Pre GE2025 Askofu Bagonza: KKKT ina Mkuu wa Kanisa mmoja tu, Dereva wawili hawawezi kuendesha gari moja kwa wakati mmoja

Pre GE2025 Askofu Bagonza: KKKT ina Mkuu wa Kanisa mmoja tu, Dereva wawili hawawezi kuendesha gari moja kwa wakati mmoja

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kama Askofu Shoo akigombea ubunge kupitia CCM, hata mimi ntampigia kampeni. Chadema wamemlia hela zake kwa muda mrefu, bora amegundua uongo wao.
 
Nje ya mada kidogo kuna mapadri waliuawa na kutupwa kwenye matenk ya maji tena kanisani, mbona sisikii kanisa likishinikiza polisi wafanye uchunguzi haraka? Au tuamini ni INSIDE JOB?
 
Askofu Dr Bagonza wa KKKT Dayosisi ya Karagwe amesema Kwa sasa Taifa limefika Mahali pagumu sana sana

" Kuna watu wanatumia Dini Kueneza Siasa na kuna watu wanatumia Siasa Kueneza Dini Mimi natumia Ujinga Kueneza Dini na Siasa"

Source: Jambo TV

Aliyemuelewa baba askofu naomba Ufafanuzi tafadhali nisije kuchuma Dhambi Bure 🐼
 
Askofu Dr Bagonza wa KKKT Dayosisi ya Karagwe amesema Kwa sasa Taifa limefika Mahali pagumu sana sana

" Kuna watu wanatumia Dini Kueneza Siasa na kuna watu wanatumia Siasa Kueneza Dini Mimi natumia Ujinga Kueneza Dini na Siasa"

Source: Jambo TV

Aliyemuelewa baba askofu naomba Ufafanuzi tafadhali nisije kuchuma Dhambi Bure 🐼
Hahaa.......wewe unatumia nini? Siasa kueneza uchawa.
 
Mnara wa babeli. Sijawahi kuona clip ya Bagonza na Mwamakula wakihubiri kanisani, wao ni siasa tu
 
Pameanza kuchangamka kweli lakini ni kwa maneno tu !
Unadhani Watanzania wanapenda mabadiliko yoyote, chief? Ufahari wa Bongo ni kutunishiana misuli twitani, Insta, FB na kwenye mitandao mingine ya kijamii.

Baada ya hapo, watu wanasalimiana kwa furaha, wenye kununa nao walee; tunalala halafu kesho yake inatukuta mzigoni tukiganga yaliyopo na yajayo.

Ndiyo maana haishangazi kuwakuta watu kiduchu kwenye mikutano, mijadala na maamuzi nyeti kabisa kitaifa.
 
Siku chache baada ya Askofu Dkt. Fredrick Shoo kueleza matamanio yake ya kuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akipewa muhula wa pili wa uongozi wa Taifa letu baada ya muhula wake wa kwanza kumalizika, wadau mbalimbali wameibuka na hisia tofauti wapo wale walioonesha kumuunga mkono lakini pia wapo wale walioonesha kutokubaliana na hoja hiyo

Mmoja wa waliojitokeza na kuipinga hoja hiyo kwa ukali na uwazi ni Askofu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe Askofu Dkt. Benson Bagonza ambaye amesema kilichozungumzwa na Askofu Dkt. Shoo si msimamo wa KKKT bali ni msimamo wake binafsi ambao pia pengine mipaka yake inapaswa kuishia kwenye Dayosisi yake pekee

"Nona KKKT imepamba moto kutokana na matamshi ya mmoja wa Maaskofu wake, kwa kimbelembele nilichonacho naomba umma wa Watanzania uelewe yafuatayo:-

(i) KKKT ina Mkuu mmoja tu (wa Kanisa ambaye ni Askofu Dkt. Alex Gehaz Malasusa), dereva wawili hawawezi kuendesha gari moja kwa wakati mmoja;

(ii) KKKT hakuna cheo kinaitwa 'Mkuu wa Kanisa mstaafu', tunaweza kuwa na cheo cha 'liyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa', hivi sasa tuna 'aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa' ambaye amechaguliwa tena kuwa Mkuu wa Kanisa, kama angekuwa mstaafu asingechaguliwa, inawezekana 'aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa' akachaguliwa kuwa Mkuu tena, sitashangaa aliyepita hivi karibuni kuchaguliwa tena;

(iii) Kama kuna mstaafu, 'astaafu', si lazima kuhudhuria; si lazima kusema, ukipenda, usipende kwa niaba, ukichukia, usichukie kwa niaba, kila ulimi una uwezo wa kuonja wenyewe;

(iv) KKKT ni shirikisho, siyo Kanisa moja, ukitaka kusema kwa niaba ya shirikisho, unashawishi siyo kuburuza, hatujashawishika na hatujakaa;

(v) Nampenda Rais Samia (Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) lakini sijatumwa na Kanisa, naweza kumpenda na kukikosoa chama chake (Chama cha Mapinduzi -CCM), naweza kukipenda chama chake nikamkosoa yeye, hayo nitayasemea Karagwe siyo penginepo, na nikiyasema, ni yangu na tumbo langu siyo ya Wanyambo wala Walutheri walio wenye vyama vyao (yaani wanaotoka kwenye vyama tofauti vya siasa) kwa Nyambo haturuhusu mgeni kupiga mluzi katika nyumba ya mwenyeji;

(vi) Kanisa lina wanachama wa vyama vyote na waumini wasio na vyama, CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo) msitutolee macho na CCM (Chama cha Mapinduzi) msishangilie, shoka lipo shinani, mti usiozaa matunda unakatwa;

(vii) Rais Samia (Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) ana uwezo wa kujiharibia, tusimharibie, CCM ina uwezo wa kujiharibia, haijaomba msaada wa kuisaidia kuharibu, lipo kundi linalodhani linamsaidia Rais Samia wakati linamharibia, lipo linalodhani linamharibia lakini linamjenga, anayesimama na 'haki' anamsaidia Rais Samia;

(viii) Tuna tatizo Kitaifa, kuna watu wanatumia Dini kueneza siasa, na kuna watu wanatumia siasa kueneza Dini, mimi si mmoja wa hao wawili (2), mimi natumia ujinga kueneza Dini na siasa, wajinga tu ndio wananisikiliza na kunifuata, wewe mjuaji kaa pembeni tuendelee na safari;

(ix) Nikisema jambo mkanishangilia, mnanipa kiburi cha kusema bila kufikiri, nidhamu ya washangiliaji huja kwa kutafakari, si kuhemka, mkishangilia, mnamnyima msemaji nidhamu ya kufikiri kabla ya kusema, anayesema kweli hahitaji kukumbuka alisema nini jana;

(x) Mungu analipenda Taifa hili (Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) kuliko mtu au chama chochote kinavyoweza kudai kulipenda, usiombe Mungu akuonyeshe anavyolipenda hili Taifa, ina gharama nzito kushuhudia Mungu anavyolipenda hili Taifa, hata anayerudi nyuma ana mbele anakoelekea, ukisifiwa kuwa na mbio, jihadhari usipitilize nyumbani kwenu" -Askofu Dkt. Bagonza

Andiko la Askofu Dkt. Bagonza bila shaka huenda likaibua hisia mseto kama ilivyokuwa tamko la Askofu Dkt. Shoo kutokana na ukweli na kwamba watu hao wawili wana ushawishi wao binafsi lakini pia ushawishi wao ni ngumu kuutenganisha na Kanisa la KKKT
nadhan hakuna jambo au wazo jipya wala fikra mbdala ambalo Baba Askofu Bagonza amelieleza zaidi ya kupingana kisiasa na Askofu mwenzie kitu ambacho ni kawaida kabisa.

Hata baada ya Askofu Malasusa kuchaguliwa tena kwenye wadhifa wa kanisa alionao hivi sasa, huyu Askofu wa Karagwe Dr.Bagonza aling"aka sana na kuandika kwamba kwenye uchaguzi wao wa kumchagua mkuu wa kanisa hilo huwa hawachagui wao bali kiongozi wa kanisa hilo huchaguliwa kutoka mahali Fulani ambako hakuweka wazi ni wapi.

Kiufupi Askofu Bagonza hua ana chuki binafsi sana dhidi ya maoni na mitazamo ya maaskofu wa kanisa hilo, lakini pia anatamani sana kua kiongozi mkuu wa kanisa hilo Tanzania.

Lakini ujuaji wake mwingi umemfanya akose ushawishi kabisa ndani ya kanisa hilo ispokua ana ushawishi kiasi nje ya kanisa hilo, ambao hata hivyo hauna athari zozote kisiasa nchini , kwasababu ana hulka ya kupinga mawazo na mitazamo huru ya wengine bila kueleza wazo na mtazamo mbadala na bora bora zaidi ya wengine 🐒
 
Back
Top Bottom