#COVID19 Askofu Niwemugizi, asitisha Misa na Ibada zote Jimbo la Rulenge, awataka waumini Wasali Majumbani pia Wajikinge na Corona

#COVID19 Askofu Niwemugizi, asitisha Misa na Ibada zote Jimbo la Rulenge, awataka waumini Wasali Majumbani pia Wajikinge na Corona

Safi sana,huu ndio utumishi wa Mungu tunaouhitaji.

Better late than never.

Waumini katika maeneo mengine, mjiongeza,msisubiri taarifa kama hii kwani si kila kiongozi wa dini atafanya hivi katika maeneo yenu.

Viongozi wa madhehebu mbalimbali(RC,KKKT.n.k) wanaokutana kutoa matamko ya pamoja(waraka) kama ya kukemea maovu,kukemea wanasiasa,n.k,walipaswa kuwa wamekutana na kuja na tamko kama hili; hivyo, tunatumai tangazo hili litatumika kama mfano kwa viongozi wengine wa dini waliobaki.

Baba Askofu,katika hili,umevaa viatu vilivyowapwaya wengi wakiwemo viongozi wa dini na wasio viongozi wa dini.

Hongera sana Baba Askofu!
Mimi huwa nawashangaa wenye mtazamo kama huu. Kwani wewe ni Mungu hata ujigambe kwamba unahitaji maaskofu kama hawa? Who are you?

Sent from my SM-A720F using Tapatalk
 
Ingependeza Askofu wa DSM angekuwa wa kwanza.
Lkn huu ni mfano naamini wengine watarespond

Haitii akilini kuzuia ibada ya jumuiya na kuacha misa zenye watu wengi.
Kusali hulazimishwi ukijisikia kusali nenda hujisikii usiende acha kutupia lawama zisizo na msingi watu .

Unaogopa kuwa utapata corona ukienfa kanisani kuwa Mungu atakupa corona kanisani kwake usiende

Tamko la nini wakati kusali ni hiari yako Wewe Fanya maamuzi kuwa utaenda au huendi.Hufungwi pingu kwenda kanisani
 
Usiwe mkali kiongozi jamaa alitakiwa akujuze tu, nikuwa papa anazaidi ya mwezi amelifunga kanisa itali na amejifungia ndani hatoki nje ibada anafanyia ndani
Mwoga asiye na imani anaogopa kuwa Mungu atampa corona kwenye ibada!!!!! Kazi ya Mungu sio kugawa corona ibadani lioga hilo halina imani ndio maana limejifungia ndani.
 
Niwemugizi ndio awe kardinali wetu.Ni Askofu mwema na mweledi sana.
 
Kusali sio hulazimishwi ukijisikia kusali nenda hujisikii usiende acha kutupia lawama zisizo na msingi watu .

Unaogopa kuwa utapata corona ukienfa kanisani kuwa Mungu atakupa corona kanisani kwake usiende

Tamko la nini wakati kusali ni hiari yako Wewe Fanya maamuzi kuwa utaenda au huendi.Hufungwi pingu kwenda kanisani
Mungu hatoi Corona mkusanyiko unaleta maambukizi..., kwenda kwake au kutokwenda huenda kukaleta tofauti ya kuongeza au kutokuongeza maambukizi., effect yake sio ya kwake tu bali jamii inayomzunguka..

Mchuma Janga hula na Wakwao - The Case of Corona and Social Distancing - JamiiForums
 
Mwoga asiye na imani anaogopa kuwa Mungu atampa corona kwenye ibada!!!!! Kazi ya Mungu sio kugawa corona ibadani lioga hilo halina imani


Ni kweli , hata hakuna haja ya kunawa mikono na kuvaa barkoa kwani ikiwa wao na wewe ni Mkristo wa kweli ni lazima uyakumbuke maneno ya Yesu aliposema

Bwana akasema: “Kama mngekua na imani kiasi cha chembe ya haridali mngeuambia mkuyu huu, ng'oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.” (Luka17:7).

Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia mkiwa na imani , msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, ngo'ka ukatupwe baharini, litatendeka. na yoyote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.
(Mathayo 21:21-22)

SASA TUNAKUOMBA WEWE KAMA UNAYO KWELI IMANI BASI ANZA KUIAMBIA KORONA ONDOKA ULIMWENGUNI ,

ILI TUPATE NAFUU , VYENGINEVYO NA WEWE UTAKUWA NI MMOJA WA MATAPELI TU NA WALA HUNA IMANI YOYOTE NA YESU NnA WALA WEWE SI MKRISTO
 
Kwa hiyo usha confirm kwamba pasaka ndo chanzo cha idadi ya wagonjwa kuongezeka ghafla....incubation ya COVID-19 ni siku ngapi kwani?
Incubarion ni siku 2-14. Average ni siku 5.5.
 
Mungu hatoi Corona mkusanyiko unaleta maambukizi..., kwenda kwake au kutokwenda huenda kukaleta tofauti ya kuongeza au kutokuongeza maambukizi., effect yake sio ya kwake tu bali jamii inayomzunguka..

Mchuma Janga hula na Wakwao - The Case of Corona and Social Distancing - JamiiForums
Biblia inatamka wazi wawili watatu wakikusanyika kwa jina langu Mimi Niko katikati yao .Haisemi corona iko katikati yao

Mkusanyiko Wa Mungu ni Mungu anakuwa katikati ya kusanyiko sio corona. huyo askofu ni mpagani mkubwa
 
Biblia inatamka wazi wawili watatu wakikusanyika kwa jina langu Mimi Niko katikati yao .Haisemi corona iko katikati yao

Mkusanyiko Wa Mungu ni Mungu anakuwa katikati ya kusanyiko sio corona. huyo askofu no mpagani mkubwa
Nitakuwa mpuuzi nikianza kukubishia wewe kuhusu imani yako wakati imani ni yako..., Tatizo hio imani yako ikiwa chanzo au muendelezo wa kuweka maisha yangu au afya yangu hatiani, hapo utakuwa hunitendei haki (love thy neighbour)

Mkusanyiko unaongeza maambukizi (hayo tumeambiwa na wataalamu wa huu ugonjwa) unless otherwise unataka kuniambia majibu ya kujikinga na Corona yapo kwenye bible, basi tuendelee kufuata wataalamu wanasemaje..., nadhani hapo ndani mwenu mpo wawili, watatu kusanyikeni yeye awe kati yenu....
 
Kumbe bado kuna watumishi wa MUNGU...wanayemuogopa MUNGU kuliko kukosa fedha....MUNGU akutunze askofu
Huyo hamuogopi Mungu anaogopa Corona angekuwa anaogopa Mungu asingezuia ibada kufanyika kanisani.Hana lolote
 
Mkusanyiko unaongeza maambukizi (hayo tumeambiwa na wataalamu wa huu ugonjwa) unless otherwise unataka kuniambia majibu ya kujikinga na Corona yapo kwenye bible, basi tuendelee kufuata wataalamu wanasemaje..., nadhani hapo ndani mwenu mpo wawili, watatu kusanyikeni yeye awe kati yenu....
Utaalamu ni nje ya kanisa sio ndani ya kanisa.Mungu abakie Mungu na mambo yake

Mkusanyiko Wa Mungu ni Wa kupata baraka toka kwake sio corona
 
Hivyo brother magu hataenda tena kuhutubia kanisani akiwa Chato
 
Utaalamu ni nje ya kanisa sio ndani ya kanisa.Mungu abakie Mungu na mambo yake

Mkusanyiko Wa Mungu ni Wa kupata baraka toka kwake sio corona
Iwapo Uwepo wa Imani utahatarisha maisha hata yasio wa wenye imani basi kama hao wenye imani hawawezi kuacha kuchanganyikana na wengine na kuhatarisha maisha yao.., ubinadamu na ustaarabu unasema watu hao inabidi watafute mbinu mbadala..., after all when in Rome live like Romans...,
 
askofu Kakobe,askofu Gwajima sambamba na mzee wa bapa igeni mfano huo
Mungu kaagiza kuwa msiache kukusanyika huyo Askofu Nani amuige yeye anasema marufuku kukusanyika kwenye ibada!!! Mungu ni mkubwa kuliko huyo Askofu mpiga marufuku watu kukusanyika Ibadan. hakuna cha kuiga kwa huyo askofu mpagani
 
Mkuu wa nchi ametangaza siku tatu za maombolezo kwa ajiri ya nchi kama mfalme wa Ninawi alivyofanya.Unafahamu fika kuwa kila utawala hapa duniani unatoka kwa Mungu, uwe mzuri au Mbaya.

Neno la mfalme huwa linaheshimika na Mungu analiheshimu. Rais wetu Magufuli amenena maneno mema juu ya Mungu na hii lazima Mungu atakuwa upande wake regadless ana dhambi au hana kwa sababu ameonyesha unyenyekevu kuliko wewe Askofu .

Mwenye unyenyekevu atainuliwa tu lakini mwenye kiburi atashushwa wakati Mkuu wa nchi anahimiza watu kuomba wewe Askofu unatangaza waumini wasiende kanisani. Unafikiri ndiyo umewapenda waumini wako?

Umwonyesha udhaifu mkubwa wa imani, hufai kuwa askofu. Umechanganya imani na siasa hufai kuongoza kondoo. Umemdhalilisha aliyekufia msalabani kwa sababu umeenda kinyume na matakwa ya mfalme wa nchi(rais) umeenda kinyume na Mungu, umeenda kinyume na Biblia.

Mbona sasa hao waumini wako ni wa mfalme wa nchi ambaye yeye Amemheshimu aliyezifanya mbingu na nchi. Kanisa tujifunze kuheshimu katiba, tujifunze kuendana na Biblia. Moyoni umejaa chuki halafu unajifanya mtumishi wa Mungu.Mungu yupi huyo labda miungu.

Nashauri ukatubu wewe uendaye kinyume na matakwa ya mfalme vinginevyo waweza kuwa mfano wa manabii ya baali kipindi cha Elia Mtishbi.
 
Back
Top Bottom