Askofu Mwamalanga: Mbowe kubambikiwa kesi ya ugaidi ni kitendo cha kuibandika kinyesi Tanzania mbele ya Mataifa

Askofu Mwamalanga: Mbowe kubambikiwa kesi ya ugaidi ni kitendo cha kuibandika kinyesi Tanzania mbele ya Mataifa

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
ASKOFU MWAMALANGA ATUMA UJUMBE MZITO KUHUSU FREEMAN MBOWE!

"Mpendwa Askofu Mwamakula, nakutumia ujumbe huo ninataka usomwe na watu wote!

Kukamatwa kwa Mheshimiwa Freeman Mbowe na kubambikiwa Kesi ya Ugaidi ni kitendo cha kulibandika kinyesi Taifa la Tanzania mbele ya mataifa. Kwetu sote Watanzania, tunamuona Mbowe kuwa ni mtu mwadilifu miongoni mwa wanasiasa wa vyama vyote nchini. Hivyo, Mheshimwa Mbowe kupewa kesi ya Ugaidi ni kitendo cha aibu kwa Watanzania. Aliyepanga bandiko hilo bado hajafaulu. Lengo lake ni kuitia moto jamii ya Watanzania!

Ninawasihi Watanzania kumtegemea Mungu Mwenyezi mia kwa mia; nanyi mtaona haki yake itakavyoshuka haraka na kutuliza mioyo yetu! Msiogope wala msinung'unike, fanyeni sala na dua, adhabu zao ni sasa. Duniani kote, Mbowe anaheshimika kama mwanasiasa salama na safi. Msiogope! Tazama, mipango ya shetani juu ya nchi yetu haitafaulu. Ombeni rehema za Mungu Mwenyezi kila mtu mahali alipo. Yesu Kristo ni yote katika yote. Amini na Amina! Ujumbe huu usomwe na kila mtu

Ujumbe huu umetolewa nami Askofu William Mwamalanga kwenye Kongamano la Amani kwa Afrika linalofanyika Lusaka, Zambia na kushirikisha viongozi wa dini wa nchi za Maziwa Makuu kwa kuiombea Afrika. Ndipo Dkt. Wood Edwards kutoka Uingereza akaomba kuiombea Tanzania ili inusurike na dhambi ya uonevu unaoendelea nchini Tanzania.

Mimi Askofu William Mwamalanga nimeubariki ujumbe huu kwani ni ujumbe hakika wa Mungu Mwenyezi kwa Watanzania kwani vitendo vya kubambikia watu kesi vimeota mizizi nchini pamoja na kumwaga damu zisizo na hatia. Ole wao wafanyao ubambikiaji huo na ole wao wawatumao watu kufanya hayo!

Askofu William Mwamalanga - Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maaskofu na Mashehe ya Kamati na Amani"
 
MTU GAIDI MNASEMA MNAPAKA TAIFA KINESI WAKATI MBOWE NDIYO KAICHAFUA TANZANIA KWA KUFANYA UGAIDI KUWENI NA AKILI MSIFIKIRIE KWA KUTUMIA MASABURI
 
kinyesi cha nani sasa anachokizungumzia. na tunajua wanadamu wote wawe maaskofu, wachungaji, majambazi, wanasiasa, watakatifu au wasafi huwa wanatoa kinyesi baada ya kula. atuambie icho kinyesi ni cha nani na kama yeye ana ushahidi kwamba hiyo kesi ni ya kubambikizwa. watu kama hawa jpm ndio aliwakomesha, na tunamshukuru kwa hilo huko aliko.
 
ASKOFU MWAMALANGA ATUMA UJUMBE MZITO KUHUSU FREEMAN MBOWE!

"Mpendwa Askofu Mwamakula, nakutumia ujumbe huo ninataka usomwe na watu wote!

Kukamatwa kwa Mheshimiwa Freeman Mbowe na kubambikiwa Kesi ya Ugaidi ni kitendo cha kulibandika kinyesi Taifa la Tanzania mbele ya mataifa. Kwetu sote Watanzania, tunamuona Mbowe kuwa ni mtu mwadilifu miongoni mwa wanasiasa wa vyama vyote nchini. Hivyo, Mheshimwa Mbowe kupewa kesi ya Ugaidi ni kitendo cha aibu kwa Watanzania. Aliyepanga bandiko hilo bado hajafaulu. Lengo lake ni kuitia moto jamii ya Watanzania!

Ninawasihi Watanzania kumtegemea Mungu Mwenyezi mia kwa mia; nanyi mtaona haki yake itakavyoshuka haraka na kutuliza mioyo yetu!
Askofu Mwamalanga amekosa heshima kwa vyombo vyetu vya sheria.
naamini anafahamu kabisa kuwa chombo chenye kutoa Haki ni Mahakama, sasa anapata wapi ujasiri wa kusema Mbowe kabambikiwa wakati bado kesi haijasikilizwa na kuamuliwa?!

Hivi huyu askofu mwamalanga nafahamu ju ya utawala wa sheria?
Hadi Mbowe kuunganishiwa na wenzake tufahamu kuwa kuna ushahidi dhidi yake. tusubiri tuache vyombo vyetu vifanye kazi zake kwa mujibu wa sheria.
 
Sidhani kama watawala wetu wameona athari za huu ubambikaji kesi unavyoweza kuleta athari kwa nchi yetu. Sijui kwanini hawawazi ya mbeleni
 
Back
Top Bottom