Askofu Gwajima amesema Mungu anayemtumikia alijitambulisha kwa majina tofauti tofauti kulingana na nyakati na jukumu husika.
Alijiita Jehova, Niko ambaye Niko, Mungu mwenyezi, Bwana wa majeshi nk
Hivyo mtumishi wa Mungu unaweza kufanya kazi yoyote ilimradi tu kazi hiyo siyo katazo la kibiblia.
Askofu Gwajima ametangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Kawe wilayani Kinondoni.
Maendeleo hayana vyama!
Awadanganye wanaoelewa polepole. Kwanza, ni kweli kabisa mtumishi wa Mungu anaweza kufanya kazi yoyote ilimradi tu kazi hiyo sio katazo la Mungu. Na katika context ya hoja yake sisi waumini pia inatuhusu. Hapa, tafsiri sahihi ya 'mtumishi wa Mungu' inapaswa kuwa kila anayeliitia jina la Yesu ni mtumishi wa Mungu, yaani sisi waumini wa Kikristo, kwa mujibu wa Biblical perspective, ni watumishi wa Mungu pia.
Kazi moja ya muhimu sana, ambayo Mungu amewapa watumishi wa Mungu kwa tafsiri ile ya wachungaji, maaskofu (hata mitume na manabii) ni kufanya "checks and balance". Hii ndio kazi ambayo akina Gwajima wanapaswa kuifanya. Na ili uweze kufanya "checks & balance" ni lazima ujiweke kando na vyama siasa. Kwa wanaolisheshimu jukumu hili la Kimungu, wanapopata msukumo wa kuingia kwenye siasa, jambo la kwanza na la haraka kufanya huwa ni kujivua uchunga kondoo wa Bwana. Hii ni kwa sababu maisha ya siasa yanazalisha dhambi kila siku.
Makanisa mengi yameweka kwenye Katiba zake marufuku kwa wachungaji wake kujiingiza kwenye siasa. Kwa wasiojua, hata marehemu Mama Rwakatare alipopata msukumo wa kuingia kwenye siasa, alihangaika kutaka kulikabidhi kanisa lake TAG ili yeye ajikite moja kwa moja kwenye siasa, lakini ilishindikana kwa sababu mbalimbali ambazo sio muhimu sana kuzitumia hapa.
Dk. Chakwera, president elect wa Malawi alikuwa Askofu Mkuu wa Malawi Assemblies of God kwa miaka mingi mpaka aliposikia wito wa kuingia kwenye siasa kwenye mwaka 2013. Alijiuzulu uongozi wa kanisa la kujiunga na chama cha upinzani ambako alienda kugombea uenyekiti na kushinda kwa kishindo, kabla ya mwaka 2016 kujitosa kugombea urais. Kwa hiyo wanaotumia mfano wa Dk. Chakwera katika suala hili la Gwajima watakuwa wanafanya fallacy!
Labda tukumbushane hili. Mfumo wa makanisa haya ya akina Gwajima, ni mfumo ambao unafanya makanisa yale kuwa sawa na kampuni binafsi. yaani, kanisa la 'Ufufuo na Uzima' ni mali binafsi ya Gwajima. Kwahiyo, anaweza kulitumia anavyotaka yeye mwenyewe hata kama Katiba inamzuia. Anayetaka kunibishia kabla hajafanya hivyo, akaulize 'Ufufuo na Uzima' ni lini wachungaji waliwahi kufanya uchaguzi wa Askofu Mkuu wakamchagua Gwajima! Ni imani yangu kwamba hata jambo hili la kujiiingiza kwenye siasa litakuwa sio shirikishi, amua mwenyewe! Kwa wenye akili nyingi wanaweza kujua haraka athari yake..
Je, Gwajima ameingia kwenye siasa na matumaini gani? Swali hili ni muhimu sana. Nimesikiliza interview yake na kitivi kimoja cha mtandaoni. Muelewe pia watu wajanja wajanja wa aina ya Gwajima, interview zao sasa hawafanyi na media serious, wanajua watabanwa maswali magumu watatibuliwa deal. Katika mahojiano yale amepigapiga siasa, na hajaweza kujieleza katika namna ambayo inamwingia haraka mtu ambaye yuko bold na kichwa chake kinaweza kuchekecha!
Tafakuri yangu inanituma kwenye hitimsho hili: Gwajima anaweza kuwa ametumwa au amejituma kugombea, kwa nia ya kwamba jina lake lisikike ndani ya CCM kuwa naye ni "mkerereketwa". Kwa wanaofuatilia siasa za CCM za hivi karibuni, watakubaliana na mimi kwamba makada na wasaka fursa wengi, wamegundua kuwa ukitia nia kwenye uchaguzi wa ubunge hata ukishindwa kuna uwezekano huko mbele ukapata uteuzi.
lakini, naamini Gwajima anafahamu kwamba kama JPM atashinda kwenye urais, Bunge linawasubiri akina Kessy kutimiza ile ahadi ambayo inasubiriwa kwa hamu na Ndugai, na Gwajima anafaa sana akiungana na Kessy kwenye huu mchezo! Sasa kwanini asipate hata ubunge wa kuteuliwa?