Askofu Gwajima: Tanzania inashindwa kuendelea mbele kutokana na kutokuwa na muendelezo wa utawala mmoja kwenda mwingine

Point ni njema ila kwa vile mama hatokei kanda fulani haruhusiwa kuasisi yale anayoyaona yanafaa katika uongozi wake,tuliwaambia mkatuona sisi yo wazalendo,mnaona sasa!
Hivi kwanini mnakaririshwa vibaya hivi unafikiri Gwajima ni iliterate kama wanaokutuma jaribuni kuchukua mawazo yanayojenga sio Gwajima amemshinda Mdee ndo imekuwa nongwa
 
Tangu Baba wa Taifa atatungazie kuwa kilimo ndiyo uti wa mgongo wa Taifa letu. Hakutaka kabisa kugusa madini. Kama kilimo kingewekewa mikakati ya kueleweka na kwa ardhi tuliyonayo tungekuwa tunalisha Afrika nzima kwa mazao mbalimbali.

Vyuo vya kilimo vingekua na short prommes za mafunzo kwa wakulima wanaofadhiliwa na vyama vyao vya ushirika.

Kila kijiji kingekua na nyumba na shamba la mfano ambalo wanafunzi wa vyuo vya kilimo wanakwenda field kwa miezi mitatu kufanya kazi na wananchi.

Maduka ya zana za kilimo kuleta za a za kisasa na wananchi kununua hata kwa mikopo.

Vyama vya ushirika kuendeshwa na wenye elimu kuanzia ya masoko, Fedha na public relations. Vijitafutie masomo nje ya nchi.
 
Gwajima kadata anahisi yupo madhabahuni ambapo ni ruksa kupitisha propaganda

Eti "tuwe na tafsiri yetu ya maendeleo" Kwanza sisi si tuliambiwa tupo uchumi wa kati?

Huo uchumi wa kati ulikuwa unakadiriwa kwa kuangalia itifaki zipi?

Tukiruhusu wanasiasa kama hawa 10 wawe wawakilishi wa wananchi huko bungeni basi nchi itakuwa iko mahala pabaya sana.

Anataka tuungane tukatae tafsiri ya maendeleo inayotambulika ulimwenguni kote halafu tutafute neno letu ambalo litakuwa linatufariji.

Hapo ni sawa na mwalimu anayeshindwa kufundisha wanafunzi wakafaulu akasema ili kuwa na idadi ya wafaulu wengi inatakiwa tuwe na tafsiri yetu ya ufaulu tusitumie tafsiri hii, hivyo kuanzia saizi kila atakayepata alama moja atahesabika kafaulu haijalishi hata kama yaliyobaki kakosa yote
 
Reactions: Pep
Hivi kwanini mnakaririshwa vibaya hivi unafikiri Gwajima ni iliterate kama wanaokutuma jaribuni kuchukua mawazo yanayojenga sio Gwajima amemshinda Mdee ndo imekuwa nongwa
Unaweza kuwa Literate kama Professor Lipumba,Palamagamba Kabudi,Gwajima na Ally Bashir wengineo lakini ujinga wa mawazo na upumbavu ukawa navyo kichwani
 
9we
Well said my friend!!!

Gwajima Josephat kaongea vyema kabisaaa, lakini given kwamba hoja yake ina lengo fulani lililojificha chini ya carpet kwa muda/kipindi hiki hiyo hoja yake hebu ikae pembeni tumuache Mh. Rais Samia Suluhu Hassan afanye yale anayoyaona yeye yanafaa kulifanyia Taifa kama walivyofanya watangulizi wake. Namuomba sana Gwajima aache kum-pre empty Rais wetu Samia.

Rais mstaafu Ally Hassan Mwinyi kipindi kileee alivyokwenda kumpongeza Hayati JPM kwa kazi nzuri anayoifanya alisema tumpe support JPM kwa yale anayoyafanya kwasababu kila zama na kitabu chake. Kwahiyo tumuache nae Rais Samia aandike kitabu chake kama walivyofanya watangulizi wake, tusimuingilie tafadhalini sana!!!

Halafu naomba nimkumbushe Gwajima Josephat kwamba kuwa na moja kitaifa ni wazo zuri lakini inategemeana na nyakati na majira pia. Kwa mfano, Kabla ya Mwl. Nyerere kugatuka mamlakani tulikuwa na mfumo wa chama kimoja lakini hali ikaja kubadilika na kuingia kwenye vyama vingi kutokana na nyakati.

Pia wakati wa Mwl. Nyerere tulikuwa na Public Enterprises lakini hiyo sera ikaja kubadilika kutokana na nyakati, tulikuwa na sera ya vijiji vya ujamaa lakkni ikaja kubadilika kutokana na nyakati.

Mwisho, hebu tumwache mama yetu Samia Suluhu Hassana tuone anatupeleka wapi kama tulivyowaacha watangulizi wake ukizingatia kuwa yeye amesema kipindi chake hiki ni awamu ya SITA.

Asante!
 
Ndo maana alkua anataka jpm atawale milele?

Akamfufue Basi arudi aendeleze, so uwa anajinadi anafufua watu.
 
Kawakilisha hoja nzuri, kabisaaaaaa! Taifa lisilo na dira ni sawa na jumba la uchunguzi wa mambo ya anga (observatory) lisilo na "telescope" (kiona mbali).
 
Sina shaka na uwezo wa kujieleza na ata kupambanua mambo wa Askofu Gwajima na leo nafikiri kaongea logic sana. Ni kweli kama Taifa tunapitia wakati mgumu sana mana kila Rais anayeingia anaanza moja na wakati huo tunakuwa tayari tuko mbele ila tunarudishwa kuanza upya.

Ni vema kuwa ata na vision ya miaka 30 na kila chama waingize hiyo ktk Ilani yao ili yyte anayeshinda akute tayari kuna mambo ambayo lazima ayakamilishe na lazima aanze nayo ktk kuyaendeleza pale alipoishia mtangulizi wake.

Ili tuweze kufanikiwa haya yote ni wazi tunahitaji katiba mpya ambayo pia itamuelekeza Rais kuangalia zaidi vision ili tuweze kufikia lengo.

Kongole sana kwa Askofu Gwajima, naamini ataendelea kujiweka tofauti na genge na wanafiki.
 
Gwajima anashindwa kutambua kwamba vision namba moja ya taifa ni katiba halafu hayo mengine yanafuata.

Gwajima anashindwa kutambua tatizo mama la nchi hii ni ccm na viongozi wengi wanafiki kama yeye utaendelea vipi kama taifa wakati viongozi hawapatikani kwa kura za wananchi bali kwa masanduku ya kura zakutengeneza stationary ?

Gwajima anashindwa kutambua kuwa awamu ya tano ndiyo awamu pekee iliyoharibu nchi kiasi cha kuondoa hata ustaarabu wa kawaida wa nchi na nchi kutawaliwa kishetani.

Pengine jibu pekee tunaloweza kupata kutoka kwenye hoja ya Gwajima ni kwamba na yeye amepata AQCQUIRED STUPIDITY
 
Kweli kabisa mkuu, tuna shida kubwa sana ya kushindwa kuchukua mawazo ya mtu kwasababu aliyetoa mawazo tunamchukia.
 
naam Askofu amegusa penyewe. yani tunavyoenda ni sawa na timu ya mpira isiyokuwa na falsafa yake ya uchezaji (kwa wale wapenzi wa soka wananielewa hapa)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli mtu wa Mungu watu wabaya husahau kusimamia sheria mama(katiba ya nchi) Gwajima alitafakari hilo.
 
Imeandikwa wapi vilee! Labda kweli lkn pia huwezi kuwatumikia mabwana 2. Nikifikisha miaka 50 nafungua huduma yangu ya soda ya upako
 
Askofu Rashid ana point kidogo ... hasa kwa Tanzania ambayo imeongozwa na Chama Kimoja miaka yote. Kama kweli wanatekeleza Ilani ya CCM inakuwaje kunakuwa na tofauti za kimtazamo kati ya awamu na awamu?

Eti anadai Waislamu wenzau .... Askofu Rashid bwana......!!
 
Haya mambo angetakiwa aongee wakati JPM yupo kwenye power
 
Tatizo ni bunge... Mpango wa taifa na Dira ya taifa ndio vipo haijalishi Rais gani kaingia.

Mawaziri wakidai bajeti wabunge wanapaswa kugoma yaliyomo kwenye mpango wa taifa, ilani, na dira ya taifa ndio yapitishwe.

Sasa ilani inasema katiba mpya afu Rais anaingia anadai sio ajenda yake..... Hapo ndio ilipaswa wabunge wakatae bajeti ya serikali yake mpaka aheshimu ilani yake. Sasa kma wabunge wanapiga makofi tu utamlaumu Rais?

Bunge ni dhaifu period
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…