Asilimia kubwa ya Biashara /uwekezaji wa Watanzania/Wazawa hautupi nafasi ya kuja siku moja kushindana huko Duniani

Kaka n
ok mimi nitajaribu ku summarize maelezo yako kama ifuatavyo

Kwa maelezo yako unamaanisha Unahitaj vijana waje na bussness ideas ambazo watawekeza kwenye startups ili baadae hizo startup zije kuwa biashara/kampuni kubwa kuliko kuja na bussness ideas ambazo hazinaga wigo mpana wa kwenda mbali na zinaishia kuwa biashara za "kujikimu"

Changamoto ya unalolishauri ni hizi hapa

moja ili tufanikiwe kuzalisha wafanyabiashara wa kimataifa ambao watazalisha bidhaa / huduma
Za kushindana kwenye soko la
Dunia. Ni lazima mfumo Mzima wa Elimu ubadilike

huwezi kutegemea kijana ambaye toka shule ya msingi bado anafundishwa kwa kutumia mitaala ya kukaririshwa "Burma wanaongoza kulima
Mahindi" huyu mtu anakaririshwa hadi chuo kikuu hakuna sehemu anatengenezewa akili Ya kuwa mbunifu halafu utegemee aje na bussness idea ya kushindana dunia

Pili ili hizo idea zigeuzwe kuwa startup bussness maana yake lazima capital ihusike.. serikali itengeneze mazingira rafiki na utamaduni wa ku suponsor startups bussiness

Kupitia wizara ya kazi, sayansi na teknolojia wangekuwa wana mafungu ya kusponsor pontetial bussiness Ideas walau kwa kuanzia kila baada ya miaka miwili, na kuwekeza kwemye startups.. wangekuja na mipango hata ya kushindanisha idea kila
Mwaka na kumi bora wakapata sponsorship

Nje ya hapo vijana wetu watakuwa wanaanzisha biashara za kujikimu tu
 
Biashara yoyote kwenda kimataifa ni wewe mwenyewe utakavyo ifanya
Club 1OAk ipo USA imetoboa mpk Dubai
 
Kwani wale wajasiriamali wa kutengeneza sabuni hawawezi kujengewa uwezo waka enda kushindana huko kenya?
 
Kwani wale wajasiriamali wa kutengeneza sabuni hawawezi kujengewa uwezo waka enda kushindana huko kenya?
Hatuwezi shindana kwa sabuni, Sabani na wale ni forced entrepereneurs, wanatengeneza sabani sio kwa kupenda, sio kutoka moyoni bali ni hali ngumu ya maisha ukiwaitia kazi wanaacha sa hio kuzalisha hizo sabuni.
 
Tatizo la Tanzania, imekuwa na serikali za kuwekwa vitu kwenye maandishi na matamshi ila utekelezaji umekuwa sifuri na malengo mengi hayatimii ipasavyo.

Hayo maswali uliyoyandika yalishaainishwa katika dira ya maendeleo ya 2000-2025 na mpango WA maendeleo WA 2011-2016.

Dira ya taifa iliainisha kuwa ifikapo 2025 Tanzania iwe semi industrialised nation na ukuaji WA uchumi WA zaidi 8%.

Mpango WA maendeleo ukashindilia kabisa kwamba katika miaka 15 iliyobaki Tanzania iwe industrialised nation na iwe imefika pato la Kati la $3000.

Na ikadai Tanzania lazima ishindane globally Kwa kuwa global competitive firms, Kwa kuanzia viwanda vilivyotarajiwa kuanzishwa ni
1. Fertilizers na chemical industry
2. Steel and iron industry
3. Pharmaceutical industry
4. Textile industry..

Kwa maana ya kwamba hizi raw materials zinapatikana nchini.

Lakini mpaka sasa hakuna lolote lilotimizwa na Tanzania imeshindwa kuwa industrialised nation.

Kikwete alikuwa anajua direction lakini hakuwai kuwa serious kwenye utekelezaji WA huo mpango aliosuka na makamu WA rais WA sasa filip mpango.

Magufuli hakuwai na direction yoyote wala blueprint, Chini ya Samia hakuna matumaini kwenye industrialization na technological capacity building, unaweza kuona kwenye swala zima la bandali na uwekezaji mpya WA nje WA kuchimba madini ya chuma ambayo kiujumla haitowezesha watanzania ku-master na ku-originate tech ya uchimbaji WA chuma. Isipokuwa nchi itaendelea kuuza raw materials na mnufaika mkubwa ni mwekezaji WA nje. Utegemezi chuma cha nje kupungua 2027 Tanzania

Kuna flaws nyingi Sana kwenye hizi Sera za kufungua nchi kama inavyochagizwa na rais
 
Tunatumia teknolojia ama Maujanja na biadhaa ambazo hatuzizalishi

We consume what we do not produce, being the end result of neocolonialism
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…