Askofu Gwajima na Jerry Silaa waitwa kwenye Kamati ya Bunge kujieleza kwa kusema uongo na kushusha hadhi ya Bunge

Askofu Gwajima na Jerry Silaa waitwa kwenye Kamati ya Bunge kujieleza kwa kusema uongo na kushusha hadhi ya Bunge

Ngoja Tusubiri Mchuzi Uishe NYAMA ziko CHINI
1629554056063.jpg
1629554056379.jpg


Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Hao wabunge wote wanaonewa tu.

Chanjo ni hiyari na hii chanjo ni usanii tu haina maana yoyote.

Wabunge hawalipi kodi. Kiasi wanacholipia Kodi ni kidogo sana ila kikubwa zaidi ya 80% hakikatwi kodi.

Hii nchi haiwezi kupata maendeleo chini ya ccm.
 
Mwambieni tu awafukuze Ubunge ndo ndo atajua kilichokunja mkia wa mbwa.
Yeye mwenyewe Kongwa alibebwa na JPM,leo kaanza mdomo ili tu kulinda kibarua chake.
unakipi cha kumfanya ndugai wewe
 
Kwahiyo wewe umejigeuza mtetezi wa wapinga chanjo, na wasumbua wenye hiari ya chanjo sio, wao kukataa chanjo nu hiari yao ila sii kuwazuia wenye hiari au kuwapotosha wengine.
 
Spika wa Bunge amewaita Mbunge Josephat Gwajima na Jerry Slaa mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya bunge

Wanatakiwa kujibu tuhuma mbalimbali ikiwemo kusema uongo na kushusha hadhi na heshima ya bunge

Gwajima ametakiwa afike Dodoma Agosti 23 saa saba mchana, Slaa ametakiwa afike Agosti 24 Saa saba mchana

View attachment 1901574

Mbunge wa Kawe (CCM), Josephat Gwajima pamoja na Mbunge wa Ukonga (CCM) Jelly Silaa wameitwa mbele ya Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge ili kujibu tuhuma mbalimbali ikiwemo kusema uongo na kushusha hadhi na heshima ya Bunge.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Agosti 21, 2021 na Kitengo cha Mawasiliano Ofisi ya Bunge, imeeleza wabunge hao wameitwa mbele ya Kamati hiyo kwa agizo la Spika wa Bunge Job Ndugai.

“Wanatakiwa kufika mbele ya Kamati hiyo kwa mujibu wa kanuni ya 4 (1) (a) na (b) ya nyongeza ya nane ya Kanuni za Kudumu za Bunge, toleo la Juni 2020 ambayo inaipa mamlaka Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuchunguza mambo yanayohusu maadili ya wabunge yanayopelekwa na Spika” imesema taarifa hiyo.

Hata hivyo taarifa imeeleza kuwa, Mbunge Gwajima anatakiwa kufika kwenye Kamati hiyo siku ya Jumatatu Agosti 23, 2021 saa saba mchana na Mbunge Silaa anatakiwa kufika Jumanne Agosti 24 saa saba kamili mchana.

“Yeyote kati ya waliotajwa hatafika mbele ya Kamati kwa siku na muda uliotajwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake kwa mujibu wa kifungu cha 17 na 34 (1) (a) cha sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge, Sura ya 296, Toleo la mwaka 2020” imesema taarifa hiyo
Inapotokea wameitwa km hv huwa wanapewa nauli na pesa ya kujikimu km wanavyofanyiwaga ktk vikao vya kawaida???
 
Kwahiyo wewe umejigeuza mtetezi wa wapinga chanjo, na wasumbua wenye hiari ya chanjo sio, wao kukataa chanjo nu hiari yao ila sii kuwazuia wenye hiari au kuwapotosha wengine.
Kama nyie mnapigia kampen watu wachome...acha uf...a
 
Hii kamati ndio ndugu Pasco Mayalla aliwahi kuitwa nadhani, akabadilika sana toka aende huko
Alitishiwa kupotezwa, akawa mdogo kama piriton! Tangu siku alivyorudi akaenda Lumumba kukabidhi akili kwa Polepole yeye akabaki anatembea na kopo tu!
 
Kosa alilolifanya Gwajima ni kuamua kutumikia Mabwana wawili , Mbaya zaidi anaenda Kwa bwana huyu na masharti na taratibu za Bwana mwingine kitu ambacho hakipo. Akubali amekengeuka ama sivyo ataaibishwa mchana kweupe
Mungu hadhihakiwi
Yeye alishasema hawezi kuwa Mbunge wala Rais Hivyo ni kujishusha hadhi.
 
Jerry kusema wabunge watoe tozo kwenye mishahara yao imekuwa nongwa, khaaa! Na kila baada ya miaka 5 wanafunga mikataba ya ajira zao za ubunge wanapewa marupuru yao yote haijalishi mbunge ataendelea kwa vipindi vingapi? Tena hiyo hiyo serikali inayafanya mambo tofauti kabisa kwa wafanyakazi wake wengine fikiria walimu, makarani, askari kama yule aliye kuwa analalamika hadharani akisema mke wake ni mwalimu ana ahueni kuliko yeye. Ulinganishe watumishi wote hawa na wabunge ambao spika wao anamwita Jerry kwenye kamati kwa kosa la nafsi yake kumsuta na kuwaambia wenzake walipe tozo kutoka kwenye mishahara yao.

Kweli wabunge wetu wasingeona fahari mh Mwigulu akitutangazia kwamba tumekusanya bilioni kadhaa kutoka kwenye tozo ya miashara ya miezi 3 ya wabunge na fedha hizi tayari zimepelekwa kuchimba visima vya maji kadhaa kwenye vituo vya afya/ shule zilizo na changamoto ya huduma hiyo ya maji.
 
Back
Top Bottom