Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

Naunga mkono hoja 100%.
Duniani kwingineko, watu hawasalimiani kwa kuulizana maswali (eg Habari za asb ???) ambapo jibu lake huwa ni la uongo (Nzuri).

Au mtu mmoja kujishusha kwa mwingine (shikamoo - marahaba) ambayo hujenga akili za utumwa.

Wenzetu husalimiana kwa kutakiana kheri tu (Good morning) na jibu lake huwa nawe pia.
Na matokeo yake watu hao wanakuwa na kheri.

http://sw.m.wikipedia.org/wiki/Shikamoo
 
Mimi nafikiri tutumie tu kwasababu likipitwa na wakati litafutika! Kumbuka tulikuwa tunatumia neno NDUGU miaka ile ya Mwalimu lakini hivi sasa halitumiki mara nyingi.
 
Hebu dadavua kidogo lugha yangu!
Kwamka mbee kanyi? maana yake Umeamakaje mzee wangu?

Jibu lake! Nashicha pyu Maana yake Ni salama kabisa..

Hiyo shikamoo binafsi siifagilii sana kutokana imebeba utumwa ndani yake
 
tabia ni kama ngozi, kuibadili ni ngumu sana ndivyo nionavyo ugumu wa kubadili salamu ambayo kwa miaka zaidi ya 50 tumekuwa tukiitumia
 
Napingana na wewe kwenye hili Aweda.

Kumbuka Matumizi ya Lugha yanaendana na Mazingira, Maana na wakati, Mazingira ya Enzi hizo si ya sasa, na Maana iliyokuwa imekusudiwa kipindi hicho si maana sasa, kwa hiyo tuedelee kuitumia.
 
mi naona hakuna tatizo nikimwamkia shikamoo mama au baba (nashika miguu yako ) nao wakijibu shika mara saba ok wanastahili tatizo liko kwa wale wazee wa dot.com ukiwaamkia wanazuga au kuuchuna kabisaa
 
ndugu yangu Fundisi c kweli kuwa watalii wanafundishwa salamu iyo ,ila wanafundishwa kusema -jambo, karibu, hakuna matata, asante (sana) ni maneno ambayo n common na yana tafsiri yake . shikamoo & marahaba haina tafsiri kwa mgeni
 
tabia ni kama ngozi, kuibadili ni ngumu sana ndivyo nionavyo ugumu wa kubadili salamu ambayo kwa miaka zaidi ya 50 tumekuwa tukiitumia

aaaa wapi ngozi siku hizi zinabadilishwa
 
Mimi Kamwe siitumii hii salamu kamwe. Niliacha kuitumia nilipomaliza Form IV. Mwanzoni wakati naoa Wakwe zangu walinishangaa sana, Walidhani sina Adabu lakini sasa wameshanizoea.
 
Basi tutafute salaam ingine yenye kuleta heshima....
 
wabongo wanavyopenda kunyenyekewa hii salamu lazima iwepo milele
 
Mimi mpenzi wangu tu ndio huwa ananiamkia na tena nikimkoleza tu.Inafaa shikamoo iwe kwa wanawake tu tena kwa mabwana zao wanaowalalia tu.Sio dume zima lina ndevu kama beberu eti linabana pua "SHIKAMOOOO" .Ni salamu ya kishoga kabisa hii.
 
SHIKAMOO - MARAHABA SHIKAMOO MARAHABA.

Shikamoo ilikuwa ni salamu za watumwa kwa mabwana zao.
je, sisi watanzania tuna sababu ya kuendelea kutumia salamu hii yenye historia mbaya? Aulizaye anataka kujua na ni jambo jema, naombeni msaada wenu.
Mkuu Shemeji Aweda, asante kuliulizia hili!, lugha inazaliwa, inakuwa na mwishowe inakufa!, lugha nyingi za kale saa hizi ni marehemu na lugha mpya za kisasa zinaibuka!.

Kukua kwa lugha kunatokana na kuingia kwa maneno mapya kila uchao, na huku maneno ya zamani yakitoweka.

Hata kama shikamoo kwa lugha ya Kiarabu ilimaanisha hivyo, kwa Lugha ya Kiswahili ni neno la heshima kwa mdogo kwenda kwa mkubwa, hivyo lina positive canotation meaning ya heshima, halina sababu ya kufutwa kwa sababu kwa sasa Shikamoo ni salaam ya heshima kwa lugha ya Kiswahili na sio ile ya kitumwa ya Kiarabu!.

Neno likiwa na positive canotation meaning, linapaswa kuendelea kutumika kwa positivity ya canotation meaning yake!. Vivyo hivyo lugha ya Kiswahili imeundwa kwa maneno ya kukopa kutoka lugha mbalimbali zikiwemo lugha za Kibantu, mfano neno "nina", "mae", "mayo" na "nyoko" maana yake ni mama kwa lugha za Kibantu, kufuatia mtindo wa kumtukania mtu mama yake, kwa kukitaja kile kiungo cha "K" na linafuatia jina la "K... mama yako", "K... mae", "K...nyoko", "K... nina", tusi ni ile "K" linalofuatia ni jina la mama!. Kufuatia bad canotation meaning ya tusi hilo, sasa imefikia hata mtu akisema neno "nyoko", linatafrisiwa kama tusi, wakati kihalali kabisa "nyoko" ni "mama!".

Shikamoo iendelee kwa sana, tena zaidi ya heshima, pia siku hizi shikamoo hutumiwa na wadada kama kinga, ili ile mibaba inayopenda dogo dogo, ikiisha amkiwa tuu shikamoo, hapo binti anakuwa ameweka kinga libaba lisimtokee!, na hata akitokea mtu ni size yako kabisa tena halali yako, akikuamkia shikamoo ujue sio heshima tena bali ni kinga kukuzuia us advance!.

Mimi nikikutana na hizi "shikamoo za kunyimana" huwa siziitikii "marahaba" bali naitikia "poa", ili nikiamua nisikutane na kizingiti cha "shikamoo!".

Thanks.

Pasco.
 
mleta mada ungetujuza hii tafsiri ya kushika miguu ni katika lugha gani.maana huu si msamiati au naau. jina ni jina tu mradi jamii inatambua na kuelewa. ukimwuliza yeyote na hata wewe ulivyofundishwa darasani je uliwahi kufundishwa tafsiri hiyo?kama sivyo kwa kila mtu basi maana imeshabadilika na jamii haina matatizona hilo.endelea kuamkia ndugu hakunaga shida
 
Personally hii salamu siipendi ata kusikia!
Mabwana vs Watwana
 
Back
Top Bottom