Pre GE2025 Askofu Bagonza: Miaka mitano imepita lakini Dkt. Bashiru bado hana mpinzani

Pre GE2025 Askofu Bagonza: Miaka mitano imepita lakini Dkt. Bashiru bado hana mpinzani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
MIAKA 5 IMEPITA LAKINI Dr. BASHIRU BADO HANA MPINZANI!

Miaka 5 iliyopita, siku kama ya leo, Dr. Bashiru Ally, akiwa Katibu Mkuu wa CCM, alisema maneno mazito. Kwa maoni yangu, hayajajibiwa mpaka leo. Naheshimu kimya chake ambacho kina nguvu kuliko maneno yake. Ni juu yetu kudadavua uzito wa maneno yake yenye umri wa miaka 5 lakini yasiyochuja.

Katika kutafakari, niliandika hivi:

Duh!! Najua hili limegusa sana. Kila gazeti litaandika na sisi "mashabiki waandamizi" hatukosi cha kuchangia. Dr. Bashiru ni mtu makini, hawezi kukosa ufafanuzi. Anapojiandaa kufanya hivyo, ajue matamshi yake yanaweza kumaanisha moja ya haya au yote kwa pamoja:

1. Wapiga kura hawaamui mshindi, dola ndiyo inaamua ( Wananchi mpige kura, msipige, mtupatie kura au mtunyime, haisaidii lolote).

2. Tume ya Taifa ya Uchaguzi siyo huru na haina lolote. Dola ndiyo inaamua mshindi.

3. Chama tawala hakina uwezo kuliko dola na hakishiki hatamu. Dola ndiyo imeshika hatamu.

4. Dola haina uhuru wa kujiamulia, bali inaagizwa na chama tawala (inatumiwa).

5. Hata wabunge na madiwani wa upinzani walioshinda, ni kwa fadhila za dola.

6. Tunapoteza raslimali kuendesha uchaguzi uliokwishaamuliwa na dola.

7. Kwa kuwa dola ndiyo inaamua, siku ikiamua vinginevyo, hata chama tawala kitaondoka madarakani.

Naamini sivyo alivyomaanisha lakini masikioni ndivyo alivyosikika. Kuna haja ya kujisikiliza kabla hujasikilizwa.

Pimeni maneno haya kwa muktadha wa:

1. No Reform, No Election
2. Hatuondoki madarakani mpaka Yesu
arudi,
3. Hata mpigie kura kule kwingine, sisi
tutaunda serikali,
4. Atakayemtangaza mpinzani hana kazi
(Awe DED au Afisa wa umma)
5. Huwezi kumpigia mpinzani halafu ukadai uletewe maendeleo.

Kwenye kampeini tujifunze kuweka akiba ya maneno.
1741363073984.jpg
1741363068055.jpg
1741363085934.jpg
 
Dola ni nini ?
Labda tuanzie hapo kwanza...
 
Askofu Bagonza, saa ngapi unasoma biblia? Mbona uko busy na siasa? Si uvue majoho ya uaskofu uingie uwanja wa siasa, tunajua ww ni CHADEMA, si uchukue fomu gombea nafasi yoyote ya kisiasa alafu utakuwa umeingia uwanjani kucheza ngoma yenyewe.

Askofu, huoni unapata shida sana uko katika wito wa uaskofu, ila mawazo yako yapo siasani, njoo huku ucheze siasa, unachanganya mafaili askofu huoni, acha kuisema CCM, njoo uwanjani upambane na CCM uione ilivyo, maandishi tu hayasaidii kitu chochote.
 
Tatizo mulisikiliza heading mkaenda kuandika gazeti.

Mungesikiliza na content mgetumia hizo content kupata kura nyingi mno.
Hivi mkuu, kwa zama hizi hasa awamu ya 5, na awamu ya 6 ambapo watendaji wanaosimamia uchaguzi wapo, unatarajia wingi wa kura zitampa ushindi mgombea ?

Hayo mambo yaliishia kipindi Cha Kikwete, Tena kwa kuona aibu kuiba kura....
Sasa hivi Jimbo lolote kama CCM Ina maslai nalo...haijalishi wingi wa kura upo upande Gani ...ni lazima CCM atangazwe...
Na kwa hali hiyo...Kuna uwezekano pia akatangazwa mpinzani lakini kwa kificho kuwa ukienda bungeni kaa kimya....au kuhadaa Jumuiya ya kimataifa

Sasa huoni demokrasia imekufa vibaya Tanzania
 
MWALIMU NYERERE ANAMALIZA KWA USHAIRI KWENYE KITABU CHAKE.

UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.

Ole wake Tanzania Tusipoisaidia
Niwezalo nimelifanya kushauri na kuonya nimeonya.

tahadhali nimetoa ushauri na kuonya nimeshatoka kitini zaidi nifanye nini.

Namlilia Jaalia atumulikie njia Tanzania ailinde WAOVU wasiishinde.

Amina Tena Amina Amina Tena amina



UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.
MWALIMU JK NYERERE
 
Askofu aliingia kwenye Dini by accident. Angefaa kuwa mwanasiasa mzuri zaidi.
Kukosoa au kuzungumzia au kushauri kuhusu uongozi wa nchi hakuhitaji uwe mwanasiasa, hili ndilo tatizo la watanzania wengi. Tena hii kazi unaifanya vizuri zaidi unapokuwa siyo mwanasiasa by professional. Ni kazi ya kila mwananchi.
 
Askofu Bagonza, saa ngapi unasoma biblia? Mbona uko busy na siasa? Si uvue majoho ya uaskofu uingie uwanja wa siasa, tunajua ww ni CHADEMA, si uchukue fomu gombea nafasi yoyote ya kisiasa alafu utakuwa umeingia uwanjani kucheza ngoma yenyewe.

Askofu, huoni unapata shida sana uko katika wito wa uaskofu, ila mawazo yako yapo siasani, njoo huku ucheze siasa, unachanganya mafaili askofu huoni, acha kuisema CCM, njoo uwanjani upambane na CCM uione ilivyo, maandishi tu hayasaidii kitu chochote.
Bibilia inakataza kutenda dhambi,Hivyo,kiongozi bagonza hatakiwi kukaa kimya pale maovu anapoyaona na endapo akikaa kimya atakuwa ametenda dhambi kubwa sana
 
MIAKA 5 IMEPITA LAKINI Dr. BASHIRU BADO HANA MPINZANI!

Miaka 5 iliyopita, siku kama ya leo, Dr. Bashiru Ally, akiwa Katibu Mkuu wa CCM, alisema maneno mazito. Kwa maoni yangu, hayajajibiwa mpaka leo. Naheshimu kimya chake ambacho kina nguvu kuliko maneno yake. Ni juu yetu kudadavua uzito wa maneno yake yenye umri wa miaka 5 lakini yasiyochuja.

Katika kutafakari, niliandika hivi:

Duh!! Najua hili limegusa sana. Kila gazeti litaandika na sisi "mashabiki waandamizi" hatukosi cha kuchangia. Dr. Bashiru ni mtu makini, hawezi kukosa ufafanuzi. Anapojiandaa kufanya hivyo, ajue matamshi yake yanaweza kumaanisha moja ya haya au yote kwa pamoja:

1. Wapiga kura hawaamui mshindi, dola ndiyo inaamua ( Wananchi mpige kura, msipige, mtupatie kura au mtunyime, haisaidii lolote).

2. Tume ya Taifa ya Uchaguzi siyo huru na haina lolote. Dola ndiyo inaamua mshindi.

3. Chama tawala hakina uwezo kuliko dola na hakishiki hatamu. Dola ndiyo imeshika hatamu.

4. Dola haina uhuru wa kujiamulia, bali inaagizwa na chama tawala (inatumiwa).

5. Hata wabunge na madiwani wa upinzani walioshinda, ni kwa fadhila za dola.

6. Tunapoteza raslimali kuendesha uchaguzi uliokwishaamuliwa na dola.

7. Kwa kuwa dola ndiyo inaamua, siku ikiamua vinginevyo, hata chama tawala kitaondoka madarakani.

Naamini sivyo alivyomaanisha lakini masikioni ndivyo alivyosikika. Kuna haja ya kujisikiliza kabla hujasikilizwa.

Pimeni maneno haya kwa muktadha wa:

1. No Reform, No Election
2. Hatuondoki madarakani mpaka Yesu
arudi,
3. Hata mpigie kura kule kwingine, sisi
tutaunda serikali,
4. Atakayemtangaza mpinzani hana kazi
(Awe DED au Afisa wa umma)
5. Huwezi kumpigia mpinzani halafu ukadai uletewe maendeleo.

Kwenye kampeini tujifunze kuweka akiba ya maneno.
View attachment 3262791View attachment 3262792View attachment 3262793

Huu ndiyo Ukweli mchungu Sana
 
Back
Top Bottom