Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

Mkuu ulivyosema ni sawa,nami nilijaribu sana kufuatilia asili ya salaam hii,ufafanuzi niliopewa niliuamini kwani maswali yangu yalikuwa kama shikamoo ni salaam,kwa nini jibu lake liwe marahaba?

Jibu nililopewa ni kwamba:

Watumwa walikuwa wakikamatwa na wake zao wanafungwa minyororo na kuwekwa kwenye msafara wakibebeshwa mizigo. Aliyekuwa akionyesha kuchoka na kudhoofu na kushindwa kuendelea na safari aliuawa kwa upanga na wengine waliendelea.

Sasa ilipotokea hivyo kwa mke wa mtu,mwenye mke au ndugu wa mhanga akataka kupigana walimtishia naye kumuua na ili ajisalimishe alisema shikamoo yaani niko chini ya miguu yako na alijibiwa mara-haba,ikiwa na maana kwamba usizoee hii tabia maana msamaha kama huu unatokea mara haba.

Ki ukweli baada ya kupewa ufafanuzi huu niliichukia hii salaam,Lkn cha kujikumbusha ni kwamba mashuleni tunajifunza somo la historia,ambalo kwa kweli linatukumbusha machungu waliyoyafanya wakoloni lkn mpaka leo halijafutwa somo hili.

Hivyo na hii salaam inabidi tuizoee kwamba haina tena maana kama ile ya zamani bali ni tendo la kuonyesha heshima ya mdogo kwa mkubwa aliyemzidi na si vinginevyo.
 
Wakuu, napenda kuelezea kidogo kuhusu hili neno Shikamoo, ambalo karibu kila Mtanzania anapokutana na mtu alie mzidi umri akitaka kumjulia hali utaskia shkamoo Mzee, mama, n.k.

Neno hili huwa linatumika kwa maana ya salam yani kumjulia mtu hali, wakati linamaana nyingine tofautikabisa, Kimsingi salami hii tafsiriyake haina maana ya kumjulia mtu hali, nitofauti kabisa na salam zingine zenye Maneno kama habari za asubuhi, umeamkaje, umeshindaje n.k.

Hata katika salamu za kilugha huwezi kukuta neno ambalo tafsiri yake ni salam kwa maana ya kujuliana hali lenye maana au tafsiri sawa na shikamoo. Kwa mfano wanyakyusa asubuhi mtoto atamwambia mzazi wake "twalubhunju" maana yake habari za asubuhi, Badala ya shikamoo ambayo maana yake ni kusema "NIKO 'CHINI YA MIGUU YAKO'.

Kama kuna tafsiri nyingine ya shkamoo iwekwe hapa tuione.
 
Ndio salam kwa mtu mkubwa kuwa uko chini ya miguu yake au unamtukuza kwa heshima, na baada ya hapo inafuatia kujuana hali kama vile 'habari zenu' au 'hamjambo'
 
Katika lugha kuna mambo mawili,maana na tafsiri...kama shikamoo tafsiri yake ni nakushika miguu,basi maana yake itakuwa kumwambia mtu aliyekuzidi umri-Heshima yako.
 
ndo hivyo nipo chini ya miguu yako, ila ndo tunaamini salamu kwa mtu aliyekuzidi
 
Huwa majiuliza swali moja, kwa nini kiswahili tu ndio lugha yenye salam kama hii na si lugha zingine za kibantu na hata lugha zingine za ng'ambo kama kiingereza, kiarabu, kifaransa nk. pia hazina salam kama hii?
 
Sikamoo-nakushika miguu
Marhaba-asante.

Cheichei jee? Mwenye kujua maana yake atujuze
Ahsante bi-AN,

haya yote ni ufunguzi wa mawasiliano

maana ya Chei chei ni :- Shiy-shiy (kitu,kitu?)

Shikamoo ni Adabu/Heshima kutoka kwa mdogo kumfikia mkubwa:- yaani nipo chini ya miguu yako !!
( chifu alikubali kutukuzwa salam kutoka kwa watu wake )

Lakini wapo wengine husalimiana kwa miguno, au vijisauti kadhaa!!
mshana jr Katavi mville jr mnyama k
 
Last edited by a moderator:
Iko hivi. Kwa waliosoma historia ya waarabu enzi za utumwa watakuwa wanaelwa maana ya shkamoo.

Shikamoo ni neno la kiarabu lenye maana ya nipo chini ya miguu yako. Na lilitumiwa hasa na wafungwa ambao walikuwa wakilitumia kuwasalimia waarabu(Wakoloni wao).

Na Marahaba maana yake ni 'Ninakubali' likimaanisha amekubali salaam yake.

Kwa Hivyo: Kila lugha inakopa baadhi ya maneno kutoka lugha nyingine ili kukamilika, kwa hiyo hata kiswahili kilikopa baadhi ya maneno ya kiarabu na kutoka lugha nyingine za kibantu.

Ni hayo tu.
 
Iko hivi. Kwa waliosoma historia ya waarabu enzi za utumwa watakuwa wanaelwa maana ya shkamoo.

Shikamoo ni neno la kiarabu lenye maana ya nipo chini ya miguu yako. Na lilitumiwa hasa na wafungwa ambao walikuwa wakilitumia kuwasalimia waarabu(Wakoloni wao).

Na Marahaba maana yake ni 'Ninakubali' likimaanisha amekubali salaam yake.

Kwa Hivyo: Kila lugha inakopa baadhi ya maneno kutoka lugha nyingine ili kukamilika, kwa hiyo hata kiswahili kilikopa baadhi ya maneno ya kiarabu na kutoka lugha nyingine za kibantu.

Ni hayo tu.
Ahsante kwa ufafanuzi mzuri....,FYI, Kiswahili hakikukopa tuu ktk lugha ya kiarabu, ila kimenyakuwa asilimia kubwa na pia kujinasibu ndani ya lugha ya kuu ya kiarabu na hadi sasa misemiati mipya hutokana kwenye lugha ya kiarabu.
 
Ahsante bi-AN,

haya yote ni ufunguzi wa mawasiliano

maana ya Chei chei ni :- Shiy-shiy (kitu,kitu?)

Shikamoo ni Adabu/Heshima kutoka kwa mdogo kumfikia mkubwa:- yaani nipo chini ya miguu yako !!
( chifu alikubali kutukuzwa salam kutoka kwa watu wake )

Lakini wapo wengine husalimiana kwa miguno, au vijisauti kadhaa!!
mshana jr Katavi mville jr mnyama k
Hapo kwenye chei chei bado sijakupata vizuri
 
Sikamoo-nakushika miguu
Marhaba-asante.

Cheichei jee? Mwenye kujua maana yake atujuze

مرحبا، مرحبتين
، marhaba marhabteyn,
Kumbe mpaka salamu tumecopy kwa jamaa
 
Back
Top Bottom