Pre GE2025 Askofu Bagonza: KKKT ina Mkuu wa Kanisa mmoja tu, Dereva wawili hawawezi kuendesha gari moja kwa wakati mmoja

Pre GE2025 Askofu Bagonza: KKKT ina Mkuu wa Kanisa mmoja tu, Dereva wawili hawawezi kuendesha gari moja kwa wakati mmoja

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nondo tupu! Wazazi wa Bagonza hawakupoteza ada zao.
Dr Bagonza we People of Karagwe are proud of You Sir ! A true son of Tanzania . We wish we had at two people of your Calibre in this Nation. Great thinker and a straight forward man. ELCT Karagwe did indeed pick a right person for the Job. Keep it Up Sir ! Nakumbuka uliwahi kuseoma huko siku za nyuma ( wakati wa Awamu ya 5) kwamba hakuna Mtu anayepaswa kukunyanganya Haki yako ya Kuongea ambayo ulipewa na Mwenyezi Mungu pekee na you were very right .
Wazazi wako tunawapongeza kwa kukulea na kukufanya uwe kama wewe hap Duniani.
 
Nondo tupu! Wazazi wa Bagonza hawakupoteza ada zao.
Dr Bagonza we People of Karagwe are proud of You Sir ! A true son of Tanzania . We wish we had at two people of your Calibre in this Nation. Great thinker and a straight forward man. ELCT Karagwe did indeed pick a right person for the Job. Keep it Up Sir ! Nakumbuka uliwahi kuseoma huko siku za nyuma ( wakati wa Awamu ya 5) kwamba hakuna Mtu anayepaswa kukunyanganya Haki yako ya Kuongea ambayo ulipewa na Mwenyezi Mungu pekee na you were very right .
Wazazi wako tunawapongeza kwa kukulea na kukufanya uwe kama wewe hap Duniani. Mungu akuzidishie hekima, ujasiri na Maisha marefu hapa duniani . You one of the rarest species of men in this Planet ! We need to protect you as we do for other rare species of creatures !
 
KKKT Ina MKUU MMOJA TU

Naona KKKT imepamba moto kutokana na matamshi ya mmoja wa Maaskofu wake. Kwa kimbelembele nilicho nacho naomba umma wa watanzania uelewe yafuatayo:

1. KKKT ina Mkuu mmoja tu. Dereva wawili hawawezi kuendesha gari moja kwa wakati mmoja.

2. KKKT hakuna cheo kinaitwa “Mkuu wa Kanisa Mstaafu”. Tunaweza kuwa na cheo cha “Aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa”. Hivi sasa tuna “aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa” ambaye amechaguliwa tena Mkuu wa Kanisa. Kama angekuwa Mstaafu asingechaguliwa. Inawezekana “aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa” akachaguliwa kuwa Mkuu tena. Sitashangaa aliyepita hivi karibuni, kuchaguliwa tena.

3. Kama kuna mstaafu, ASTAAFU. Si lazima kuhudhuria; si lazima kusema. Ukipenda, usipende kwa niaba. Ukichukia, usichukie kwa niaba. Kila ulimi una uwezo wa kuonja wenyewe,

4. KKKT ni shirikisho, siyo kanisa moja. Ukitaka kusema kwa niaba ya shirikisho, unashawishi siyo kuburuza, Hatujashawishika na hatujakaa.

5. Nampenda rais Samia, lakini sijatumwa na kanisa. Naweza kumpenda na kukikosoa chama chake. Naweza kukipenda chama chake nikamkosoa yeye. Hayo nitayasemea Karagwe siyo penginepo. Na nikiyasema, ni yangu na tumbo langu; siyo ya Wanyambo wala Walutheri walio wenye vyama vyao. Wanyambo haturuhusu mgeni kupiga mluzi katika nyumba ya mwenyeji.

6. Kanisa lina wanachama wa vyama vyote na waumini wasio na vyama. Chadema msitutolee macho na CCM msishangilie. Shoka lipo shinani, mti usiozaa matunda unakatwa.

7. Rais Samia ana uwezo wa kujiharibia. Tusimharibie. CCM ina uwezo kujiharibia; haijaomba msaada wa kuisaidia kuharibu. Lipo kundi linalodhani linamsaidia rais Samia, wakati linamharibia. Lipo linalodhani linamharibia lakini linamjenga. Anayesimama na HAKI anamsaidia rais Samia.

8. Tuna tatizo kitaifa: Kuna watu wanatumia dini kueneza siasa. Na kuna watu wanatumia siasa kueneza dini. Mimi si mmoja wa hao wawili. Mimi natumia ujinga kueneza dini na siasa. Wajinga tu, ndio wananisikiliza na kunifuata. Wewe mjuaji kaa pembeni tuendelee na safari.

9. Nikisema jambo mkanishangilia, mnanipa kiburi cha kusema bila kufikiri.
Nidhamu ya washangiliaji huja kwa kutafakari; si kuhemuka. Mkishangilia, mnamnyima msemaji nidhamu ya kufikiri kabla ya kusema. Anayesema kweli hahitaji kukumbuka alisema nini jana.

10. Mungu analipenda Taifa hili kuliko mtu au chama chochote kinavyoweza kudai kulipenda. Usiombe Mungu akuonyeshe anavyolipenda hili taifa. Ina gharama nzito kushuhudia Mungu anavyolipenda hili taifa.

Hata anayerudi nyuma ana mbele anakoelekea. Ukisifiwa kuwa na mbio, jihadhari usipitilize nyumbani kwenu.

Source: FB page yake

Pia soma
bora amemjibu shoo. ana kimbelembele sana na ule mdomo wake.
 
Yaani Ukisikia PHD ndio hizi sasa, nimesoma hadi nikarudia tena baadae nikakumbuka mchungaji wangu nae ana PHD ila nikaogopa kumwambia baba mchungaji wangu kuwa PHD aliyonayo ni fake aisee
Siyo kama zile za Fake za wanasiasa wa Kibongo wanazogawiwa na UDOM na vyuo vingine fake hapa nchini. Wanazidhalilisha hasa maana mawazo na matamshi yao huwa hayareflect hizo PhD zao za mchongo !
 
Askofu Shoo amekua wa hovyo sana!
Lakini huyu Mnyambo wa moto sanaa🤣🤣🤣
[3. Kama kuna mstaafu, ASTAAFU. Si lazima kuhudhuria; si lazima kusema. Ukipenda, usipende kwa niaba. Ukichukia, usichukie kwa niaba. Kila ulimi una uwezo wa kuonja wenyewe]
 
Askofu Shoo amekua wa hovyo sana!
Lakini huyu Mnyambo wa moto sanaa🤣🤣🤣
[3. Kama kuna mstaafu, ASTAAFU. Si lazima kuhudhuria; si lazima kusema. Ukipenda, usipende kwa niaba. Ukichukia, usichukie kwa niaba. Kila ulimi una uwezo wa kuonja wenyewe]
 
Askofu Shoo amekua wa hovyo sana!
Lakini huyu Mnyambo wa moto sanaa🤣🤣🤣
[3. Kama kuna mstaafu, ASTAAFU. Si lazima kuhudhuria; si lazima kusema. Ukipenda, usipende kwa niaba. Ukichukia, usichukie kwa niaba. Kila ulimi una uwezo wa kuonja wenyewe]
 
Huyu Askofu kumbe nae ana kichwa kizuri...nitaanza kumfuatilia...
Huyu alifaa awe Kanisa Takatifu la Mitume...
Wewe huyu ni Kichwa hasa, na uzuri wake ana uzalendo wa kweli katika kutetea haki na maslahi ya Taifa lake, ukiweka pembeni mambo ya Imani yake. Anatimiza wajibu wake vuziri kama Mchungaji wa Kiroho lakini pia asiyetaka watu wake walishwe kimwili na aliongeza kusema pia na Katika Vichwa vyao wajue haki zao na anafanya yote vizuri sana. I wish na wachungaji na Viongozi wengine wa Imani zote hapa Nchini wangeiga mfano huu wake. Unfortyunately wengine wengi wao ni wanafiki na wanatanguluza uchawa kwa viongozi ili washibishe matumbo yao na kupewa bahasha nono kwa kujikomba kwao
 
Lakini huyu Mnyambo wa moto sanaa🤣🤣🤣
[3. Kama kuna mstaafu, ASTAAFU. Si lazima kuhudhuria; si lazima kusema. Ukipenda, usipende kwa niaba. Ukichukia, usichukie kwa niaba. Kila ulimi una uwezo wa kuonja wenyewe]
Great thinker !
 
. Nampenda rais Samia, lakini sijatumwa na kanisa. Naweza kumpenda na kukikosoa chama chake. Naweza kukipenda chama chake nikamkosoa yeye. Hayo nitayasemea Karagwe siyo penginepo. Na nikiyasema, ni yangu na tumbo langu; siyo ya Wanyambo wala Walutheri walio wenye vyama vyao. Wanyambo haturuhusu mgeni kupiga mluzi katika nyumba ya mwenyeji.
Big Brain always inteligent
 
Hilo lidubwasha lako lina nn zaidi ya ubaguzi. Magu alifanya ubaradhuli mwingi si askofu wa padre aliyekemea kisa mRC mwenzao. RC ni wadini wabaguzi
Wewe sasa unaishi kwa unafiki tu, kwani humjui Askofu Niwemugizi ni kiasi gani alikuwa anakosaoa JPM mpaka wakakosana? Usiishi kwa hisia na mihemuko hiyo.
 
Tokenu kwenye madhehebu ni alama ya mnyama
Udhehebu sio ukristo
Mungu hayupo kwenye madhehebu
 
Unapomwasi shetani (kuwa traitor kwa shetani) kwa kukataa mifumo yake ya utendaji ya kishetani na kazi zake zote, na mambo yake, huo bila shaka ni uasi mtakatifu unaompa aliyeukataa uzima tele na kuketishwa na Yesu Kristo katika ufalme wake wa mbinguni ukiwa hapahapa duniani...!!

Martin Luther, mwasisi wa Kanisa la Kilutheri Duniani aliukataa ushetani wa Kikatoliki, akaiponya roho na nafsi yake na kutusaidia sisi wengi kupona pia...

Kwa hiyo huhitaji kupewa sababu hata moja achilia mbali hizo 100 maana hata sasa unaogelea kwenye "ujinga wa kiroho" na ndio maana huwezi kuelewa kama ambavyo hata sasa huelewi na hauko tayari kuelewa...!!
Akaishia kutengeneza vikundi vilivyozalisha matapeli kama Gwajima na wengineo.

Mara kadha wa kadha mchungaji wako Kimaro yule ya Dsm amesikika akiwapa wakatoliki na muslims maua yao, sasa jiulize kati ya yeye aliyesomea uchungaji na wewe maamuma , nani mjinga wa kiroho ?
 
Back
Top Bottom