Askofu Gwajima anamuonea Waziri Gwajima kijinga

Askofu Gwajima anamuonea Waziri Gwajima kijinga

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Ziko dawa, chanjo, na njia za matibabu ambazo zimeachwa kutumia wakati hapo mwanzo zilipitishwa na kuruhusiwa kutumiwa. Mfano, watu wameacha kutumia dawa kali kutibu minyoo, indocid, chloroquine na SP kutibu malaria, kuacha kutumia spirit kusafisha eneo la kuchoma sindano, kunyoa nywele za kinena wakati wa kwenda kwenye upasuaji, nk. Dawa, chanjo na njia za tiba zinabadilishwa na kuacha kutumiwa mara TU sayansi itakapogundua kuwa Ina madhara, haina faida au Kuna njia, dawa, chanjo mbadala nzuri zaidi ambayo inaleta matokeo bora kwenye jambo lile.

Sioni kosa la Waziri yuleyule, WHO ileile, TFDA ileile, TBS ileile, kukubali kuachana au kuongeza njia, dawa, au chanjo kwenye zile za awali. Huwezi kusema kwakuwa kuna penicillin kwa kutibu kaswende tusikubali aina nyingine za antibiotics kama erythromycin, azithromycin, ciproflaxin, etc.

Waziri Gwajima anakosa gani kutangaza dawa mpya na nzuri ya kutibu gonorhea, pumu, kisukari na covid-19 badala ya zile za zamani ? Kama kuna mtu anaemshangaa Waziri kwa hili basi mtu huyo ni ama mwehu au ana ajenda nyingine pana zaidi kuliko covid-19.

Tunapomtizama Askofu Gwajima msimtazame peke yake, watazameni pamoja na timu ya awamu ya tano iliyonyang'anywa usukani. Askofu na Polepole inawezekana wanatumika kama loud speaker TU kwenye mission fulani.
 
Hii vita ni ya kifamilia! Na bahati nzuri Rais nae anaifurahia. Hivyo ukiamua kumtetea Gwaji girl, kuna wadau wengine hapa watakuja kumtetea Gwaji boy.

Dawa pekee ya hii vita, ni kuwatenganisha tu. Aidha kumuondoa Gwaji girl kwenye hiyo Wizara (na hapa Gwaji boy atakua ameshinda pambano kwa tko), au kumsimamisha ubunge Gwaji boy (na hivyo Gwaji girl kuonekana ndiye mshindi)

Nje ya hapo, ni vijembe tu baina yao! mwanzo mwisho.
 
Mimi furaha yangu ni jinsi wanavyochambana kama machangudoa fulani hivi.
Waumini wa makanisa haya wote ni wale wenye shida hii na Ile. Wako tayari kusikiliza mipasho kanisani. Amri Inasema usisengenye!!!!! Na kusengenya ni kumsema vibaya mtu ambaye hayuko miongoni mwenu kwa wakati huo
 
Kama
Ziko dawa, chanjo, na njia za matibabu ambazo zimeachwa kutumia wakati hapo mwanzo zilipitishwa na kuruhusiwa kutumiwa. Mfano, watu wameacha kutumia dawa kali kutibu minyoo, indocid, chloroquine na SP kutibu malaria, kuacha kutumia spirit kusafisha eneo la kuchoma sindano, kunyoa nywele za kinena wakati wa kwenda kwenye upasuaji, nk. Dawa, chanjo na njia za tiba zinabadilishwa na kuacha kutumiwa mara TU sayansi itakapogundua kuwa Ina madhara, haina faida au Kuna njia, dawa, chanjo mbadala nzuri zaidi ambayo inaleta matokeo bora kwenye jambo lile.

Sioni kosa la Waziri yuleyule, WHO ileile, TFDA ileile, tbs ileile, kukubali kuachana au kuongeza njia, dawa, au chanjo kwenye zile za awali. Huwezi kusema kwakuwa kuna penicillin kwa kutibu kaswende tusikubali aina nyingine za antibiotics kama erythromycin, azithromycin, ciproflaxin, etc.

Waziri Gwajima anakosa gani kutangaza dawa mpya na nzuri ya kutibu gonorhea, pumu, kisukari na covid-19 badala ya zile za zamani ? Kama kuna mtu anaemshangaa Waziri kwa hili basi mtu huyo ni ama mwehu au ana ajenda nyingine pana zaidi kuliko covid-19.

Tunapomtizama Askofu Gwajima msimtazame peke yake, watazameni pamoja na timu ya awamu ya tano iliyonyang'anywa usukani. Askofu na Polepole inawezekana wanatumika kama loud speaker TU kwenye mission fulani.
Kama ndivyo alikua na ulazima gani gwagima mke kuleta mambo ya mkonoa baunsa na Amina chifupa kwenye agenda ambayo haikua na uhusiano na mambo binafsi?
Hapo inaonyesha hawaheshimiani.na mashemeji zake.
Kazi hiyo ya uwazili inaweza kukoma muda wowote na hiyo heshima ikaisha sasa ataenda kwa shemejie huku alimtolea mambo machafu hadhalani?

Pia viongozi wa kiafrika lazima wajifunze kuwa na misimamo na sio njaa tu, na kama wanataka kutetea njaa basi wawe wazi kuwa walikua wanalinda ugali wao na sio kuruka sarakasi kwenye mawe.

Kwani kujiuzuru wanaona shida gani?
Ni kwamba ulikua tofauti na mambo yamebadilika una achia wengine maisha yanaendelea.
 
Taperi gwajima afukuzwe kwenye chama na ubunge, na ashtakiwe kwa kesi ya uhaini
 
Hii vita ni ya kifamilia! Na bahati nzuri Rais nae anaifurahia. Hivyo ukiamua kumtetea Gwaji girl, kuna wadau wengine hapa watakuja kumtetea Gwaji boy.

Dawa pekee ya hii vita, ni kuwatenganisha tu. Aidha kumuondoa Gwaji girl kwenye hiyo Wizara (na hapa Gwaji boy atakua ameshinda pambano kwa tko), au kumsimamisha ubunge Gwaji boy (na hivyo Gwaji girl kuonekana ndiye mshindi)

Nje ya hapo, ni vijembe tu baina yao! mwanzo mwisho.
Wakumfukuza Rashid ubunge ni kumwonea.
Rashid askofu ana hoja kuwa waziri hana uhalali wa kuhamasisha chanjo kwani awali alipinga na aliabudu mizizi. Kwanini hili tunalikwepa?
 
Uswahili mwingi
Hao wanachambana kama wote wanawake yaani mpaka baba mkwe
Hawa watu wana bahati wanaishi kwenye society inayoendekeza mambo haya na ndio way of life
Kwa kweli kati ya wote. Babamkwe/Baba mzazi amekosea sana. Na hii inaonekana kwenye family hiyo Gwajima (askofu) ni untouchable.
 
Gwajiboy ana bit za kale eti choma chanjo afu tukuone baada ya miaka mitano utakuwaje??? wtf
 
Ziko dawa, chanjo, na njia za matibabu ambazo zimeachwa kutumia wakati hapo mwanzo zilipitishwa na kuruhusiwa kutumiwa. Mfano, watu wameacha kutumia dawa kali kutibu minyoo, indocid, chloroquine na SP kutibu malaria, kuacha kutumia spirit kusafisha eneo la kuchoma sindano, kunyoa nywele za kinena wakati wa kwenda kwenye upasuaji, nk. Dawa, chanjo na njia za tiba zinabadilishwa na kuacha kutumiwa mara TU sayansi itakapogundua kuwa Ina madhara, haina faida au Kuna njia, dawa, chanjo mbadala nzuri zaidi ambayo inaleta matokeo bora kwenye jambo lile.

Sioni kosa la Waziri yuleyule, WHO ileile, TFDA ileile, TBS ileile, kukubali kuachana au kuongeza njia, dawa, au chanjo kwenye zile za awali. Huwezi kusema kwakuwa kuna penicillin kwa kutibu kaswende tusikubali aina nyingine za antibiotics kama erythromycin, azithromycin, ciproflaxin, etc.

Waziri Gwajima anakosa gani kutangaza dawa mpya na nzuri ya kutibu gonorhea, pumu, kisukari na covid-19 badala ya zile za zamani ? Kama kuna mtu anaemshangaa Waziri kwa hili basi mtu huyo ni ama mwehu au ana ajenda nyingine pana zaidi kuliko covid-19.

Tunapomtizama Askofu Gwajima msimtazame peke yake, watazameni pamoja na timu ya awamu ya tano iliyonyang'anywa usukani. Askofu na Polepole inawezekana wanatumika kama loud speaker TU kwenye mission fulani.
Kwamba WHO waliikanusha kwanza penicillin halafu baadae wakaanza kuipigia chapuo tena?
Hizi chanjo zilikuwepo na alisema hazifai, sio kwamba hazikuwepo na tiba asili pekee ndio iliokuwapo.
 
Back
Top Bottom