Asante Rais Samia Kutuletea Prof. Kabudi Pale Sheria, Ni Best Brain, High IQ. na Bingwa wa Katiba. Je, Atakuwa Mkweli Ubatili wa Katiba na Sheria au?

Asante Rais Samia Kutuletea Prof. Kabudi Pale Sheria, Ni Best Brain, High IQ. na Bingwa wa Katiba. Je, Atakuwa Mkweli Ubatili wa Katiba na Sheria au?

Aksante Raisi Samia kumuleta kabudi,Sina maslahi yoyote na kabudi lakini niliumizwa mnooooooo,ulipomtimua Kisha ukaleta akina nape na makamba,niliuchukia mnooooooo utawala wa awanu ya sita,Ila Sasa kwa kumrejesha kabudi,umecheza Kama Pele,bado kalemani,ukimrejesha na huyo hakika utakuwa maradona wa siasa za Africa,pia angalia na nje ya ccm Kuna watu wazuri Sana kwenye maeneo korofi ya kiutawala, fanya maamuzi magumu kabisa,Kama alivyofanya mtangulizi wako alipomuibua kafulila na kabudi,mkapa Naye alimwibua SheIn,please angalia na nje ya ccm,pia wapi watu hujawatumia,pole pole na bashiru ally ,usiwaogope hizo ni hazina za nchi
 
Wanabodi
Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za Kwa Maslahi ya Taifa, zinazo zungumzia jambo lolote la kisiasa, kiuchumi au kijamii kwa mtindo wa swali halafu jibu utatoa wewe mwenyewe .

Mada ya leo ni pongezi na shukrani kwa Rais Samia kumteua tena Prof. Palamagamba John, Aidan Mwaluko Kabudi, kuwa waziri wetu wa Sheria.

Kwa maoni yangu binafsi, ulimuondoa Prof. Shivji , Prof. Chris Peter Maina, na Prof. Gamalieli Mgongo Fimbo kwenye unguii wa katiba, anayefuata ni Prof. Kabudi, ila tukija kwenye overall the best of the best, Prof. Palamagamba Kabudi is the best, amewapita wote on several avenues.

Prof Kabudi is one of the best brains this country has and has ever had. The best brain inapimwa kwa IQ test. Sisi Tanzania hatuna amplitude test za kupima IQ za watu wetu, tunatumia matokeo ya mitihani ya kidato cha 4, 6 na GPA za chuo kikuu.

Soma Pia: Kwa uteuzi wa Prof. Kabudi katiba na sheria tukubaliane tu Mwambukusi atanyoosha mikono kama ilivyokuwa kwa Lissu na kudhibitiwa

Japo sijui scores za Prof. Kabudi za form 4 na form 6,
ni division 1 ya points ngapi, ila enzi zile kusoma sheria ilikuwa ni lazima uwe na division 1 kali.

Kwenye nchi za Afrika Mashariki, chuo kikuu cha kwanza kufundisha sheria ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kilichoanzishwa October 1961, siku chache kabla ya uhuru wa Tanganyika na kilichukua wanafunzi kutoka nchi zote tatu za Afrika Mashariki, Tanzania, Kenya na Uganda.

Na mimi pia nilisomea sheria yangu LL.B chuo kikuu cha Dar es Salaam na kupita mikononi mwa Prof. Palamagamba Kabudi, sio tuu kama mwalimu wangu bali yeye ndiye alikuwa supervisor wangu wa my LL.B dissertation, hivyo ni mtu ninayemfahamu kwa karibu.

Wakati nikiwa mikononi mwake mpaka ninamaliza UDSM kuna vitu sikuvifahamu kumhusu Prof. Kabudi, ila mwaka 2011 wakati chuo kikuu cha Dar es Salaam kinaadhimisha Diamond Jubilee, Prof. Palamagamba Kabudi alitunukiwa tuzo ya outstanding GPA, kwa muda wote wa miaka 50 ya chuo kikuu cha Dar es Salaam, recoding ya GPA ya Prof. Kabudi, ya 4.9 haukuwahi kuvunjwa mpaka wakati huo, na sikuwahi kusikia kama kuna Mwanafunzi mwingine yeyote amewahi kuifikia, hivyo kuna uwezekano Prof. Kabudi ni one of the best brains of the best that we have!.

Nimesema one of, kwasababu kuna uwezekano tuna best brains kuliko Prof. Kabudi lakini hawakwenda shule hivyo hawajulikani lakini kuna watu wanafanya mambo makubwa kimya kimya, na kuna Watanzania wengi brains wanaosoma ughaibuni, huwa hawarejei nchini, Wazungu wanawashika.

Kitu kingine cha ziada kumhusu Prof. Kabudi, ni multi talented, ana kipaji cha usimulizi, oratorio talent, ana kipaji cha kupiga kinanda na ni mcha Mungu aliyelelewa kwenye uchamungu.

Hii sio mara ya kwanza kwa Prof. Kabudi kuteuliwa Waziri, aliteteuliwa na Magufuli kwenye serikali ya awamu ya 5, Rais Samia akamuondoa, sasa ni Samia amemteua tena Wizara ile ile ya sheria.

Mtu kuwa the best brain, high IQ na bingwa wa Katiba ni jambo moja, na uelewa wa katiba, na utekelezaji wa majukumu yake kiweledi ni jambo jingine.

Serikali inafanya kazi kwa mtindo wa uwajibikaji wa pamoja, a collective responsibility hata kama jambo fulani haliko sawa lakini waliowengi wanakubaliana nalo, wewe ukiliona haliko sawa na hukubaliani nalo, kanuni ya uwajibikaji wa pamoja inakutaka ukae kimya.

Prof. Kabudi ni mwalimu wa somo la katiba pale UDSM, amefundisha mamia ya wanafunzi, kanuni kuu ya katiba inasema Katiba ndio sheria Mama, Sheria nyingine yoyote atakayotenda kinyume cha Katiba ni Sheria batili.

Prof. Kabudi ni miongoni mwa wale ma Amicus Curiae (marafiki wa mahakama) watatu wa ile kesi ya Mtikila ambapo Mahakama Kuu ilitoa hukumu kuhusu ubatili wa Katiba yetu kunajisiwa na sheria batili ya uchaguzi inayokwenda kinyume cha Katiba.

Ushauri wao ni Mahakama isiliingilie Bunge kwenye utungaji wa sheria lakini anajua kuwa Bunge letu lilitunga sheria batili, likafanya mabadiliko batili ya katiba, likauchomekea ubatili huo ndani ya Katiba yetu kiubatili.

Mahakama Kuu ikaamuru huo ni ubatili, mabadiliko ya katiba ni batili na sheria hiyo pia ni batili, ila kwa heshima ya Bunge, kwa vile ni Bunge ndilo lililofanya ubatili huo, mahakama ya Rufani ikajizima data na kusema "the Court is not the custodians of the will of the people", yaani Mahakama sio mtunzaji wa mahitaji ya jamii, mtunzaji wa mahitaji ya jamii ni Bunge kwasababu ndilo linawawakilisha wananchi.

Mahakama ya Rufaa ikalirudisha jambo hilo la ubatili wa Katiba na Ubatili wa Sheria kwa Bunge ndilo lirekebishe. Bunge letu mpaka hivi ninavyo andika hapa, halikuwahi kuurebisha ubatili huo wa katiba na ubatili huo wa sheria, hii ina maana mpaka hii leo Tanzania tuna katiba yenye ubatili na tuna sheria batili!.

Rais Samia alipoingia akaunda kikosi kazi kuhusu katiba, watu tukaitwa kutoa maoni yetu kuhusu mustakabali mwema wa siasa za nchi yetu.

Mimi ni miongoni mwa tuliotoa maoni na mimi nilipata fursa kuzungumza mara 3.

Kitu cha ajabu sana ni serikali hii ya Rais Samia ikatunga muswada wa sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule ulioshabatilishwa na Mahakama kwa kutumia kifungu kile kile batili cha Katiba kilichochomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu!.

Bunge letu nalo lilivyo Bunge la ajabu, likaipitisha sheria hiyo hivyo hivyo ilivyo pamoja na ubatili wake, na kumpelekea Rais Samia kuisaini kuwa sheria na Rais Samia ameisha isaini sheria hiyo batili ya uchaguzi na tunayokwenda kuifanyia uchaguzi mkuu wa 2025, huku tukijiandaa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa bila uwepo wa sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa!.

Naamini uteuzi huu wa Prof. Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa sheria ni mpango wa Mungu kwa Tanzania, kumletea Rais Samia watu bold watakao mwambia ukweli kuwa Tanzania imekuwa ikilaaniwa kutokana na dhulma kubwa hii ya kupoka haki za Watanzania za kuchagua na kuchaguliwa zimeporwa na kipengele batili ndani ya katiba yetu na sheria batili.

Kiukweli pale mwanzo Prof. Kabudi alikuwa anamuogopa sana Rais Magufuli hadi kuteleza ulimi kumuita mungu!, na yeye kujiita ameokotwa Jalalani.

Swali sasa ni je this time around atakuwa mkweli toka ndani ya nafsi yake?. Atamweleza Rais Samia kuhusu ubatili wa Katiba yetu na sheria yetu mpya ya uchaguzi ambayo Rais Samia ameisani hivi majuzi?, au atajizima tena data kama alivyojizima enzi za JPM?

Time will tell.

Mungu Mbariki Prof. Kabudi kusimama kwenye kweli.

Mungu Mbariki Rais Samia kukubali kuambiwa ukweli wa ubatili wa Katiba na Sheria na kuufanyia kazi

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali.
Kaka ninachojua ukishateuliwa na ccm wanakung'oa ubongo unabaki na kichwa empty, hapo ni mapimbio
 
Hii tabia ya kusifia GPA kali binafsi imepitwa na wakati sana...dunia inaenda kasi sana. Uwezo wa akili upimwa kwa namna mtu anatumia akili na taaluma yake kusaidia jamii yake na kuleta maendeleo..
Kuna watu wanauwezo mkubwa wa kukariri, kutafakari waliyoambiwa darasani, kuunganisha dota za kinadharia kujibu mtihani na kufaulu..lkn kwenye practicality na transformation ya knowledge kwa ajili ya faida ya wengi hawana msaada.
Hawa wakina Kabudi kama kweli they are bright wanapaswa kuwa na open mindedness na uthubutu wa kuongelea katiba yetu kwa manufaa ya wote....kama hayo hayafanyiki ni mara elfu mkulima wa darasa la saba, aliajiri watu 50, anayelipa kodi serikalini na hiyo inanunua dawa na kujenga miundo mbinu..
Kunywa juice baridi nitalipa
 
Pamoja na sifa nyiiiingi ulizomuwekea kwenye title ya uzi wako, ni ndoto tu za kawaida za kibongo kuamini eti zamu hii atafanya hayo uliyosema. Hajawahi kuwa na impact huko nyuma leo ndo kawa mpya? Kwani anashika hizi nafasi mara ya kwanza? Why wakili msomi unaamini leo kawa na hizo sifa? Anyway maisha ni hayahaya ya kibongo kila mtu anatafuta mshahara tu, kwetu sisi uteuzi maana yake ni promotion na impact yake ni more personal income na access to rushwa kubwa zaidi!
 
Kabudi aanze kushughulikia mkataba wa kihuni wa dp world na kukomboa makinikia yetu ambayo Kwa Sasa wazungu wanajichotea tu watakavyo kupeleka kwao na kujipatia faida nyingi zaidi
 
Huyo karudishwa hapo apambane na madudu yake aliyoyafanya kwa kuvunja mikataba na kuleta sheria za kijinga yeye na mwendazake. Maana kila alipoulizwa alisingizia wanaoshughulikia hizi kesi hawana uwezo.

Mama Samia akaona isiwe tabu, wewe si ndiye mwenye uwezo nazo na ni madudu yako. Njoo upambane nayo.

Tumuombee mema tu, lakini ana zigo kubwa alilojiundia mwenyewe kwa ujinga wake wa kujipendekeza tu.

Adui wa Tanzania ni ujinga.
 
Kaka ninachojua ukishateuliwa na ccm wanakung'oa ubongo unabaki na kichwa empty, hapo ni mapimbio
Hapana aise at least ukiwa na smart brain kwenye cabinet,itakuongoza kuona kwa jicho la tatu,kuliko hao akina Nape na makamba,hii panga pangua Haina afya,aangalie na nje y CCM,pia na Kuna wanataaluma Bora Sana,angazia jicho huko mheshimiwa Raisi ,ebu ona wafuatao waliibuliwaje na MAGUFULI:- ashatu kijaji,abdallah posi,bashiru,ukiondoa pole pole yeye Alikuwa mwanasiasa,wakina sagini nk,Kuna watu wako fresh Sana,Ila hawajajipambanua tu kutokana na kukwepa matope ya kuchafuana kisiasa
 
Wanabodi
Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za Kwa Maslahi ya Taifa, zinazo zungumzia jambo lolote la kisiasa, kiuchumi au kijamii kwa mtindo wa swali halafu jibu utatoa wewe mwenyewe .

Mada ya leo ni pongezi na shukrani kwa Rais Samia kumteua tena Prof. Palamagamba John, Aidan Mwaluko Kabudi, kuwa waziri wetu wa Sheria.

Kwa maoni yangu binafsi, ulimuondoa Prof. Shivji , Prof. Chris Peter Maina, na Prof. Gamalieli Mgongo Fimbo kwenye unguii wa katiba, anayefuata ni Prof. Kabudi, ila tukija kwenye overall the best of the best, Prof. Palamagamba Kabudi is the best, amewapita wote on several avenues.

Prof Kabudi is one of the best brains this country has and has ever had. The best brain inapimwa kwa IQ test. Sisi Tanzania hatuna amplitude test za kupima IQ za watu wetu, tunatumia matokeo ya mitihani ya kidato cha 4, 6 na GPA za chuo kikuu.

Soma Pia: Kwa uteuzi wa Prof. Kabudi katiba na sheria tukubaliane tu Mwambukusi atanyoosha mikono kama ilivyokuwa kwa Lissu na kudhibitiwa

Japo sijui scores za Prof. Kabudi za form 4 na form 6,
ni division 1 ya points ngapi, ila enzi zile kusoma sheria ilikuwa ni lazima uwe na division 1 kali.

Kwenye nchi za Afrika Mashariki, chuo kikuu cha kwanza kufundisha sheria ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kilichoanzishwa October 1961, siku chache kabla ya uhuru wa Tanganyika na kilichukua wanafunzi kutoka nchi zote tatu za Afrika Mashariki, Tanzania, Kenya na Uganda.

Na mimi pia nilisomea sheria yangu LL.B chuo kikuu cha Dar es Salaam na kupita mikononi mwa Prof. Palamagamba Kabudi, sio tuu kama mwalimu wangu bali yeye ndiye alikuwa supervisor wangu wa my LL.B dissertation, hivyo ni mtu ninayemfahamu kwa karibu.

Wakati nikiwa mikononi mwake mpaka ninamaliza UDSM kuna vitu sikuvifahamu kumhusu Prof. Kabudi, ila mwaka 2011 wakati chuo kikuu cha Dar es Salaam kinaadhimisha Diamond Jubilee, Prof. Palamagamba Kabudi alitunukiwa tuzo ya outstanding GPA, kwa muda wote wa miaka 50 ya chuo kikuu cha Dar es Salaam, recoding ya GPA ya Prof. Kabudi, ya 4.9 haukuwahi kuvunjwa mpaka wakati huo, na sikuwahi kusikia kama kuna Mwanafunzi mwingine yeyote amewahi kuifikia, hivyo kuna uwezekano Prof. Kabudi ni one of the best brains of the best that we have!.

Nimesema one of, kwasababu kuna uwezekano tuna best brains kuliko Prof. Kabudi lakini hawakwenda shule hivyo hawajulikani lakini kuna watu wanafanya mambo makubwa kimya kimya, na kuna Watanzania wengi brains wanaosoma ughaibuni, huwa hawarejei nchini, Wazungu wanawashika.

Kitu kingine cha ziada kumhusu Prof. Kabudi, ni multi talented, ana kipaji cha usimulizi, oratorio talent, ana kipaji cha kupiga kinanda na ni mcha Mungu aliyelelewa kwenye uchamungu.

Hii sio mara ya kwanza kwa Prof. Kabudi kuteuliwa Waziri, aliteteuliwa na Magufuli kwenye serikali ya awamu ya 5, Rais Samia akamuondoa, sasa ni Samia amemteua tena Wizara ile ile ya sheria.

Mtu kuwa the best brain, high IQ na bingwa wa Katiba ni jambo moja, na uelewa wa katiba, na utekelezaji wa majukumu yake kiweledi ni jambo jingine.

Serikali inafanya kazi kwa mtindo wa uwajibikaji wa pamoja, a collective responsibility hata kama jambo fulani haliko sawa lakini waliowengi wanakubaliana nalo, wewe ukiliona haliko sawa na hukubaliani nalo, kanuni ya uwajibikaji wa pamoja inakutaka ukae kimya.

Prof. Kabudi ni mwalimu wa somo la katiba pale UDSM, amefundisha mamia ya wanafunzi, kanuni kuu ya katiba inasema Katiba ndio sheria Mama, Sheria nyingine yoyote atakayotenda kinyume cha Katiba ni Sheria batili.

Prof. Kabudi ni miongoni mwa wale ma Amicus Curiae (marafiki wa mahakama) watatu wa ile kesi ya Mtikila ambapo Mahakama Kuu ilitoa hukumu kuhusu ubatili wa Katiba yetu kunajisiwa na sheria batili ya uchaguzi inayokwenda kinyume cha Katiba.

Ushauri wao ni Mahakama isiliingilie Bunge kwenye utungaji wa sheria lakini anajua kuwa Bunge letu lilitunga sheria batili, likafanya mabadiliko batili ya katiba, likauchomekea ubatili huo ndani ya Katiba yetu kiubatili.

Mahakama Kuu ikaamuru huo ni ubatili, mabadiliko ya katiba ni batili na sheria hiyo pia ni batili, ila kwa heshima ya Bunge, kwa vile ni Bunge ndilo lililofanya ubatili huo, mahakama ya Rufani ikajizima data na kusema "the Court is not the custodians of the will of the people", yaani Mahakama sio mtunzaji wa mahitaji ya jamii, mtunzaji wa mahitaji ya jamii ni Bunge kwasababu ndilo linawawakilisha wananchi.

Mahakama ya Rufaa ikalirudisha jambo hilo la ubatili wa Katiba na Ubatili wa Sheria kwa Bunge ndilo lirekebishe. Bunge letu mpaka hivi ninavyo andika hapa, halikuwahi kuurebisha ubatili huo wa katiba na ubatili huo wa sheria, hii ina maana mpaka hii leo Tanzania tuna katiba yenye ubatili na tuna sheria batili!.

Rais Samia alipoingia akaunda kikosi kazi kuhusu katiba, watu tukaitwa kutoa maoni yetu kuhusu mustakabali mwema wa siasa za nchi yetu.

Mimi ni miongoni mwa tuliotoa maoni na mimi nilipata fursa kuzungumza mara 3.

Kitu cha ajabu sana ni serikali hii ya Rais Samia ikatunga muswada wa sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule ulioshabatilishwa na Mahakama kwa kutumia kifungu kile kile batili cha Katiba kilichochomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu!.

Bunge letu nalo lilivyo Bunge la ajabu, likaipitisha sheria hiyo hivyo hivyo ilivyo pamoja na ubatili wake, na kumpelekea Rais Samia kuisaini kuwa sheria na Rais Samia ameisha isaini sheria hiyo batili ya uchaguzi na tunayokwenda kuifanyia uchaguzi mkuu wa 2025, huku tukijiandaa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa bila uwepo wa sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa!.

Naamini uteuzi huu wa Prof. Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa sheria ni mpango wa Mungu kwa Tanzania, kumletea Rais Samia watu bold watakao mwambia ukweli kuwa Tanzania imekuwa ikilaaniwa kutokana na dhulma kubwa hii ya kupoka haki za Watanzania za kuchagua na kuchaguliwa zimeporwa na kipengele batili ndani ya katiba yetu na sheria batili.

Kiukweli pale mwanzo Prof. Kabudi alikuwa anamuogopa sana Rais Magufuli hadi kuteleza ulimi kumuita mungu!, na yeye kujiita ameokotwa Jalalani.

Swali sasa ni je this time around atakuwa mkweli toka ndani ya nafsi yake?. Atamweleza Rais Samia kuhusu ubatili wa Katiba yetu na sheria yetu mpya ya uchaguzi ambayo Rais Samia ameisani hivi majuzi?, au atajizima tena data kama alivyojizima enzi za JPM?

Time will tell.

Mungu Mbariki Prof. Kabudi kusimama kwenye kweli.

Mungu Mbariki Rais Samia kukubali kuambiwa ukweli wa ubatili wa Katiba na Sheria na kuufanyia kazi

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali.
Huyo Chawa Mzee jamii ilishampuuza, uchawa unafaa watu wa kariba ya Baba Revo na Stive Nyerere siyo Profesa mzima unazidisha uchawa hadi binadamu unamuita Mungu.

Zee la hovyo kabisa huyu Kabudi, watu wa Kilosa wa ccm na vyama vingine wajipange kumpumzisha ubunge huyu chawa.
 
Huyo karudishwa hapo apambane na madudu yake aliyoyafanya kwa kuvunja mikataba na kuleta sheria za kijinga yeye na mwendazake. Maana kila alipoulizwa alisingizia wanaoshughulikia hizi kesi hawana uwezo.

Mama Samia akaona isiwe tabu, wewe si ndiye mwenye uwezo nazo na ni madudu yako. Njoo upambane nayo.

Tumuombee mema tu, lakini ana zigo kubwa alilojiundia mwenyewe kwa ujinga wake wa kujipendekeza tu.

Adui wa Tanzania ni ujinga.
Hapa nakubaliana na wewe, hili zaa lilivyo jinga eti linatupiga kamba alivyokwenda UN New York katibu mkuu wa UN alikuwa anaangaika kumtafuta yeye ili waonane.

Yani Magufuli aliharibu akili za wasomi wengi wakageuka vituko, mara dawa hii kule Madagascar anaigawa Rais mwenyewe uku mijicho kama gong'ole imemtoka.
 
Katika machawa wa hovyo miongoni mwa wale tunaoamini ni wasomi nguli ni huyu Profesa Kabudi!

Hafai kwa uchawa wake,!
Watanzania tuna vichwa vya mende
Kesi zote za kimataifa tulizo funguliwa mhusika mkuu ni huyu Kabudi, pro. Alie diriki kusema kaokotaa jalalani1. Prof alie thubutu kumuita mtu Mungu. Usitegemee jipya kwa huyu mzee wa kusifu na kuabudu wanadamu
 
Mkuu haya mambo ya kusifia ujinga yanakushushia hadhi yako bila wewe kujua. Ni bora ukakaa kimya kuliko husifia ujinga. Watu wenye akili na wanaokujua wanakushangaa sana japo hawakuambii ukweli kuwa unapotea. Mfano mzuri angalia heshima ya Kabudi ilivyoshuka baada ya kujivua akili mpaka kusema ametokea jalalani, mwishowe akamuita Jiwe kuwa ni Mungu. Jiulize hadhi ya Kabudi kwa sasa ni sawa na ile hadhi yake kabla ya Jiwe regime?
umesoma mpaka mwisho masta chief?
 
Back
Top Bottom