Askofu Nyaisonga avishangaa Vyama vya Upinzani kususia uchaguzi. Ahimiza waumini kujitokeza kupiga kura na kuchagua viongozi

Askofu Nyaisonga avishangaa Vyama vya Upinzani kususia uchaguzi. Ahimiza waumini kujitokeza kupiga kura na kuchagua viongozi

Baba Askofu mkuu amepotoka sana! Jamani hilo taahira lina dalili za madigiteta ndiyo maana linafanya kila juhudi kujipendekeza kwa kabisa ili wasilikemee! Yaani askofu anaanza.kukemea katikati badala ya kuanzia kule walikoanza.kuchafua mchakato!
 
Hadi kanisa lifafanue na kuhimaza. Hilo peke yake ni kuonesha kuna shida. Lakini kanisa linazungumzia kukaa meza moja, hivi ni kweli kanisa hilo halikupata kuona mwenendo usio sawa?
 
Ofcourse kama ni kweli kayasema hayo ni mzigo wa kanisa lote ukizingatia pia kwa sasa yeye ndiye alama ya umoja wa Kanisa Nchini aikiwa kama Raisi wa TEC na kama sio inabidi ukanushwe. Lakini tusisahau huo sio waraka wala tamko bali yalikua ni mahubiri yake katika ibada anayoyatoa kama padre mwingine tu. In short something is very right or very wrong somewhere.
Hili jambo linanitatiza kidogo unamsoma mleta mada anasema Paroko nae kahubiri alichotumwa . Ahsante kwa kunikumbusha sio waraka au tamko la TEC.
Hapa kama ndivyo ulivyosema basi kanisa si la kubebeshwa lawama kama alivyochangia barafu na Malcom Lumumba
Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Peter O'bay naye amehubiri kile alichotumwa na wakubwa zake, kuhimiza watu wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi
 
Nimesikiliza mahubiri ya Askofu Mkuu na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tz,Mhashamu Askofu Nyaisonga, ameelekeza lawama zake katika vyama vya upinzani,akijenga hoja kuwa havikutumia busara na elimu katika kufikiri na kujitoa katika uchaguzi.

Amehimiza kuwa kujitoa sio suluhu,wanapaswa kukaa meza moja na serikali kutatua hiyo changamoto,amesisitiza kuwa waliojitoa wamekosea,hivyo kasema msimamo wa maaskofu Wakatoliki ni kutokubaliana na kusisia uchaguzi,na wamehimiza waumini kujitokeza wa wingi jumapili kupiga kura.

Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Peter O'bay naye amehubiri kile alichotumwa na wakubwa zake, kuhimiza watu wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi, hii ni kusema, kanisa katoliki linaungana na Polepole, Jafo na TAMISEMI kuubariki uchaguzi wa serikali za mitaa ambao mchakato wake umejaa utata mtupu,utata ambao hata makada wazoefu wa CCM wanaona aibu kwa yaliyotokea. Hili ndio kanisa Katoliki na msimamo wake umetangazwa na Rais wa TEC. Kanisa limeridhika na mchakato, halitaki kugombana na serikali, limewakana waumini wake waliogoma toka mwanzo kujiandikisha kwa kuona ubovu wa demokrasia kwa sasa.

Katika maandishi ya kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed", mwandishi alijaribu kuelezea kwa undani jinsi kanisa, na hasa kanisa la Vatican wakati mwingi lilivyoshiriki kuungana na serikali katika kuisaidia kufikia adhma yake, mwandishi ameeleza nafasi ya wamisionari katika kuitawala Afrika, jinsi walivyotangulia na kuwatengenezea njia wakoloni, kuanzia Congo ya DR mpaka Afrika ya Kusini,Kaskazini na Mashariki ya Afrika. Mwandishi anasema kanisa huangalia kwanza maslahi ya viongozi wake kabla ya waumini wake.

Inaelezwa kuwa wakati wa utawala wa Kifashisti kule Italia, Mussolini aliona tishio la Kanisa Katoliki ktk kufikia malengo yake. Maana kwa wakati ule, kanisa lilikuwa na ushawishi wa kila sekta ya maisha ya kiroho na kimwili na serikali ilikuwa na ushawishi mdogo tu ya maisha ya kisiasa.

Alichokifanya Mussolin ni kujipendekeza kwa kanisa na kutoa "rushwa" ili yote atakayoyafanya kanisa katoliki lililokuwa na nguvu sana Italia libaki kimyaa.Na Alifanikiwa...

Kwanza aliamua kumbatiza mwanae wa kiume, ambaye hapo awali hakuwa amebatizwa.Hapa akaliteka kanisa kwa karata ya kwanza.

Pili alimua kufunga ndoa ya kikanisa,baada ya kuwa amekaa miaka 11 na ndoa ya bomani na mkewe Rachele.Hii ikawa karata ya pili ya kujisogeza na kujiweka karibu na kanisa ili kutimiza malengo yake ya ufashisti.

Karata nyingine;aliamuru kufungwa kwa maduka yote ya vileo(wine shops) na kufuta leseni za clubs zote za usiku ili kuendana na kauli ya kanisa ya kupunguza uovu mitaani kwa ulevi na anasa za usiku.Hapa kanisa katoliki likanasa mtegoni.

Alienda mbali mpaka akatangaza kuwa "Public Swearing",yaani kujiapiza hadharani jina la Mungu kama "Public Crime"...Yaani mwananchi ukiwa mtaani mnabishana,mtu akikwambia sema Haki ya Mungu...Ukisema tu "Haki ya Mungu sijaenda nyumba ndogo mwezi wa pili sasa".Basi ujue wewe una kesi ya jinai ya kujibu.Hapa alitaka kulifurahisha kanisa kwa amri ile isemayo "Usitaje bure jina la bwana Mungu wako"

Mussolini akaamuru kupigwa marufuku vidonge vya majira na kampeni zote za matumizi ya uzazi wa mpango kama ulivyo msimamo wa kanisa.Wakati huo kanisa lilitaka wanawake wabaki nyumbani ili kulea watoto na kukuza familia vyema.Mussolini akalipigia chapuo hili na kulitungia sheria ili kuwafurahisha wazee wa kanisa.

Akatunga sheria ambayo ilifutilia mbali talaka kwa ndoa hata za bomani.Hii ilikuwa ni njia ya kuungana na kanisa ktk ndoa ya mke mmoja na isiyo na talaka mpaka Mungu awatenganishe.Ndoano hii ikanasa vizuri kwa kanisa.Hawakupepesuka wala kutikisika.Mambo yote ya ndoa yakaondolewa serikalini na kubaki kuwa in "Full Control of the Catholic Church".Wale wapenda mteremko wa ndoa za bomani wakakosa pa kwenda.

Akatoa 109 acres ktk mji wa Roma ili yajengwe makao makuu ya Papa(Vatican) baada ya kuwa yalipokonywa wakati wa "Unification of Italy" ya miaka ya 1870's,na akatoa amri kanisa lilipwe zaidi ya £130 milioni kwa wakati ule.Hii ilikuwa ni ndoano iliyoingia sawasawa kwa kanisa,na kanisa halikusema lolote juu ya "ufashisti" wa Mussolini hadharani;japo liliouona na kuuhisi kwake na kwa waumini wake.

Vatican ikawa nchi ndani ya mji,wakapewa mamlaka juu ya Post Office,jeshi dogo,polisi na "Rail station".Baada ya hapo,ugomvi ukawa ni nani anatakiwa ku-control Elimu?Mussolini alihitaji sekta ya elimu ili apandikize "ufashist" kwa watoto,na kanisa lilitaka elimu ili kupandikiza imani ya kikatoliki kwa watoto.

Mambo haya yote ambayo baadae,waumini wasio rasharasha waliona ni kama rushwa kwa kanisa ili liweze kusifia na kukaa kimya juu ya serikali ya kifashisti ya Mussolin yalifanikiwa.

Si ajabu Papa John Paul II alikuja kuiomba jumuiya ya waumini na wasio waumini ktk jubilei ya miaka 2000 ya Ukristo kwa yale yote kanisa iliyoyakosea ktk kukuwa kwake.Hili la kuukumbatia uonevu wa serikali isiyojali usawa ya Mussolini lilikuwa ni moja ya kosa la Kanisa.

Hakukuwa na Kardinali,askofu wala kasisi(padre) aliyeikemea serikali isiyo ya kidemokarasia ya Utawala wa Mussolini.Mengi yalitokea na kanisa lilikaa kimyaaa.Waumini waliteseka,waliumia na walipata machungu ya maisha...Lakini kanisa lilisema hewalaaa,huu ni utawala mzuri tu,maana umerudisha heshima ya Papa katika nchi ya Italia.

Hatumaanishi kuwa sasa Tanzania tuna ufashisti,lakini tunakubaliana kuwa kwa sasa Tanzania maisha ya chuki za kisiasa,mienendo ya kidemokrasia na ushiriki wa watu katika siasa huru umekengeuka sana.

Kuwa baba wa kiroho na kuongea kinyume cha yale waumini wako ambao ni sehemu ya wananchi wa Tanzania wanalalamika,ni kuwa upande wa pili badala ya ule wa waumini wako.

Ndio maana wale wanafunzi wa historia ya kale,wanaweza kustuka na kuona kuwa kanisa linaendelea kuwa upande tofauti na wanaoonewa.Kanisa libaki kuwa mali ya waumini wanyonge,liachane na urafiki wa mashaka kama ule wa Mussolini na Vatican enzi hizo za zama za giza za Ulaya.

Kama kanisa la wakati huo lilibaki kimya juu ya ufashisti wa Benitho Mussolini,hili la kwetu la Tanzania,lisibaki kimya juu ya uonevu wa kidemokrasia,vurugu za kuinajisi demokrasia unaonekana kufanywa waziwazi kabisa na serikali.Kutoa kauli za aina hii hadharani,mbele ya mimbari na katika altare takatifu,inatupa mashaka na tutaamua kurudi na kupekua kurasa za kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed"

Tukizifunua kurasa hizi;Tutahitimisha kwa kusema,Rais wa TEC amesimama upande wa serikali,amesimama na wanaodhaniwa kuminya demokrasia na mizizi yake,taswira ya waumini ambao ndio raia wenyewe kutokupendezwa na haya yanayoendelea haujaletwa na vyama vya upinzani,maana waumini walianza kugoma kujiandikisha mpaka pale walipohimizwa kwa lazima.

Hizi ni dalili kuwa si tu hatua ya kugomea uchaguzi imeasisiwa na vyama pinzani,bali ilishaanza kutendwa na waumini ambao ndio wapiga kira wenyewe.

Tutamkumbusha RAIS WA TEC na Askofu Mkuu wa Mbeya Nyaisonga kuwa kuutumikia mwili ni gharama zaidi ya kuitumikia roho.Ndio maana Lugha Mama ya Kanisa ya Kilatini ikasema "Nemo Liber Est Qui Corpori Servit"(No One is Free who is a slave of his body)

Tuitumikie Roho inayodumu milele,kuliko mwili unaooza na kuliwa na nyenyere.View attachment 1265377View attachment 1265378
TEC na Bakwata ni vitengo vya CCM
 
Huyu Askofu hajielewi,Ni meza ipi ya mazungumzo iliyoandaliwa?

Kama haya ni maamuzi ya baraza,hii ni aibu kwa kanisa Katoliki ambalo tulitegemea likemee uovu lakini limeamua kushirikiana na watesi wetu.
 
Hakuna cha intelijensia wala upuuzi mwingine wowote. Huyu amesukumwa na urafiki wake binafsi na mtawala. Na hili tamko kwa vyovyote ni lake yeye binafsi na syndicate yake.

Huyu Askofu, analinajisi Kanisa Katoliki.

Uko sahihi, haiwezekani zoezi lililoendeshwa kwa uhuni wa kitoto kiasi hiki, kisha kanisa katoliki wasione na kutoa tamko la huyo askofu. Kanisa la RC kwa kauli hii linapaswa kujitathmini kwa kutoka kwenye haki na kuamua kuwa sehemu ya siasa chafu.
 
Kumbe ndo maana wanatuambia usiangalie matendo yangu ila iman ya kanisa lako,hapa nmenotise kitu na kwa hali hii watapoteza waumini wengi sana ikiwemo mm,bora hata kua kkkt kule atleast wana misimamo iliyonyooka
 
Safisana askofu hakika uliyoyasema ni mfano wa kuigwa kwa viongozi wa vyama vya siasa!kuliko kususa wangekaa meza moja na serikali! Ubarikiwe Sana baba askofu

How realistic is this proposition ya vyama shindani kukaa meza moja na serikali? Mimi sidhani inawezekana. Ingawa vingozi wetu wa sasa kila siku wanatenda kinyume na kauli zao tukumbuke kuwa Rais alishapata kudai kuwa hawezi kukutana na washindani wake kwa sababu anahofia wanamtuma Bahraini! Ukweli ni kwambà sababu zinazofanya asikutane nao ni zile zile zinazofanya vyama vya upinzani kufunguliwa kufanya siasa na vyombo vya habari kudhibitiwa.
 
Wakatoriki tuliyo wengi tunapenda kutii uongozi uliyowekwa madarakani kwa ridhaa ya wananchi bila kutumia nguvu, ghiliba ,wanataka haki itendeke kwa chaguzi zote.Hakuna mwananchi anayetaka abaguliwe,na kunyimwa haki zake za msingi kulingana na katiba.Viongozi wangeshauri tuwe na mazingira mazuri ya uchaguzi yaliyo sawa kama vyama vyote vilivyosajiriwa wakae kwanza waelewane maana sisi sote tumeumbwa kwa sura ya Mwenyezi Mungu ,waunde tume iliyo huru ya uchaguzi.Kama hakuna impartiality there is no need for election
 
Usituletee ujinga wewe askofu nyaisonga, sisi si wajinga, sisi ambao tuko katika vyama vya upizani sio wote ambao ni wakatoliki, na pia najua sio wakatoliki wote wanakuunga mkono, sikiza kwa maakiini wewe askofu, kama umekula hela ya ccm na mungu wa kina wanaccm magufuli sisi wengine hatujakula hela ya ccm na hatutaki hela iliyoimbiwa kota kwa walipa kodi,hatutaki hela ya magufuli na ccm yake, hujui vile wananchi wanaumia , wewe uko na hela ya kutosha, huna mke au watoto(hata kaa maaskofu wengine na mapadre wa katoliki wako na wasichana kibao wanaolala nao kwa siri)sisi ndio tunaumia huko kwa kukosa ajira, misharaha haijaongezwa kwa miaka 4,wapizani kubadikiwa kesi, wengine kupigwa risasi, waandishi wa habari kutekwa na kuuawa huko mto ruvuma, na wakati hii nyote inajili wewe mkuu wa katoliki na maaskofu wenza munapiga makofi tu, sababu? hamna shinda yeyote hela iko kibao ya sadaka, ikiisha munaitisha hela huko roma na mambo mengi, baba askofu LEAVE US ALONE WE OPPOSITION PLS, achana na sisi, endelea kuabundu mungu wako magufuli na binguni yake inayoitwa ccm, freedom will came one day, wewe askofu umekuwa kibaraka wa magufuli na wauaji wake wa uvccm
 
Binafsi Roha Mtakatifu ananielekeza kutopiga kura..!
 
Nimesikiliza mahubiri ya Askofu Mkuu na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tz,Mhashamu Askofu Nyaisonga, ameelekeza lawama zake katika vyama vya upinzani,akijenga hoja kuwa havikutumia busara na elimu katika kufikiri na kujitoa katika uchaguzi.

Amehimiza kuwa kujitoa sio suluhu,wanapaswa kukaa meza moja na serikali kutatua hiyo changamoto,amesisitiza kuwa waliojitoa wamekosea,hivyo kasema msimamo wa maaskofu Wakatoliki ni kutokubaliana na kusisia uchaguzi,na wamehimiza waumini kujitokeza wa wingi jumapili kupiga kura.

Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Peter O'bay naye amehubiri kile alichotumwa na wakubwa zake, kuhimiza watu wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi, hii ni kusema, kanisa katoliki linaungana na Polepole, Jafo na TAMISEMI kuubariki uchaguzi wa serikali za mitaa ambao mchakato wake umejaa utata mtupu,utata ambao hata makada wazoefu wa CCM wanaona aibu kwa yaliyotokea. Hili ndio kanisa Katoliki na msimamo wake umetangazwa na Rais wa TEC. Kanisa limeridhika na mchakato, halitaki kugombana na serikali, limewakana waumini wake waliogoma toka mwanzo kujiandikisha kwa kuona ubovu wa demokrasia kwa sasa.

Katika maandishi ya kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed", mwandishi alijaribu kuelezea kwa undani jinsi kanisa, na hasa kanisa la Vatican wakati mwingi lilivyoshiriki kuungana na serikali katika kuisaidia kufikia adhma yake, mwandishi ameeleza nafasi ya wamisionari katika kuitawala Afrika, jinsi walivyotangulia na kuwatengenezea njia wakoloni, kuanzia Congo ya DR mpaka Afrika ya Kusini,Kaskazini na Mashariki ya Afrika. Mwandishi anasema kanisa huangalia kwanza maslahi ya viongozi wake kabla ya waumini wake.

Inaelezwa kuwa wakati wa utawala wa Kifashisti kule Italia, Mussolini aliona tishio la Kanisa Katoliki ktk kufikia malengo yake. Maana kwa wakati ule, kanisa lilikuwa na ushawishi wa kila sekta ya maisha ya kiroho na kimwili na serikali ilikuwa na ushawishi mdogo tu ya maisha ya kisiasa.

Alichokifanya Mussolin ni kujipendekeza kwa kanisa na kutoa "rushwa" ili yote atakayoyafanya kanisa katoliki lililokuwa na nguvu sana Italia libaki kimyaa.Na Alifanikiwa...

Kwanza aliamua kumbatiza mwanae wa kiume, ambaye hapo awali hakuwa amebatizwa.Hapa akaliteka kanisa kwa karata ya kwanza.

Pili alimua kufunga ndoa ya kikanisa,baada ya kuwa amekaa miaka 11 na ndoa ya bomani na mkewe Rachele.Hii ikawa karata ya pili ya kujisogeza na kujiweka karibu na kanisa ili kutimiza malengo yake ya ufashisti.

Karata nyingine;aliamuru kufungwa kwa maduka yote ya vileo(wine shops) na kufuta leseni za clubs zote za usiku ili kuendana na kauli ya kanisa ya kupunguza uovu mitaani kwa ulevi na anasa za usiku.Hapa kanisa katoliki likanasa mtegoni.

Alienda mbali mpaka akatangaza kuwa "Public Swearing",yaani kujiapiza hadharani jina la Mungu kama "Public Crime"...Yaani mwananchi ukiwa mtaani mnabishana,mtu akikwambia sema Haki ya Mungu...Ukisema tu "Haki ya Mungu sijaenda nyumba ndogo mwezi wa pili sasa".Basi ujue wewe una kesi ya jinai ya kujibu.Hapa alitaka kulifurahisha kanisa kwa amri ile isemayo "Usitaje bure jina la bwana Mungu wako"

Mussolini akaamuru kupigwa marufuku vidonge vya majira na kampeni zote za matumizi ya uzazi wa mpango kama ulivyo msimamo wa kanisa.Wakati huo kanisa lilitaka wanawake wabaki nyumbani ili kulea watoto na kukuza familia vyema.Mussolini akalipigia chapuo hili na kulitungia sheria ili kuwafurahisha wazee wa kanisa.

Akatunga sheria ambayo ilifutilia mbali talaka kwa ndoa hata za bomani.Hii ilikuwa ni njia ya kuungana na kanisa ktk ndoa ya mke mmoja na isiyo na talaka mpaka Mungu awatenganishe.Ndoano hii ikanasa vizuri kwa kanisa.Hawakupepesuka wala kutikisika.Mambo yote ya ndoa yakaondolewa serikalini na kubaki kuwa in "Full Control of the Catholic Church".Wale wapenda mteremko wa ndoa za bomani wakakosa pa kwenda.

Akatoa 109 acres ktk mji wa Roma ili yajengwe makao makuu ya Papa(Vatican) baada ya kuwa yalipokonywa wakati wa "Unification of Italy" ya miaka ya 1870's,na akatoa amri kanisa lilipwe zaidi ya £130 milioni kwa wakati ule.Hii ilikuwa ni ndoano iliyoingia sawasawa kwa kanisa,na kanisa halikusema lolote juu ya "ufashisti" wa Mussolini hadharani;japo liliouona na kuuhisi kwake na kwa waumini wake.

Vatican ikawa nchi ndani ya mji,wakapewa mamlaka juu ya Post Office,jeshi dogo,polisi na "Rail station".Baada ya hapo,ugomvi ukawa ni nani anatakiwa ku-control Elimu?Mussolini alihitaji sekta ya elimu ili apandikize "ufashist" kwa watoto,na kanisa lilitaka elimu ili kupandikiza imani ya kikatoliki kwa watoto.

Mambo haya yote ambayo baadae,waumini wasio rasharasha waliona ni kama rushwa kwa kanisa ili liweze kusifia na kukaa kimya juu ya serikali ya kifashisti ya Mussolin yalifanikiwa.

Si ajabu Papa John Paul II alikuja kuiomba jumuiya ya waumini na wasio waumini ktk jubilei ya miaka 2000 ya Ukristo kwa yale yote kanisa iliyoyakosea ktk kukuwa kwake.Hili la kuukumbatia uonevu wa serikali isiyojali usawa ya Mussolini lilikuwa ni moja ya kosa la Kanisa.

Hakukuwa na Kardinali,askofu wala kasisi(padre) aliyeikemea serikali isiyo ya kidemokarasia ya Utawala wa Mussolini.Mengi yalitokea na kanisa lilikaa kimyaaa.Waumini waliteseka,waliumia na walipata machungu ya maisha...Lakini kanisa lilisema hewalaaa,huu ni utawala mzuri tu,maana umerudisha heshima ya Papa katika nchi ya Italia.

Hatumaanishi kuwa sasa Tanzania tuna ufashisti,lakini tunakubaliana kuwa kwa sasa Tanzania maisha ya chuki za kisiasa,mienendo ya kidemokrasia na ushiriki wa watu katika siasa huru umekengeuka sana.

Kuwa baba wa kiroho na kuongea kinyume cha yale waumini wako ambao ni sehemu ya wananchi wa Tanzania wanalalamika,ni kuwa upande wa pili badala ya ule wa waumini wako.

Ndio maana wale wanafunzi wa historia ya kale,wanaweza kustuka na kuona kuwa kanisa linaendelea kuwa upande tofauti na wanaoonewa.Kanisa libaki kuwa mali ya waumini wanyonge,liachane na urafiki wa mashaka kama ule wa Mussolini na Vatican enzi hizo za zama za giza za Ulaya.

Kama kanisa la wakati huo lilibaki kimya juu ya ufashisti wa Benitho Mussolini,hili la kwetu la Tanzania,lisibaki kimya juu ya uonevu wa kidemokrasia,vurugu za kuinajisi demokrasia unaonekana kufanywa waziwazi kabisa na serikali.Kutoa kauli za aina hii hadharani,mbele ya mimbari na katika altare takatifu,inatupa mashaka na tutaamua kurudi na kupekua kurasa za kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed"

Tukizifunua kurasa hizi;Tutahitimisha kwa kusema,Rais wa TEC amesimama upande wa serikali,amesimama na wanaodhaniwa kuminya demokrasia na mizizi yake,taswira ya waumini ambao ndio raia wenyewe kutokupendezwa na haya yanayoendelea haujaletwa na vyama vya upinzani,maana waumini walianza kugoma kujiandikisha mpaka pale walipohimizwa kwa lazima.

Hizi ni dalili kuwa si tu hatua ya kugomea uchaguzi imeasisiwa na vyama pinzani,bali ilishaanza kutendwa na waumini ambao ndio wapiga kira wenyewe.

Tutamkumbusha RAIS WA TEC na Askofu Mkuu wa Mbeya Nyaisonga kuwa kuutumikia mwili ni gharama zaidi ya kuitumikia roho.Ndio maana Lugha Mama ya Kanisa ya Kilatini ikasema "Nemo Liber Est Qui Corpori Servit"(No One is Free who is a slave of his body)

Tuitumikie Roho inayodumu milele,kuliko mwili unaooza na kuliwa na nyenyere.View attachment 1265377View attachment 1265378
[/QUO. Naama roman
 
Haya ni maoni ya Baba Askofu, naamini wote mmeyasikia na mtayaheshimu. Msimkashifu wala kumsemea yaliyo mabaya mtumishi wa Mungu kwa kutoa maoni yake ambayo kwake yeye anaamini yapo sahihi. Kutofautiana ni kawaida sana, tusiwe kama wale ambao watumishi wa Mungu wakinena yanayowafurahisha wanawasifu ila wakinena yasiyowafurahishi wanawakejeli na kuwaambia waache kuchanganya dini na siasa.

Katika kusimamia haki usiamini nguvu ya mtu mwingine yeyote bali nguvu yako tu. Baba hata Mama yako wanaweza kukuacha pamoja na kuwa wewe ndio unawatafutia chakula. Ni vipi kwa mtu mwingine anayejitegemea mwenyewe kwa kila kitu?
 
fumbo la mfumo ndani ya mfumo imejionyesha kama jua

na hii similarity inashangaza..

ameondoka Pengo ,watu wakashukuru alipokuja Ruwaichi..

Kutanabahi amekuja Askofu Nyaisonga...na mtazamo wake huku ukichagizwa na dhana ya mfumo...usioonekana lakini upo

*akili kumkichwa ndio hii ya Askofu nyaisonga
 
Niliwahi kueleza hapa jukwaani taarifa kutoka kwa Askofu mmoja kutoka inner circle ya Kanisa Katoliki. Mimi pia ni mkatoliki halisi wa imani aliyewahi kuhudumu ndani ya kanisa.

Askofu yile alieleza kuwa Kanisa Katoliki, baada ya waraka wa kwaresma, ulioeleza mapungufu mengi ya watawala wa awamu hii, uhusiano wake na mtawala mkuu ulififia sana kufikia hatua ya kujenga uadui. Inner circle ya Kanisa waliazimia kuurudisha uhusiano huo uliokuwa umezoeleka.

Hatua ya kwanza ilikuwa kumpata Rais wa TEC ambaye ana mahusiano binafsi ya karibu na mtawala, na huyo hakuwa mwingine bali huyu Rais wa TEC wa sasa. Hilo lilifanikiwa.

Na ninarudia tena, chini ya uongozi wa sasa wa TEC, msitegemee kauli yoyote ile kutoka TEC itakayokuwa kinyume na matakwa ya watawala. Kanisa, kama lilivyo bunge na mahakama, wamejumuishwa. Mark my words.

Mimi niliyasikia haya wakati wa kipindi cha kumpata Rais mpya wa TEC. Jambo la kujiuliza, hivi hizi dini zetu zipo kwaajili ya imani au maslahi fulani? Ni dini au watu fulani ndio wanaozifanya dini kuwa syndicate ya matakwa binafsi ya watu fulani?
Kama na Kanisa Katoliki linalamba soli ya Jiwe basi halina maana. Nami nawatupia lawama maaakofu wote walio compromise na Serikali kwa sababu ya mahusiano mabaya. Hebu waenda DRC wakaona RC ilivyo shamiri
 
Hadi kanisa lifafanue na kuhimaza. Hilo peke yake ni kuonesha kuna shida. Lakini kanisa linazungumzia kukaa meza moja, hivi ni kweli kanisa hilo halikupata kuona mwenendo usio sawa?
Na halitakuja kuona kamwe ndani ya awamu hii
 
Back
Top Bottom