Askofu Niwe Mugizi jimbo Katoliki Rulenge Ngara Kagera, kuongoza kampeni ya kupinga katiba mpya

Askofu Niwe Mugizi jimbo Katoliki Rulenge Ngara Kagera, kuongoza kampeni ya kupinga katiba mpya

R.B

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2012
Posts
6,296
Reaction score
2,575
Askofu Niwemgizi wa jimbo Katoriki jimbo kuu Rulenge amesema ataongoza kampeni ya kura ya hapana kupinga katiba mpya.

Askofu atangaza kufia katiba
• Ni Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki
• Aahidi kuhamasisha waumini waipigie kura ya hapana

NA JOSEPHAT ISANGO

WAKATI Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk. Alli Mohamed Shein, wakitarajiwa kukabidhiwa Katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalumu la Katiba, Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC) ambaye pia ni Askofu wa Jimbo la Rulenge- Ngara, Mhashamu Severini Niwe Mugizi,amewataka Watanzania waikatae, na kwamba yupo tayari kufa kwa ajili ya kupigania katiba bora.

Askofu Niwe Mugizi amesema haungi mkono Katiba iliyopendekezwa kwa kuwa haina ukweli wala uadilifu. "Wao walibadili kanuni ili kupata yanayowapendeza. Mimi nawasihi kwa unyoofu, ingawa najua sasa suala la kudai katiba mpya ni kelele ambayo haitaisha, tuwe na upendo na nchi yetu na viongozi wetu, lakini pale wakifanya yasiyofaa tuwaambie ukweli bila woga. Niko tayari kufa kwa ajili ya kusema ukweli kwa sababu tumetangaziwa vita," alisema.

Akizungumza na mamia ya waumini wa Kanisa hilo kwenye Kituo cha Hija cha Katoke Jimbo la Rulenge-Ngara majuzi, Askofu huyo alisema kwa kuwa katiba hiyo imepitishwa kwa mabavu na hila, yeye hawezi kuhamasisha waumini wake waiunge mkono. Ameifananaisha katiba hiyo inayopendekezwa na nyumba iliyoezekwa kwa dhahabu lakini imejengwa kwenye msingi wa mchanga. "Haiwezi kudumu," alisema.

Aliwaeleza kuwa alishamwambia hata Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kwamba iwapo katiba mpya haitazingatia mambo ya msingi yaliyopendekezwa na Watanzania atawahamasisha waumini kupiga kura ya hapana "Naawambia kabisa, katiba ile ni wazi walipaswa kuboresha, na ndiyo ilikuwa kazi yao. Kweli kuna vitu wameboresha, kuna vitu wameongeza ongeza pale, lakini kuna vitu vya msingi sana wameviondoa. Mimi binafsi siafiki kabisa," alisema.

Alisema kwa mfano, katiba inayopendekezwa haitoi uthibitisho wa kulinda uhai wa kuishi tangu kutungwa mimba bali inasema kila mtu ana haki ya kuishi. "Siafiki siafiki hata kidogo. Watu walipendekeza vitu fulani viwepo kwenye katiba, mfano mgombea binafsi watakwambia wameweka kwenye katiba lakini ukiangalia masharti yaliyowekwa ni magumu kiasi kwamba mgombea binafsi hawezi kufaulu.

"Nasema, sitaki kurefusha, na wameshasikia hadi imefika mahali sisi maaskofu tukaitwa wapuuzi tuliofanya kazi isiyo na utukufu, lakini tuwaambie kuwa sisi hatukutumwa na wanasiasa kufanya kazi tunayofanya. Pale ambapo ukweli na uadilifu vinakosekana hatupaswi kukaa kimya. Mchakato wote wa katiba haukuwa na uadilifu na ukweli, ndiyo maana mimi siafiki," alisema.

Askofu huyo aliwashauri waumini kupiga kura wakiwa na dhamiri hai, huku akiwatahadharisha watakaopiga kura za ndiyo halafu mambo yakakwama siku za usoni wasilaumu kuwa askofu hakuwaambia.
 
Mkuu,,,naww unakuwa km mgeni humu jukwaani unaletaje habari isiyokamilika?
 
Duh hawa jamaaa wakatoliki huwa ni noma, wakiamua jambo huwa hawarudi nyuma.

If you sideline the church hakika ypu are heading towards failure, thats for sure.

go go askofu Niwemugizi, tuko sote sawa. Tupo na wewe hatua zote!
 
mkuu ni jambo jema kwa viongozi wa dini kusema ukweli kama walivyo viongozi wao
 
Nashangaa nchi ilivyogawanyika,nchi hii inakwenda kuangamia,kuporomoka kwa ulaya mashariki na sovieti ilikuwa hivi hivi,unaweza kushangaa kuna taasisi zinaendeshwa kidini tu,upinzani unadidimizwa,uwizi wa mali ya umma,upendeleo serikalini.Utashangaa katiba ya nchi inaandikwa but nchi imegawanyika.
 
Aliyeongea hayo si huyo Askofu bali boss wwke Lowasa
 
Nashangaa nchi ilivyogawanyika,nchi hii inakwenda kuangamia,kuporomoka kwa ulaya mashariki na sovieti ilikuwa hivi hivi,unaweza kushangaa kuna taasisi zinaendeshwa kidini tu,upinzani unadidimizwa,uwizi wa mali ya umma,upendeleo serikalini.Utashangaa katiba ya nchi inaandikwa but nchi imegawanyika.
Hao wanaopiga mayowe ni watu walioshindwa. Nchi hii ni zaidi ya huyo askofu wa Rulenge
 
mkuu ni jambo jema kwa viongozi wa dini kusema ukweli kama walivyo viongozi wao
Kinachokera ni kuona viongozi hao wa kiroho wakitoa matamko baada ya kushinikizwa na mtu anayeutamani urais kwa udi na uvumba
 
Kinachokera ni kuona viongozi hao wa kiroho wakitoa matamko baada ya kushinikizwa na mtu anayeutamani urais kwa udi na uvumba
Kwani wewe ukikereka kuna hasara gani kwa taifa?
BTW Fungua uzi wako uendelee kumsakama Lowasa acha kuharibu huu uzi.
 
Askofu Niwemgizi wa jimbo Katoriki jimbo kuu Rulenge amesema ataongoza kampeni ya kura ya hapana kupinga katiba mpya.

Akiamua kuingia siasa tunamwambia karibu ila asije piga yowe.Sababu tuna uzoefu wa maaskofu katoliki kuongoza na kuleta vurugu hasa Rwanda na kusababisha mauaji ya kimbari.Vurugu zikilipuka ajue hatatambuliwa kama askofu hakuna mwenye muda huo.Ajue vita haina macho nondo na mawe yakianza kurushwa yatarushwa hadi kwenye kiti chake na kofia lake la Uakofu.

Lakini tunajua kuwa kuna maaskofu ambao ni wahamiaji haramu ambao wanataka kulipa kisasi kwa kutimuliwa ndugu zao kwa kisingizio cha katiba mpya.Wametumwa. Na huyo kama ni kweli KASEMA atakuwa ametumwa na M23.Vyombo vya Usalama mzingireni hadi kwenye kitanda anacholala.
 
Mauaji unayaongelea wewe yeye amesema anapinga katiba. Sasa kwakuwa CCM ni vipofu mnakimbilia mauaji ili kutishsa watanzania waoga na wapumbavu. Kupinga katiba kunahusiana vipi na mauaji kama sio ukenge huo?

Yeye apinge kwenye ballot box na si kuhamasisha waamini wake waungane na mawazo yake ya kipumbavu. Yeye kala mlungula wa Lowasa. Asianze kuwalisha sumu wenzake
 
Hao wanaopiga mayowe ni watu walioshindwa. Nchi hii ni zaidi ya huyo askofu wa Rulenge

angalieni linyani hili la kike nalo likitoa maoni. ivi wewe chabruma aka makonda wa uvccm huoni nchi nzima ikilia mchakato huu kufanywa na ccm kwa manufaa ya ccm haifai na wewe unakejeli. kweli makonda hufai hata kujumuika katika jamii ya wtatanzania
 
Yeye apinge kwenye ballot box na si kuhamasisha waamini wake waungane na mawazo yake ya kipumbavu. Yeye kala mlungula wa Lowasa. Asianze kuwalisha sumu wenzake

Wewe ndio una mawazo ya kipumbavu.
 
Back
Top Bottom