Askofu Bagonza amnanga mkulu kimafumbo, soma kwa kifupi

Askofu Bagonza amnanga mkulu kimafumbo, soma kwa kifupi

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776
a Askofu Bagonza


AKILI na IMANI

Hivi kipi kinaanza? Kipi kinawezesha kingine? Imani ndiyo inakuongoza kuwa na akili au akili inakuongoza kuwa na imani na kuitegemea?

Wanaopuuza umuhimu wa kutumia akili, wawaulize wazazi ambao kwa bahati mbaya wana watoto au jamaa waliopungukiwa na akili, kwa kuzaliwa au kupata tatizo hilo ukubwani. Zawadi kubwa, ya pekee na ya thamani aliyotupa Mungu ni akili. Tunaitumia kutambua na kufanya maamuzi. Hata imani tunayoienzi na kumwamini muumba wetu, tunawezeshwa na akili aliyotupa muumba huyo huyo.

Ndiyo maana pamoja na kwamba Mungu yupo:

1. Tunajenga Nyumba na kulala ndani yake, hatulali nje ili Mungu atulinde.

2. Tunajenga uzio mkubwa kuzunguka Nyumba, hatuaiachi nyumba ili Mungu atulinde.

3. Tunafuga Mbwa wakali, licha ya kuwa na Uzio.

4. Tunaajiri walinzi wenye silaha, kana kwamba uzio na mbwa havitoshi.

5. Tunaweka na CCTV kamera licha ya kuwa tuna walinzi, uzio na mbwa wakali.

6. Tunanunua na bima kubwa kuonyesha kuwa wizi bado upo licha ya kuwa tuna yote hayo.

7. Usiku tunaamka mara tatu-tatu kuona kama walinzi wapo. Tunaajiri walinzi na wao wanatuajiri kuwachunga usiku.


Pamoja na yote hayo, Mungu aweza kutuchukua kutoka katikati ya ulinzi wote huo. Anatupa akili tuzitumie kujilinda, lakini anabaki na uwezo wa mwisho juu ya maisha yetu.

Hatuwezi kuacha kutumia akili eti kwa sababu yeye yupo. Na hatuwezi kutegemea akili tu eti kwa sababu akili katupa yeye. Imani na akili vyote ni mali ya Mungu, yeye katukabidhi tuvitumie.
Hatuwezi kuacha kuvaa Mask/Barakoa eti Mungu yupo, kwani huko VATICAN na MECCA dini zilipoanzia Mungu hayupo, yupo Tanzania pekee? UCHUMI vs MAISHA YA WATU! [MSISITIZO NI WANGU]


TUSIHUKUMIANE na TUSILAUMIANE.
 
Asilimia 90 ya vitu alivyoviorodhesha mimi sina katika hivyo mimi nina Akili na Imani tu.
Barakoa sivai ndani sijifungii na Corona sipati hii homa imekuzwa sana kuliko uhalisia wa madhara yake.
Corona ni homa ya kawaida ambayo naamini asilimia kubwa ya watanzania wamewahi kuugua kabla lakini walikuwa hawajijui lakini baada ya kuwapata wazungu na kuwaathiri sana ndio shida ilipoanzia.
Mtumishi fanya kazi ya Mungu achana na siasa Watanzania tuchape kazi.
HONGERA JPM NAIPENDA TANZANIA
 
Asilimia 90 ya vitu alivyoviorodhesha mimi sina katika hivyo mimi nina Akili na Imani tu.
Barakoa sivai ndani sijifungii na Corona sipati hii homa imekuzwa sana kuliko uhalisia wa madhara yake.
Corona ni homa ya kawaida ambayo naamini asilimia kubwa ya watanzania wamewahi kuugua kabla lakini walikuwa hawajijui lakini baada ya kuwapata wazungu na kuwaathiri sana ndio shida ilipoanzia.
Mtumishi fanya kazi ya Mungu achana na siasa Watanzania tuchape kazi.
HONGERA JPM NAIPENDA TANZANIA
Mstari wa kwanza tu unaonyesha wewe ni MATAGA na unafikiria kwa kutumia MASABURI, baki hivyo hivyo
 
Asilimia 90 ya vitu alivyoviorodhesha mimi sina katika hivyo mimi nina Akili na Imani tu.
Barakoa sivai ndani sijifungii na Corona sipati hii homa imekuzwa sana kuliko uhalisia wa madhara yake.
Corona ni homa ya kawaida ambayo naamini asilimia kubwa ya watanzania wamewahi kuugua kabla lakini walikuwa hawajijui lakini baada ya kuwapata wazungu na kuwaathiri sana ndio shida ilipoanzia.
Mtumishi fanya kazi ya Mungu achana na siasa Watanzania tuchape kazi.
HONGERA JPM NAIPENDA TANZANIA
Tangu lini homa ya kawaida inaua maelfu kwa siku moja? THINK.
 
Asilimia 90 ya vitu alivyoviorodhesha mimi sina katika hivyo mimi nina Akili na Imani tu.
Barakoa sivai ndani sijifungii na Corona sipati hii homa imekuzwa sana kuliko uhalisia wa madhara yake.
Corona ni homa ya kawaida ambayo naamini asilimia kubwa ya watanzania wamewahi kuugua kabla lakini walikuwa hawajijui lakini baada ya kuwapata wazungu na kuwaathiri sana ndio shida ilipoanzia.
Mtumishi fanya kazi ya Mungu achana na siasa Watanzania tuchape kazi.
HONGERA JPM NAIPENDA TANZANIA
Hatuwezi kuyathibitisha hayo kwa sababu hatukuoni, ni bora ukae kimya tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom