Askari huyu wa JWTZ akamatwe na kushtakiwa kwa kosa la ujangili

Askari huyu wa JWTZ akamatwe na kushtakiwa kwa kosa la ujangili

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Nakumbuka mwaka 2020 aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamis Kigwangalla alimtuhumu aliyekuwa Meya wa Iringa kuwa ametenda kosa la ujangili baada ya kupakia picha kwenye mtandao wa Twitter akiwa amemuua nyoka aina ya chatu. Zaidi soma Dtk. Kigwangalla amtuhumu Alex Kimbe kwa ujangili baada ya kuua chatu

Leo nimekutana na video ikimuonesha Askari wa JWTZ akiwa anajinadi kwa kumuua nyoka mkubwa aina ya chatu. Ukimsikiliza vizuri utagundua kwamba nyoka huyo hakuwa katika mazingira ya kuleta madhara yoyote kwa binadamu, ni kwamba alikuwa katika mazingira yake ya maisha ya kila siku. Kitendo cha Askari huyo kumuua bila sababu za msingi si kitu cha kufumbia macho.

Nyoka mkubwa kama yule anachukua muda mrefu kufikia ukubwa ule, na pia anapitia katika mazingira hatari tokea kuanguliwa ikiwa pamoja na kuwindwa na wanyama wengine hatari. Anapoweza kukabiliana na hatari zote mpaka kufikia ukubwa ule ni suala la kushukuru.

Huyu Askari angetumia busara hata kuwaita maafisa wanyama pori waje kumchukua, mnyama kama huyu ni kivutio kikubwa sana cha utalii, anaweza akaleta mapato makubwa sana akiwekwa kwa snake park

 
Wewe hata kule kwetu nyati akijichanganya kwenye anga za watu majiko lazima yapate taabu...nyoka kavamia eneo la kazi na huyo askari anahakikisha mazingira yako salama..kama kesi zipo hivo wengi wetu ni majangiri..mimi binafsi nilishaua nyoka wengi tu wanaovamia nyumbani.
 
Ki ukweli mimi imeniuma sana. Nyoka yule alikuwa mkubwa sana, ambapo angeenda kuwaripotia maafisa wanyama pori, wamkamate na akahifadhiwe mahali ili awe ni utalii. Nyoka yule alikuwa mkubwa sana, Kichwa kikubwa Kuliko mbuzi. Askari huyu akamatwe ili iwe fundisho kwa wengine.Chatu si Sawa na Nyoka wengine, hana Sumu na pia ni nadra sana kusikia amemmeza binadamu. Huyu Askari angeenda kupambana na Simba ili tuone huo ushujaa wake na siyo kwenda kumuonea kumbe asiye na madhara kwa binadamu
 
Pumbavu kabisa hili ng'ombe, eti ndio ushujaa, Mavi kabisa hii mijitu
lilikuwa linamkimbiza huyo nyoka alikuwa anapita na zake
Ni hadi ameze mtoto ndipo mseme angemuua. Kumbuka huyo sio kiumbe rafiki hata kidogo na alipokuwepo kuna naingiliano ya karibu na watu. Wewe ni kati ya Ndezi wanaokosoa kila jambo
 
Ni hadi ameze mtoto ndipo mseme angemuua. Kumbuka huyo sio kiumbe rafiki hata kidogo na alipokuwepo kuna naingiliano ya karibu na watu. Wewe ni kati ya Ndezi wanaokosoa kila jambo
Wewe ni Mporipori, akili zako na zangu haziwezi kuafikiana kutokana na mifumo tofauti yetu kimaisha
 
Back
Top Bottom