Askofu Dkt. Bagonza amshukia Lugola kwa kumfananisha Magufuli na Yesu. Asema hii laana lazima itafune mtu na Taifa

Bagonza, kama mtu kampa sifa mwenzake kumfananisha na Mola, hiyo laana ataibeba mwenyewe maana hakuna aliyemtuma! Mwambie muhusika moja kwa moja siyo kutishia taifa kwa makosa ya mtu mmoja! Kuna watu kwetu wanaitwa baba mtakatifu, mwakilishi wa mungu duniani; mbona husemi mzee! Dunia ni ngumu mzee muamuzi wa mambo Haya yupo na anaona.
 
Mtu wa kwanza kulaani matamshi ya lugola angekuwa ni yule aliyefananishwa na Yesu,cha ajabu kakaa kimya.Hii no hatari kwa Ligola na aliyesifiwa
 
Mungu wetu hafananishwi. Mungu wetu halinganishwi. Mungu wetu hashindanishwi. Ni ibada ya sanamu kupenda kitu kingine kuliko unavyompenda Mungu wako. Ni ibada ya sanamu kuchukia kitu kingine kuliko unavyomchukia shetani. Ni ibada ya sanamu kumlinganisha Muumbaji na uumbaji wake.
 
Mtu wa kwanza kulaani matamshi ya lugola angekuwa ni yule aliyefananishwa na Yesu,cha ajabu kakaa kimya.Hii no hatari kwa Ligola na aliyesifiwa
Na hatakaa akemee maana ana penda sana kusifiwa na kuabudiwa..
 

Askofu Bagonza: Enzi za Mwl Nyerere pamoja na kuwa na university 1 tu, tulidhibiti ujinga. Sasa ni zaidi ya universities 50 lakini wajinga wameongezek
 
Msemaji angekuwa wa kile chama cha konyagi,angeandika kuunga mkono.
 
Mkuu umeandika kama mwana ccm, au uko upande huo?
 
Mafisadi gani mkuu? Au na wewe ni matanga?
 
Tena wapo wengine wanaitwa Jesus wala hakemei na wapo wengine huko mtani wanaitwa akina God wala hasemi lolote, kisa kasikia magufuli kaja juu. Hakuna mwanadamu mwenye mamlaka ya kuwa Judgmental kwa mwanadamu mwenzake, Bagonza apunguze chuki ya kisiasa kwa magufuli.
 
Mh rais anapenda kutukuzwa ndio maana akina Lugola, Kessy na wengineo wasaka vyeo wanajua ukimsifu bwana mkubwa anakuteua.
Na wenyewe wanapiga mule mule sema huyu Kange amepitiliza

Kusifia kupo, hata mm nasifia sana tu na napenda kusifiwa pia ila kwa kiasi na kutufanya kufuru. Lugola anafanya kufuru, hapo ndio tunasema anafanya upuuzi, na Mh. Rais hapendi hilo kabisa, mm na wana dunia kibao tunaona makuu Mh. Rais anayofanyia nchi yetu, ni kweli anafanya kazi kubwa sana, na tunasifu kwa sana ila sio kukufuru, eg kumlinganisha Mh. Rais na Yesu, hapa hapanaa, na ni kufuru Lugola kafanya, Lugola anaonyesha ujinga wake uliopitiliza mara nyingi wazi wazi.. Bado kasamehewa kwa kosa kubwa, badala afunge mdomo wake uliokosa hekima anaendelea kujichafua bila kujua, naelewa Askofu Bogonza hampendi Mh. Rais, ila kwa hili mm nasimamia ukweli, Lugola kakufuru
 
Mkuu hajasema yeye ni yesu ila amesema NI KAMA.
 
Mkuu hajasema yeye ni yesu ila amesema NI KAMA.

Hakuna wa kumfananisha na Yesu, hiyo ni kukufuru, Amri ya Kwanza ya Mungu inasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na Usiwaabudu Miungu wengine,.. Ukisema tu fulani ni Kama Yesu, kosa kubwa hilo, Mungu wetu ni Mungu mwenye Wivu, hivyo kuna namna milioni na milioni za kusemea na kumsifia Mh. Rais anayofanya au lugha nyingine ya kumsemea makuu anayofanya, ila usiseme ni kama Yesu. Mimi ni supporter number one wa Mh. Rais wetu ila hili nakataa, Lugola anakufuru
 
MSikilizeni kangi mmulewe. Magufuli hawezi kufikia matendo ya Yesu Kristo hata kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…