Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

Habari wana JF,

Kuna hii salamu inayotumika sana na watu wengi wa kila kabila hapa nchini na hata nje ya nchi ya ''SHIKAMOO''halafu jibu lake likiwa ni''MARA HABA''.

Mimi niliwahi kuambiwa na mwalimu wangu wa HISTORY kuwa SHIKAMOO, M.Ynipo chini ya miguu yako, sasa kama ni hivyo, je watu wanaielewa kweli maana hiyo?

Salamu hii ninachojua mimi hutumika kuashiria heshima kwa mtu anayekuzidi umri, lakini huwa ninashangaa baadhi ya maeneo unakuta Mtu mkubwa eti anamsalimia mdogo SHIKAMOO, na siyo kwamba hajui kama amemzidi umri, la hasha! anakuwa anajua bali hufanya hivyo kutokana na kipato alichonacho yule mdogo kwamba japo ni mdogo lakini utajiri wake hufanya watu wakubwa zaidi yake kumpa SHIKAMOO, Je hii ni sawa?

Karibuni kwa maoni..
 
Kama kamzidi pesa ila umri Mdogo kutokana na Maelezo yako ni kuwa yupo chini ya miguu yake kipesa sio umri...by the way its meaningless unaweza ukaamkiwa shkamoo na usiweze kuakisi huo ukubwa kutokana na matendo au jinsi unavojiweka katika jamii
 
Kwanza maana yake sio niko CHINI ya miguu yako, BALI nakushika miguu yako, SHIKAMOO, NA- SHIKA- MOO, moo ni miguu,,
 
Kama kamzidi pesa ila umri Mdogo kutokana na Maelezo yako ni kuwa yupo chini ya miguu yake kipesa sio umri...by the way its meaningless unaweza ukaamkiwa shkamoo na usiweze kuakisi huo ukubwa kutokana na matendo au jinsi unavojiweka katika jamii

kwa hiyo unapingana na tafsiri ya mwalimu wangu????.
 
Ninavyojua jua Mimi, MTU mzima anapomwamkia mtu Mdogo shikamoo ile ni Kwa ajili ya kitu chake au cheo chake au nafasi yake katika jamii inayomzunguka.

Eeeeeewaaaah! wewe nimekuelewa sasa,tunaenda sawa.Lakini wewe ukisalimiwa na mtu anayekuzidi utamwambia MARAHABA???.
 
Unaweza kuwa upo sawa lakini kuna uharibifu wa lugha unaingilia hapo, unapoleta taarifa ya chini ya miguu yako watu wanakwenda kwenye uelewa tofauti..
 
Hiyo ni salamu ya kitumwa ambayo ilikuwa inatumika wakati wa utumwa,mtumwa alipaswa siku zote kutambua kuwa kuna aliyekuwa na mamlaka makubwa juu yake na anapaswa kumsujudia na kuonyesha kwa vitendo utayali wa kumtumikia muungwana wake.Hii salamu imedumu kwa miaka mingi sana hasa ukanda wote wa pwani ya nchi zetu zilizopita katika kipindi cha utumwa wa kiarabu, na imeendelea kutumika hivyo kwa mazoea tu bila hata kutafakari maana na matumizi yake hadi siku ya leo.
 
Salamu ya shikamoo haiji kuchuja wala kupotea kwa sababu ndio utamaduni tuliokuwa nao na tumeukuta.

Mfano mtoto hawezi kusema naomba si kumi bila kuanza na "sikamoo"

mambo mengine hayajadiliki, ila naona hili neno kwangu limebaki kwa watu ninaowafahamu tu.

SIO UNALISALIMIA LIMAMA ALAFU LINAKUKAUSHIA
 
Back
Top Bottom