#COVID19 Askofu Niwemugizi, asitisha Misa na Ibada zote Jimbo la Rulenge, awataka waumini Wasali Majumbani pia Wajikinge na Corona

#COVID19 Askofu Niwemugizi, asitisha Misa na Ibada zote Jimbo la Rulenge, awataka waumini Wasali Majumbani pia Wajikinge na Corona

Yani ulivyo tutusa unataka mimi niwaze kama wewe ?

Kwani papa anashindwa nini kuingilia?

Yanayoendelea Italy sio Tanzania

Usije ukafiri unauwezo mkubwa wa kuyatafakari mambo kumbe umejaa ujinga tu kichwani mwako

Shika adabu yako usinizoee



Sent using Jamii Forums mobile app
Umejiunga jf juzijuzi tuu.lkn unadandia kila topic,huku ukijitanabaisha kama mpinga sugu wa mbeya.hebu kua muungwana,usituonyeshe jinsi ulivyo zero brain,utakwama tuu.ccm oyee
 
Naunga mkono hoja ya Askofu. Naitaka serikali yangu ya Tanzania ichukue hatua madhubuti ili kuwakinga watu dhidi Corona.
Serikali ijifunze kuwa mara baada sikukuu ya Pasaka wagonjwa wameongezeka maradufu kwa sababu ya mikusanyiko iliyopindukia. Hivyo naitaka serikali ifuate nyayo za Askofu Niwemugizi kwa kutekeleza yafuatayo:
Moja, Mikusanyiko yote mikubwa ipigwe marufuku.
Pili Askari kanzu wawekwe kwenye stendi na vituo vya mabasi ili kuhakikisha ile social distance inazingitiwa nchi nzima. Ifahamike kuwa hii ni Vita na wakati wa Vita Askari ni lazima wawe mstari wa mbele kuwatetea wananchi. Amiri Jeshi mkuu Sasa ndio wakati wa kuwatumia Askari kwa manufaa ya Watanzania, siyo kwenye korosho za hasara.
Nne, Kuwe na lockdown ya safari za wakazi kutoka mji mkubwa mmoja kwenda mahali pengine hasa maeneo ya vijijini.
Tano, masoko na minada ipangwe kwa Askari kuhakikisha watu wanazingatia umbali wa kukaa, kupanga bidhaa au wanyama wao wanaouzwa
Sita, maji yasikatike kwenye miji yenye wakazi wengi. Kwa kuwa kipindi hiki maji yanatumika sana, serikali itoe fedha na kuzipa mamlaka za miji na majiji ili kuwapunguzia watumiaji gharama.
Saba, Makonda na wakuu wengine wa mikoa viherehere wadhibitiwe ili waache matamko ya kibabylon.
Hongera Askofu.
 
Naunga mkono hoja ya Askofu. Naitaka serikali yangu ya Tanzania ichukue hatua madhubuti ili kuwakinga watu dhidi Corona.
Serikali ijifunze kuwa mara baada sikukuu ya Pasaka wagonjwa wameongezeka maradufu kwa sababu ya mikusanyiko iliyopindukia. Hivyo naitaka serikali ifuate nyayo za Askofu Niwemugizi kwa kutekeleza yafuatayo:
Moja, Mikusanyiko yote mikubwa ipigwe marufuku.
Pili Askari kanzu wawekwe kwenye stendi na vituo vya mabasi ili kuhakikisha ile social distance inazingitiwa nchi nzima. Ifahamike kuwa hii ni Vita na wakati wa Vita Askari ni lazima wawe mstari wa mbele kuwatetea wananchi. Amiri Jeshi mkuu Sasa ndio wakati wa kuwatumia Askari kwa manufaa ya Watanzania, siyo kwenye korosho za hasara.
Nne, Kuwe na lockdown ya safari za wakazi kutoka mji mkubwa mmoja kwenda mahali pengine hasa maeneo ya vijijini.
Tano, masoko na minada ipangwe kwa Askari kuhakikisha watu wanazingatia umbali wa kukaa, kupanga bidhaa au wanyama wao wanaouzwa
Sita, maji yasikatike kwenye miji yenye wakazi wengi. Kwa kuwa kipindi hiki maji yanatumika sana, serikali itoe fedha na kuzipa mamlaka za miji na majiji ili kuwapunguzia watumiaji gharama.
Saba, Makonda na wakuu wengine wa mikoa viherehere wadhibitiwe ili waache matamko ya kibabylon.
Hongera Askofu.
Michango kama hii ikiwa mingi inaweza 'kuwaamsha'. Kuna wanaosifia hata 'uharo bin uharisho'.
 
Bado hawa wapiga makelele sijui watafunga lini tupumzike na maspika mitaani
 
Kanisa Katoliki Jimboni Rulenge-Ngara, wamesitisha kabisa Ibada/misa. Watu wasali nyumbani! Pia amewataka waumini wajikinge na COVID-19 na kuchukua tahadhari


Kanisa Katoliki Jimbo la Rulenge-Ngara limesema limesitisha Ibada za Misa, maadhimisho mengine yanayokusanya Waumini wengi Kanisani na sala za Jumuiya kwa muda wa mwezi mmoja kuanzia Aprili 19, 2020

Askofu Severine Niwemugizi wa Jimbo hilo amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kutafakari alama za nyakati na kujifunza kutoka kwa watu wa Ulaya, Marekani na nchi za jirani na hatua ambazo Baba Mtakatifu alizichukua kwa kutoa maelekezo kwa Maaskofu Wakatoliki Duniani na namna ya kuadhimisha Ibada

Amesema pamoja na kumshukuru Rais Magufuli kutotoa amri ya kufunga Makanisa na Misikiti, akihimiza kufanya ibada kumuomba Mungu atunusuru na janga hili, kama Mchungaji wa Jimbo la Rulenge-Ngara ameamua kuchukua uamuzi huo

Aidha, Askofu Niwemugizi amesema pale itakapowezekana wataomba redio Kwizera irushe adhimisho la Misa fupi na Waamini wafuatilie redioni. Baada ya mwezi kuisha Kanisa litaangalia hali ilivyo ili kama iliongeze muda

Pia, amewataka mapadre kuadhimisha misa peke yao kwa niaba ya waumini kuwaombea na kuiombea dunia ili Mungu atunusuru na #COVID19 hili na kuagiza sala za Jumuiya kufanyika ndani ya familia kwa familia moja moja
View attachment 1422602


Amenifurahisha sana.
Nikienda huko Ziwa Magharibi nitamtembelea kumsalimia. Ametoa mfano wa kuigwa.
 
Ingependeza Askofu wa DSM angekuwa wa kwanza.
Lkn huu ni mfano naamini wengine watarespond

Haitii akilini kuzuia ibada ya jumuiya na kuacha misa zenye watu wengi.

Atafanya hivyo sababu sasa jimbo la Dar lina askofu wa kanisa.Hapo nyuma tulikuwa na askofu wa CCM
 
Kutokana na hiki ulichoandika hapa huoni Askofu nae kuna mamlaka anatakiwa kuisikiliza?

Labda sifahamu, hivi kati ya Askofu na Kadinali nani yupo juu ya mwingine?

Kama itatokea Kadinali yupo juu ya Askofu, sitashangaa siku za mbeleni hilo tamko la leo la Askofu likatenguliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kadinari sio daraja ni hadhi askofu ana mamlaka kuliko kadinari maana ata mlei wa kawaida anaweza kuwa kadinari


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Yani ulivyo tutusa unataka mimi niwaze kama wewe ?

Kwani papa anashindwa nini kuingilia?

Yanayoendelea Italy sio Tanzania

Usije ukafiri unauwezo mkubwa wa kuyatafakari mambo kumbe umejaa ujinga tu kichwani mwako

Shika adabu yako usinizoee



Sent using Jamii Forums mobile app
Ungekuwa mpole ukawaza vizuri huenda usingetukana! Haitakiwa tusubiri iwe Kama ilivyo kwa Papa ndo makanisa yafungwe! Inatakiwa tuchukue hatua mapema ili tusifike huko

Waswahili wanamsemo wao usemao 'ukiona mwenzio ananyolewa, chako tia maji" walikuwa na maana kubwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Askofu angekaimisha ibada kwa shemasi haya ni maamuzi ya kidikteta

Waumini hawajashirikishwa

Papa aingilie kati

Sent using Jamii Forums mobile app
Katika kanisa katoliki,askofu ndiye msemaji wa mwisho wa Jimbo,anaamua anavyoona inafaa ndani ya Jimbo lake. Kwa hiyo hata papa aliamua pia hivyo hivyo kufuta misa za mikusanyiko. Pia huwa hakuna kiongozi wa kanisa katoliki katika level ya nchi.
 
Atafanya hivyo sababu sasa jimbo la Dar lina askofu wa kanisa.Hapo nyuma tulikuwa na askofu wa CCM
Hapana
Umekosea.
Kila mwenye daraja anafungwa kwa cannon law kufanya siasa au kushiriki siasa kwenda kupata Madaraka au kukalia kiti cha maamuz. Askofu hafungwi kuwa na maoni binafsi ambayo hayapingi imani ya kanisa.

Kuwa na mapenzi na ccm basi yupo mwenye mapenz na cdm hivyo hawapaswi kufanya maamuz ya kufundisha, kutakatifuza na kuchunga kwa kutumia hayo mapenzi bali imani ya kanisa na fadhila za kimungu na kibinadamu.

Daima maoni ya Askofu yule hayakuwahi kuathiri kanisa LA DSM kwa utendaji. Na alifanya vizuri mpaka ( yesu aliposhushwa msalabani) staafu kwa sheria.

Mheshimu tafadhali kwani si kosa kutofautiana mtazamo. Licha ya kupinga mawazo ya maaskofu wenzake lkn waamini wake walipata kufundishwa maoni hayo. Je si fadhila hiyo.
 
Kutokana na hiki ulichoandika hapa huoni Askofu nae kuna mamlaka anatakiwa kuisikiliza?

Labda sifahamu, hivi kati ya Askofu na Kadinali nani yupo juu ya mwingine?

Kama itatokea Kadinali yupo juu ya Askofu, sitashangaa siku za mbeleni hilo tamko la leo la Askofu likatenguliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa utaratibu wa Roman Catholic Church, Askofu haripoti kwa Kadinali. Kadili kazi yake kubwa ni kumchagua Papa.

Mara nyingi kadili huwa pia ni Askofu japo siyo lazima. Unaweza kuwa kadinali na usiwe Askofu wa Jimbo lolote.

Ulikwishawahi kusikia jambo mara moja Kadinali Pengo akiwapa maelekezo maaskofu?
 
Kwa utaratibu wa Roman Catholic Church, Askofu haripoti kwa Kadinali. Kadili kazi yake kubwa ni kumchagua Papa.

Mara nyingi kadili huwa pia ni Askofu japo siyo lazima. Unaweza kuwa kadinali na usiwe Askofu wa Jimbo lolote.

Ulikwishawahi kusikia jambo mara moja Kadinali Pengo akiwapa maelekezo maaskofu?
Washauri wa papa na warithi kiti cha petro.

Kwa sasa wanateua wenye daraja tu.

2017 papa aliteua padri kuwa kadinali toka Asia
 
Askofu pekee mwenye akili timamu Tanzania.
Wengine wote ni majanga tu bila kujali dhehebu.

Huyu akili zake sawa na imamu wa ule msikiti wa dar uliositisha matumizi hadi waandae utaratibu mzuri utakao punguza hatari ya maambukizi ya hili gonjwa.
 
Back
Top Bottom