Askofu Bagonza: Jakaya Kikwete hana ushawishi wowote kwenye Awamu ya Sita

Askofu Bagonza: Jakaya Kikwete hana ushawishi wowote kwenye Awamu ya Sita

Nikisikia kiongozi wa dini anajihusisha na masuala ya siasa huwa nakwazika sana.

Sana sana nafarijika napoona anahimiza waamini wajikite katika kufuata misingi yote pasipo kuvunja sheria za nchi.
Mbona Josephat Gwajima ni mbunge tena kwa kuiba kura na hujawahi kunyanyua mkia hata kidogo?! Askofu Bagonza akikemea uovu tena nje ya ulingo wa siasa unaanza kuwashwawashwa. Kwendraa.
 
Yaaani mimi huwa mawashangaa kikwete ana lipi la maana zaidi ya uswahili wa kipuuzi na ujinga!
Utawala wa yule Mzee ulisaidia kuwatoa wengi kwenye nyumba za kupangisha au mbavu za mbwa!
Uongozi wake uliwajenga wengi kuamini katika juhudi na maarifa yao!
Wengi walianzisha na kuendesha shughuli rasmi za kiuchumi!
Alifanya wananchi wakajua thamani yao; mmoja mmoja na katika makundi yao!
Aliposema maisha bora sio wote walimuelewa. Lakini kwa sasa wengi wanazidi kumuelewa!
Hawa waliochukua atamu wamefanikiwa kupora madaraka na maamuzi kutoka kwa mikononi mwa wananchi na kujimilikisha wao kwa msaada wa karibu wa vyombo vya mabavu!
Kuna mfanano mkubwa sana baina ya Tanzania ya sasa na Korea Kaskazini au China. Inavyoelekea kwa sasa jukumu pekee la mwananchi ni kuishi kwa kupiga makofi na si vinginevyo!
 
Nikisikia kiongozi wa dini anajihusisha na masuala ya siasa huwa nakwazika sana.

Sana sana nafarijika napoona anahimiza waamini wajikite katika kufuata misingi yote pasipo kuvunja sheria za nchi.
ANAGOMBEA UDIWANI??? 🤣🤣🤣
KWELI AKILI NI NYWELE
 
Kwahiyo wakifanya hayo ya kiuchumi ni sawa ila wakikosoa serikali haitakiwi?.acha kutangatanga ndugu.dini ni kazi kama kazi nyingine.kama ambavyo kiongozi wa kisiasa anaweza akawa mhumini wa dini ndivyo ambavyo mkulima anaweza kua mwalimu na mchungaji kua mwanasiasa.zaidi ya hapo ni porojo tu kwasababu hatutaki kukosolewa.hao viongozi wa dini wangekua wanasifia tu kamwe usingesikia hizi porojo za kwamba kiongozi wa dini asihubiri mambo ya kisiasa ila kwavile wanakemea maovu ambayo watawala hawapendi kusikia ndipo zinakuja hizi hoja mfu.
Yesu alifanya mambo ya kiuchumi bila kuwa mwanasiasa na alikataa kuwa mwanasiasa alilisha maelfu wakala Hadi kusaza bila msaada wa serikali Wala chama Cha siasa Wala katiba mpya Wala msaada wa kuchangisha toka kwa wazungu na bila kuwa na NGO

Hawa maaskofu Kama Bagonza sababu hawakuitwa na Mungu walijipeleka kutafuta ajira hawaelewi wanawezaje kuwa na impact kwenye nchi bila kuwa wanasiasa tatizo analo Bagonza,Gwajima ,Askofu Shoo wa KKKT na Askofu katoliki wa Jimbo kuu la Dar es salaam,Niwemugizi nk
 
Ujinga na upumbavu hautaisha nchi hii...

Kwa hakika ni ujinga na upumbavu wa kudhani JK ana mkono kwenye Awamu ya 6.

Ni ujinga na upumbavu uliopitiliza kudhani wajinga walikuwa awamu ya 4 na kuwa eti werevu ni awamu za 5 na 6.

Hivi kwani Selfies na beberu kuna aliyeziona?
 
Bagonza nyege za kisiasa ziko juu
Nimestuka sana. Tafakari uiombee nafsi yako radhi kwa Mungu pamoja na mwenzio aliyemuita Askofu na Mtumishi wa MUNGU mpumbavu. Vinginevyo laana itakuwa juu yenu kuanzia leo hii.
Pili, Askofu Bagonza na wengine wengi wa jinsi yake ndio haswa wanaujua wito wao mkuu walioitiwa wa kupigania haki, utu na ukweli bila kuogopa. Kwa maneno mengine kupiga vita dhuluma, uonevu na hata ujangili wa kisiasa. Ni ajabu kwamba siku hizi ukipigania haki, usawa na uhuru unaitwa CHADEMA. Tafsiri yangu ni kwamba watawala wa sasa wahahusishwa na kuwa kinyume na hayo. Ni hatari kweli kweli. Askofu na Maaskofu na Masheikh ipiganieni haki msikae kimya na wala msiwaachie wachache. Ndio wito mkuu wa Kanisa, Misikiti na hata wasio na dini rasmi. Endelea Baba Bagonza nchi ipone.
 
JK ni aina ya Rais anayepaswa kuongoza Taifa ambalo limeshaendelea tayari na watu wake kwa zaidi ya 80% wanajielewa na wamestaarabika na mifumo iko tayari...
JK anaweza kuongoza nchi yeyote Ulaya au hata USA..

JPM anafaa na alifaa kuliongoza Taifa kama hili ambali bado haliko tayari kimifumo na zaida ya 80% ya watu wake ni wajinga na wapumbavu wasiojielewa... Watanzania bado wako kwenye stage ya kuswagwa kama punda au ng'ombe na wakishavuka hiyo stage sasa ndio wanapaswa kuongoza watu kama JK....Unafikiri hawa wapumbavu wala rushwa na wezi wa mali za umma + wauza madawa nk utawashughulikia kimama kwa kuwalealea wataacha...hizi hela za miradi bila kuwa kiongozi mkorofi unafikiri miradi itakwenda...

Bado Watanzania wako kwenye stage ya mijeledi na kuswagwa..
Maneno hayo japo yanawaudhi wengi humu ndani ila ukikaa na kutafakari vyema...kuwatafakari watanzania vile ilivyo.... kuwatafakari wapinzani nao....unamaizi UADHIMU WAKE....
 
Hebu tuangalie nini kipimo cha awamu
Kwa ilivyo kwa sasa ni mtu anayekuwa rais
Nyerere- awamu ya kwanza- 1962-1985
Mwinyi- awamu ya pili -1985-1995
Mkapa- awamu ya tatu -1995-2005
Kikwete- awamu ya nne- 2005-2015
Magufuli- awamu ya tano- 2015-2021
Samia- awamu ya sita- 2021---- 2030 Mungu akipenda
 
Nimestuka sana. Tafakari uiombee nafsi yako radhi kwa Mungu pamoja na mwenzio aliyemuita Askofu na Mtumishi wa MUNGU mpumbavu. Vinginevyo laana itakuwa juu yenu kuanzia leo hii.
Pili, Askofu Bagonza na wengine wengi wa jinsi yake ndio haswa wanaujua wito wao mkuu walioitiwa wa kupigania haki, utu na ukweli bila kuogopa. Kwa maneno mengine kupiga vita dhuluma, uonevu na hata ujangili wa kisiasa. Ni ajabu kwamba siku hizi ukipigania haki, usawa na uhuru unaitwa CHADEMA. Tafsiri yangu ni kwamba watawala wa sasa wahahusishwa na kuwa kinyume na hayo. Ni hatari kweli kweli. Askofu na Maaskofu na Masheikh ipiganieni haki msikae kimya na wala msiwaachie wachache. Ndio wito mkuu wa Kanisa, Misikiti na hata wasio na dini rasmi. Endelea Baba Bagonza nchi ipone.
Sikatai Ila kazidi
 
Back
Top Bottom