Asante kwa aliyetuletea Fiston Mayele, Yanga tulikosa mshambuliaji wa aina yake kwa muda mrefu kidogo

Asante kwa aliyetuletea Fiston Mayele, Yanga tulikosa mshambuliaji wa aina yake kwa muda mrefu kidogo

Habari wanamichezo,
Juzi niliangalia goli alilofunga Mayele, kasi yake alvyopokea mpira, utulivu wake, akili yake ya kufunga, control yake hakika niseme asante Engineer Hersi kwa kutuletea huyu mtu. Wanayanga tulimkosa huyu mtu kwa muda mrefu sana tangu Yanga ya Donald Ngoma nadhani hatujapata complete striker kama huyu.

Ananikumbusha forward za Yanga ie Makumbi Juma, Jerry Tegete, Iddi Moshi, Mmachinga, Sekilojo, Ambani, Mogella, mwamba Kizota et al!

Endelea kututetemesha Fiston Kalala Mayele, hakika ukiondoka wanayanga tutakukumbuka sana kwa kazi yako iliyotukuka na style yako unique kabisa ya kutetema ambayo naamini hata watani zangu Makolo FC wanaipenda japokua inawaumiza sana maana huwa unatetema kwa karaha zaidi hasa hasa ukiwaweka goli wao!

Refer ngao za hisani zote mbili!
Ulimakafu Mshana Jr Soma Tena Elli Utingo green rajab
 
Kama MFUNGAJI wako hana ufungaji bora hata ndondo cup uzi ufutwe [emoji2089][emoji2089][emoji2089]
 
Back
Top Bottom