Askofu Gwajima: Tanzania inashindwa kuendelea mbele kutokana na kutokuwa na muendelezo wa utawala mmoja kwenda mwingine

Askofu Gwajima: Tanzania inashindwa kuendelea mbele kutokana na kutokuwa na muendelezo wa utawala mmoja kwenda mwingine

Du Wanapata shida sana na kifo cha mtukufu wanataka vyote alivyotaka mtukufu viendelezwe hata kama havina tija. Yeye mtukufu alivunja vunja vyote vya watangulizi wake na kuanza vyake ambavyo vilikuwa wala havufuati mpango wa taifa wa maendeleo wala CCM wala alichotaka kupeleka nchi nako hakujulikani. Rais wa sasa atafuataje kwenda kulingamiza Taifa la hasha nchi hii ni ya wote.
Watukome!
 
Nimesikiliza, jamaa kaongea point kubwa tangu Bunge lianze, kila Rais anakuja na mishe zake, anaharibu mfumo uliopo anaanza upya, mfano jiwe kaja kafumua fumua kila kitu , mfumo wa Elimu kafumua , mfumo wa biashara kaufmua ,mfumo wa utumishi kaharibu haribu huko na kabla hata hajaseti mambo akafa ....yaan mnarudi nyuma maili buku.

Kwa kweli tunatakiwa tuwe na maono ya kimkakati aisee, kuwe na long run plan na short run plan, wakat wa uchaguz kila chama mbali na agenda zao lazima waonyeshe jinsi watakavyokamilisha agenda za kimkakati , na hapa ndo umhimu wa katiba mpya!

Hatuwezi kuendelea Kwa kutegemea mawazo ya mtu mmoja kuwaza anayotaka yeye yawe..... Anaharibu lililopo na hata kuvunja katiba ili atimize anayotaka yeye , aaah.

Mfano mradi wa Bandari wa Bagamoyo Kwa namna yyte Ile ni wa muhimu, Bandari ya DSM tayari ipo congested na overwhelmed na pia inaelekea kuwa beyond rehabilitation. Ni heri tujadili kwamba tutafte wapi hela ya kujenga tuachane na wahisani wenye masharti magumu , na sio kuupiga chini moja Kwa moja!
Ila huwa tunaambiwa wanatekeleza ilani sikuwai jua kua nchi huwa inaongozwa Kwa matakwa ya raisi anataka nn ,kumbe ilani ni useless
 
Nimesikiliza, jamaa kaongea point kubwa tangu Bunge lianze, kila Rais anakuja na mishe zake, anaharibu mfumo uliopo anaanza upya, mfano jiwe kaja kafumua fumua kila kitu , mfumo wa Elimu kafumua , mfumo wa biashara kaufmua ,mfumo wa utumishi kaharibu haribu huko na kabla hata hajaseti mambo akafa ....yaan mnarudi nyuma maili buku.

Kwa kweli tunatakiwa tuwe na maono ya kimkakati aisee, kuwe na long run plan na short run plan, wakat wa uchaguz kila chama mbali na agenda zao lazima waonyeshe jinsi watakavyokamilisha agenda za kimkakati , na hapa ndo umhimu wa katiba mpya!

Hatuwezi kuendelea Kwa kutegemea mawazo ya mtu mmoja kuwaza anayotaka yeye yawe..... Anaharibu lililopo na hata kuvunja katiba ili atimize anayotaka yeye , aaah.

Mfano mradi wa Bandari wa Bagamoyo Kwa namna yyte Ile ni wa muhimu, Bandari ya DSM tayari ipo congested na overwhelmed na pia inaelekea kuwa beyond rehabilitation. Ni heri tujadili kwamba tutafte wapi hela ya kujenga tuachane na wahisani wenye masharti magumu , na sio kuupiga chini moja Kwa moja!
Na ndiyo maana tumepiga kelele saana kuwa hii nchi inayohitaji katiba mpya itakayojenga mfumo dhabiti tukiwa tunamaanisha tuwe na sheria zinazomuongoza rais anayeingia kufuata vipaumbele vya taifa na sio vipaumbele vya 'one man show' mwisho wa siku mtu mmoja anasimamisha mradi wa gesi anarukia mradi wa maji.
 
Chidi bwayi hajaridhika namna raia walivyoteswa na dikteta uchwara, uchaguzi ukifanyika kwa haki watu kama rashidi hawatanusa hata harufu ya bunge...
Si ndio maana anataka muendelezo, maana anajua bila huo hatarudi
 
Wote hao hakuna kabisa cha maana,,
Kinachotakiwa ni katiba bora na uwazi+uwajibakaji tu
 
Mi nafikiri maendeleo ya kitu au jambo lolote, linaanza na wewe mwenyewe

Alichozungumza jamaa Ni jambo la muhimu Sana na pengine kwa siku za usoni linaweza kutokea

Lakini, muhimu zaidi wakati tunasubiri unatakiwa kuanzia ngazi ya chini, hapa nazungumzia familia

Lengo ni kuwa na maisha bora, hivyo kama mzazi au mlezi hakikisha unaweka malengo ya juu ya familia yako iweje alafu unatekeleza

Hatimaye hata mwisho wako unapofikia unakuwa katika Hali ya jambo ulilotaka kufanya japo halijatimia kwa ukubwa wake lakini umeonesha uthubutu na sio 'kulalamika'

Mwisho, haya tunayoyakudia yatokee kwa % kubwa hatutayashudia
Tunatakiwa kuweka misingi.
 
Sasa Gwajima hilo umeongea mbona lipo wazi na ni marais wanaotokana na chama chako wenye kufanya hivyo...

Hilo jambo wala hukupaswa kusubiri bunge kulitamka, ungeliwakilisha tu ndani ya chama chako kwenye vikao vyenu...
 
Mimi huwa simkubali huyu jamaa lakini katika hili kaongea ukweli kabisa na hilo ndio tatizo letu. Tuchukulie mfano Dubai wao waliweka malengo wanataka kuwa number one kwa kila kitu hawataki number 2 kwa kila wanalofanya, kama ndege, airport, utalii na sijui bandari na mengi tu lakini sio kwamba ndio wamekuwa number one kwa kila kitu lakini hayo ndio malengo yao na kila mtu apiganie hayo.

Sasa sisi kama Tanzania ni lazima tujiwekee vision je lipi tutakaloweza kututoa hapa na kutupeleka pale. Kama tunataka tuwe number one kwa kilimo Africa, tunataka tuwe nchi yenye elimu bora, afya bora na hii mifano tu basi iwe ni ilani ya kila chama iwe sharti mengine ya nyongeza kuboresha sawa tu lakini washindane sera za kutufikisha katika vision yetu. Naunga mkono hoja
Haya yaliyo tufikisha ni udhaifu wa katiba yetu sisi wenyewe ya 1977, wa TZ Wenzangu mkae mkijua kupititia katiba ambayo ndio muongozo wetu wanamna gani tunataka kuongozwa ili hayo yasijirudie turudi kwenye rasimu ya katiba ya Mzee Warioba ambayo wananchi walishirikiswa otherwise tukaendelea kuimba ngonjera hizo hizo hadi kiama
 
Mbunge wa Jimbo la Kawe Josephat Gwajima akitoa mchango kuhusu hotuba iliyotolewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amesema nchi nyingi za Kiafrika zimekuwa haziendelea kwa kasi ya maendeleo kutokana na kushindwa kutumia rasimali kwani inaendana na 'manpower'.

Pia ameeleza kuwa Tanzania inashindwa kuendelea mbele kwa kasi kwasababu hakuna muendelezo wa Regime moja kwenda nyingine ambapo kila Rais anaingia madarakani na mipango yake hivyo huathiri maendeleo ya ukuaji wa mipango iliyoanzishwa.

Gwajima amtolea mfano Nyerere alietawala miaka 20 na kuacha viwanda 411, alipokuja Mwinyi aliboresha baadhi ya mambo lakini hakuendelea na wazo la viwanda na alipoingia Mkapa akauza vyote kwa kuvibinafsisha hivyo kukosa muunganiko kati ya 'regime' ya kwanza na regime ya tatu.

Gwajima amesema watakesha kama hamna huo muunganiko kwani hata Rais wa awamu ya nne hakushughulika na viwanda, bali mambo mengine lakini awamu ya tano akaamua kushughulika na viwanda, vilevile ambavyo awamu ya tatu ilivibinafsisha na kuviuza.

Gwajima amesema ni hatari kwasababu katiba inampa nafasi kila Rais anayeingia madarakani kwa namna yake, hekima yake na kwa namna anavyotafasiri yeye maendeleo.

Amesema siku moja atakapopatikana Rais ambaye hayuko sawasawa watu wataishia kulia na kutoa ombi la kuwa na vision ya kuwa na miaka 50 ya Taifa na anapoingia Rais lazima ilani ya chama chake izungumze mambo ambayo Taifa imejiwekea kama maono.

Gwajima amehoji endapo akatokea Rais ambae anafanya mambo yake yasiyo kwenye ilani kama kuna mtu wa kumuuliza mwenyekiti wa chama cha mapinduzi na Amiri Jeshi mkuu!



Inashindwa kuendelea kutokana na kuwa na matapeli kama yeye kwenye uongozi wakati ni mwizi na tapeli wa kawaida anayepaswa kunyea debe.
 
Hii nchi swala la maendeleo tusahau kabisa

Huu ndio ukweli au nasema nasema uongo ndugu zangu

Hii nchi inaongozwa kwa muda mrefu na watu wasio na uelewa kabisa wa Dunia ya kisasa,hebu fikiria channel za YouTube zote ni free kasoro zinazomilikiwa na watanzania walioko Tanzania
  • Nimemuelewa Ask. Gwajima, nafikiri maelezo yake yanasema “TUNATAKA KATIBA MPYA”, ameongeo kimsimbo zaidi ila maelezo yake yanasimbua kila kitu. Kama kila kila Rais akiingiia aliongoza kwa namna yake... hekima zake na utashi vinaamua vipaumbele maana yake... Kwa akili ya kawaida ‘maono ya miaka 50 au 30’ yatatekelezwa vipi katika utawala wa katiba ambayo inaacha mwanya wa kila Rais kuongoza kwa namna yake? Askofu hapa ‘anatutonya’ kwamba katiba tuliyonayo haifai. Inashindwa kulazimisha mwendelezo wa tawala moja na nyingine. Bila utuo tutabaki kuwa na mipango mingi kwenye makaratasi, linaanzishwa hili linaachwa. Katiba hii inaruhusu kila ‘steringi kuja na mapigo’ yake , kama tunataka mapigo saresare katiba mpya inahitajika.
  • Kwani hatujawahi kuwa na maono? Tumewahi na tunayo yaliwekwa miaka 20+ iliyopita : THE TANZANIA VISION 2025, mpango ambao uliandikwa miaka ya tisini na kitu. Maono yanazungumza vitu vingi vitamu, mpaka najiuliza ni sisi wabongo ‘tumetunga’ ama vipi, ni zama za Ndg. Rais Mkapa, ni maono hayo. Ndani humo kuna mambo ya utawala bora, Maendeleo ya TEHAMA, Elimu, Sayansi na Teknolojia, Viwanda, Kilimo: kama vitu vilivyotiliwa mkazo.
  • Hakuna mwendelezo wa dhati katika matendo. Tumekuwa watamu katika kuunda na kutunga mipango kwenye makaratasi. Kuna sera tamu-tamu zilizotungwa ili kuirejelea hayo maono ya 2025, tatizo ni utekelezaji na huku ‘kuongoza kwa namna yake’ .Kuna sheria zingine zinatungwa na zinajichanganya na maono, kwa sababu zinatungwa kwa ajili ya watu fulani– tunashida, shida ya mfumo.
  • Maono ya 2025, ambayo babu zetu walitunga (kama wewe ni kizazi cha ‘dotikom‘ — umezaliwa 1990s) yanazunguzia maendeleo ya TEHAMA, kuwa na mtanzania mwenye elimu na weledi wa kutosha kiasi cha kuwa na umahiri na ushindani katika soko la hapa ndani na duniani kwa ujumla. Sheria zikitungwa ilikukomesha watu fulani inaharibu mtiririko na muunganiko wa maono yetu. Kwa mfano, kumiliki chaneli ya You Tube kuwa gharama kubwa kwa Tanzania na vifurushi vya data, na sheria zingine zingine zinasimbua nini... Zinatoa maana ya kwamba wakati watunga maono waliona mbali, na walikuwa na uwezo huo wote— kuona mbali na karibu; waendeleza maono wana miopia, haoni mbali wanaona karibu tu! Wapi “WAPI KILIMO KWANZA” ? Wapi “BIG RESULT NOW, BRN”?
  • Maono yashikamanishwe na falsafa, katiba, sera, sheria na elimu ya nchi. Maono yasijulikane na viongozi na watumishi wa serikalini pekee, hata mtoto wa chekechea anatakiwa aungamanishwe na “jambo letu la kitaifa”. Tatizo mipango mingi inafeli kwa sababu ya maono ya Taifa kushikiliwa na watu wachache na kuwa na mzigo nayo ilihali ‘wananzengo’ hatuelewi kinachoendelea, siasa chafu zinasababisha kutunga sheria zinazokomoa hawa ili kuneemesha wale. Mbaya zaidi, siasa chafu, hazioani kabisa na maono.
  • Tanzania Nchi yangu! Tunahitaji katiba mpya, kama hili hatulioni tutarajie zaidi kuwa na maendeleo ya nasibu, kuendelea kutokana na namna ya ‘kuongoza kwa aina yake’!
  • Screenshot_20210413-001101.png
 
Mbunge wa Jimbo la Kawe Josephat Gwajima akitoa mchango kuhusu hotuba iliyotolewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amesema nchi nyingi za Kiafrika zimekuwa haziendelea kwa kasi ya maendeleo kutokana na kushindwa kutumia rasimali kwani inaendana na 'manpower'.

Pia ameeleza kuwa Tanzania inashindwa kuendelea mbele kwa kasi kwasababu hakuna muendelezo wa Regime moja kwenda nyingine ambapo kila Rais anaingia madarakani na mipango yake hivyo huathiri maendeleo ya ukuaji wa mipango iliyoanzishwa.

Gwajima amtolea mfano Nyerere alietawala miaka 20 na kuacha viwanda 411, alipokuja Mwinyi aliboresha baadhi ya mambo lakini hakuendelea na wazo la viwanda na alipoingia Mkapa akauza vyote kwa kuvibinafsisha hivyo kukosa muunganiko kati ya 'regime' ya kwanza na regime ya tatu.

Gwajima amesema watakesha kama hamna huo muunganiko kwani hata Rais wa awamu ya nne hakushughulika na viwanda, bali mambo mengine lakini awamu ya tano akaamua kushughulika na viwanda, vilevile ambavyo awamu ya tatu ilivibinafsisha na kuviuza.

Gwajima amesema ni hatari kwasababu katiba inampa nafasi kila Rais anayeingia madarakani kwa namna yake, hekima yake na kwa namna anavyotafasiri yeye maendeleo.

Amesema siku moja atakapopatikana Rais ambaye hayuko sawasawa watu wataishia kulia na kutoa ombi la kuwa na vision ya kuwa na miaka 50 ya Taifa na anapoingia Rais lazima ilani ya chama chake izungumze mambo ambayo Taifa imejiwekea kama maono.

Gwajima amehoji endapo akatokea Rais ambae anafanya mambo yake yasiyo kwenye ilani kama kuna mtu wa kumuuliza mwenyekiti wa chama cha mapinduzi na Amiri Jeshi mkuu!



Gwajima si askofu bali askopo
 
Gwajima asituchose hapa.

Kashindwa kutununulia nyavu za kuvulia samaki deep sea wana Kawe akama alivyoahidi. Kashindwa kutupeleka wana Kawe Birmingham kula bata kama alivyoahidi. Mafuriko kwenye barabara za kule Boko hata hatusemi.

Yote tisa, kumi kashindwa hata ku perform core activity yake ya kufufua watu - kamuacha rafiki yake mpendwa Magufuli azikwe tu hivi hivi wakati ana kipawa cha kufufua kweli!!
Lakini umeelewa alichoongea mkuu

Kaongea point hakuna haja ya kupinga kila kitu
Siipendi ccm Ila jamaa kaongea point kubwa Sana

I have learned to look things in a bigger perspective ways
 
Halafu cha kushangaza wote ni wa kutoka maccm lakini bado anaharibu kila kitu badala ya kuendeleza alipoishia mwenzie.
Nimesikiliza, jamaa kaongea point kubwa tangu Bunge lianze, kila Rais anakuja na mishe zake, anaharibu mfumo uliopo anaanza upya, mfano jiwe kaja kafumua fumua kila kitu , mfumo wa Elimu kafumua , mfumo wa biashara kaufmua ,mfumo wa utumishi kaharibu haribu huko na kabla hata hajaseti mambo akafa ....yaan mnarudi nyuma maili buku.

Kwa kweli tunatakiwa tuwe na maono ya kimkakati aisee, kuwe na long run plan na short run plan, wakat wa uchaguz kila chama mbali na agenda zao lazima waonyeshe jinsi watakavyokamilisha agenda za kimkakati , na hapa ndo umhimu wa katiba mpya!

Hatuwezi kuendelea Kwa kutegemea mawazo ya mtu mmoja kuwaza anayotaka yeye yawe..... Anaharibu lililopo na hata kuvunja katiba ili atimize anayotaka yeye , aaah.

Mfano mradi wa Bandari wa Bagamoyo Kwa namna yyte Ile ni wa muhimu, Bandari ya DSM tayari ipo congested na overwhelmed na pia inaelekea kuwa beyond rehabilitation. Ni heri tujadili kwamba tutafte wapi hela ya kujenga tuachane na wahisani wenye masharti magumu , na sio kuupiga chini moja Kwa moja!
 
Back
Top Bottom