#COVID19 Askofu Gwajima: Ni jambo baya sana kuwapa Chanjo ya Corona Wanajeshi, Polisi na watu wa Usalama

#COVID19 Askofu Gwajima: Ni jambo baya sana kuwapa Chanjo ya Corona Wanajeshi, Polisi na watu wa Usalama

Ni hali ya hatari kubwa kwa ugonjwa huu unaouwa (ambalo ni tatizo la kisayansi) unapoachwa kufanyiwa siasa au mzaha.

Ni hatari zaidi hali hiyo inapoachwa kuendelea, wakati serikali iliyo na dhamana ya kutulinda, ikiwa imechagua kuwa kama mpenzi mtazamaji tu.

View attachment 1868361

Haiingii akilini ni vipi serikali kutumia nguvu kwenye kongamano la Chadema kwa sababu za kudhihibiti Corona lakini si huyu anayehamasisha watu kutochukua tahadhari!

Kwa mujibu wa maelekezo haya ya wizara ya afya:

View attachment 1868673

Ni wazi kuwa kwa makusudi Mh. Mbunge amedhamiria kufanya upotoshaji wa makusudi.

Kwa mwendo huu wa kuzikumbatia siasa uchwara zenye kuweka maslahi binafsi mbele tungali na safari ndefu sana.

-------
My take:

Uzi huu chini unaihusu sana serikali kwa sasa na hasa mheshimiwa SSH:

Mmeuita sana na kuutukuza,lazima uwashinde tu
 
Baada ya jana mbunge wa Kawe mh Gwajima kuwataka watanzania waikatae chanjo ya Corona leo wameibuka wabunge machachari wa CCM January Makamba na Dr Kigwangalla na kumjibu

Kigwangalla amemtaka Askofu Gwajima ajisomee majalada ya sayansi na kama hawezi basi aende ofisini kwake akampe twisheni kwa sababu yeye ni daktari wa binadamu kitaaluma.

Naye January Makamba amemtaka askofu Gwajima kuacha kutumia nafasi yake ya uongozi wa kiroho kuupotosha Umma

Mungu ni mwema wakati wote!
 
Mbona siku hizi za Korona wajinga mmeongezeka saana,

Jinga kabisa, Kanisa lifungwe kwa sababu zipi, Yule anahubiri kile kilichoko kwenye kitabu chake, na kitabu chake kinasema, hata baba yake mzazi akimzuia kuhubiri anaouhuru wa kumuona ni kama siyo baba yake tena, na huyo unayemsema, atausimamia ukweli wa kitabu anachokiamini na yuko tayari kukifia, utamtisha nini hapo?

Biblia ilionya juu ya siku za mwisho kwamba kutakuweko na chapa ya shetani na chapa hiyo ya shetani kwa atakayeikataa ataandamwa, hatauza wala kununua, atatengwa kama yatima, atateswa, lakini avumiliaye Hadi mwisho,huyo ataokoka

halafu wewe unaandika ujinga tu, mimi mwenyewe hapa stochanjwa na liwalo na liwe
Huu ndiyo unaitwa utapeli kwa kutumia neno la Mungu. Unaootosha wajinga wa neno la Mungu kwa kutumia maandiko.

Hata katika magumu gani sitamwacha Mungu. Nitawasikiliza wale ambao Mungu amewaleta kwetu ili kulihuisha neno lake.

Kamwe sitapumbazwa wala kupotoshwa na matapeli na walio wakala wa shetani, kama Gwajima, anayelitumia neno la Mungu kutimiza uovu na ukahaba wake.
 
Huu ndiyo unaitwa utapeli kwa kutumia neno la Mungu. Unaootosha wajinga wa neno la Mungu kwa kutumia maandiko.

Hata katika magumu gani sitamwacha Mungu. Nitawasikiliza wale ambao Mungu amewaleta kwetu ili kulihuisha neno lake.

Kamwe sitapumbazwa wala kupotoshwa na matapeli na walio wakala wa shetani, kama Gwajima, anayelitumia neno la Mungu kutimiza uovu na ukahaba wake.

Ufunuo wa Yohana 13:16-18
Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao;

tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake

Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.
 
Hatutaki wote mchanjwe, kwanza hazitoshi.
Tunachotaka ni muache upotoshaji mkiongozwa na askofu wenu uchwara gwajifix
Mwanzoni kabla chanjo hazijaja walikuwa wakizipigania zije na kusema chanjo ni hiari hivyo tusizuie wanaotaka kuchanjwa hivyo ziletwe wanaotaka kuchoma watachoma na wasiotaka wasichome, ila sasa baada ya chanjo kuja naona hawataki tena hiari wanataka wote tuchanjwe.
 
Habari!

Hili jambo nililisikia 2020 toka kwa waumini 2 wa Gwajima.

Mimi niko karibu na waumini kadhaa wa Askofu Gwajima ambapo kati yao 2 ninafanya nao kazi ofisi moja, idara moja. Na hao wote ni wachungaji wa kikundi (Ministry pastors) wa kanisa la Ufufuo na Uzima.

Aliamini huenda angerithi mikoba ya Magufuli 2025 lakini Magufuli ametangulia mbele za haki.

Je, atasubiri mpaka 2030 pindi atakapomaliza Rais Samia Suluhu?
Hapana.

Hataweza kusubiri 2030 bali atajaribu karata yake ya bahati 2025.

Msitegemee 100% kuwa Gwajima atamuunga mkono Rais Samia Suluhu kwa sasa.

Gwajima mtu mwenye akili nyingi anaweza kuipiga ngome ya mama na ikapigika. Ngoja tusubiri.

Hii ni tetesi hivyo naomba msiufute huu uzi, hauna dhamira ya uchochezi.
 
Habari!
Hili jambo nililisikia 2020 toka kwa waumini 2 wa Gwajima.
Mimi niko karibu na waumini kadhaa wa Askofu Gwajima ambapo kati yao 2 ninafanya nao kazi ofisi moja, idara moja. Na hao wote ni wachungaji wa kikundi ( Ministry pastors) wa kanisa la Ufufuo na Uzima.
Aliamini huenda angerithi mikoba ya Magufuli 2025 lakini Magufuli ametangulia mbele za haki.
Je, atasubiri mpaka 2030 pindi atakapomaliza Rais Samia Suluhu?
Hapana.
Hataweza kusubiri 2030 bali atajaribu karata yake ya bahati 2025.
Msitegemee 100% kuwa Gwajima atamuunga mkono Rais Samia Suluhu kwa sasa.
Gwajima mtu mwenye akili nyingi anaweza kuipiga ngome ya mama na ikapigika.
Ngoja tusubiri.
Hii ni tetesi hivyo naomba msiufute huu uzi, hauna dhamira ya uchochezi.
Pesa pesa pesaaaaaa... Bill Gates kakuona😀
 
Ni wazo baya sana kuwachanja chanjo ya Corona askari wa majeshi yetu kwa sababu hatujui usalama wa hizo chanjo.

Baba Gwajima amesema anapinga kwa 100% vyombo vya dola kuchanjwa kwa sababu tunaweza kupoteza taifa. Askofu Gwajima amesema haya Kanisani kwake leo.

Askofu Gwajima amewataka wafuasi wake na wapiga kura wa jimbo la Kawe wakatae kabisa kuchanja kwa sababu watapata hasara kubwa sana maishani.

" Naikataa kabisa chanjo ya Corona " amesisitiza baba askofu.

Chanzo: Mtandao wa You tube!
Wote wana kesi za kujibu. Ushahidi na uhalisia wa kesi ndiyo utakaotambua haki ya kila moja. Ni kosa kuingilia uhuru wa mahakama
 
Maagizo leo ni full frontal assault kwenda kwA Gwajima,,,,😂....Kwani si tumekubaliana tujenge uchumi kwanza?
 
Habari!
Hili jambo nililisikia 2020 toka kwa waumini 2 wa Gwajima.
Mimi niko karibu na waumini kadhaa wa Askofu Gwajima ambapo kati yao 2 ninafanya nao kazi ofisi moja, idara moja. Na hao wote ni wachungaji wa kikundi ( Ministry pastors) wa kanisa la Ufufuo na Uzima.
Aliamini huenda angerithi mikoba ya Magufuli 2025 lakini Magufuli ametangulia mbele za haki.
Je, atasubiri mpaka 2030 pindi atakapomaliza Rais Samia Suluhu?
Hapana.
Hataweza kusubiri 2030 bali atajaribu karata yake ya bahati 2025.
Msitegemee 100% kuwa Gwajima atamuunga mkono Rais Samia Suluhu kwa sasa.
Gwajima mtu mwenye akili nyingi anaweza kuipiga ngome ya mama na ikapigika.
Ngoja tusubiri.
Hii ni tetesi hivyo naomba msiufute huu uzi, hauna dhamira ya uchochezi.
Mropokaji huyo na urais wapi na wapi?
 
Back
Top Bottom