Askari polisi wafariki ajalini Msoga

Askari polisi wafariki ajalini Msoga

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Ajali imetokea leo alfajiri katika eneo la Mavi ya Ng'ombe kwenye Kijiji cha Mboga, Kata ya Msoga baada ya gari iliyokuwa imebeba maafisa wa polisi aina ya Toyata Crester yenye namba za usajili T.323 BAL iliyokuwa ikiendeshwa na Mkaguzi msaidizi wa Polisi, Ndwanga Dastani (28) aliyekuwa akitokea Chalinze kuelekea Lugoba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Pius Lutumo, ajali hiyo imetokea baada ya gari hilo kuacha njia na kugonga karavati na kisha kupinduka na kusababisha vifo vya watu watatu pamoja na majeruhi mmoja.

Waliofariki kwenye ajali hiyo ni pamoja na dereva wa gari hiyo Ndwanga Dastani, Polisi Konstebo Emiliana Charles (26) waliokuwa askari wa Kituo cha Polisi Chalinze na Karimu Simba (27) aliyekuwa karani wa Mahakama ya Wilaya ya Lugoba.

Aliyejaruhiwa katika ajali hiyo ni Polisi Konstebo Mwanaidi Shabani (25), askari wa Kituo cha Polisi Chalinze ambaye amejeruhiwa maneneo mbalimbali ya mwili na amepelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Aidha taarifa hiyo imesema, uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Lugoba.

Azam

Screenshots_2023-03-06-08-10-23.png
 
Mkaguz msaidiz wa miaka 28! Miaka 20 mbele angekuwa dcp, lakn kaz ya mola haina makosa.

Pumziken makamanda.
 
Ajali imetokea leo alfajiri katika eneo la Mavi ya Ng'ombe kwenye Kijiji cha Mboga, Kata ya Msoga baada ya gari iliyokuwa imebeba maafisa wa polisi aina ya Toyata Crester yenye namba za usajili T.323 BAL iliyokuwa ikiendeshwa na Mkaguzi msaidizi wa Polisi, Ndwanga Dastani (28) aliyekuwa akitokea Chalinze kuelekea Lugoba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Pius Lutumo, ajali hiyo imetokea baada ya gari hilo kuacha njia na kugonga karavati na kisha kupinduka na kusababisha vifo vya watu watatu pamoja na majeruhi mmoja.

Waliofariki kwenye ajali hiyo ni pamoja na dereva wa gari hiyo Ndwanga Dastani, Polisi Konstebo Emiliana Charles (26) waliokuwa askari wa Kituo cha Polisi Chalinze na Karimu Simba (27) aliyekuwa karani wa Mahakama ya Wilaya ya Lugoba.

Aliyejaruhiwa katika ajali hiyo ni Polisi Konstebo Mwanaidi Shabani (25), askari wa Kituo cha Polisi Chalinze ambaye amejeruhiwa maneneo mbalimbali ya mwili na amepelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Aidha taarifa hiyo imesema, uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Lugoba.

Azam
Huwa hawaogopi tochi kwakuwa wao ndio wanapiga, speed zao zinatisha, sasa huumbuliwa na ajali. Anayway wapumzike kwa amani
 
Back
Top Bottom