Askofu Dkt. Bagonza amshukia Lugola kwa kumfananisha Magufuli na Yesu. Asema hii laana lazima itafune mtu na Taifa

Askofu Dkt. Bagonza amshukia Lugola kwa kumfananisha Magufuli na Yesu. Asema hii laana lazima itafune mtu na Taifa

Bagonza, kama mtu kampa sifa mwenzake kumfananisha na Mola, hiyo laana ataibeba mwenyewe maana hakuna aliyemtuma! Mwambie muhusika moja kwa moja siyo kutishia taifa kwa makosa ya mtu mmoja! Kuna watu kwetu wanaitwa baba mtakatifu, mwakilishi wa mungu duniani; mbona husemi mzee! Dunia ni ngumu mzee muamuzi wa mambo Haya yupo na anaona.
 
Mtu wa kwanza kulaani matamshi ya lugola angekuwa ni yule aliyefananishwa na Yesu,cha ajabu kakaa kimya.Hii no hatari kwa Ligola na aliyesifiwa
 
Anaandika Baba Askofu Rev.Dr.Benson Bagonza (PhD), Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
___________
Kufuru haina kinga. Kwa Wakristo, dhambi isiyosameheka katika Agano Jipya ni kumkufuru Roho Mtakatifu. Na katika Agano la Kale ni ibada ya sanamu (idolatry). Amri ya kwanza aliyopewa Musa inasema, "Mimi ni Bwana Mungu wako, usiwe na miungu mingine" (Kutoka 20:3-6).
_
Kufuru haina kinga duniani wala mbinguni. Ghadhabu ya Mungu iko wazi katika vitabu vyake vyote.

Tuzitendee haki kumbukumbu zetu;

1. Mwaka 2005 mjinga mmoja alitumia uhuru wake vibaya huko Denmark. Akachora katuni yenye kumdhihaki Mtume Muhammad (S.A.W). Dunia nzima iliwaka moto.

2. Mwaka 2010 mpuuzi mwingine huko Marekani akachoma moto Quran tukufu. Hakuna jiwe lililosalia juu ya jiwe.

3. Mwaka 2012 huko Mbagala utoto ukavuka mipaka. Msahafu ukakojolewa. Amani yetu ilitoweka kwa muda. Majivu yakawa majivu.

4. Huko Sumbawanga, msimu wa uchaguzi kama huu, ulimi wa mmoja uliteleza. Akaufananisha UTATU mtakatifu na mafiga matatu ya chama chake. Hapakutosha. Mzee Pinda (mtu wa amani), ana cha kusimulia mpaka leo.

Mungu wetu hafananishwi. Mungu wetu halinganishwi. Mungu wetu hashindanishwi. Ni ibada ya sanamu kupenda kitu kingine kuliko unavyompenda Mungu wako. Ni ibada ya sanamu kuchukia kitu kingine kuliko unavyomchukia shetani. Ni ibada ya sanamu kumlinganisha Muumbaji na uumbaji wake.

Hatumtendei haki Mungu kumlinganisha na aliowaumba. Hatuwatendei haki wale tuwapendao kwa kuonesha kuwa tunawapenda kuliko tunavyompenda aliyewaumba.

Walinzi na waangalizi wa imani (viongozi wa dini), kama hatuwezi kukemea hili (la Lugola) basi angalau tuchukie na tuonekane kweli tumechukizwa.!
Mungu wetu hafananishwi. Mungu wetu halinganishwi. Mungu wetu hashindanishwi. Ni ibada ya sanamu kupenda kitu kingine kuliko unavyompenda Mungu wako. Ni ibada ya sanamu kuchukia kitu kingine kuliko unavyomchukia shetani. Ni ibada ya sanamu kumlinganisha Muumbaji na uumbaji wake.
 
Mtu wa kwanza kulaani matamshi ya lugola angekuwa ni yule aliyefananishwa na Yesu,cha ajabu kakaa kimya.Hii no hatari kwa Ligola na aliyesifiwa
Na hatakaa akemee maana ana penda sana kusifiwa na kuabudiwa..
 
Anaandika Baba Askofu Rev.Dr.Benson Bagonza (PhD), Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
___________
Kufuru haina kinga. Kwa Wakristo, dhambi isiyosameheka katika Agano Jipya ni kumkufuru Roho Mtakatifu. Na katika Agano la Kale ni ibada ya sanamu (idolatry). Amri ya kwanza aliyopewa Musa inasema, "Mimi ni Bwana Mungu wako, usiwe na miungu mingine" (Kutoka 20:3-6).
_
Kufuru haina kinga duniani wala mbinguni. Ghadhabu ya Mungu iko wazi katika vitabu vyake vyote.

Tuzitendee haki kumbukumbu zetu;

1. Mwaka 2005 mjinga mmoja alitumia uhuru wake vibaya huko Denmark. Akachora katuni yenye kumdhihaki Mtume Muhammad (S.A.W). Dunia nzima iliwaka moto.

2. Mwaka 2010 mpuuzi mwingine huko Marekani akachoma moto Quran tukufu. Hakuna jiwe lililosalia juu ya jiwe.

3. Mwaka 2012 huko Mbagala utoto ukavuka mipaka. Msahafu ukakojolewa. Amani yetu ilitoweka kwa muda. Majivu yakawa majivu.

4. Huko Sumbawanga, msimu wa uchaguzi kama huu, ulimi wa mmoja uliteleza. Akaufananisha UTATU mtakatifu na mafiga matatu ya chama chake. Hapakutosha. Mzee Pinda (mtu wa amani), ana cha kusimulia mpaka leo.

Mungu wetu hafananishwi. Mungu wetu halinganishwi. Mungu wetu hashindanishwi. Ni ibada ya sanamu kupenda kitu kingine kuliko unavyompenda Mungu wako. Ni ibada ya sanamu kuchukia kitu kingine kuliko unavyomchukia shetani. Ni ibada ya sanamu kumlinganisha Muumbaji na uumbaji wake.

Hatumtendei haki Mungu kumlinganisha na aliowaumba. Hatuwatendei haki wale tuwapendao kwa kuonesha kuwa tunawapenda kuliko tunavyompenda aliyewaumba.

Walinzi na waangalizi wa imani (viongozi wa dini), kama hatuwezi kukemea hili (la Lugola) basi angalau tuchukie na tuonekane kweli tumechukizwa.!

Askofu Bagonza: Enzi za Mwl Nyerere pamoja na kuwa na university 1 tu, tulidhibiti ujinga. Sasa ni zaidi ya universities 50 lakini wajinga wameongezek
 
Anaandika Baba Askofu Rev.Dr.Benson Bagonza (PhD), Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
___________
Kufuru haina kinga. Kwa Wakristo, dhambi isiyosameheka katika Agano Jipya ni kumkufuru Roho Mtakatifu. Na katika Agano la Kale ni ibada ya sanamu (idolatry). Amri ya kwanza aliyopewa Musa inasema, "Mimi ni Bwana Mungu wako, usiwe na miungu mingine" (Kutoka 20:3-6).
_
Kufuru haina kinga duniani wala mbinguni. Ghadhabu ya Mungu iko wazi katika vitabu vyake vyote.

Tuzitendee haki kumbukumbu zetu;

1. Mwaka 2005 mjinga mmoja alitumia uhuru wake vibaya huko Denmark. Akachora katuni yenye kumdhihaki Mtume Muhammad (S.A.W). Dunia nzima iliwaka moto.

2. Mwaka 2010 mpuuzi mwingine huko Marekani akachoma moto Quran tukufu. Hakuna jiwe lililosalia juu ya jiwe.

3. Mwaka 2012 huko Mbagala utoto ukavuka mipaka. Msahafu ukakojolewa. Amani yetu ilitoweka kwa muda. Majivu yakawa majivu.

4. Huko Sumbawanga, msimu wa uchaguzi kama huu, ulimi wa mmoja uliteleza. Akaufananisha UTATU mtakatifu na mafiga matatu ya chama chake. Hapakutosha. Mzee Pinda (mtu wa amani), ana cha kusimulia mpaka leo.

Mungu wetu hafananishwi. Mungu wetu halinganishwi. Mungu wetu hashindanishwi. Ni ibada ya sanamu kupenda kitu kingine kuliko unavyompenda Mungu wako. Ni ibada ya sanamu kuchukia kitu kingine kuliko unavyomchukia shetani. Ni ibada ya sanamu kumlinganisha Muumbaji na uumbaji wake.

Hatumtendei haki Mungu kumlinganisha na aliowaumba. Hatuwatendei haki wale tuwapendao kwa kuonesha kuwa tunawapenda kuliko tunavyompenda aliyewaumba.

Walinzi na waangalizi wa imani (viongozi wa dini), kama hatuwezi kukemea hili (la Lugola) basi angalau tuchukie na tuonekane kweli tumechukizwa.!
Msemaji angekuwa wa kile chama cha konyagi,angeandika kuunga mkono.
 
Bagonza anafikili anaweza kuchukua nafasi ya mungu? Hawezi ku finally hukumu ya mungu kwa binadamu hata siku moja, pia akumbuke kuna watu wanaitwa yesu hapa duniani kwa maana hiyo hao hawatasamehewa kwa vile wamejiita jina la yesu?

Pia lazima ajue mfano sio lazima iwe kitu halisi,
Ujuaji anaotaka kujifanya anao Bagonza unamuondolea hadhi ya kuwa Askofu.

Kuna wanasiasa wanasema uongo na anajuwa wanasema uongo na wengine ni waumini wake mbona hatujaona andiko kuwakemea ili waache uongo kwa kuwa vitabu vya dini vinasema usimsemee mtu uongo, pia uongo ni zaidi ya mchawi, sasa hilo halijui?

Mapenzi yake kisiasa hayamzuii kuacha uaskofu ili aje apambane kama mwanasiasa kwa kuwa yeye hatakuwa wa kwanza, kuna Dr slaa, kuna marehem rwakatale kuna msigwa na wengine wengi.
Yeye anashambulia upande wa CCM tu je huko Upinzani ni watakatifu?

Maaskofu wa hivi laana zao watazibeba wenyewe maana mungu anaiona mioyo yao inavyohangaika na maovu wanayowaza kika siku.
Bagonza ajitathimini.
Mkuu umeandika kama mwana ccm, au uko upande huo?
 
Utatu mtakatifu ni mambo yaliyosukwa tu na wajanja! Kamwe huwezi kumgawa Mungu eti nafsi tatu!! Najibu swali! Alimlinganisha JPM na Yesu (nabii) kwa kuwa amejitoa mhanga kama Yesu alivyoteseka ili kuukomboa ulimwengu. Anaikomboa Tz kutoka mikononi mwa mafisadi. Ni hatari kwake ila amejitoa mhanga.
Mafisadi gani mkuu? Au na wewe ni matanga?
 
Bagonza anafikili anaweza kuchukua nafasi ya mungu? Hawezi ku finally hukumu ya mungu kwa binadamu hata siku moja, pia akumbuke kuna watu wanaitwa yesu hapa duniani kwa maana hiyo hao hawatasamehewa kwa vile wamejiita jina la yesu?

Pia lazima ajue mfano sio lazima iwe kitu halisi,
Ujuaji anaotaka kujifanya anao Bagonza unamuondolea hadhi ya kuwa Askofu.

Kuna wanasiasa wanasema uongo na anajuwa wanasema uongo na wengine ni waumini wake mbona hatujaona andiko kuwakemea ili waache uongo kwa kuwa vitabu vya dini vinasema usimsemee mtu uongo, pia uongo ni zaidi ya mchawi, sasa hilo halijui?

Mapenzi yake kisiasa hayamzuii kuacha uaskofu ili aje apambane kama mwanasiasa kwa kuwa yeye hatakuwa wa kwanza, kuna Dr slaa, kuna marehem rwakatale kuna msigwa na wengine wengi.
Yeye anashambulia upande wa CCM tu je huko Upinzani ni watakatifu?

Maaskofu wa hivi laana zao watazibeba wenyewe maana mungu anaiona mioyo yao inavyohangaika na maovu wanayowaza kika siku.
Bagonza ajitathimini.
Tena wapo wengine wanaitwa Jesus wala hakemei na wapo wengine huko mtani wanaitwa akina God wala hasemi lolote, kisa kasikia magufuli kaja juu. Hakuna mwanadamu mwenye mamlaka ya kuwa Judgmental kwa mwanadamu mwenzake, Bagonza apunguze chuki ya kisiasa kwa magufuli.
 
Mh rais anapenda kutukuzwa ndio maana akina Lugola, Kessy na wengineo wasaka vyeo wanajua ukimsifu bwana mkubwa anakuteua.
Na wenyewe wanapiga mule mule sema huyu Kange amepitiliza

Kusifia kupo, hata mm nasifia sana tu na napenda kusifiwa pia ila kwa kiasi na kutufanya kufuru. Lugola anafanya kufuru, hapo ndio tunasema anafanya upuuzi, na Mh. Rais hapendi hilo kabisa, mm na wana dunia kibao tunaona makuu Mh. Rais anayofanyia nchi yetu, ni kweli anafanya kazi kubwa sana, na tunasifu kwa sana ila sio kukufuru, eg kumlinganisha Mh. Rais na Yesu, hapa hapanaa, na ni kufuru Lugola kafanya, Lugola anaonyesha ujinga wake uliopitiliza mara nyingi wazi wazi.. Bado kasamehewa kwa kosa kubwa, badala afunge mdomo wake uliokosa hekima anaendelea kujichafua bila kujua, naelewa Askofu Bogonza hampendi Mh. Rais, ila kwa hili mm nasimamia ukweli, Lugola kakufuru
 
Kusifia kupo, hata mm nasifia sana tu na napenda kusifiwa pia ila kwa kiasi na kutufanya kufuru. Lugola anafanya kufuru, hapo ndio tunasema anafanya upuuzi, na Mh. Rais hapendi hilo kabisa, mm na wana dunia kibao tunaona makuu Mh. Rais anayofanyia nchi yetu, ni kweli anafanya kazi kubwa sana, na tunasifu kwa sana ila sio kukufuru, eg kumlinganisha Mh. Rais na Yesu, hapa hapanaa, na ni kufuru Lugola kafanya, Lugola anaonyesha ujinga wake uliopitiliza mara nyingi wazi wazi.. Bado kasamehewa kwa kosa kubwa, badala afunge mdomo wake uliokosa hekima anaendelea kujichafua bila kujua.
Mkuu hajasema yeye ni yesu ila amesema NI KAMA.
 
Mkuu hajasema yeye ni yesu ila amesema NI KAMA.

Hakuna wa kumfananisha na Yesu, hiyo ni kukufuru, Amri ya Kwanza ya Mungu inasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na Usiwaabudu Miungu wengine,.. Ukisema tu fulani ni Kama Yesu, kosa kubwa hilo, Mungu wetu ni Mungu mwenye Wivu, hivyo kuna namna milioni na milioni za kusemea na kumsifia Mh. Rais anayofanya au lugha nyingine ya kumsemea makuu anayofanya, ila usiseme ni kama Yesu. Mimi ni supporter number one wa Mh. Rais wetu ila hili nakataa, Lugola anakufuru
 
Hakuna wa kumfananisha na Yesu, hiyo ni kukufuru, Amri ya Kwanza ya Mungu inasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na Usiwaabudu Miungu wengine,.. Ukisema tu fulani ni Kama Yesu, kosa kubwa hilo, Mungu wetu ni Mungu mwenye Wivu, hivyo kuna namna milioni na milioni za kusemea na kumsifia Mh. Rais anayofanya au lugha nyingine ya kumsemea makuu anayofanya, ila usiseme ni kama Yesu.
MSikilizeni kangi mmulewe. Magufuli hawezi kufikia matendo ya Yesu Kristo hata kidogo.
 
Back
Top Bottom