Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pameanza kuchangamka kweli lakini ni kwa maneno tu !Dah! Itoshe tu kusema pameanza kuchangamka sasa.
Huenda wewe utakuwa ni rofa usiye jitambuaSasa mbona wamejaa kila kanisa, tuwe masheik sasa
Kosoa alichoandika kama una hoja. Jamii forums ni Kwa great thinkers sio Facebook hapahuyu bagonza naye ni kichaa kama yule wa chadema mwamakula
Hahaa.......wewe unatumia nini? Siasa kueneza uchawa.Askofu Dr Bagonza wa KKKT Dayosisi ya Karagwe amesema Kwa sasa Taifa limefika Mahali pagumu sana sana
" Kuna watu wanatumia Dini Kueneza Siasa na kuna watu wanatumia Siasa Kueneza Dini Mimi natumia Ujinga Kueneza Dini na Siasa"
Source: Jambo TV
Aliyemuelewa baba askofu naomba Ufafanuzi tafadhali nisije kuchuma Dhambi Bure 🐼
Siasa kama Mwamposa na MakondaMnara wa babeli. Sijawahi kuona clip ya Bagonza na Mwamakula wakihubiri kanisani, wao ni siasa tu
Dokta 🐼Hahaa.......wewe unatumia nini? Siasa kueneza uchawa.
Unaichanganya mno akili ukiiambia eti huko nyuma inakorudi ndiko mbele kwenyewe."Hata Anaye Rudi Nyuma,,,Ana Mbele Anakoelekea"
Unadhani Watanzania wanapenda mabadiliko yoyote, chief? Ufahari wa Bongo ni kutunishiana misuli twitani, Insta, FB na kwenye mitandao mingine ya kijamii.Pameanza kuchangamka kweli lakini ni kwa maneno tu !
Akiongea maneno usiyoyapenda yuko chadema akiongea maneno unayoyapenda yuko ccmKama Askofu Shoo akigombea ubunge kupitia CCM, hata mimi ntampigia kampeni. Chadema wamemlia hela zake kwa muda mrefu, bora amegundua uongo wao.
nadhan hakuna jambo au wazo jipya wala fikra mbdala ambalo Baba Askofu Bagonza amelieleza zaidi ya kupingana kisiasa na Askofu mwenzie kitu ambacho ni kawaida kabisa.Siku chache baada ya Askofu Dkt. Fredrick Shoo kueleza matamanio yake ya kuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akipewa muhula wa pili wa uongozi wa Taifa letu baada ya muhula wake wa kwanza kumalizika, wadau mbalimbali wameibuka na hisia tofauti wapo wale walioonesha kumuunga mkono lakini pia wapo wale walioonesha kutokubaliana na hoja hiyo
Mmoja wa waliojitokeza na kuipinga hoja hiyo kwa ukali na uwazi ni Askofu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe Askofu Dkt. Benson Bagonza ambaye amesema kilichozungumzwa na Askofu Dkt. Shoo si msimamo wa KKKT bali ni msimamo wake binafsi ambao pia pengine mipaka yake inapaswa kuishia kwenye Dayosisi yake pekee
"Nona KKKT imepamba moto kutokana na matamshi ya mmoja wa Maaskofu wake, kwa kimbelembele nilichonacho naomba umma wa Watanzania uelewe yafuatayo:-
(i) KKKT ina Mkuu mmoja tu (wa Kanisa ambaye ni Askofu Dkt. Alex Gehaz Malasusa), dereva wawili hawawezi kuendesha gari moja kwa wakati mmoja;
(ii) KKKT hakuna cheo kinaitwa 'Mkuu wa Kanisa mstaafu', tunaweza kuwa na cheo cha 'liyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa', hivi sasa tuna 'aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa' ambaye amechaguliwa tena kuwa Mkuu wa Kanisa, kama angekuwa mstaafu asingechaguliwa, inawezekana 'aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa' akachaguliwa kuwa Mkuu tena, sitashangaa aliyepita hivi karibuni kuchaguliwa tena;
(iii) Kama kuna mstaafu, 'astaafu', si lazima kuhudhuria; si lazima kusema, ukipenda, usipende kwa niaba, ukichukia, usichukie kwa niaba, kila ulimi una uwezo wa kuonja wenyewe;
(iv) KKKT ni shirikisho, siyo Kanisa moja, ukitaka kusema kwa niaba ya shirikisho, unashawishi siyo kuburuza, hatujashawishika na hatujakaa;
(v) Nampenda Rais Samia (Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) lakini sijatumwa na Kanisa, naweza kumpenda na kukikosoa chama chake (Chama cha Mapinduzi -CCM), naweza kukipenda chama chake nikamkosoa yeye, hayo nitayasemea Karagwe siyo penginepo, na nikiyasema, ni yangu na tumbo langu siyo ya Wanyambo wala Walutheri walio wenye vyama vyao (yaani wanaotoka kwenye vyama tofauti vya siasa) kwa Nyambo haturuhusu mgeni kupiga mluzi katika nyumba ya mwenyeji;
(vi) Kanisa lina wanachama wa vyama vyote na waumini wasio na vyama, CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo) msitutolee macho na CCM (Chama cha Mapinduzi) msishangilie, shoka lipo shinani, mti usiozaa matunda unakatwa;
(vii) Rais Samia (Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) ana uwezo wa kujiharibia, tusimharibie, CCM ina uwezo wa kujiharibia, haijaomba msaada wa kuisaidia kuharibu, lipo kundi linalodhani linamsaidia Rais Samia wakati linamharibia, lipo linalodhani linamharibia lakini linamjenga, anayesimama na 'haki' anamsaidia Rais Samia;
(viii) Tuna tatizo Kitaifa, kuna watu wanatumia Dini kueneza siasa, na kuna watu wanatumia siasa kueneza Dini, mimi si mmoja wa hao wawili (2), mimi natumia ujinga kueneza Dini na siasa, wajinga tu ndio wananisikiliza na kunifuata, wewe mjuaji kaa pembeni tuendelee na safari;
(ix) Nikisema jambo mkanishangilia, mnanipa kiburi cha kusema bila kufikiri, nidhamu ya washangiliaji huja kwa kutafakari, si kuhemka, mkishangilia, mnamnyima msemaji nidhamu ya kufikiri kabla ya kusema, anayesema kweli hahitaji kukumbuka alisema nini jana;
(x) Mungu analipenda Taifa hili (Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) kuliko mtu au chama chochote kinavyoweza kudai kulipenda, usiombe Mungu akuonyeshe anavyolipenda hili Taifa, ina gharama nzito kushuhudia Mungu anavyolipenda hili Taifa, hata anayerudi nyuma ana mbele anakoelekea, ukisifiwa kuwa na mbio, jihadhari usipitilize nyumbani kwenu" -Askofu Dkt. Bagonza
Andiko la Askofu Dkt. Bagonza bila shaka huenda likaibua hisia mseto kama ilivyokuwa tamko la Askofu Dkt. Shoo kutokana na ukweli na kwamba watu hao wawili wana ushawishi wao binafsi lakini pia ushawishi wao ni ngumu kuutenganisha na Kanisa la KKKT