina wiki mbili kwenye hiyo nyumba ,akaja rafiki yangu na yeye choka mbaya tukawa tunapiga stori na yeye alikuja kunililia njaa tangu Jana yake hakula...Mara pa mlio wa sms kwenye laini ya tigo kucheki ni elfu 30 moyo ukafanya paah bila kuchelewa nikaenda kuitoa ile hela nikapata elfu 28.

Hao Cha kwanza mgahawani ita menyu gonga pale sahani mbili kila mtu Mara simu ikaita napokea ni mdada akaomba arudishiwe hela japo elfu 20 tu maana alikua anamtumia kaka yake atoe ili apate elfu 20 ya matibabu ya kijana wake na iliyobaki apate rizki ya chakula...dah kwa ukaidi nikagoma sijaona hela ,aliniomba Sana nikamwambia sijaona hela Basi akaniambia neno moja "Kama hiyo rizki ni yako halali Basi Mungu atakuacha Ila Kama sio ya halali utapoteza vingi na utajutia kwa dhulma yako" nikakata simu nikamblock(blacklist).Ila hakukoma alitumia namba nyingine alinisumbua siku nzima nikaamua kutoa laini.

Sijui Kama ilihusiana na lile tukio lakini miezi 11 baadae nikapata pesa za kutosha kwangu(kiuanafunzi) Ila zilipotea vibaya nilipata uchungu balaa.ikabdi nikatoe sadaka ile 30 kwa nia kua namlipa Yule dada niliichenji na kugawa kwa wale omba omba kila niliyemkuta mpaka ikaisha ile siku yote,maana sikua na namna ya kumpata.

Now Sina shida ila fikra zangu naamini nililipia ile hela kwa njia nyingine ndo nikawa salama.

NB😀hulma haifai wazee
Aisee sasa nifanyeje na nilishaitumia na sijawahi pigiwa na mtu kwamba kakosea kutuma
 
Back
Top Bottom