Asante Mo Dewji kwa kufanyia kazi maoni yangu kuhusu Sportspesa

Wewe sijui hata kama umemaliza kidato Cha nne?!!nyie ndio mnafanya jukwaa la michezo lionekane ni jukwaa la watu wasio na shule!!
 
Wewe sijui hata kama umemaliza kidato Cha nne?!!nyie ndio mnafanya jukwaa la michezo lionekane ni jukwaa la watu wasio na shule!!
Nina Masters kaka sio lazima kuchangia kila mada inayopita mbela yako kwani unaweza kuwafanya wazazi wako (kama bado wako hai) wajutie pesa waliyokupelekea shule kwamba kwanini wasingelimia mahindi huko kijijini kwenu. zero brain wewe
 
Nina Masters kaka sio lazima kuchangia kila mada inayopita mbela yako kwani unaweza kuwafanya wazazi wako (kama bado wako hai) wajutie pesa waliyokupelekea shule kwamba kwanini wasingelimia mahindi huko kijijini kwenu. zero brain wewe
Masters sigara kama ni hio sawa!! Sijui hata unaelewa Masters ni nini?!! Ngonjera unaleta hapa!!nina uhakika kwa michango yako ninayosoma hapa!!!kama ulijitaidi sana!! basi una ziro ya kidato cha nne kata.
 
20B hata ikiingia, basi ni kwenye akaunti ya Simba, sio ya Yanga. Cha ajabu Yanga ndio wanaoongoza kuidai
 
Simba wangejiuliza Man U anapata kiasi gani kwenye TV, na Simba wanapata kiasi gani kwenye TV.
Jibu ni USD 630 million kwa mwaka 2020.
Mkataba wa Azam Tv na Bodi ya Ligi ni USD 10 million kwa miaka 5; yaani USD 2 million kwa mwaka kwa timu zote za ligi.
Simba hapo sanasana anapata 200mil. ambayo ni kama USD 100,000/- kwa mwaka. Na mkataba unaishia mwaka huu.

Swali ni kwanini Dewji hazungumzii Azam TV anazungumzia Sportspesa?

Jibu:
Katika utafiti wowote wa mapato ya michezo, TV hutumika kama chombo cha kupima population assignment.
Watafiti hutumia Average TV viewership (Broadcasting) na mahudhurio (Match day) kama "n". Pia kampuni za matangazo hutumia hii ku- bargain bei ya TV commercial.
Hata kit sponsorship huwa haisemwi tu kutoka kichwani. Mnakaa mezani na wewe kama mwenye timu unatoa takwimu zako za Match day viewership (average) kwenye TV na Uwanjani.
Data za Matchday hasa kwenye TV za Tanzania si rahisi kuzipata, kwa hiyo kubargain kwa kutumia hii njia, si rahisi. Ingawa data za uwanjani zipo ila ni ndogo sana na huwa affected na mambo mengi.

Njia ya pili ni mauzo ya merchandise. Yaani jezi, bilauri, key holders etc ...
Hii pia ni njia mojawapo ya kuwaambia sponsors kwamba, angalia mimi nauza kiasi hiki kwa mwaka. Ukiweka matangazo yako utakuwa na uhakika wa kuongeza mapato kwa sababu mimi navutia macho mengi ambayo inamaanisha mifuko mingi. Hii method ni ya uhakika na pia ni rahisi kupata Data zake hapa Tanzania.

Manchester walipata Mauzo ya USD 345 milion; Je Simba walipata mauzo ya USD milioni ngapi? Wakiweza kufananisha hii, basi hiyo proportion waitumie pia kubargain na SportsPesa.
Siyo kuongea tu.
 
Asante nimekuwa nikichomeka hivi vimada kwenye nyuzi nyingi humu ili kuwaelewesha maana ya huu mfumo mpya na ilivyo ngumu sana kutengeneza faida kwenye sports industry huku man utd timu yangu ikiwa reference. Juzi niliandika humu leicester city imereport hasara ya 37m paunds last week

Nilikuwa nasubiri mtu aje achokoze hili la tv and image rights alizopewa azam. Kwa macho yangu nakuhakikishia karibu robo tatu ya watanzania wanalipia vifurushi vya azam ili kuangalia mechi za simba na yanga, kama wanabisha waangalie idadi ya transactions zinazofanyika masaa mawili kabla ya simba au yanga kucheza mechi. Siku hizi wakati wa mechi watu hawaonekani mtaani wamejazana kwenye ma bar na vibanda umiza mpaka vijijini kwahiyo kuna mamilioni ya watu wanaofuatilia hizi timu i mean tv moja wanaangalia watu 30+. Sijui kama viongozi wa simba na yanga wanalifahamu hili au wanalifumbia macho makusudi.

azam wameathiri mapato ya uwanjani kwa kiasi kikubwa na zaidi dar.

Ushauri: simba na yanga wakae watengeneze proposal kwa tff ili kila timu iingie mkataba na azam kivyake, mfano man utd iliishia round of 16 uefa lakini ilipata hela nyingi kuizidi juve iliyocheza fainali.. sasa hivi timu za england zimekuwa na pesa nyingi kutokana na deal mpya ya sky sports. Barca na madrid wana negotiate na broadcaster direct
Ikishindikana simba na yanga wakatae mechi zao kurushwa. Hela anayotoa azam kwa simba na yanga ilitakiwa kuwa mara 15 ya sportpesa
 
hivi muwekazaji anaweza kuwa mjinga wa kuandika upuuzi namna hii kwenye mitandao???

Huyu Mudi ana akili sawa-sawa kweli????
 
timu za Simba na yanga wamekuwa wazembe sana hata ukiangalia kwenye udhamini mwingine wa vodacom bado wanapata pesa kidogo juzijuzi KCB walidhamini ngumi lakini pesa waliyoweka ni kubwa kuliko hata wanayoweka kwenye mpira ambao unashirikisha timu kumi na nae kulinganisha na pambano moja la ngumi.
Hispania Barcelona na Madrid pesa wanazopata ni kwenye mgao wa tv ni nyingi kuliko wanazopata vilabu vingine ila hapa unakuta kiongozi wa simba au yanga yupo huku akichungulia agombee tff au agombee ubunge.
 
Watu wananunua decoder za azam ili kuangalia simba na yanga tu. Usione watu wajinga wanagombania nafasi za uongozi kwenye hizi timu 2, mayai anaposema kuna viongozi wapo wanaishi kupitia yanga hakuwa mjinga, huwenda asingekuwa muajiriwa wa muhindi angefafanua how?
Je, kuna watu tuliowapa dhamana ya timu hizi timu 2 wanavuta vibunda ili kusaini dili mbovu na kujifanya kama hawaoni dhuluma hii?
Ningefurahi sana iwapo mo angehoji mkataba wa azam na sio hawa sportpesa ambao wanatoa kikubwa kuliko azam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…