Askofu Nyaisonga avishangaa Vyama vya Upinzani kususia uchaguzi. Ahimiza waumini kujitokeza kupiga kura na kuchagua viongozi

Askofu Nyaisonga avishangaa Vyama vya Upinzani kususia uchaguzi. Ahimiza waumini kujitokeza kupiga kura na kuchagua viongozi

Askofu ni kula kulala mnufaika wa sadaka zetu hivo ajui chochote wala hana uchungu wowote,angekuwa anabeba zege asingetamka hayo
Kazi anayofanya askofu, au kiongozi yeyote wa dini mkweli, anayetambua kwamba Mungu ni Mungu wa haki, kazi yake ni kubwa hata kuliko kubeba zege. Hapa Siongelei wachumia tumbo.
 
Mkuu umelikuza sana hili jambo, Tanzania haina mfanano wowote na Italy ya Musolin.

Sijui ni kwanini huwa hamtaki kuwafanya wapinzani wawe responsible kwa makosa yao??

Yaani kulialia tu kwa almost kila kitu.

Sijui tunajenga jamii ya aina gani??

Ambayo kuna ka kikundi ka watu hakataki kufuata utaratibu wowote ila kana haki ya kupata kila kitu.

Upinzani wetu na ufananisha na madereve boda boda barabarani.
 
Askofu wa TEC si mungu ni mwanadamu, Askofu wa TEC hawezi kuamua wananchi wamchague nani? Kiongozi wa dini mwenye hofu ya mungu atasema kweli daima hatapindisha ,Askofu mwenye hofu ya mungu huonya aonapo pindi serikali inapofanya sivyo ndivyo,

Askofu wa kweli yuko tayari kuwatetea wanyonge wapate haki zao.
Anaempinga askofu huyo atakuwa ana mapepo si bule. Mi naamini kabisa askofu kaongozwa na roho mtakatifu kuwahubiria watu kweli, kabla ya kumshambulia hebu tujitafakari wapinzani wapi tumejikwaa. Ikifikia hatua tunawapinga viongozi watakatifu hiyo ni dalili ya laana
 
Kwa Bwana Magu Kila Goti Litapigwa..

somo kutoka katika Waraka wa kwanza wa Nyaisonga kwa Wakatoliki

(1 Nya 2019 :18-8)
 
Daaahhh................yaaaani Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume.
 
Niliwahi kueleza hapa jukwaani taarifa kutoka kwa Askofu mmoja kutoka inner circle ya Kanisa Katoliki. Mimi pia ni mkatoliki halisi wa imani aliyewahi kuhudumu ndani ya kanisa.

Askofu yile alieleza kuwa Kanisa Katoliki, baada ya waraka wa kwaresma, ulioeleza mapungufu mengi ya watawala wa awamu hii, uhusiano wake na mtawala mkuu ulififia sana kufikia hatua ya kujenga uadui. Inner circle ya Kanisa waliazimia kuurudisha uhusiano huo uliokuwa umezoeleka.

Hatua ya kwanza ilikuwa kumpata Rais wa TEC ambaye ana mahusiano binafsi ya karibu na mtawala, na huyo hakuwa mwingine bali huyu Rais wa TEC wa sasa. Hilo lilifanikiwa.

Na ninarudia tena, chini ya uongozi wa sasa wa TEC, msitegemee kauli yoyote ile kutoka TEC itakayokuwa kinyume na matakwa ya watawala. Kanisa, kama lilivyo bunge na mahakama, wamejumuishwa. Mark my words.

Mimi niliyasikia haya wakati wa kipindi cha kumpata Rais mpya wa TEC. Jambo la kujiuliza, hivi hizi dini zetu zipo kwaajili ya imani au maslahi fulani? Ni dini au watu fulani ndio wanaozifanya dini kuwa syndicate ya matakwa binafsi ya watu fulani?
Jana uzi huu niliupuuza sikutaka hata kuusoma nikafikiri tu kuna mkichaa mmoja kaja na yake, leo nimekuta thread nyingi kuhusu hili. Basi ni wazi kama aliesema hili ndio bossi wa TEC, kanisa katoliki limeamua kumkumbatia kaisari na kuacha watu wake wakione chochote kinachofikiriwa na wakubwa. Tuseme yaliyo moyoni nao hupita humu na kuyasoma nakila mwenye uwezo au sauti aseme yake kuhusu hili. Makanisa wakati wa UKUTA walikwenda kwa JIWE kujaribu kumkutanisha na WAPINZANI hadi leo JIWE amekataa, leo askofu anasema WAPINZANI wakae na kuongea na JIWE. Hivi wanafikiri yaliyotokea ni bahati mbaya serikali hii inaweza kuyabadilisha? Inasikitisha lakini ndiyo hivyo tena KONDOO wametelekezwa na mchungaji. Kanisa Katoliki lijitafakari tena.
 
Niliwahi kueleza hapa jukwaani taarifa kutoka kwa Askofu mmoja kutoka inner circle ya Kanisa Katoliki. Mimi pia ni mkatoliki halisi wa imani aliyewahi kuhudumu ndani ya kanisa.

Askofu yile alieleza kuwa Kanisa Katoliki, baada ya waraka wa kwaresma, ulioeleza mapungufu mengi ya watawala wa awamu hii, uhusiano wake na mtawala mkuu ulififia sana kufikia hatua ya kujenga uadui. Inner circle ya Kanisa waliazimia kuurudisha uhusiano huo uliokuwa umezoeleka.

Hatua ya kwanza ilikuwa kumpata Rais wa TEC ambaye ana mahusiano binafsi ya karibu na mtawala, na huyo hakuwa mwingine bali huyu Rais wa TEC wa sasa. Hilo lilifanikiwa.

Na ninarudia tena, chini ya uongozi wa sasa wa TEC, msitegemee kauli yoyote ile kutoka TEC itakayokuwa kinyume na matakwa ya watawala. Kanisa, kama lilivyo bunge na mahakama, wamejumuishwa. Mark my words.

Mimi niliyasikia haya wakati wa kipindi cha kumpata Rais mpya wa TEC. Jambo la kujiuliza, hivi hizi dini zetu zipo kwaajili ya imani au maslahi fulani? Ni dini au watu fulani ndio wanaozifanya dini kuwa syndicate ya matakwa binafsi ya watu fulani?
Kuna baadhi ya viongozi wetu wa dini hakika kuna wakati wanajivunjia heshima wenyewe, sijui ni kwa nini wanashindwa kuiga mfano wa wenzao waliokuwepo wakati ule wa awamu ya kwanza ambapo serikali ilkuwa inawaheshimu sana na kila wakati serikali ilikuwa ikikumbana na changamoto yeyote ilikuwa ikiwaita kuwaomba ushauri, sasa hivi maswala ya imani za dini eti yanapelekwa serikalini kuomba ushauri, na matokeo yake serikali imewadharau viongozi wa dini nao wanahaha kujikomba kwake ili wapendwe, sasa hivi hata mkuu wa wilaya anaweza kutoa vitisho, kejeli, matamko na au maagizo kwa viongozi wakuu wa dini ?.
 
Binafsi nachukulia kwamba mjadala wa uhalali wa uchaguzi wa serikali za mitaa umefungwa rasmi kufuatia tamko la Baba Askofu Nyaisonga wa Kanisa kubwa kabisa nchini.

Awali wakati wa Baraza la Maulidi viongozi wa Bakwata wakiongozwa na Mufti Abubakar waliwataka Waislamu wote nchini kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa bila ya kuwa na visingizio vyovyote.

Naye Baba Askofu Nyaisonga ametoa wito kama huo wa kuwataka Wakristo wote na wale wenye mapenzi mema kushiriki uchaguzi huo kwa 100%.

Mjadala umefungwa, shime Watanzania tujitokeze kwa wingi 24/11/2019 kuchagua viongozi wetu wa serikali za mitaa.

Amen!

Maendeleo hayana vyama!
 
Nimesikiliza mahubiri ya Askofu Mkuu na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tz,Mhashamu Askofu Nyaisonga, ameelekeza lawama zake katika vyama vya upinzani,akijenga hoja kuwa havikutumia busara na elimu katika kufikiri na kujitoa katika uchaguzi.

Amehimiza kuwa kujitoa sio suluhu,wanapaswa kukaa meza moja na serikali kutatua hiyo changamoto,amesisitiza kuwa waliojitoa wamekosea,hivyo kasema msimamo wa maaskofu Wakatoliki ni kutokubaliana na kusisia uchaguzi,na wamehimiza waumini kujitokeza wa wingi jumapili kupiga kura.

Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Peter O'bay naye amehubiri kile alichotumwa na wakubwa zake, kuhimiza watu wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi, hii ni kusema, kanisa katoliki linaungana na Polepole, Jafo na TAMISEMI kuubariki uchaguzi wa serikali za mitaa ambao mchakato wake umejaa utata mtupu,utata ambao hata makada wazoefu wa CCM wanaona aibu kwa yaliyotokea. Hili ndio kanisa Katoliki na msimamo wake umetangazwa na Rais wa TEC. Kanisa limeridhika na mchakato, halitaki kugombana na serikali, limewakana waumini wake waliogoma toka mwanzo kujiandikisha kwa kuona ubovu wa demokrasia kwa sasa.

Katika maandishi ya kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed", mwandishi alijaribu kuelezea kwa undani jinsi kanisa, na hasa kanisa la Vatican wakati mwingi lilivyoshiriki kuungana na serikali katika kuisaidia kufikia adhma yake, mwandishi ameeleza nafasi ya wamisionari katika kuitawala Afrika, jinsi walivyotangulia na kuwatengenezea njia wakoloni, kuanzia Congo ya DR mpaka Afrika ya Kusini,Kaskazini na Mashariki ya Afrika. Mwandishi anasema kanisa huangalia kwanza maslahi ya viongozi wake kabla ya waumini wake.

Inaelezwa kuwa wakati wa utawala wa Kifashisti kule Italia, Mussolini aliona tishio la Kanisa Katoliki ktk kufikia malengo yake. Maana kwa wakati ule, kanisa lilikuwa na ushawishi wa kila sekta ya maisha ya kiroho na kimwili na serikali ilikuwa na ushawishi mdogo tu ya maisha ya kisiasa.

Alichokifanya Mussolin ni kujipendekeza kwa kanisa na kutoa "rushwa" ili yote atakayoyafanya kanisa katoliki lililokuwa na nguvu sana Italia libaki kimyaa.Na Alifanikiwa...

Kwanza aliamua kumbatiza mwanae wa kiume, ambaye hapo awali hakuwa amebatizwa.Hapa akaliteka kanisa kwa karata ya kwanza.

Pili alimua kufunga ndoa ya kikanisa,baada ya kuwa amekaa miaka 11 na ndoa ya bomani na mkewe Rachele.Hii ikawa karata ya pili ya kujisogeza na kujiweka karibu na kanisa ili kutimiza malengo yake ya ufashisti.

Karata nyingine;aliamuru kufungwa kwa maduka yote ya vileo(wine shops) na kufuta leseni za clubs zote za usiku ili kuendana na kauli ya kanisa ya kupunguza uovu mitaani kwa ulevi na anasa za usiku.Hapa kanisa katoliki likanasa mtegoni.

Alienda mbali mpaka akatangaza kuwa "Public Swearing",yaani kujiapiza hadharani jina la Mungu kama "Public Crime"...Yaani mwananchi ukiwa mtaani mnabishana,mtu akikwambia sema Haki ya Mungu...Ukisema tu "Haki ya Mungu sijaenda nyumba ndogo mwezi wa pili sasa".Basi ujue wewe una kesi ya jinai ya kujibu.Hapa alitaka kulifurahisha kanisa kwa amri ile isemayo "Usitaje bure jina la bwana Mungu wako"

Mussolini akaamuru kupigwa marufuku vidonge vya majira na kampeni zote za matumizi ya uzazi wa mpango kama ulivyo msimamo wa kanisa.Wakati huo kanisa lilitaka wanawake wabaki nyumbani ili kulea watoto na kukuza familia vyema.Mussolini akalipigia chapuo hili na kulitungia sheria ili kuwafurahisha wazee wa kanisa.

Akatunga sheria ambayo ilifutilia mbali talaka kwa ndoa hata za bomani.Hii ilikuwa ni njia ya kuungana na kanisa ktk ndoa ya mke mmoja na isiyo na talaka mpaka Mungu awatenganishe.Ndoano hii ikanasa vizuri kwa kanisa.Hawakupepesuka wala kutikisika.Mambo yote ya ndoa yakaondolewa serikalini na kubaki kuwa in "Full Control of the Catholic Church".Wale wapenda mteremko wa ndoa za bomani wakakosa pa kwenda.

Akatoa 109 acres ktk mji wa Roma ili yajengwe makao makuu ya Papa(Vatican) baada ya kuwa yalipokonywa wakati wa "Unification of Italy" ya miaka ya 1870's,na akatoa amri kanisa lilipwe zaidi ya £130 milioni kwa wakati ule.Hii ilikuwa ni ndoano iliyoingia sawasawa kwa kanisa,na kanisa halikusema lolote juu ya "ufashisti" wa Mussolini hadharani;japo liliouona na kuuhisi kwake na kwa waumini wake.

Vatican ikawa nchi ndani ya mji,wakapewa mamlaka juu ya Post Office,jeshi dogo,polisi na "Rail station".Baada ya hapo,ugomvi ukawa ni nani anatakiwa ku-control Elimu?Mussolini alihitaji sekta ya elimu ili apandikize "ufashist" kwa watoto,na kanisa lilitaka elimu ili kupandikiza imani ya kikatoliki kwa watoto.

Mambo haya yote ambayo baadae,waumini wasio rasharasha waliona ni kama rushwa kwa kanisa ili liweze kusifia na kukaa kimya juu ya serikali ya kifashisti ya Mussolin yalifanikiwa.

Si ajabu Papa John Paul II alikuja kuiomba jumuiya ya waumini na wasio waumini ktk jubilei ya miaka 2000 ya Ukristo kwa yale yote kanisa iliyoyakosea ktk kukuwa kwake.Hili la kuukumbatia uonevu wa serikali isiyojali usawa ya Mussolini lilikuwa ni moja ya kosa la Kanisa.

Hakukuwa na Kardinali,askofu wala kasisi(padre) aliyeikemea serikali isiyo ya kidemokarasia ya Utawala wa Mussolini.Mengi yalitokea na kanisa lilikaa kimyaaa.Waumini waliteseka,waliumia na walipata machungu ya maisha...Lakini kanisa lilisema hewalaaa,huu ni utawala mzuri tu,maana umerudisha heshima ya Papa katika nchi ya Italia.

Hatumaanishi kuwa sasa Tanzania tuna ufashisti,lakini tunakubaliana kuwa kwa sasa Tanzania maisha ya chuki za kisiasa,mienendo ya kidemokrasia na ushiriki wa watu katika siasa huru umekengeuka sana.

Kuwa baba wa kiroho na kuongea kinyume cha yale waumini wako ambao ni sehemu ya wananchi wa Tanzania wanalalamika,ni kuwa upande wa pili badala ya ule wa waumini wako.

Ndio maana wale wanafunzi wa historia ya kale,wanaweza kustuka na kuona kuwa kanisa linaendelea kuwa upande tofauti na wanaoonewa.Kanisa libaki kuwa mali ya waumini wanyonge,liachane na urafiki wa mashaka kama ule wa Mussolini na Vatican enzi hizo za zama za giza za Ulaya.

Kama kanisa la wakati huo lilibaki kimya juu ya ufashisti wa Benitho Mussolini,hili la kwetu la Tanzania,lisibaki kimya juu ya uonevu wa kidemokrasia,vurugu za kuinajisi demokrasia unaonekana kufanywa waziwazi kabisa na serikali.Kutoa kauli za aina hii hadharani,mbele ya mimbari na katika altare takatifu,inatupa mashaka na tutaamua kurudi na kupekua kurasa za kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed"

Tukizifunua kurasa hizi;Tutahitimisha kwa kusema,Rais wa TEC amesimama upande wa serikali,amesimama na wanaodhaniwa kuminya demokrasia na mizizi yake,taswira ya waumini ambao ndio raia wenyewe kutokupendezwa na haya yanayoendelea haujaletwa na vyama vya upinzani,maana waumini walianza kugoma kujiandikisha mpaka pale walipohimizwa kwa lazima.

Hizi ni dalili kuwa si tu hatua ya kugomea uchaguzi imeasisiwa na vyama pinzani,bali ilishaanza kutendwa na waumini ambao ndio wapiga kira wenyewe.

Tutamkumbusha RAIS WA TEC na Askofu Mkuu wa Mbeya Nyaisonga kuwa kuutumikia mwili ni gharama zaidi ya kuitumikia roho.Ndio maana Lugha Mama ya Kanisa ya Kilatini ikasema "Nemo Liber Est Qui Corpori Servit"(No One is Free who is a slave of his body)

Tuitumikie Roho inayodumu milele,kuliko mwili unaooza na kuliwa na nyenyere.View attachment 1265377View attachment 1265378
Tatizo la huyu askofu ni la kisaikolojia zaidi.
Huyu ni mtu anaeishi kambini bila familia. Hana mke , hana watoto na hajui uchungu wa mwana kama isemwavyo uchungu wa mwana aujuae ni mzazi.

Sasa mtu wa namna hii kumkabidhi jukumu la kuzisimamia familia ili hali yeye hana familia yake mwenyewe aliye iweza kwa kuisimamia ndio hivyo maumivu, maudhi, uonevu, ukandamizaji, ubabe na mengi ya namna hiyo hayata isha katika jamii inayosimamiwa na mtu wa aina ya askofu Nyaisonga.
 
Hakika nilikusoma vyema katika ile mada.
Lakini sasa inanibidi nianze kujiuliza, na kuwasihi nanyi wenzangu kukuna vichwa juu ya "ushawishi/nguvu" za huyu mtu mmoja anayeteka kila kitu.

Tunaelewa wazi hana uwezo wa kujenga mifumo ya kumsaidia aeneze mawazo yake kwa wengine, ila yeye njia yake kuu ni 'nguvu/mabavu.'

Kwa kutumia njia hii ameweza kuteka kila kitu - mihimili yote, Bunge na Mahakama. Kwa njia hiyo hiyo ameweza kuteka dini zote?; ingawaje mtu anaweza akasema njia hizo hazijatumika BAKWATA. Wao walichopewa na kuridhika nacho ni 'rushwa' ya kujengewa nyumba ya ibada. Alipofanya hivyo akawaziba midomo.

Amejaribu kutumia njia hizo hizo hata kwa raia.
Wasiokubaliana naye, kama vyama vya upinzani, suluhu ni mabavu. Upande wa wananchi, amefanya kila kitu aonekane anawajali wananchi zaidi - miradi mikubwa na hata rushwa za kugawa manoti mitaani.

Zaidi ya hapo, hajajenga chochote cha kuimarisha anayoyasimamia. CCM yenyewe ipo tu sasa hivi kama chombo chake cha kukitumia wakati wowote apendavyo yeye.

Kwa hiyo, yote haya yanafanyika kwa sababu anvyo vyombo vya kulazimisha watu wafuate anavyopenda yeye. Bila hivi vifaa, hana msingi wowote wa kumweka alipo.

Mkuu haya ni kama utani lakini ndio hivyo yanatokea. Tutarajie mabaya ya kutisha huko mbeleni.
 
Kanisa katoliki limeingia kwenye uporaji wa Democracy Ngoja tusubiri matokeo coz naona wamekubali kumsujudia Mungu MTU kiongozi wa Malaika
 
Back
Top Bottom