Askari wa JWTZ Atuhumiwa Kwa Mauaji ya Mke Wake wa Ndoa Huku Akijaribu Yeye Mwenyewe Kujiua Bila Mafanikio

Askari wa JWTZ Atuhumiwa Kwa Mauaji ya Mke Wake wa Ndoa Huku Akijaribu Yeye Mwenyewe Kujiua Bila Mafanikio

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Askari huyo wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) anayeenda kwa jina la Daniel Warioba alijaribu kujiua kwa kunywa sumu baada ya tukio hilo lakini hakufanikiwa.

Uchunguzi wa tukio hilo la kutisha lililotokea Mlandizi Mkoani Pwani bado unaendelea na taarifa kamili itatolewa na mamlaka husika ambayo ni Jeshi la Polisi

Inadaiwa Kuwa chanzo cha tukio la kikatili ni mfarakano uliochangiwa pamoja na mambo mengine wivu wa kimapenzi baina ya wanandoa hao

Mtuhumiwa huyo kwa Sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi ya tukio hilo.

Tunatoa pole kwa familia ya Mwendazake aliyehudumu kama Mwalimu Katika uhai wake

=====

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linamshikilia Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Koplo Daniel Warioba (43) kutoka Kikosi cha 92 TJ kwa tuhuma za kumuua Mke wake Joyce Ismail (35) ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Ruvu Darajani

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana huu katika eneo la Janga, Wilaya ya Kipolisi Mlandizi.

Kamanda Wankyo alisema askari huyo anadaiwa kumchoma mke wake na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili na kumsababishia kifo.

Kwa mujibu wa Kamanda Wankyo, baada ya kutekeleza mauaji hayo, mtuhumiwa anadaiwa alitaka kunywa sumu kwa lengo la kujiua.

Wankyo alisema polisi wamemkamata mtuhumiwa huyo na anaendelea kupata matibabu katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa ya Tumbi, huku chanzo cha tukio hilo kikiendelea kuchunguzwa.
 
Tukio limetokea Mlandizi mkoa wa Pwani. Huyo mama aliyeuwawa ni mwl wa shule ya msingi. Chanzo Star tv habari
 
Askari huyo wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) anayeenda kwa jina la Daniel Warioba alijaribu kujiua kwa kunywa sumu baada ya tukio hilo lakini hakufanikiwa

Uchunguzi wa tukio hilo la kutisha na kusikitisha bado Unaendelea na taarifa kamili itatolewa na mamlaka husika ambayo ni Jeshi la Polisi

Inadaiwa Kuwa chanjo cha tukio la kikatili ni mfarakano uliochangiwa pamoja na mambo mengine wivu wa kimapenzi baina ya wanandoa hao
Mtuhumiwa huyo kwa Sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi ya tukio hilo.

Tunatoa pole kwa familia ya Mhanga

NB: Moderator tafadhali rekebisha heading isomeke JWTZ badala ya Polisi.
Watu wanauana kitaa wamejaa kibao wewe umeona ya Mjeda tu.?
 
Askari huyo wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) anayeenda kwa jina la Daniel Warioba alijaribu kujiua kwa kunywa sumu baada ya tukio hilo lakini hakufanikiwa

Uchunguzi wa tukio hilo la kutisha na kusikitisha bado Unaendelea na taarifa kamili itatolewa na mamlaka husika ambayo ni Jeshi la Polisi

Inadaiwa Kuwa chanjo cha tukio la kikatili ni mfarakano uliochangiwa pamoja na mambo mengine wivu wa kimapenzi baina ya wanandoa hao
Mtuhumiwa huyo kwa Sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi ya tukio hilo.

Tunatoa pole kwa familia ya Mhanga

NB: Moderator tafadhali rekebisha heading isomeke JWTZ badala ya Polisi.
Waache tu wauwane wapungue, maana wamezoea kutumia nguvu kubwa kukandamiza wananchi na upinzani, sasa kuliko kutumia hiyo nguvu kukandamiza upinzani bora aitumie kujiua mwenyewe
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linamshikilia Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Koplo Daniel Warioba (43) kutoka Kikosi cha 92 TJ kwa tuhuma za kumuua Mke wake Joyce Ismail (35) ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Ruvu Darajani

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana huu katika eneo la Janga, Wilaya ya Kipolisi Mlandizi.

Kamanda Wankyo alisema askari huyo anadaiwa kumchoma mke wake na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili na kumsababishia kifo.

Kwa mujibu wa Kamanda Wankyo, baada ya kutekeleza mauaji hayo, mtuhumiwa anadaiwa alitaka kunywa sumu kwa lengo la kujiua.

Wankyo alisema polisi wamemkamata mtuhumiwa huyo na anaendelea kupata matibabu katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa ya Tumbi, huku chanzo cha tukio hilo kikiendelea kuchunguzwa.

Chanzo: Millard Ayo

Muwe mnamaliza Kwanza Udangaji ( Uhuni ) wenu na mkishaona mmemaliza ndipo muwe pia mnakubali Kuolewa na Wanaume wa Kikurya sawa?
 
Ushauri mbovu!

Una maanisha mwanamke akidanga kifo kitakuwa halali yake?

Kwa hiyo kwa kuwa kadanga auawe?

Kosa la kudanga na adhabu ya kifo havirandani kabisa.

Makosa mawili hayatengenezi uhalali.

Two wrongs never make right.

Kumuua mdangaji, hakumuondolei muuaji hatia.

Kusingekuwa na sheria basi tungehalalisha uhuni mwingi, mfano, Mkurya ukimuudhi anakuua. Rubish!
 
Ushauri mbovu!

Una maanisha mwanamke akidanga kifo kitakuwa halali yake?

Kwa hiyo kwa kuwa kadanga auawe?

Kosa la kudanga na adhabu ya kifo havilandani kabisa.

Makosa mawili hayatengenezi uhalali.

Two wrongs never make right.

Kumuua mdangaji, hakumuondolei muuaji hatia.

Kusingekuwa na sheria basi tungehalalisha uhuni mwingi, mfano, Mkurya ukimuudhi anakuua. Rubish!
Maneno mengi halafu ni 'Rubbish' tupu.
 
Back
Top Bottom