Askofu Kassala atoa ‘Dikrii’ ya kufungwa kwa Kanisa Kuu la Kiaskofu Jimbo la Geita

Jengo lililofungwa ni cathedral kama saint Joseph kwa Dar. Hapo hapo ilipo cathedral kuna makanisa (majengo mengine) au parokia jirani, kwa hiyo misa na ibada zote za kila siku zinafanyika kama kawaida. Ila lile jengo ndio (tuseme) linasafishwa au linatakaswa kwa muda huu.
 
Sakramenti ya Ekaristi Takatifu ni moyo wa Kanisa, Kwani ndiyo Mwili na Damu ya Yesu Kristu
Sijui wa RC mtakuwa na akili ya kumwabudu Mungu lini?
Ndio maana hamjui hata kufungua biblia zaidi ya mapokeo ya Kirumi na sheria za kanisa tu.

Haya endelea kutukana
 
Uharibifu uliofanyila ni mkubwa sana
Hatujui mtekelezaji alitumwa au ni utashi wake.

Unamajisi vitu ambavyo vimewekwa wakfu ni kujitafutia balaa. Kama hutaki kuamini wanachokiamini watu wengine dawa ni kuachana nao wafanye yao na wewe fanya yako ilimuradi jauvunji sheria na amani baina yenu.

Ahojiwe mtuhumiwa nani yupo nyuma yake.

Mimi sinaga imani na Katoliki lakini tutaelezana kwenye hoja na si kutumia matendo kulazimisha hoja
 
Kwa wasiofahamu

Ekaristi ni mojawapo kati ya sakramenti saba za Kanisa ambazo ni alama wazi zilizowekwa na Yesu Kristo mwenyewe ili kutuletea neema ya wokovu. Tofauti na sakramenti zingine Ekaristi ni Kristo mwenyewe katika maumbo ya mkate na divai.

Ekaristi ni kitovu na kilele cha maisha ya Kanisa, kwa kuwa kwayo Kristo anachagamana na Kanisa lake na waamini wake wote na sadaka ya sifa na shukrani iliyotolewa mara moja Msalabani kwa Mungu Baba. Kwa sadaka hii anamimina neema za wokovu kwa mwili wake ambao ni Kanisa (KKK 1407). Ekaristi Takatifu ni roho ya Kanisa (Denz.3364). Ni Sakramenti ya umoja na upendo, kimsingi, Ekaristi ni kiini kamili katika Kanisa, na Kanisa haliwezi kitu pasipo hiyo. Kwasababu ni Kristo mwenyewe anayejitoa kweli kama sadaka kwa ajili ya Kanisa katika Ekaristi Takatifu na ni katika Ekaristi Kanisa hufikia uhalisia wake wa juu wa asili yake, yaani, kuwa linaonekana, la daima, na alama wazi ya neema ya wokovu ya Mungu iliyopo duniani kupitia Kristo.

Kumbe Ekaristi inaunda Kanisa na Kanisa linaitengeneza Ekaristi, na ndimo linamochota nguvu za kiroho.
.Hivyo hakuna jumuiya ya Kikristo inayoweza kujengwa na kusimama imara bila adhimisho la Sakramanti Kuu ya Ekaristi Takatifu (Presbyterorum Ordinis, n. 6). Katika Ekaristi Takatifu fumbo la Ukombozi wetu linawekwa hai na kufikia kilele katika sadaka ya Bwana, kama inavyotamkwa katika maneno ya konsekrasio: “huu ndio Mwili wangu utakaotolewa kwa ajili yenu na hii ndiyo Damu yangu itakayomwagika kwa ajili yenu”, “Fanyeni hivi kwa kunikumbuka mimi” (Luka 22:19-20).

Kwa haya machache nadhani mnapata picha ni jinsi gani unajisi na kufuru iliyofanyika ni mkubwa kiasi gani. Hivyo ili kuondoa najisi hiyo, Ni lazima toba zifanyike pasipo kutumia kanisa na vifaa hivyo vilivyotiwa najisi, Mpaka vitakapotakasika na kitabarukiwa tena.
 
Hivi hatuwezi kuwsomba Maaskofu wakafunga dikrii kwenye hazina yetu zinakoibiwa kodi zetu kuwanyoosha wahuni na wezi
 
shangaa sasa. jengo lipo watu wapo ,viongozi wapo ni kitu gani hicho kilichoharibiwa hadi ibada zisitishwe
kuna vi miungu huko vimejeruhiwa
ila jamaa ni mkatili, eti mlevi, mlevi akazima hadi cctv cameras
Vitu usivyovijua na havikuhusu visikupe headaches.Kazania yale unayoyapenda na kuyaamini.
 
Ni ibada tena kubwa mno; isipokuwa swali langu ni kwamba waumini wanakusanyikia wapi sasa?
Kwenye Parokia zao,wa Geita Ambao walikuwa wanasali Kanisa kuu wanaweza kutafutiwa alternative Nyingine,Mfano kutengenezewa ma-tent nje ya Kanisa lililofungwa au km Kuna ukumbi wanaweza kusalia humo.Siku 20 sio nyingi kihivyo.
 
Nashukuru sana ndugu mwerevu
Alichokueleza ndiyo sahihi.Kinachoelezwa ni mtu/watu kufanya uharibifu kanisani.Kunajisi vitu vya kanisa.Sasa huo ulawiti ulifanyikia kwenye mabenchi au altareni ndani ya kanisa?Jifunze kuelewa na kuoanisha mambo.
 
Hii ni sawa na itkafu tu malipizi sio mchezo dogo yule lazima afe au awe ndondocha na kupotea kusiko julikana

USSR
Hekima ya Mungu ituongoze tusifikie sisi kufanya conclusions ambazo Mungu hakusudii kuzifanya.

Hata akibadilika na kutubu kwa aliyoyafanya ni bora alimradi hilo lipate kibali kutoka kwa Mungu mwenyewe.
 
Mmmh Mambo yamekuwa yamoto,mashambulizi kila kona,kanisa limemuona kijana mwizi ila halijamuona Padri mlawiti. Wacha sisi tuendelee kuomba amani mashariki ya kati.
Haya matukio mawili umeyafuatilia kwa umakini na ukaribu?

Huyo padre mlawiti ulipata habari kwamba alishasimamishwa na Kanisa ikaachiwa serikali ku-deal nae kama ambavyo inge-deal na mimi au na wewe kama tungekuwa tumetenda jinai?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…