Asilimia 60 chali matokeo ya kidato cha nne

Asilimia 60 chali matokeo ya kidato cha nne

Kusema kweli mimi nilifanya kazi nyingi ktk wilaya za mkoa wa Pwani (sijui upande wa Zbar) kwa zaidi ya miaka 6 sasa. Na nilifanya kazi na walimu na wanafunzi wa shule za misingi na sekondary.

Sishangai na matokeo haya kwa upande wa mkoa wa Pwani kwa sababu wanafunzi wengi sana kuanzia kidato cha pili wanaanza kufikiri kuolewa kuliko kuendelea na shule. Hii pia inatokana na utamaduni wa kucheza watoto wa kike /kumtoa mwali (mkoleni) ambao kisaikolojia unamfanya afikirie masuala ya Ndoa kuliko Shule baada ya kutolewa mwali.

Niliwahi kufanya kazi na Diwani mmoja msomi kidogo mzaliwa na wa Pwani (mzaramo) akawa anapinga ngoma hizi za asili kwa hoja kwamba inaharibu watoto wa kike. Matokeo ya msimamo wa Diwani huyo kuangushwa ktk hatua za kura ya maoni ya chama chake 2010.

Japokuwa ukizungumzo na watu wazima wanapinga kwamba wanahamasisha tabia mbaya kwa watoto wao lakini ukweli utabaki pale pale kwamba Mkoleni au kutoa mwali ni utamaduni unaohitaji kubadilishwa ili kuboresha mfumo wa Elimu. Watoto wa kike baada ya kutolewa mwali matokeo yao yanabadilika darasani na hili hata waalimu wanashuhudia kabisa. Matokeo yake sasa naona hata waalimu wanaanza kukata tamaa.

Sikubaliani na madai ya hujuma ktk baraza la mitihani kama alivyodokeza mleta mada.

Hivi hao 7% waliopata div 1-3 tanzania nzima ni wa kutoka mikoa ipi? Kuna tatizo kubwa sana na lazima lijadiliwe kwa kina na sio kutupia mikoa fulani.
Mtu yeyote anayetoka na kushangilia kuwa waislam ndio waliofeli kwa hii 7% ya div 1-3 huenda amefungwa na kiakili.
 
tatizo tunachanganya uislamu na uswahili, mtakumbuka kuwa hata university ya kwanza duniani ilikuwa cairo, waislamu hawako nyuma kielimu, ila bahati mbaya uislamu wa TANZANIA UMEJIKUTA UKO MAENEO YA USWAHILI! TOFAUTISHA USWAHILI NA UISLAMU
 
Katika matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne, yaliyotangazwa na Baraza la Mtihani NECTA!! yanaonyesha kuwa shule hizi kumi ndizo zinazo vuta Mkia!

(1) MIBUYUNI, ya ZANZIBAR, (2)NDAME YA UNGUJA (3)NAMNDIMKONGO YA PWANI. (4)CHITETEKETE YA MTWARA. (5)MAENDELEO YA DAR. (6)KWA MNDOLWA TANGA. (7)UNGULU MOROGORO. (8)KIKALE YA PWANI. (9)MKUMBO YA TANGA. (10)TANGONI TANGA!

Nacho jiuliza je ni kwanini shule hizi ndizo zimekuwa za Mwishoni, je ni kwa ajili ya kwamba watu wengi wa Mikoa hii,huthamini zaidi wanachokiita ELIMU AKHERA, na sio ELIMU DUNIA? ,Au baraza la Mitihani taifa NECTA wamehujumu hizi shule?

NB :
Mikoa hii ndio Ngome za Ccm,na kwamba watu wa mikoa hii bado hawana uelewa wa kutosha na ndio,maana Mkoa kama Tanga Pwani na Morogoro, hazijawahi kuchagua Mbunge wa Upinzani, tangia kuanzishwa kwa Mfumo wa vyama Vingi 1992!


Jando na unyago

mix with yours
 
wachawi wao, magaidi wao, chuki wao, kubebwa wabebwe wao serikalini ila mtu kama huna akili huna. tuwekeeni cv ya sheikh wao hata moja tuone, kitu madrasa kuzaliwa hadi kufa.
 
leo tmu aliesoma katika shule izo ndo amekuwa raisi wa nchi. afu tunajiuliza kwanini hatuendelei.
 
kusoma hizi zaidi..........right to left

flicker-arabic_alphabet.jpg

mkuu umegraduate mwaka gani madrassa!!!!!!!!!!!???
 
Ulitaka mikoa gani wafeli?
Actually, sipendi watoto wafeli! Lakini kwa kuwa tayari Maji yalishamwagika (Walishafeli),basi ningependa wote Waliofeli wangetoka Mikoa yote ambayo bado Wanawaunga Mkoloni Mweusi [Ccm],Mkono kundelea Kutuburuza!! Lakini tukiwaambia hawaelewi bado wanasema Kidumu Chama chama Mapinduzi!!
Naamini muda sio mrefu,watajua kwanini tunawaambia CCM,ni JANGA LA TAIFA, na kuendelea kuwachagua ni kuendelea Kujichimbia KABURI!

MUNGU IBARIKI TANZANIA!!!!
MUNGU IBARIKI CHADEMA!!!!
 
S1930 J. M. KIKWETE SECONDARY SCHOOL
[h=3]DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 0 DIV-IV = 17 FLD = 110[/h][h=3][/h]S1884 PIUS MSEKWA SECONDARY SCHOOL
[h=3]DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 2 DIV-IV = 21 FLD = 128[/h][h=3][/h]S1852 NGWILIZI SECONDARY SCHOOL
[h=3]DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 0 DIV-IV = 10 FLD = 32[/h]
S1806 YUSUF MAKAMBA SECONDARY SCHOOL
[h=3]DIV-I = 0 DIV-II = 1 DIV-III = 11 DIV-IV = 52 FLD = 344[/h][h=3][/h]S1803 LOWASSA SECONDARY SCHOOL
[h=3]DIV-I = 0 DIV-II = 4 DIV-III = 9 DIV-IV = 51 FLD = 131[/h][h=3][/h]S1796 DR. DIDAS MASABURI SECONDARY SCHOOL
[h=3]DIV-I = 0 DIV-II = 2 DIV-III = 9 DIV-IV = 35 FLD = 17[/h][h=3][/h]S2724 PROF. PHILEMON SARUNGI SECONDARY SCHOOL
[h=3]DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 1 DIV-IV = 13 FLD = 78[/h][h=3][/h]S3113 ANNA ABDALAH SECONDARY SCHOOL
[h=3]DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 1 DIV-IV = 17 FLD = 76[/h][h=3][/h]P1360 BILAL ISLAMIC SEMINARY CENTRE
[h=3]DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 0 DIV-IV = 39 FLD = 163[/h]Hapo juu ni orodha ya Shule za secondary zenye majina yenu na kama sikosei ni nyinyi ndo mlizozifungua(Zindua) na katika uzinduzi mlitoa ahadi kemkem juu ya kuzifanya shule hizi kuwa za mfano na nyie mtakuwa walezi wa shule hizo, je mmetekeleza ahadi mlizotoa? jibu ni hakuna na inawezekana mmeishasahau kama mliwahi kuzisikia na leo majina yenu yanawakilisha kufeli huku mnajisikiaje kushuhudia majina yenu yakiaibika kiasi hiki.
 
Mara kadhaa na kujirudiarudia:-
Raia wameuawa na Polisi, JK unasema hayatatokea tena!
Makanisa yanachomwa moto, JK unasema hayatatokea tena.
Ulimboka anateswa nusu kufa, JK unasema Serikali haihusiki na hayatatokea tena.
Viongozi wa dini hasa ya kikristo wanapigwa risasi kujeruhiwa na kuuawa, JK unasema hayatatokea tena.
Wanafunzi wanafeli kwa kiwango cha zero asilimia 60, JK unamkumbatia Waziri wa Elimu ambaye analeta tafiti dhaifu na majibu ya kisanii.
Ukatuondolea Spika makini ukatuletea spika, mnyanyasaji, mkandamizaji na mnyamazishaji wa upinzani, JK unatabasamu.
Awamu yako imeandamwa na migomo mingi ya Vyuo, Walimu na Madaktari, JK haujaleta ufumbuzi na mpango suluhishi wa kudumu zaidi ya ubabe, vitisho na majibu mepesi.
Umeulizwa, kwa nini watanzania ni maskini, JK umejibu eti hujui huku ukichekacheka na kutabasamu.
Umeruka ruka angani kwa kodi zetu tena ukatuacha tunahangaika na masuala makubwa kama Kuchinja na Gesi Mtwara, JK ukaja na majibu mepesi na maneno ya kutuliza bila mpango kabambe na tamko rasmi la usawa na haki.
JK huna uwezo na huna nia ya kuendelea kuwa Kiongozi wetu pia huna sababu ya kuendelea kung'ang'ania Cheo ambacho huna uwezo nacho.
Uongozi wa Nchi unahitaji mengi zaidi ya kutabasamu, kusafiri sana nje, kuhutubia, kutoa majibu na matamko mepesi kwa masuala nyeti ya Taifa.
Safari hii huna kipya cha kutuambia zaidi ya ule wimbo wa "SIJUI, TUNA NIA NJEMA, TUKO KWENYE MCHAKATO WA KUWABAINI NA HAYATATOKEA TENA"
Wimbo huu sasa basi!
Tumechoka, tumekinai na hatutaki!
 
[h=5]Kama aongozae chombo cha elimu anashindwa kutofautisha kati ya Zanzibar na Zimbabwe....sembuse wanafunzi wake kufaulu ????[/h]

Tafakari....................chukua hatua.................chagua CHADEMA 2015
 
Kwa kweli huwa nashindwa kuelewa inakuaje Somo la kiswahi nalo wanafunzi wanapata F? Sio kwamba ni Kujisifia, Ila Mimi wakati nasoma Ndo Somo Nililo Faulu kwa kiwango cha juu kabisa kuliko masomo yote, ingawa hata mengine nilifanya vizuri

Na niliapa kuto feli kiswahili, Nilifeli, english kwa sababu si lugha yetu, ila si kiswahili
 
Kama aongozae chombo cha elimu anashindwa kutofautisha kati ya Zanzibar na Zimbabwe....sembuse wanafunzi wake kufaulu ????



Tafakari....................chukua hatua.................chagua CHADEMA 2015

Unanikumbusha mbali jamani:

Mulugo in Action_5239514_orig.png
 
Mara kadhaa na kujirudiarudia:-
Raia wameuawa na Polisi, JK unasema hayatatokea tena!
Makanisa yanachomwa moto, JK unasema hayatatokea tena.
Ulimboka anateswa nusu kufa, JK unasema Serikali haihusiki na hayatatokea tena.
Viongozi wa dini hasa ya kikristo wanapigwa risasi kujeruhiwa na kuuawa, JK unasema hayatatokea tena.
Wanafunzi wanafeli kwa kiwango cha zero asilimia 60, JK unamkumbatia Waziri wa Elimu ambaye analeta tafiti dhaifu na majibu ya kisanii.
Ukatuondolea Spika makini ukatuletea spika, mnyanyasaji, mkandamizaji na mnyamazishaji wa upinzani, JK unatabasamu.
Awamu yako imeandamwa na migomo mingi ya Vyuo, Walimu na Madaktari, JK haujaleta ufumbuzi na mpango suluhishi wa kudumu zaidi ya ubabe, vitisho na majibu mepesi.
Umeulizwa, kwa nini watanzania ni maskini, JK umejibu eti hujui huku ukichekacheka na kutabasamu.
Umeruka ruka angani kwa kodi zetu tena ukatuacha tunahangaika na masuala makubwa kama Kuchinja na Gesi Mtwara, JK ukaja na majibu mepesi na maneno ya kutuliza bila mpango kabambe na tamko rasmi la usawa na haki.
JK huna uwezo na huna nia ya kuendelea kuwa Kiongozi wetu pia huna sababu ya kuendelea kung'ang'ania Cheo ambacho huna uwezo nacho.
Uongozi wa Nchi unahitaji mengi zaidi ya kutabasamu, kusafiri sana nje, kuhutubia, kutoa majibu na matamko mepesi kwa masuala nyeti ya Taifa.
Safari hii huna kipya cha kutuambia zaidi ya ule wimbo wa "SIJUI, TUNA NIA NJEMA, TUKO KWENYE MCHAKATO WA KUWABAINI NA HAYATATOKEA TENA"
Wimbo huu sasa basi!
Tumechoka, tumekinai na hatutaki!

Mtamlaumu sana Jk lakini yote hayo mmeyapalilia wenyewe. CDM mlipanda majukwaani huku mkisema nchi haitatawalika, mkawashawishi madaktari na walimu kugoma eti kwa sababu tu unatafutwa umaarufu wa kisiasa. Mkafanya kampeni za uchaguzi kwa kutumia sms zenye udini. Hakuna sababu ya kutafuta mchawi ni matunda ya siasa rahisi, siasa zisizo na hoja bali matumizi ya nguvu.
 
Kwa kweli huwa nashindwa kuelewa inakuaje Somo la kiswahi nalo wanafunzi wanapata F? Sio kwamba ni Kujisifia, Ila Mimi wakati nasoma Ndo Somo Nililo Faulu kwa kiwango cha juu kabisa kuliko masomo yote, ingawa hata mengine nilifanya vizuri

Na niliapa kuto feli kiswahili, Nilifeli, english kwa sababu si lugha yetu, ila si kiswahili

kwa sababu wewe ulikuwa unaamini mtihani utafanya wewe mwenyewe, wanafunzi wa siku hizi wanafikiri mtihani watafanyiwa na wazazi wao, huku wazazi wakifikiri mtihania atafanya Rais wa nchi.
 
Back
Top Bottom