Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapo umechukua uhalisia wa neno, lakini katika kiswahili neno hili linatumika kama salamu, tazama mfano mwingine:
mambo: haina maana ya salamu lakini watu wanatumia kama salamu.
upo hapo?
Iko hivi. Kwa waliosoma historia ya waarabu enzi za utumwa watakuwa wanaelwa maana ya shkamoo.
Shikamoo ni neno la kiarabu lenye maana ya nipo chini ya miguu yako. Na lilitumiwa hasa na wafungwa ambao walikuwa wakilitumia kuwasalimia waarabu(Wakoloni wao).
Na Marahaba maana yake ni 'Ninakubali' likimaanisha amekubali salaam yake.
Kwa Hivyo: Kila lugha inakopa baadhi ya maneno kutoka lugha nyingine ili kukamilika, kwa hiyo hata kiswahili kilikopa baadhi ya maneno ya kiarabu na kutoka lugha nyingine za kibantu.
Ni hayo tu.
MwanaFalsafa1,
Kila kitu ulichoandika hapo juu umepatia. Ni neno la kitumwa kweli lakini ndio hivyo mababu zetu kwa kupenda umwinyi wakaliendeleza tu. Mara nyingi mimi huwa nalikuwepa neno hilo kwa kutumia "asalam aleykum".
Ukimsalimia mtu aliyekuzidi umri "habari yako "ni kukosa heshima?
Kwa nilivyosikia mimi neno shikamoo maana yake ni "niko chini ya miguu yako.
Pia nimesikia hilo neno ni la kitumwa na lilikuwa linatumiwa na watumwa kuwaonyesha heshima wakuu wao.
Kuna baadhi ya watu nawajua hawapendi kupewa shikamoo na hata wakipewa hawajibu marahaba.
Je kama hili neno ni la kitumwa, kwanini sisi tuendelee kulitumia kama neno linaloashiria heshima?
Kama lilitumika kuwakandamiza mababu zetu kwanini na sisi tulipe nafasi? Au tunalitumia kama wenzetu Wamarekani weusi wanavyo tumia neno "nigga" ambalo lilitumika kudharau mababu zao na kulifanya la kwetu sasa?
Habari,
Nashangaa watu Tanzania peke yake hutumia neno shikamo kama salamu ya kumtunikia mtu heshima ilhali ni utumwa wa kisaikolojia, shikamo ni neno la kiharabu humaanisha nipo chini ya miguu yako.
Huu ni ujinga uliopitiliza hata mataifa yote hamna kitu kama hichi, kwanza hata tafsiri yake hakuna iwe kwa lugha yeyote duniani na kingine uende dukani useme eti naomba hahaha hii nchi ni vichekesho unaomba huku unatoa sarafu.
Ndio maana hata mkiambiwa laleni hakuna kufanya lolote mnafanya kweli ujinga mwalimu aliukemea nyie mkaukumbatia.
Toa salamu mbadala hapa basi