Katika hili la kufunga Kanisa, mimi mawazo yangu yanatofautiana kidogo na uamuzi aliouchukua Baba Askofu.
Assuming zilikuwa ni hujuma ambazo zililenga kudhoofisha Ibada Kanisani, na kwamba zinaweza kujirudia tena, je tutaendelea kufunga MaKanisa kwa muda hadi lini, kisa wezi? Kwa nini isiwe kwamba baada ya mwizi kuvamia, ndiyo iwe kichocheo cha Ibada kuongezeka zaidi kukemea uovu huo ili usije ukajirudia tena? Mara zote Kanisa la Mungu liko vitani na adui huwa hata siku moja hatoi nafasi ya kulifanya lipumzike; kwa nini tuvamiwe na adui halafu ndiyo wakati huo tusitishe mapigano?
Kwa vile ni mara ya kwanza, ni sawa Baba Askofu aendelee na uamuzi wake ila kama itakuja kutokea kwa mara nyingine, japo hatuombei hilo, ninamuomba sana Baba Askofu azidishe Ibada badala ya kufunga Kanisa