t blj
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 7,035
- 16,705
Hata kama ndege zote zilinunuliwa kwa wakati mmoja , the fact ni kuwa hazifanyi safari ya aina moja , maana yake ni kuwa zina milage tofauti tofauti, inawezekana ndege ya mwisho ikadai matengenezo mapema kuliko ile ya mwanzo.Wamejitetea kindezi
Msemaji wa ATCL ndugu Josephat Mwingira amesema pamekuwepo na mabadiliko ya mara kwa mara ya ratiba za ndege zao takribani wiki mbili sasa kwa sababu ndege nyingi zilikuwa kwenye matengenezo makubwa.
Mwingira amesema nyingi ya ndege zao zilinunuliwa kwa wakati mmoja ndio maana hata matengenezo yake hufanyika pamoja na kamwe ATCL haiwezi kurusha ndege yenye hitilafu.
Mwingira amewataka mawakala wa kuuza tiketi kuweka namba zao za simu na kuchukua namba za wateja ili wawe wanapewa taarifa ya mapema pindi yanapotokea matatizo.
Source: Star tv habari!